Maji ya uhai

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,848
2,669
Hivi karibuni kumekuwa na minong'ono kuwa maji ya uhai sio salama. Kwa kuthibitisha hilo, chupa nyingi ukizitazama kwenye kitako zina kovu linalosadikika ni kutokana na kuzibwa kwa super glue baada ya kuingiza maji kwa kutumia sindano. Kama ni kweli, hii ni hatari. Wahusika wanatakiwa kujibu hizi tuhuma na kuhakikisha wanaondokana na hii kashfa kabla biashara yao haijaingia doa
 
duh hii kali kama kweli Bongo hayo yanatendeka tuna safari ndefu kuheshimu biashara za watu!
 
Nilipokua nasoma thread yako pemben nlikua na chupa za maj ya uhai kama mbili. Zote nimechek ni kama ulvonena.

Mbona 2takufa mwaka huu.
Tatizo ukicheki seal ni very genuine. Na ndio mi huchek hiyo 2 nnaponunua. Kumbe wapumbavu hilo wanalitambua!
Nimechoka!
 
Nadhani watakuwa wastaarabu kama watatokeza hapa kujibu juu ya hilo tundu lililopakwa pattex, ili kuweka mambo sawa..huh!
 
Tunauawa na wataalam wetu wasiofanya homework zao vyema na kuchukua hatua dhidi ya bidhaa feki.
Niliktumia maji uhai last week nilipatwa na matatizo ya tumbo kinoma. we acha tu
 
Mi leo nimeenda sehem nikanunua uhai ya 500/= nikacheki nikakuta yana kovu ila nikashindwa kuyarudisha. Nilichojimbia ni kuwa sitanunua tena haya maji. Ni lazima wajitokeze kujibu tuhuma
 
Mwee! na ya litre 12 je? Mbona mtanifanya nichanganyikiwe,mwenzenu kila siku lazima nipitie kwa mangi kununua kabla sijaenda home!
 
Maji gani masafi hapa bongo, kila product ina tatizo. Nendeni kwenye problem hiyo tfda na tbs wanafanya nini? Afterall kama kuna tatizo kubwa litaonekana. Pia kuna propaganda za kibiashara siyo kila kitu ukiambiwa ok check chupa za maji yote
 
Hata kama ni kweli nasikitika kusema kuwa biashara yao itazidi kuendelea vizuri.
kwanza kwa sababu wa TZ we dont care about quality and our health na tunapenda vya bei rahisi.
Pili TFDA,TBS ipo usingizini,wakiamka tushaathirika.Kwani vitu vingapi vya kichina vimejaa madukani ni fake? sembuse maji ya uhai?
 
Hata kama ni kweli nasikitika kusema kuwa biashara yao itazidi kuendelea vizuri.
kwanza kwa sababu wa TZ we dont care about quality and our health na tunapenda vya bei rahisi.
Pili TFDA,TBS ipo usingizini,wakiamka tushaathirika.Kwani vitu vingapi vya kichina vimejaa madukani ni fake? sembuse maji ya uhai?


TFDA na TBS wanafanya nn? ukiangalia taarifa za habari utawaona TBS wameenda kutembele maduka ya dawa ya vipodoz tena kariakoo, sehemu nyingine na mikoani inakuwaje? mtaani kwetu vimejaa vitu feki kuanzia biscut, pipi, maji, nguo, simu, vifaa vya ujenzi, vya nyumbani n.k. na ukijifanya unatafuta original utasafiri kwenda mjini kwenye maduka ya uhakika kama ya TPDF na baadhi yenye uhakika. Tena kama haitoshi lazima uwe mjanja unaye vijua vitu.
Mungu atusaidie vinginevyo Tanzania yetu hii itaendelea kuwa DAMPO!
 
Hivi karibuni kumekuwa na minong'ono kuwa maji ya uhai sio salama. Kwa kuthibitisha hilo, chupa nyingi ukizitazama kwenye kitako zina kovu linalosadikika ni kutokana na kuzibwa kwa super glue baada ya kuingiza maji kwa kutumia sindano. Kama ni kweli, hii ni hatari. Wahusika wanatakiwa kujibu hizi tuhuma na kuhakikisha wanaondokana na hii kashfa kabla biashara yao haijaingia doa
Kheeeeeee ........... yethuuuuuuuu twafwaaaaaa. sikuwa nalifehemu hili........ HAYO MENGINE HAYACHOMWI SINDANO.......???
 
tbs na tdfa mmeipata hiyoo???? Au mnangoja mpaka watu waathirike ndiyo muuze sura kwenye tv????????
kuna siku nguvu ya walaji itawashitaki kwa kutowajibika na hizo ofisi ambazo mnazifanya himaya tutawanyang'anya
 
yani mkuu umelenga kunako hili tatizo lipo sana na sio uhai tu niona mpaka kilimanjaro unakuta kovu chini kabisa la super gluu ebu tujiulize hizi chupa zenye sili kamili kabisa wanapata wapi kwani inaonyesha wanapata hizi chupa tupu kisha wanajaza maji kupitia sindano kweli akuna uffisadi kwenye makampuni husika na hawa wezi na mengi yanapatikana kwa hawa wanaotembeza kwenye magari na kwa miguu
 
Sasa mbona wengi mnaandika kishabiki? Hii inanikumusha story ya mama mmoja mbaye mtoto wake wa kiume kabakwa huko Tanga. Mbakaji mwenyewe fundi Cherehani. Mama na shoga yake wameenda kwa fundi kulalamika. Badala ya kufika pale na kuanza kulia na fundi, wao wakaanza mazungumzo kati yake na wao. Mara wamsifie jamaa alivyo mkubwa, mara ohh heri hata angeliwaomba wao au dada zake wamlipie kijana deni kwa kumgawia jamaa uroda. Na mwisho ndiyo wanatoa shutuma "ona sasa umeniharibia mwanangu, hawezi hata kukaa". Wakaongea wee na mwisho hao wakajiondokea.

Kama hili ni kweli nafikiri kungelikuwa na UTARATIBU wa forrum hii kushughulikia mambo mengine yaliyo ndani ya uwezo wetu. Kama ni kweli kwa nini JF isiwe na utaratibu wa kuandika sehemu barua moja kwa moja? Ni kuwalima barua au hata kuwapigia simu hao TBS na sijui TFDA ili wafanye uchunguzi. Pia baadhi ya sample ya maji inaweza kupelekwa kwenye maabara za Vyuo kama Muhimbili, UDSM na chuo cha maji ambacho kipo Dar na wao nina uhakika wangeliweza kusolve hii kesi haraka sana.

Nina uhakika humu ndani kutakuwa na watu wenye vyombo vya kupimia water quality. Pia si ajabu hata wafanyakazi wa hizo sehemu au ndugu zao. Walishighulikie hili ili kuokoa maisha yao au ya ndugu zao. Na hata kama itaonekana kuna USHENZI wanafanyiwa hawa jamaa, basi wao wafanye uchunguzi ni nani anatoboa maji yao na kuchanganya na maji ya kawaida yenye hatari.

Mwisho kama ni kesi ya VIDUDU, basi wenye nyumba zao, mnaweza kuwa mnaweka maji kwenye paa la nyumba siku nzima juani. Ila inabidi iwe chupa inayopitisha mwanga wa jua. Mwanga ule ukichoma siku nzima, basi yale maji yanakuwa SALAMA ingawa yanaweza kuwa si SAFI. Labda jamaa wawe wanaweka sumu ndani.
 
Nilipokua nasoma thread yako pemben nlikua na chupa za maj ya uhai kama mbili. Zote nimechek ni kama ulvonena.

Mbona 2takufa mwaka huu.
Tatizo ukicheki seal ni very genuine. Na ndio mi huchek hiyo 2 nnaponunua. Kumbe wapumbavu hilo wanalitambua!
Nimechoka!
Logic ya zile seal ipo kama hivi,zile seal zinakuja na vizibo,yaani ukifunga haina tatizo,ukifungua ndio seal hukatika,so usiziamini sana hizo seal,pia mnajua kuwa asilimia 65 ya watumiaji wa JIK wanatumia zinazotengenezwa uswahilini?kifo hakikwepeki!!
 
Back
Top Bottom