Maji ni muhimu kwa mwili wa Binadamu. Kunyweni sana Maji...

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,268
33,040
Faida za kunywa maji ya kutosha

Kunywa maji safi na salama kwa kiasi kinachostahili kiafya kunaweza kuyaboresha maisha yako na kukufanya ujihisi mwenye afya na furaha zaidi . Kunywa maji ya kutosha kuna faida nyingi. Tukichukulia kunywa maji ya kutosha ni mithili biashara kati ya wewe na afya yako, biashara hii inalipa.

Zifuatazo ni baadhi ya faida za kunywa maji ya kutosha .


  • kusaidia mmeng'enyo wa chakula.
Vimengenya na Kemikali mbalimbali zinazohusika na mmen'genyo au usagaji wa chakula mwilini ziko katika hali ya mchanganyiko na maji. Ili hivi viweze kufanya kazi vizuri inatakiwa kuwe na uwiano sahihi kati yake na maji.Pia maji yanahusika katika kulainisha baadhi ya vyakula .
Pia kunywa maji ya kutosha kunaongeza ufanisi wa mwili katika kusharabu chakula.


  • Dawa ya maumivu ya kichwa.
Mara nyingine maumivu ya kichwa yanasababishwa na upungufu wa maji mwilini. Hii inamaanisha, kama una maumivu ya kichwa yanayosababishwa na upungufu wa maji mwilini unaweza kughairi kumeza vidonge vya kutuliza maumivu na kunywa maji. Hii inawezekana kwenye baadhi ya maumivu ya mgongo pia.

  • kuboresha afya ya ngozi.
Pendezesha ngozi yako kwa kunywa maji ya kutosha.
Unaweza kuboresha sura na mguso wa ngozi yako kwa kunywa maji ya kutosha kwani maji yanasaidia kuboresha tishu za ngozi na kuongeza unyevu kwenye ngozi .


  • kusaidia akili yako.
Maji yanauweka ubongo katika hali nzuri zaidi na ya ufanisi zaidi. Kunywa maji ya kutosha kunamwezesha mtu kufikiria kwa ufanisi zaidi.

  • kutatua tatizo la kukaukiwa haja kubwa (constipation)
Sehemu kikubwa ya haja kubwa ni maji. Kunywa maji ya kutosha kunaweza kukusaidia kupata haja kubwa kiulaini na mara kwa nyingi zaidi.

  • kuboresha hali ya viungo na misuli
Maji ya kutosha yanasaidia kupunguza tatizo la kubanwa misuli na pia hupunguza msuguano katika viungo vyako.

  • kuondoa uchovu
Maji yanachochea shughuli za kimetaboliki mwilini na kuongeza ufanisi wa ubongo kwa hiyo yanapunguza uchovu.

  • kupunguza uwezekano wa kupata baadhi ya magonjwa.
Uwezekano wa kupata mafua,mawe ya figo,matatizo ya ini,baadhi ya saratani n.k unaweza kupunguzwa kwa kunywa maji ya kutosha .

  • Maji yanaweza kusaidia katika kupunguza uzito.
Kama uko katika mkakati wa kupunguza uzito maji yanaweza kukusaidia kwa kiasi kikubwa. Maji huongeza kasi ya shughuli za kimetaboliki mwilini. Ongezeko hilo la kimetaboliki husababisha mwili kutumia nishati nyingi zaidi na hivyo huweza kupunguza kiasi cha nishati ambacho kitahifadhiwa mwilini katika hali ya mafuta au kupunguza kiasi cha nishati kilichohifadhiwa mwilini.

Pia ongezeko la ufanisi wa figo na ini kutokana na kunywa maji ya kutosha husaidia kutoa mazao ya mafuta ya ziada mwilini. Maji hayaongezi nishati mwilini, kwa hiyo unywapo maji badala ya juisi,soda au vyakula au vinywaji vingine ambavyo huongeza nishati au mafuta mwilini unaongeza uwezekano wa kupungua uzito.


"Usinisingizie Mimi Mzizimkavu Sijasema ushindie maji asubuhi mpaka jioni."

  • maji ni kiburudisho
kunywa maji ya kutosha kutakufanya ujisikie vizuri na pia kunaweza kupunguza safari za hospitali. Kunywa maji ya kutosha, fanya siku yako iwe poa zaidi
 
Thanks MziziMkavu
Najitahidi sana kunywa maji lita 3-4 kwa siku na ni kweli imenisaidia
Zamani nilikuwa na tatizo la kuumwa sana kichwa lakini tangu DR aliponishauri tiba ya maji
Sasa kichwa naweza kuumwa Mala moja kwa miezi sita tena nikiwa na Fatique or msongo wa mawazo
Ingawa zamani ugonjwa wangu ulikuwa kichwa
Be blessed .
 
Last edited by a moderator:
Asante sana kaka,
Nashukuru mie ni mnywaji mzuri wa maji lita 3 kwa siku,
Na tangu nilipoanza utaratibu huu nimeuzoea na vihoma vya ajabu ajabu sivipati tena!
 
Thanks MziziMkavu
Najitahidi sana kunywa maji lita 3-4 kwa siku na ni kweli imenisaidia
Zamani nilikuwa na tatizo la kuumwa sana kichwa lakini tangu DR aliponishauri tiba ya maji
Sasa kichwa naweza kuumwa Mala moja kwa miezi sita tena nikiwa na Fatique or msongo wa mawazo
Ingawa zamani ugonjwa wangu ulikuwa kichwa
Be blessed .
@FirstLady1 Ninakutakia afyaa njema

Asante sana kaka,
Nashukuru mie ni mnywaji mzuri wa maji lita 3 kwa siku,
Na tangu nilipoanza utaratibu huu nimeuzoea na vihoma vya ajabu ajabu sivipati tena!
@Cantalisia ninakutakia afya njema endelea kunywa maji usiache hata kidogo.
 
MziziMkavu.Kama tunavyo ambiwa 70% ya uzito wa mtu ni maji.
Hapo ina changanya,mi nilifikiri tungeongeza uzito kwa kunywa mengi badala ya kupunguza.
 
Last edited by a moderator:
ANGALIZO:
1.usipendelee kunywa maji baridi,wakati wote kunywa maji ambayo yako kwenye room temperature
2.epuka kunywa maji mara baada ya kula chakula,subiri muda upite.
3. do not overdo,usinywe maji kupitiliza maana matokeo yake utapoteza essential minerals through excessive mkojo(glass nne za maji asubuhi zinatosha)
 
MziziMkavu.Kama tunavyo ambiwa 70% ya uzito wa mtu ni maji.
Hapo ina changanya,mi nilifikiri tungeongeza uzito kwa kunywa mengi badala ya kupunguza.
@tz1 Ndio Watu wanywe sana Maji kwa afya zao.

dah bonge la shule sasa mimi ninaekunywa Robo glass baada ya siku tatu itakuwaje?
@Kifulambute Mkuu utakuwa huna afya nzuri na ukiumwa itakuwa ni hatari jaribu kunywa sana maji itakufanya uwe na afya nzuri mkuu jitahidi kunywa sana maji kwa afya yako.
 
Mi mwenzenu nahisi nina tatizo!!, kila ninapojitahidi kunywa maji mengi ndio ninapokwenda kutoa haja ndogo (kukojoa) kila mara. hivi ni kitu gani kinasababisha hali hii? au ndio inavyokua kwa watu wengine?
 
Mi mwenzenu nahisi nina tatizo!!, kila ninapojitahidi kunywa maji mengi ndio ninapokwenda kutoa haja ndogo (kukojoa) kila mara. hivi ni kitu gani kinasababisha hali hii? au ndio inavyokua kwa watu wengine?
@paja nono Ndio vizuri inasaidia kusafisha kwenye Figo inaonekana Figo lako mkuu linafanya kazi vizuri endelea kunywa maji kwa wingi na wala usiogope.
 

JITIBU KWA KUTUMIA MAJI


MAMBO YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZA TIBA KWA KUTUMIA MAJI:



Kanuni ya kimakisio kwa mahitaji ya maji ni; kunywa nusu ya uzito wako katika aunsi (ounces) ugawe mara mfululizo utakaoufuata kwa siku nzima. Kiasi kidogo chini au juu ya hiki, kinakubalika. Aunsi 1 = miligramu 31.25


Kanuni ya kimakisio kwa mahitaji ya chumvi ni, Robo tatu gramu za chumvi kwa kila nusu lita ya maji, nusu kijiko cha chakula kwa kila nusu galoni ya maji au kijiko kimoja cha chakula kwa kila galoni moja la maji.


Pengine umeshageuza kichwa na kunisema, "Wewe ni kichaa.....hicho ni kiasi kingi sana cha maji". Ukweli ni kuwa, ni rahisi kunywa hivyo hasa tukitumia sentensi, ''Glasi 1 ya maji mara 8 kwa siku''.


Mfano, kwa mtu mwenye uzito wa kilogramu 75:



  • Badili kilogramu kwenda aunsi kwa kuzidisha mara 2.2. Hivyo, 75x2.2 = aunsi 165.
  • Tafuta nusu ya aunsi kwa kugawa aunsi na 2. Hivyo, aunsi 165/2 = aunsi 82.5.
  • Gawanya mara mfululizo utakaoamua kuufuata kwa siku nzima, mfano mara 8 kwa siku. Kwa hiyo aunsi 82.5/8 = aunsi 10.3.
  • Badili aunsi kuwa miligramu za maji. Aunsi 1 = miligramu 31.25. Kwa hiyo aunsi 10.3x31.25 = miligramu 322.

Kwa hiyo itampasa mtu huyo mwenye uzito kilo 75, kunywa ml 322 za maji mara nane kwa siku.


Namna anavyopaswa kufuata hiyo ratiba mara 8 kwa siku:


1) Akiamka tu (mfano saa 12 kamili asubuhi), cha kwanza atakunywa maji ml 322. ataendelea na shughuli zake za asubuhi


2) Nusu saa kabla ya chakula cha asubuhi (yaani saa 12:30 asubuhi), atakunywa maji ml 322. atasubiri nusu saa ipite ndipo atapata chakula chake cha asubuhi (itakuwa saa 1 kamili asubuhi).


3) Kisha kula chakula cha asubuhi, atahesabu masaa 2 na nusu ndipo atakunywa tena maji ml 322 (itakuwa saa 3 na nusu asubuhi).


4) Atahesabu masaa 2 tena ndipo atakunywa tena ml 322 nusu saa kabla ya chakula cha mchana (itakuwa saa 6 mchana) kwa hiyo nusu saa baadaye atakula chakula cha mchana (yaani saa 6 na nusu mchana).


5) Atahesabu yapite masaa 2 na nusu baada ya chakula cha mchana ndipo atakunywa tena maji ml 322 (itakuwa saa 9 kamili alasiri).


6) Atahesabu masaa 2 na nusu yapite ndipo atakunywa maji ml 322 nusu saa kabla ya chakula cha jioni (itakuwa saa 11 na nusu jioni). Nusu saa baadaye atakula chakula cha jioni (itakuwa saa 12 kamili jioni).


7) Kisha kula chakula cha jioni, atahesabu masaa 2 na nusu tena ndipo atakunywa tena maji ml 322 (itakuwa saa 2 na nusu usiku).


Muda wowote atakapokwenda kulala kuanzia saa 4 usiku atakunywa tena maji ml 322 kumalizia mara 8 zake kwa siku.


Huyo alikuwa na kilo 75, sasa na wewe andika uzito wako na utumie fomula hiyo hapo juu ujuwe ni kiasi gani cha maji unahitaji kwa siku na kisha ufuate mara hizo 8 kama zilivyopendekezwa hapo juu. Kwa staili hii ndipo maji huwa ni zaidi ya dawa.


Kumbuka, Kunywa maji nusu ya uzito wako katika aunsi ni kiasi cha chini kabisa, lakini mahala pazuri pa kuanzia, ikiwa ni mtu unayejishughurisha zaidi na mazoezi au unaishi katika mazingira ya joto zaidi, utahitaji zaidi ya hapo.


Sasa, hutakubali kuwa kunywa maji kwa protokali hii ni kazi rahisi?.


Ikiwa haunywi kiasi hiki cha maji kwa sasa, unapaswa kuanza kuongeza kiasi cha ziada kwa taratibu sana. Hii itaupa nafasi mwili kujirekebisha kuendana na kiasi ulichoanza kukiongeza, na ikiwa hautaupa mwili muda wa kujirekebisha, basi maji yatakuwa kama dawa ya kukojosha (diuretic), yakisukuma madini na vitamini za mhimu nje ya mwili, pengine na kukusababishia madhara zaidi kuliko faida.


Watu wazee sana na watoto wadogo wanatakiwa kuanza kuongeza maji kufikia mahitaji yao kwa taratibu zaidi.


Kwa kutumia mfano wa uzito hapo juu, itakupasa kuanza na glasi 3 siku ya kwanza huku ukiongeza glasi moja zaidi kila siku inayofuata mpaka ufikie glasi zote 8.


Kumbuka kuwa, kunywa maji nusu ya uzito wako katika aunsi na kula chumvi robo tatu gramu kwa kila nusu lita ya maji, ni kanuni ya kimakisio tu. Baadhi ya wengine watahitaji maji zaidi wakati wengine watahitaji chumvi zaidi. Baada ya muda, mahitaji ya mwili kwa maji na chumvi yanaweza kuongezeka kidogo zaidi sababu ya mazingira ya joto, mazingira ya baridi au mazoezi ya viungo.


Kila mmoja lazima apate kujua kiasi cha mahitaji ya mwili wake kwa maji kuanzia sasa.


Kamwe usinywe zaidi ya aunsi 33.8 (lita moja) za maji kwa wakati mmoja ukiwa umekaa au umesimama.


Watoto wadogo kuanzia miaka 2 mpaka 12, hasa wale wepesi kujishughulisha na mazoezi wanahitaji asilimia 75 mpaka 100 za aunsi za maji katika uzito wao kwa sababu miili yao inakua muda wote na kila seli katika miili yao inayokua inayahitaji maji haya ya ziada (mytosis).


Tiba hii ya maji haitumiki kwa watoto chini ya miaka 2.


Chumvi ya kawaida ya mezani iliyoongezwa madini ya iodini, itakusaidia kidogo, chumvi ya mawe ya baharini ambayo haijasafishwa (unrefined sea salt) ndiyo nzuri zaidi sababu ya madini mengine mengi ya ziada zaidi ya 80 yaliyomo ndani yake. Chumvi ya baharini pia huwa na radha nzuri, nyeupe na umajimaji kidogo.


Namna bora za kula chumvi:


Njia ya kwanza ni kuiweka chumvi katika sehemu ya mbele ya ulimi, hakikisha unaihisi radha yake, na kisha kunywa maji juu yake yakiisafisha kuelekea chini.

Unaweza pia kuongeza chumvi ya ziada kwenye chakula chako.Tatizo la njia hii ni kuwa, chakula kinahisika kuwa na chumvi zaidi ya radha zingine.

Ukiona viwiko, vidole, miguu, mikono au kope za macho zinavimba (kuvimba kusikotokana na ajali au jeraha), au unaharisha zaidi, usitumie chumvi kwa siku 2 mpaka 3, kunywa maji halisi pekee na kisha siku ya tatu, endelea kuchukuwa chumvi tena, lakini ichukuliwe taratibu. Kamwe usitumie chumvi zaidi ya robo tatu gramu kwa kila nusu lita ya maji.


Kumbuka chumvi ikizidi hupelekea kuharisha.


Dr.Batmanghelidj anasema, kunywa maji matupu kunaweza pelekea mwili kupoteza baadhi ya madini na vitamini zake mhimu nje ya mwili na hivyo kutozipa seli muda wa kutosha kuyatumia maji. Inashauriwa kutumia vidonge vyenye vitamini nyingi kwa pamoja (multivitamins) katika kila mlo wako ili kurudishia kile kitakachokuwa kimepotea (hasa ikiwa haufanyi mazoezi na kula kiasi kingi cha mboga za majani).


Uvimbe utakapokuwa umepotea au umeacha kuharisha, unaweza kuendelea na mpango wako wa kunywa maji nusu ya uzito wako katika aunsi ingawa mara hii utayachukua kwa kiasi kidogo.


Kwa siku nzima, anza kuongeza kiasi cha unywaji wako wa maji mpaka ufikie tena nusu ya uzito wako katika aunsi, anza pia kuchukua chumvi pamoja na maji. Unatakiwa kuhakikisha kuwa unapata gramu 150 za madini ya iodine kwenye "multivitamins" zako kila siku mpaka gramu 450 kwa siku.

Ili maji yaweze kukutibu na kukukinga kwa kila ugonjwa, ni lazima....


Kisha kunywa maji, maji yanapaswa kubaki ndani ya mwili masaa 2 mpaka 2 na nusu ili kuupa mwili muda wa kutosha kuyatumia maji hayo vizuri.


Ikiwa inakulazimu kukojoa (peeing) chini ya muda wa masaa 2 tangu unywe maji, utalazimika:


a) Kuacha kunywa maji matupu, jaribu kunywa juisi (uliyotengeneza mwenyewe) ya chungwa, ya limau, ya embe, ya papai, ya parachichi, ya zabibu, juisi ya matunda mchanganyiko, au juisi nyingine yeyote isipokuwa kwa watu wanaosumbuliwa na pumu (asthma) ambao hawatakiwi kunywa juisi ya chungwa. Kumbuka usizidishe kiasi chako cha ujazo unaopaswa kunywa kwa wakati mmoja kwa sababu tu ni tamu.


Wakati huo huo mhimu kukumbuka kuongeza robo tatu gramu za chumvi katika kila nusu lita ya juisi yako.


b) Ikiwa kunywa juisi hakutasaidia kupunguza kwenda bafuni kila mara, jaribu kunywa maji huku ukila mkate. Unaweza kuongeza krimu ya siagi au jamu kwenye mkate wako (the magic bagel).


Kisha kutumia mkate siku moja au mbili unaweza kupunguza sasa kiasi cha mkate mpaka nusu yake, robo yake na mwisho juisi pekee pamoja na mlo wako.


Utapaswa kurudi taratibu tena kutoka kunywa maji juisi mpaka kunywa maji matupu tena, baada ya siku kadhaa itakupasa kujaribu aunsi 2 za maji matupu nusu saa kabla ya chakula, kesho yake aunsi 4, siku inayofuata itakuwa aunsi 6 kisha 8 na kuendelea mpaka ufikie kiasi chako unachotakiwa.


c) Ikiwa kunywa maji pamoja na kula mkate au katika juisi hakukusaidii kupunguza kwenda bafuni, Glasi ya maji (ml 250) matupu ikiongezwa na kijiko (kijiko cha chakula) kimoja cha asali au sukari halisi au walau sukari nyeupe kutakutatulia tatizo hili ukiongeza na chumvi 1/8 ya kijiko cha chai , tikisa na kisha kunywa mchanganyiko huo.


d) Hakikisha unakunywa maji kwa mjibu wa kipimo chako kulingana na uzito wako. kunywa maji mengi zaidi ya kiwango chako husababisha maji kutoka nje ya mwili mapema kabla hayajatumiwa na mwili.


e) Acha kwanza kinywaji chochote cha kutengenezwa kiwandani, acha chai ya rangi na kahawa. vinywaji hivi ni mawakala vikojoshi (diuretics), huyalazimisha maji kutoka nje ya mwili mapema kabla mwili haujayatumia. utarudi kunywa chochote ikiwa utavihitaji tena vinywaji hivyo mara utakapokuwa supa tena kiafya. Acha pia uvutaji wowote wa sigara na alkoholi.


Bilashaka umewahi kusikia msemo, "Kwa sehemu kubwa tumetokana na maji", hii ndiyo sababu zaidi ya asilimia 94 ya damu yetu ni maji, zaidi ya asilimia 85 ya ubongo wetu ni maji, huku zaidi ya asilimia 75 ya sisi ni maji.





Kwanini unywe maji glasi 1, robo saa kabla ya kula, au glasi 2, nusu saa kabla ya kula?:


Wanyama wote hunywa maji halisi (plain water). Ikiwa utawachunguza paka na mbwa, mara zote hunywa maji na kusubiri wastani wa nusu saa kabla ya kula. Ratiba inabadilika wanapokuwa wanatibiwa, hapa hunywa na kisha hula papo hapo ama baadaye.


Mfululizo huu ni mhimu ili kubaki na afya bora.


Unapokunywa maji na kusubiri nusu saa kabla ya kula, maji yanaenda tumboni na kuziamsha tezi kutoa kemikali (homoni) kuzifunika kuta za tumbo ili kuzirinda dhidi ya haidrokloriki asidi ambayo huzarishwa wakati chakula kinawekwa mdomoni.


Maji na kemikali hizo kisha huenda kwenye utumbo mdogo ambako kemikali hizi hukaa kusubiri chakula kitakachokuwa kinakuja baadaye. Maji hayo huru, yanauacha utumbo mdogo na kwenda katika seli zote za mwili na kuzijaza (kuzinyweshea) maji kama vile unavyonywesha bustani. Baada ya seli kuwa zimenyeshewa, maji yanayobaki kisha yanasukumwa tena kwenda tumboni ili kunyeshea chakula kilichofika.


Nguvu zetu hazitokani na vyakula tunavyokula, bali zinatoka katika MAJI ambayo huiweka atomu ya haidrojeni katika chakula.


Tunatembea katika haidrojeni.


Vyakula tulavyo hutupatia vitamini na madini tunayoyahitaji ili kubaki katika afya.


Ikiwa haunywi maji halisi (glasi 1 au 2) kabla ya kula chakula na kusubiri (robo saa au nusu saa), basi mwili lazima ujikope maji wenyewe.


Kama mwili utakopa maji toka katika damu, basi ateri lazima zipunguze vipenyo vyake na moyo lazima utumie nguvu nyingi ili kusukuma damu ambayo ni nene (nyingi), kitendo hiki tunakiita 'shinikizo la damu' (BP).


Ikiwa mwili utajikopa maji toka katika ubongo, utapatwa na 'kichwa kizito' au kichwa kuuma ambacho kinaweza pelekea maumivu ya kichwa.


Ikiwa unakunywa alikoholi (pombe) na inavuta maji toka kwenye ubongo, utapatwa na kutokujisikia vizuri au uchovu (hangover).


Watu wanaoishi katika nchi za baridi huweka alikoholi kwenye tenki zao za gesi ili kuvuta maji ndani ya gesi na hivyo kuifanya gesi isigande.


Kokote katika ogani au tishu mwili utakakokopa maji, lazima ogani au tishu hiyo iachiwe madhara na hivyo kusababisha maumivu ama ufanyaji kazi wa ogani au tishu hiyo usio wa kawaida kama vile kufunga choo (constipation).


kufunga choo au kupata choo kigumu sana kunatokea wakati mwili umekopa maji toka katika utumbo mdogo na sehemu ya chini ya utumbo mpana kunakopelekea taka za mwili kusimama kwenye kuta za utumbo mdogo na sehemu ya chini ya utumbo mpana (colon). Wakati mambo yako yanapokuwa na umajimaji, huteleza yenyewe chini bila kutumia nguvu yoyote.


Kila tunapopumuwa hewa nje (exhale) tunapoteza maji.


Ikiwa utahema juu ya kioo, utauona ukungu (maji). Tunapoteza glasi 4 za maji kwa kupumuwa tu kila baada ya masaa 24!!.


kama mwili utakopa maji toka mapafuni, utapatwa na pumzi fupi itakayopelekea upatwe na pumu (asthima) na matatizo mengine yanayohusiana na mfumo wa upumuwaji.


Mapafu na Moyo vinauhusiano wa karibu, kwa hiyo kama mwili utakopa baadhi ya maji toka katika mishipa ya moyo, utapatwa na maumivu ya moyo ambayo yanaweza kurahisisha kutokea kwa shambulio la moyo (heart attack).


Mishipa inahitaji damu na maji wakati unafanya mazoezi, kwa hiyo kama unatakiwa kula chakula na kisha kutembea au kupandisha ngazi (za ghorofa) na una upungufu wa maji (dehydrated), unaweza ukapatwa na pumzi fupi, shambulio la pumu, utapatwa na maumivu ya moyo (angina) au kukakamaa kwa mishipa (cramps).


Ndiyo maana wanasema; kamwe usiende kuogelea mara tu baada ya kumaliza kula kwa sababu mishipa itakakamaa.


Mwili unapokuwa katika kazi yake ya umeng'enyaji chakula, huielekeza (diverts) damu toka katika mikono na miguu kwenda katika utumbo mdogo ili kusaidia umeng'enyaji wa chakula.


Baadhi ya vyakula ni rahisi kumeng'enywa na vinawezeshwa na maji pekee, kama vile matunda na mboga za majani.


Vinywaji vingine (liquid beverages) kama vile kahawa, chai, soda na juisi, siyo maji kwa mwili. Hivi ni vyakula pia kwa sababu ulimi unaipata radha ya viongezi (additives) na siyo radha ya maji halisi, na hivyo tumbo litaitowa haidrokloriki asidi. Mwili utakishughurikia kinywaji hicho kama chakula.


Utafaidika na baadhi ya maji kama vile katika matunda na mboga za majani kwa masharti ya kinywaji hicho kutokuwa na kafeina (caffeine).


Kafeina ni kikojoshi (diuretic), huyalazimisha maji kutoka nje ya mwili.


Magonjwa mengine yanayoweza kuepukika kwa kunywa maji kabla ya kula ni pamoja na vidonda vya tumbo, tumbo kunyonga, kiungulia, mafuta yaliyozidi, kansa ya utumbo mdogo, kukinaishwa na chakula, na ernia.


Kunywa maji masaa 2 au 2 na nusu baada ya chakula kunasaidia kumalizia umeng'enyaji wa chakula na kuunywesha mwili maji baada ya kukaukiwa kulikosababishwa na kazi ya umeng'enyaji wa chakula.


kunywa maji ya kawaida katika joto la kawaida.


Magonjwa mengineyanayotibika au kukingika kwa kutumia tiba ya maji ni; Kansa, kisukari, kifua kikuu (TB), shinikizo la damu(BP), mfadhaiko (stress), matatizo ya moyo na kuzimia, magonjwa ya tumbo, magonjwa ya ngozi, magonjwa ya Ini, pumu (Asthima), mzio (Allergy), chunusi, homa, kupunguwa nguvu na kinga ya mwili, matatizo ya kina mama, magonjwa mengine ni pamoja na homa ya uti wa mgongo, kansa ya kizazi, kikohozi, kuharisha, kikundu, nyongo, matatizo ya tumbo, kupungua uzito, upungufu wa damu (anaemia), vichomi, vidonda vya tumbo, utipwatipwa, kuzeeka mapema, na magonjwa mengine mengi.


Tiba hii ni nzuri kwa wote, wagonjwa watapona na wazima watabaki na afya bora na kujirinda dhidi ya maradhi kwa maisha yao yote.


''Kuna maajabu zaidi ya milioni katika glasi moja ya maji kuliko katika dawa yeyote utakayoandikiwa na muuguzi wako – dr.Batmanghelidj''.





ANGALIZO:



  • Ikiwa hauendi chooni walau mara tatu kwa siku,unapaswa kumwona daktari kabla ya kuanza tiba hii.
  • Figo zako lazima ziwe zinafanya kazi vizuri, hii inamaanisha, kiasi cha maji unachokunywa lazima kiwe karibu sawa na unachotoa.
  • Wakati huo huo, kwenda chooni mara nyingi kwa siku kunaweza kukusababishia kupoteza vitamini mhimu, madini na elektrolaiti na kukufanya vibaya zaidi ya vizuri.
  • Unatakiwa kuwa makini sana unapoanza kuongeza uchukuaji wa maji mwilini, anza pole pole kwa kuongeza glasi 1 kila siku mpaka utakapofikia nusu ya uzito wako katika aunsi. lazima uupe mwili muda wa kujirekebisha baada ya kuzoea vinywaji kama kahawa, chai na soda, kwa kuwa vinywaji hivi huufanya mwili kujiendesha kwa namna nyingine.
  • Unaweza kuumwa na kichwa au unaweza usijisikie vizuri tu siku tatu mpaka wiki moja za kuanza tiba, usiache kunywa maji kwakuwa hayo si madhara bali ni dalili kuwa taka za sumu zimeanza kuondoka mwilini, baada ya muda utarudi katika hali yako ya kawaida.
  • Tunashauri watu wenye matatizo ya figo, Ini na moyo, kutofuata tiba hii mpaka watakapopata ruhusa ya daktari na muongozo sahihi.
  • Usinywe maji zaidi ya lita 3.78 kwa siku.
  • Usinywe maji kuanzia lita moja kwa pamoja au ukiwa umekaa katika mkao mmoja iwe kusimama au kukaa.

Kumbuka pia kuwa hii ni elimu tu na siyo kumuondoa daktari wako au chaguo lako la kutumia dawa, ni programu iliyopendekezwa kwa manufaa yako.

www.maajabuyamaji.net ni tovuti/website inayozungumzia namna ya kuyatumia maji kujikinga na kujitibu na magonjwa mengi, itembeleeni kila mara mkihitaji kujua kuhusu tiba kwa kutumia maji.
 
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom