Majeshi yetu na watu wafupi

Vakwavwe

JF-Expert Member
May 16, 2009
503
100
Kwa muda mrefu nimekuwa najiuliza kwa nini majeshi yetu i.e Jwtz,polisi,magereza wanalazimisha kuajiri watu warefu peke yao?hii imekuwa kama ukiukwaji wa haki za binadamu,watu wafupi waliowengi ni wakakamavu na wanafanya mambo makubwa sana....ni Mungu aliumba wafupi na warefu wote wakiwa na ukamilifu kabisa wanaweza kufanya chochote na lolote popote kwa kutumia nyenzo au kwa asili. Ningeshauri majeshi yetu yaajiri kwa kuangalia uwezo(competence) kwa ujuzi,elimu,ukakamavu n.k. hiki kigezo cha kuzaliwa ambacho hawezi kubadilisha inapokuwa kikwazo inambania na kumkwaza mtu mfupi. nawafahamu wafupi kibao ambao wanahamu(interest) na ni wazalendo kwelikweli wameshindwa kujiunga na majeshi kwa kigezo hiki. Wote tunajua vimo wa wachina na mataifa mengi ya kiasia kama Korea lakini wana majeshi imara sana, tanzania ina watu wachache wanaozidi futi 6 na wengi ni chini ya hapo kwa nini kung'ang'ania kigezo hiki?
wanaJF naomba mawazo yenu
 
Hakuna cha ajabu maana hata kazi zingine wakitangaza wanataja sifa. Kama una unasisitiza ina maana hata walemavu waajiriwe sasa jeshini?
 
Hakuna cha ajabu maana hata kazi zingine wakitangaza wanataja sifa. Kama una unasisitiza ina maana hata walemavu waajiriwe sasa jeshini?


Nyamungo. Umeisoma hili bandiko vizuri? kwani wafupi ni walemavu . Du.

Wapewe nafasi .Urefu sio hoja siku hizi za vita vya akili na softfication za ajabu. Ukifikiri kienzi za ujima ujima utakuta vigezo vya urefu ni issue.
 
Hicho kigezo cha "Urefu" naona kimebaki tu kwenye makaratasi au kuna watu baadhi wanakitumia kwa maslahi yao. Majeshi yetu yote huwa naona kuna mchanganyiko wa watu warefu na wafupi. Sidhani kama kuna tatizo.
 
Hicho kigezo cha "Urefu" naona kimebaki tu kwenye makaratasi au kuna watu baadhi wanakitumia kwa maslahi yao. Majeshi yetu yote huwa naona kuna mchanganyiko wa watu warefu na wafupi. Sidhani kama kuna tatizo.

tatizo lipo sana ndugu, nimewahi kuwepo huko. kigezo kikubwa ni hicho hasa kwa ambao hawana elimu ya juu(non graduates)...ukiona kuna mfupi kwenye haya majeshi na sio graduate ujue aliingilia mlango wa nyuma au aliingia kwa mpango maalumu kama michezo n.k. na mipango maalumu hii huanzishwa ili kupunguza idadi ya vijana wasio na ajira kwenye makambi ya wafanyakazi wa majeshi haya wao wanawaita vijana wa LINE. hapo ndipo utaona vituko...kipande cha dada kifupii na kinene kwelikweli unaambiwa anawakilisha wanariadha(ni kweli imetokea). kitu kinachofanya wafanyakazi wengi kutojiamini kazini ni kuingizwa kwa upendeleo kwenye kazi yenyewe...lakini vigezo kandamizi kama hivi vinapaswa kuondolewa.
 
sikuwa na sababu rasmi ya kuchangia humu ila nimewajibika kufanya hivyo. urefu una hashima yake na ubora wake. mhalifu kapanda kimo na afande ni pimbi kweli hapo kuna uwiano?
 
Askari anatakiwa kuwa na control over mhalifu na opponent wake.Askari anatakiwa awe na mwili unaomtisha mhalifu na kumpunguzia options katk fikra zake juu ya kukataa kutii amri. Mfano.Mtu morofi anayetishia uwa wengine mara anaswapo na askari mwenye urefu na mwili wa kimazoezi, na alipojaribu jikwamua na kuambulia maumivu bila chochote cha kuonyesha kuwa naweza jitoa.mhalifu hukata tamaa kam anaweza jitoa au hata jaribu pigana.Hapa askari anakuwa na option ya kutumia maneno kwa ustadi sana kuweza mweka chini ya ulinzi huyu mhalifu kifikra na hivyo kupata ushirikiano.Pia ikitoke aaskari kajaribu mshika kibaka,na wakatokea wenzake,mara waonapo mwili wa askari basi huwa wengi wao watajiuliza kama wanaweza jaribu kitu.

Kw aujumla muonekano wa askari,na jinsi atakavyoji behave+ silaha yoyote aliyo inamlainisha adui/mhalifu na kumfanya adui ashindwe fanya majaribio mengi ambayo km angejiamini basia ngeweza jaribu fight na pengine kufanikiwa.na hivyo kumfanya sari useless au kumweka hatarini.
 
Back
Top Bottom