Mtu wa Pwani
JF-Expert Member
- Dec 26, 2006
- 4,184
- 671
Kubwajinga,
Nimefurahi kuwa umeingia hapa kuchangia hii thread.
Nadhani umekuwa na mawazo ambayo hayajazama sana katika kufanya uchanbuzi na kuleta hoja zako (sina maana ninadharau hoja zako, ninaziheshimu sana tu) isipokuwa unasahau kuwa kila jambo ambalo linafanyika sasa kama limo ndani ya uwezo wa Rais kikatiba ni halali kabisa kwani huo ndiyo utaratibu na gharama za demokrasia.
Pili, usisahau kuwa rais kikatiba ndiye mtu wa mwisho kimamlaka juu ya vyombo vya ulinzi na usalama, na hii ni muhimu kwa Rais kupewa uwezo huo, lakini hata hivyo tunapomtaja Rais huwa tuna maanisha Rais kama taasisi na wala hatumwangalii JK usoni. Juu ya kwamba katiba ibadilishwe ili kuepuka kufanywa maamuzi na Rais kichaa, nadhani hiyo haijakaa vizuri labda ufafanue Rais kichaa kwa maana ya ugonjwa? kama ni ugonjwa katiba iko wazi inaelekeza kuwa kama rais incapacitated ni hatua gani za kuchukuliwa.
Tatu, kuhusu teuzi za mawaziri kushika nyadhifa kwenye wizara, hapo hakuna tatizo kama unavyofikiria wewe, Uwaziri siyo kazi au fani inayosomewa. Kazi kubwa za mawaziri ni kusimamia na kumsaidia Rais katika kuendesha serikali na hii ni political position kama alivyo Rais. Kinachotakiwa ni uwezo wa Waziri anayeteuliwa kuwa na uwezo wa kuongoza na kusimamia yale serikali iliyoko madarakani inataka kuyatimiza.
Kawaida shughuli za kiutendaji zingine za wizara husimamiwa na viongozi wakuu wa wizara husika (ambao ni wasaidizi wa waziri), baada ya hapo huwa ndiyo kuna timu za wataalam kulingana na mpangilio wa wizara husika.
Nadhani nimejitahidi kukuelezea ili tufaidike wengi kutokana na hoja zako.
ndugu yangu kuna waunda hoja na waosha vinywa humu