Majeshi yetu Comoro: Who is responsible?

Status
Not open for further replies.
Kubwajinga,
Nimefurahi kuwa umeingia hapa kuchangia hii thread.

Nadhani umekuwa na mawazo ambayo hayajazama sana katika kufanya uchanbuzi na kuleta hoja zako (sina maana ninadharau hoja zako, ninaziheshimu sana tu) isipokuwa unasahau kuwa kila jambo ambalo linafanyika sasa kama limo ndani ya uwezo wa Rais kikatiba ni halali kabisa kwani huo ndiyo utaratibu na gharama za demokrasia.

Pili, usisahau kuwa rais kikatiba ndiye mtu wa mwisho kimamlaka juu ya vyombo vya ulinzi na usalama, na hii ni muhimu kwa Rais kupewa uwezo huo, lakini hata hivyo tunapomtaja Rais huwa tuna maanisha Rais kama taasisi na wala hatumwangalii JK usoni. Juu ya kwamba katiba ibadilishwe ili kuepuka kufanywa maamuzi na Rais kichaa, nadhani hiyo haijakaa vizuri labda ufafanue Rais kichaa kwa maana ya ugonjwa? kama ni ugonjwa katiba iko wazi inaelekeza kuwa kama rais incapacitated ni hatua gani za kuchukuliwa.

Tatu, kuhusu teuzi za mawaziri kushika nyadhifa kwenye wizara, hapo hakuna tatizo kama unavyofikiria wewe, Uwaziri siyo kazi au fani inayosomewa. Kazi kubwa za mawaziri ni kusimamia na kumsaidia Rais katika kuendesha serikali na hii ni political position kama alivyo Rais. Kinachotakiwa ni uwezo wa Waziri anayeteuliwa kuwa na uwezo wa kuongoza na kusimamia yale serikali iliyoko madarakani inataka kuyatimiza.

Kawaida shughuli za kiutendaji zingine za wizara husimamiwa na viongozi wakuu wa wizara husika (ambao ni wasaidizi wa waziri), baada ya hapo huwa ndiyo kuna timu za wataalam kulingana na mpangilio wa wizara husika.

Nadhani nimejitahidi kukuelezea ili tufaidike wengi kutokana na hoja zako.


ndugu yangu kuna waunda hoja na waosha vinywa humu
 
Bahati mbaya Rais hajui anwani yako ilikuwa akuite Ikulu akuombe ushauri kuhusu kupeleka majeshi ya Tanzania Comoro!!Nafikiri next akipata address yako atakuita umpe ushauri[/QUOT


AMIRI JESHI MKUU KABLA YA KIINGIZA CHI VITANI ..NI LAZIMA KWANZA APATE USHAURI WA MKUU WA MAJESHI NA MAJEMEDARI WAANDAMIZI WA JESHI....BAADA YA HAWA KUKUBALI AU KUMSHAURI RAIS TUPIGANE AKAKUBALI..NI LAZIMA ACHUKUE USHAURI WA SEKTA NYINGINE KAMA BANK KUU[NATIONAL RESERVE]..CHAKULA ..ETS ..ILI KUKAMILISHA UAMUZI WAO TU..BAADAYE LAZIMA ALIARIFU BUNGE NA BUNGE LIKUBALI KWA KURA....

KWA HII ISHU YA COMORO ..SI VITA BALI NI PEACE MISSION...PAMOJA NA KUWA KWA IDADI YA ASKARI 750 WALIOKULE NI GHARAMA MPYA KWA WALIPA KODI HATA KAMA PESA ZITAREJESHWA NA AU....RAIS HAKULAZIMIKA KUARIFU BUNGE KWA KUWA TAYARI TUNAO ASKARI 200 TANGU MWAKA JUZI ..KABLA KIKWETE HAJAINGIA..KWA HIYO INAWEZA IKATAFSIRIWA KUWA HAO ASKARI 650 WALIOPELEKWA JUZI WAMEENDA KUONGEZZA NGUVU KWENYE JESHI LETU LILOPO KULE ..KUTOKA NA NA HALI YA FIELD[MEDANI] ILIVYO KULE...KATIKA HALI YA KIJESHI KAMA UMESHAPELEKA ASKARI MSTARI WA MBELE UNAWEZA KUENDELEA KUPELEKA IDADI YOYOTE KAMA UTAONA WALIOPO HAWAKIDHI HALI NA UWEZEKANO WA USHINDI..KWA HIYO UKISHAVULIA MAJI UNAOGA..SO ASKARI WATAENDELEA KWENDA HUKO HADI HUKO ANJUAN MAMBO YAWE SAFI....TUKISHINDWA TUTAONEKANA OVYO...NDIO MAANA LAZIMA BUSARA ITUMIKE WAKATI WA KUAMUA!!!!

KWA MSIOJUA HISTORIA YA COMORO ...COMORO INATEGEMEA ULINZI KWA ASILIMIA KUYBWA TOKA TANZANIA...NA WANAJESHI WA TZ WANA INFLUENCE KULE TANGU ENZI YA MWALIMU...AMBAKO TIMU YA KINA IDD GAHHU IMEKAA KULE MIAKA MINGI TU!.....
 
AMIRI JESHI MKUU KABLA YA KIINGIZA CHI VITANI ..

KWA MSIOJUA HISTORIA YA COMORO ...COMORO INATEGEMEA ULINZI KWA ASILIMIA KUYBWA TOKA TANZANIA...NA WANAJESHI WA TZ WANA INFLUENCE KULE TANGU ENZI YA MWALIMU...AMBAKO TIMU YA KINA IDD GAHHU IMEKAA KULE MIAKA MINGI TU!.....
Vilevile wacomoro wengi wamehusu zenj..
 
Vilevile wacomoro wengi wamehusu zenj..


TRUE kibunango..wacomoro wengi wapo na nasaba za zanzibar..na pwani ya afrika mashariki..wengi tunao hapa kama kina fatma said ali et al...na hata ukiangalia tabia za kipinzani za comoro na visiwa vyake ni kama unguja na pemba..maana comoro wamefikia mahali urais unaenda kwa kuhama kila kisiwa kwa mwa mmoja mmoja...kuna makamu wa rais watatu..wanaozungukia urais kwa zamu...na bado watu kama kina mohamed bacar wa anjuan hawatosheki...ni wazi kuwa kama hapa unguja na pemba hawakuwa ndani ya huu muungano wangekuwa wanasumbuana kama wajomba zao wangazija....udumu muungano!!!
 
Kasheshe,
Nafikiri hao uliowataja hawatoshi kuiingiza nchi nzima ya watu millioni 40 vitani. Haya ni maamuzi makubwa sana kufanywa na mtu mmoja hata kama atashauriwa hao uliowataja. After all sidhani kama Membe na Mwinyi wana ujuzi wowote wa mambo ya kijeshi maana hata wao vyeo vyao ni sehemu ya shukhrani za uchaguzi kama FMES alivyotufahamisha. Mwinyi ni MD, Membe ingawa amesoma Intern. Reltn, hajawa na uzoefu wowote wa kuwa full minister let alone kutuingiza vitani.

Kubwajinga,

Umevamia jambo usilolijua!!!

1. Sijukua kwamba tuko vitani!!! na kama tuko vitani ni kati ya Tanzania na Nchi Gani?

2. Kwa taarifa yako... kuingia vitani sio jambo rahisi kama unavyofikiri... kumbukumbu zangu zinaniambia Rais lazima apate kibali cha Bunge kuipeleka nchi vitani... Rejea maneno haya... ya Mwalimu alafu jiulize aliyasemea wapi? "Nia tunao, Sababu tunazo na Uwezo tunao wa Kumpiga...Amin....na Kuikomboa Uganda"

3. Ukishafahamu aliyasemea wapi? ni Kwa sababu gani? Basi utaacha kuvamia mambo usiyoyajua!!!

4. Soma mahusiano ya TZ na Comoro, Soma historia ya Comoro then come back and tell us!!!

5. Soma strategy za Jeshi letu za sasa... Tangu Kikwete aingie alishasema jeshi letu litakuwa linakwenda kwenye UN missions... kwa ajili ya kulinda amani etc....nadhani hii ni nzuri kwani tutajifunza mengi zaidi, kuliko kukaaa hapa tukidhani tuko powerfull kumbe hapana, wenzetu wako mbali.

6. Waulize wakuu wa Majeshi na Wanajeshi wenyewe wanavyopenda kupata hizo opportunities...

7. Baada ya hayo hapo juu karibu tena kijiweni tujadiliane
 
Mmesema Tanzania haiendi vitani lakini Membe kasema lazima kumkatama alive na ashitakiwe .Yeye atasema hakamatwi alive na ama afe ama awaue wanajeshi wetu ambao naamini hawaijui vyema Comoro wanadhani ni sawa na Zanzibar.Kumkamata watatumia njia gani kama si declaration of war ? Mimi kwa sasa sitasema ila nangoja kuanza kuona maiti zinarudi kama zile za US toka Iraq then tutarudi kuijadili hii mada tena .
 
Bahati mbaya Rais hajui anwani yako ilikuwa akuite Ikulu akuombe ushauri kuhusu kupeleka majeshi ya Tanzania Comoro!!Nafikiri next akipata address yako atakuita umpe ushauri[/QUOT


AMIRI JESHI MKUU KABLA YA KIINGIZA CHI VITANI ..NI LAZIMA KWANZA APATE USHAURI WA MKUU WA MAJESHI NA MAJEMEDARI WAANDAMIZI WA JESHI....BAADA YA HAWA KUKUBALI AU KUMSHAURI RAIS TUPIGANE AKAKUBALI..NI LAZIMA ACHUKUE USHAURI WA SEKTA NYINGINE KAMA BANK KUU[NATIONAL RESERVE]..CHAKULA ..ETS ..ILI KUKAMILISHA UAMUZI WAO TU..BAADAYE LAZIMA ALIARIFU BUNGE NA BUNGE LIKUBALI KWA KURA....

KWA HII ISHU YA COMORO ..SI VITA BALI NI PEACE MISSION...PAMOJA NA KUWA KWA IDADI YA ASKARI 750 WALIOKULE NI GHARAMA MPYA KWA WALIPA KODI HATA KAMA PESA ZITAREJESHWA NA AU....RAIS HAKULAZIMIKA KUARIFU BUNGE KWA KUWA TAYARI TUNAO ASKARI 200 TANGU MWAKA JUZI ..KABLA KIKWETE HAJAINGIA..KWA HIYO INAWEZA IKATAFSIRIWA KUWA HAO ASKARI 650 WALIOPELEKWA JUZI WAMEENDA KUONGEZZA NGUVU KWENYE JESHI LETU LILOPO KULE ..KUTOKA NA NA HALI YA FIELD[MEDANI] ILIVYO KULE...KATIKA HALI YA KIJESHI KAMA UMESHAPELEKA ASKARI MSTARI WA MBELE UNAWEZA KUENDELEA KUPELEKA IDADI YOYOTE KAMA UTAONA WALIOPO HAWAKIDHI HALI NA UWEZEKANO WA USHINDI..KWA HIYO UKISHAVULIA MAJI UNAOGA..SO ASKARI WATAENDELEA KWENDA HUKO HADI HUKO ANJUAN MAMBO YAWE SAFI....TUKISHINDWA TUTAONEKANA OVYO...NDIO MAANA LAZIMA BUSARA ITUMIKE WAKATI WA KUAMUA!!!!

KWA MSIOJUA HISTORIA YA COMORO ...COMORO INATEGEMEA ULINZI KWA ASILIMIA KUYBWA TOKA TANZANIA...NA WANAJESHI WA TZ WANA INFLUENCE KULE TANGU ENZI YA MWALIMU...AMBAKO TIMU YA KINA IDD GAHHU IMEKAA KULE MIAKA MINGI TU!.....

hata kama wanatoa ushauri, kwa kuwa rais ndiye aliyewapa nafasi hizo, kuna uwezekano mkubwa wa hawa jamaa kuwa yes men.

pia ushauri wao unapersuade wala haumbind rais.
 
Kubwajinga,

Umevamia jambo usilolijua!!!

1. Sijukua kwamba tuko vitani!!! na kama tuko vitani ni kati ya Tanzania na Nchi Gani?

2. Kwa taarifa yako... kuingia vitani sio jambo rahisi kama unavyofikiri... kumbukumbu zangu zinaniambia Rais lazima apate kibali cha Bunge kuipeleka nchi vitani... Rejea maneno haya... ya Mwalimu alafu jiulize aliyasemea wapi? "Nia tunao, Sababu tunazo na Uwezo tunao wa Kumpiga...Amin....na Kuikomboa Uganda"

3. Ukishafahamu aliyasemea wapi? ni Kwa sababu gani? Basi utaacha kuvamia mambo usiyoyajua!!!

4. Soma mahusiano ya TZ na Comoro, Soma historia ya Comoro then come back and tell us!!!

5. Soma strategy za Jeshi letu za sasa... Tangu Kikwete aingie alishasema jeshi letu litakuwa linakwenda kwenye UN missions... kwa ajili ya kulinda amani etc....nadhani hii ni nzuri kwani tutajifunza mengi zaidi, kuliko kukaaa hapa tukidhani tuko powerfull kumbe hapana, wenzetu wako mbali.

6. Waulize wakuu wa Majeshi na Wanajeshi wenyewe wanavyopenda kupata hizo opportunities...

7. Baada ya hayo hapo juu karibu tena kijiweni tujadiliane


Kasheshe,
Mkuu hapa naona umeleta kajisheshe kadogo. Ni vema ukaelewa kuwa hivi sasa tupo vitani, sawa tu na US ilivyokuwa kule Yugoslavia (Bosnia n.k)

Nataka tu ufahamu kuwa kuna engagement mbili za kijeshi, peace mission na offensive mission. Yakwetu hivi sasa ni offensive na kwa hiyo waComoro wana haki ya ku-retaliate kama wakiwa na uwezo. Ndio maana South Africa wao wameipinga hii hatua. TZ kwa sababu zetu binafsi tukajikurupusha haraka haraka kwa vile tu JK ndiye AU. Bahati nzuri ni kuwa Comoro tunapafahamu, maana tulishakuwa huko kwenye peace efforts na enzi za JKN.

Hata hivyo ninachopinga mimi sio sisi kushiriki, bali ni kwa ushiriki wetu uliohusisha maamuzi ya mtu mmoja tu na wakaribu yake ambao wengi ni 'yes men'. Maamuzi ya aina hii ni hatari kwa taifa kwani mengi yanafanywa sio kwa faida ya taifa bali kwa manufaiko ya kisiasa ya mtoa amri. Whether tuna mahusiano na Comoro au la, au kama wanajeshi wetu wanapenda kwenda kula shaba au la, hilo ni jambo lingine ambalo ambalo lingetakiwa kujadiliwa broadly, lakini maamuzi kama yalivyotolewa ni hatari sana and I hope kutakuwa na mbunge atakayesoma maoni yetu na kutoa hoja ya mabadiliko bungeni.

Ni jambo la hatari kwa JK kutupeleka vitani bila kushirikisha maoni ya vyombo vingine vya kiutawala, kama Bunge & baraza la mawaziri.
 
Mkuu Kubwajinga,

Hivi unayo kumbu kumbu yoyote ya jinsi tulivyokwenda vitani Uganda, mpaka kumuondoa Amin, eti bunge letu liliidhinisha vile vita au ni Mwalimu kama rais na Commander in chief aliamua kwa niaba yetu?

Maana kama sikosei kwenda Comoro, ni moja ya mikataba mbali mbali ya kimataifa ambayo sisi as a nation inatubana kwa kuwa member, sasa kama taifa letu lilikubali uanachama ina maana automatically inampa rais wetu kuamua kwa niaba ya taifa kulingan na hiyo mikataba ambayo tuliisaini, na kwenye hili inaonekana tunabanwa na uanachama wetu AU, au?

Kwa taarifa yako serikali ya US haikuamua kupeleka majeshi Panama, kumuondoa Gen. Noriega, ni rais Bush senior aliyeamua, halafu Congress ilifahamishwa baadaye, hata kwenda Afaghanstan, aliamua rais peke yake bila ushauri wa Congress mkuu, ni vita vya Iraq tu Congress ilipitisha kura. Commander in chief wa majeshi ya taifa, haweezi kusubiri kura ya bunge, wakati tatizo limtokea sasa, kuna ishu mbali mbali zinazo tofautiana,

Kuhusu Comoro, mkuu PM ni kweli bongo tunaingiliana na sana na huko, maana according to the dataz hata waziri wetu mdogo wa nje wa zamani, alikuwa ni m-Comoro, lakini akasaidiwa na Diria na kuingizwa kinyemela kwenye mlo.
 
Mkuu Kubwajinga,

Hivi unayo kumbu kumbu yoyote ya jinsi tulivyokwenda vitani Uganda, mpaka kumuondoa Amin, eti bunge letu liliidhinisha vile vita au ni Mwalimu kama rais na Commander in chief aliamua kwa niaba yetu?

FMES,
Kwanza ni lazima ukumbuke kuwa;
  1. Mwalimu alikuwa anajibu mashambulizi baada ya nchi kuvamiwa. Kwa hiyo tayari hii ni tofauti na kujiingiza katika vita ya kujitakia sifa.
  2. Pili, mwalimu alifanya majadiliano makubwa na baraza lake la mawaziri na hata kufikia kutuma ujumbe OAU kuwa inabidi sasa aikomboe nchi yake, ingawa OAU walipinga kitendo cha vita.
  3. Tatu, enzi za mwalimu zilikuwa ni za udikiteta, hata yeye alijua hili pale aliposema kuwa raisi ana madaraka makubwa kiasi kuwa kama angeyatumia vibaya angekuwa dikiteta, bila ya kujua kuwa alishawahi kuwa ka-dikiteta ingawa ilikuwa sio type ya akina Amini na Bokasa.
  4. JK ni mzembe na atakuwa ni mjinga kama atafikiria kuwa utawala wake una mazingira sawa na ya JKN.

Maana kama sikosei kwenda Comoro, ni moja ya mikataba mbali mbali ya kimataifa ambayo sisi as a nation inatubana kwa kuwa member, sasa kama taifa letu lilikubali uanachama ina maana automatically inampa rais wetu kuamua kwa niaba ya taifa kulingan na hiyo mikataba ambayo tuliisaini, na kwenye hili inaonekana tunabanwa na uanachama wetu AU, au?

Huu ni uongo, hatuna mkataba wowote unaotulazimisha kwenda vitani, na ndio maana hatukwenda Iraq.

Kwa taarifa yako serikali ya US haikuamua kupeleka majeshi Panama, kumuondoa Gen. Noriega, ni rais Bush senior aliyeamua, halafu Congress ilifahamishwa baadaye, hata kwenda Afaghanstan, aliamua rais peke yake bila ushauri wa Congress mkuu, ni vita vya Iraq tu Congress ilipitisha kura. Commander in chief wa majeshi ya taifa, haweezi kusubiri kura ya bunge, wakati tatizo limtokea sasa, kuna ishu mbali mbali zinazo tofautiana,

Nakushari ukasome upya katiba ya US, declaration of war ni kazi ya congress tu.

Kuhusu Comoro, mkuu PM ni kweli bongo tunaingiliana na sana na huko, maana according to the dataz hata waziri wetu mdogo wa nje wa zamani, alikuwa ni m-Comoro, lakini akasaidiwa na Diria na kuingizwa kinyemela kwenye mlo.

Hii ni sababu ya kitoto kama ndio unayotaka kutufanya tuwajibike na Komoro.
 
Kasheshe,
Mkuu hapa naona umeleta kajisheshe kadogo. Ni vema ukaelewa kuwa hivi sasa tupo vitani, sawa tu na US ilivyokuwa kule Yugoslavia (Bosnia n.k)

Nataka tu ufahamu kuwa kuna engagement mbili za kijeshi, peace mission na offensive mission. Yakwetu hivi sasa ni offensive na kwa hiyo waComoro wana haki ya ku-retaliate kama wakiwa na uwezo. Ndio maana South Africa wao wameipinga hii hatua. TZ kwa sababu zetu binafsi tukajikurupusha haraka haraka kwa vile tu JK ndiye AU. Bahati nzuri ni kuwa Comoro tunapafahamu, maana tulishakuwa huko kwenye peace efforts na enzi za JKN.

Hata hivyo ninachopinga mimi sio sisi kushiriki, bali ni kwa ushiriki wetu uliohusisha maamuzi ya mtu mmoja tu na wakaribu yake ambao wengi ni 'yes men'. Maamuzi ya aina hii ni hatari kwa taifa kwani mengi yanafanywa sio kwa faida ya taifa bali kwa manufaiko ya kisiasa ya mtoa amri. Whether tuna mahusiano na Comoro au la, au kama wanajeshi wetu wanapenda kwenda kula shaba au la, hilo ni jambo lingine ambalo ambalo lingetakiwa kujadiliwa broadly, lakini maamuzi kama yalivyotolewa ni hatari sana and I hope kutakuwa na mbunge atakayesoma maoni yetu na kutoa hoja ya mabadiliko bungeni.

Ni jambo la hatari kwa JK kutupeleka vitani bila kushirikisha maoni ya vyombo vingine vya kiutawala, kama Bunge & baraza la mawaziri.

Asante sana ndugu kwa maelezo yako mazuri
Napenda kuongezea hapo, Tanzania sasa tuaanza kutoka kwenye mbiu yetu ya Amani na Upendo, JK anapata wapi nguvu na uwezo wa kwenda kufanya offensive mission kwenye nchi za watu???
Na ni kwa sababu zipi haswa ambazo zinatufanya sisi tuingie vitani, na tunafaidika vipi?? Kama mtagundua hii ndo njia moja wapo ya kuanza kujijengea maadui na nchi nyingine, msije shangaa hao wacomorrow wa hicho kisiwa wanavaa mabomu wanakuja kujilipulia Dar

Lakini sio mimi kwanini tuende kupiga watu na kuwaua eti kwa sababu mtu fulani kachukua madaraka kwa nguvu, Watanzania Millioni 40 wanafaidika nini na hili swala
Naomba majibu kama yapo jamani
 
1. Mkuu KJ, rais Kikwete sio mjinga wala mzembe, labda wewe ndiye mzembe na mjinga, huwezi kumtukana rais wetu mkuu kwa sababu tu humtaki na hukumchagua, no kuna tuliomchagua na tunajua kuwa Tanzania tunayo matatizo aliyoyarithi toka awamu zote zilizopita, na sasa wanatokea wazembe kama wewe na kudai arekebishe yote ya miaka 45 in two years, that is nonesense, na ndio uzembe wenyewe na ujinga.

2. Vita vya Uganda bunge letu halikuamua kama unavyodai sasa liamue kuhusu Comoro, ni another nonesense rais anafuata historia ya sheria zetu, sasa kama amekuta kuwa hakuna historia ya bunge kupitisha vita vyetu, na haioni sheria ni kwa nini afuate hiyo sheria yako? Vita vya Mozambique, South Africa, Zimbabwe, hilo bunge lako liliidhinisha? Je tunayo hiyo sheria inayosema bunge tu ndio litaidhinisha vita? Hizi unazoleta ni hoja za kitoto sana, ni kweli sheria ipo US lakini ukweli ni kwamba rais wa nchi hiyo alipeleka majeshi Afaghanstan, n Panama, bila okay ya Congress, Bill Clinton alipiga Serbia bila okay ya Congress, halafu akarusha missles Sudan na Pakistan, bila okay ya Congress, sasa kama unachobisha kama sio utoto ni nini? Sheria hata ikiwepo haimzuii rais wa nchi ku-act kwa the interst of the nation bila ya ku-consult anybody ndio maana wananchi tunahitaji kutumia busara kumchagua rais knowing kuwa urais sio lelemama mkuu!

3. Mwalimu alikuwa na muda wa kutosha kulitaka bunge likutane kuidhinisha vita na Uganda, au angalau kwenda mpaka Kampala kumuondoa Amini, lakini hakufanya, sasa kama wewe ni msomi as you want us here tuamini then unapaswa kuweka ishu kwenye pande mbili na sio upande unaoutaka wewe tu bila kutupa the alternatives kwa sababu siasa kama sheria 90%, huamuliwa ka kutumia historia,

Kwa hiyo mkuu kwenye hili la rais kupeleka majeshi kokote nje ya nchi yetu, huna hoja ya msingi kwa sababu huna history wala sheria on your side, halafu next time acha matusi na lugha za choooni, sio lazima uazitumie ili hoja yako ieleweke,

Rais wa Jamhuri aliyechaguliwa na wananchi wa Tanzania, huwezi kumuita mjinga na mzembe, maana hapo peke yake unaonyesha uzembe na ujinga wako, na kwamba huna heshima wala adabu kwanza kwa rais wako, pili kwa sisi wananchi tuliomchagua, kwa hiyo hata mawazo yako sio worthy kabisa mkuu kuyasikiliza, wala kuyatilia maanani.
 
1. Mkuu KJ, rais Kikwete sio mjinga wala mzembe, labda wewe ndiye mzembe na mjinga, huwezi kumtukana rais wetu mkuu kwa sababu tu humtaki na hukumchagua, no kuna tuliomchagua na tunajua kuwa Tanzania tunayo matatizo aliyoyarithi toka awamu zote zilizopita, na sasa wanatokea wazembe kama wewe na kudai arekebishe yote ya miaka 45 in two years, that is nonesense, na ndio uzembe wenyewe na ujinga.

2. Vita vya Uganda bunge letu halikuamua kama unavyodai sasa liamue kuhusu Comoro, ni another nonesense rais anafuata historia ya sheria zetu, sasa kama amekuta kuwa hakuna historia ya bunge kupitisha vita vyetu, na haioni sheria ni kwa nini afuate hiyo sheria yako? Vita vya Mozambique, South Africa, Zimbabwe, hilo bunge lako liliidhinisha? Je tunayo hiyo sheria inayosema bunge tu ndio litaidhinisha vita? Hizi unazoleta ni hoja za kitoto sana, ni kweli sheria ipo US lakini ukweli ni kwamba rais wa nchi hiyo alipeleka majeshi Afaghanstan, n Panama, bila okay ya Congress, Bill Clinton alipiga Serbia bila okay ya Congress, halafu akarusha missles Sudan na Pakistan, bila okay ya Congress, sasa kama unachobisha kama sio utoto ni nini? Sheria hata ikiwepo haimzuii rais wa nchi ku-act kwa the interst of the nation bila ya ku-consult anybody ndio maana wananchi tunahitaji kutumia busara kumchagua rais knowing kuwa urais sio lelemama mkuu!

3. Mwalimu alikuwa na muda wa kutosha kulitaka bunge likutane kuidhinisha vita na Uganda, au angalau kwenda mpaka Kampala kumuondoa Amini, lakini hakufanya, sasa kama wewe ni msomi as you want us here tuamini then unapaswa kuweka ishu kwenye pande mbili na sio upande unaoutaka wewe tu bila kutupa the alternatives kwa sababu siasa kama sheria 90%, huamuliwa ka kutumia historia,

Kwa hiyo mkuu kwenye hili la rais kupeleka majeshi kokote nje ya nchi yetu, huna hoja ya msingi kwa sababu huna history wala sheria on your side, halafu next time acha matusi na lugha za choooni, sio lazima uazitumie ili hoja yako ieleweke,

Rais wa Jamhuri aliyechaguliwa na wananchi wa Tanzania, huwezi kumuita mjinga na mzembe, maana hapo peke yake unaonyesha uzembe na ujinga wako, na kwamba huna heshima wala adabu kwanza kwa rais wako, pili kwa sisi wananchi tuliomchagua, kwa hiyo hata mawazo yako sio worthy kabisa mkuu kuyasikiliza, wala kuyatilia maanani.
Mkuu FMES kazi hipo
Kwanza nipende kukuelewesha mambo mawiwli
Ujinga sio tusi, ni kutojua mambo fulani fulani, na ndo maana umekuwa ukisikia watu wanaenda shule ili kufuta ujinga
Uzembe sio tusi pia, ni kuwa mzito katika kufanya mambo fula fulani, au kuyafanya bila kushirikisha na kujaji athari zake hapo badae

Na sasa nakuja kwenye hili, nakuomba usipende tufanye mambo kutokana na USA wanavyofanya, USA wanaenda kwenye Vita wakiwa na interest zao, na sio bure, hakuna nchi itakayokubali kupigana bure bure, na ndo maana badae wakija kuambiwa huko kwenye congress wengi wanakubali, Sasa sisi hatuna interest kama hizo, hatuna haja ya kuingia kwenye vita. Na ikumbukwe kuwa tuliwasaidia southAfrica, Zimbabwe kuwaondoa kwenye Utumwa wa nchi yao, lakini sio Politics zao za ndani ya nchi na wao ndo wenye nchi yao twende tukapigane. Kwa sababu zipi, Tunapigana kwa faida gani, unaweza kueleza Faida Tanzania itakayopata kutoka kwenye hiyo Vita.
Na Mwisho, isiwe kwa sababu hakuna sheria inayomtaka raisi kufanya mambo fulani basi ndo anafanya tu anavyojisikia, Ndo maana watanzania wanataka mtu mwenye busara katika kuamua mambo kwa ajili yao, Unajua kufanya maamuzi kama hayo yanaweza kutusababishia matatizo badae? Na je ikitokea shida atawaeleza nini watanzania wakati hakuwambia hata kidogo kuhusu haya mambo??
 
1. Mkuu kumuita binadamu mwingine mzembe au mjinga ni matsui period, na hatuhitaji hizo lugha hapa ili kueleweka na jamii, Mkuu Mwanakijiji, hajawahi kumuita kiongozi yoyote wa taifa hayo majina, lakini hakuna asiyejua kali yake, muulize Lowassa, kumuita rais wa jamhuri hayo majina ni unacceptable na sisi wanannchi tuliomchagua, hatuwaiti viongozi wa upinzani hayo majina hata siku moja, sasa heshima ni kitu cha bure,

2. Now kwa maneno yako mwenyewe ni clear kuwa hatuna sheria inayombana rais wetu kusubiri umauzi wa bunge kabla ya kwenda vitani, unakubali kuwa vita vyote tulivyopigana na kuwasaidia nchi nyingi za Afrika, na kufikia kuwa masikini kuliko tuliowasaidia, havikuwahi kuidhinishwa na bunge,

kwa hiyo huna sheria, huna history on your side, lakini unadai rais ana makosa na unadai mpaka kwa lugha mbovu mbovu kama tuko kilabuni, kumbe ulichotakiwa kuomba ni marekebisho ya katiba, kaazi kweli kweli,

Anywaways, usiku mwema.
 
1. Mkuu kumuita binadamu mwingine mzembe au mjinga ni matsui period, na hatuhitaji hizo lugha hapa ili kueleweka na jamii, Mkuu Mwanakijiji, hajawahi kumuita kiongozi yoyote wa taifa hayo majina, lakini hakuna asiyejua kali yake, muulize Lowassa, kumuita rais wa jamhuri hayo majina ni unacceptable na sisi wanannchi tuliomchagua, hatuwaiti viongozi wa upinzani hayo majina hata siku moja, sasa heshima ni kitu cha bure,

2. Now kwa maneno yako mwenyewe ni clear kuwa hatuna sheria inayombana rais wetu kusubiri umauzi wa bunge kabla ya kwenda vitani, unakubali kuwa vita vyote tulivyopigana na kuwasaidia nchi nyingi za Afrika, na kufikia kuwa masikini kuliko tuliowasaidia, havikuwahi kuidhinishwa na bunge,

kwa hiyo huna sheria, huna history on your side, lakini unadai rais ana makosa na unadai mpaka kwa lugha mbovu mbovu kama tuko kilabuni, kumbe ulichotakiwa kuomba ni marekebisho ya katiba, kaazi kweli kweli,

Anywaways, usiku mwema.
Bado naendelea kukushangaa,
hapa hatuongelei upinzania, Neno ujinga na uzembe linaweza kumkuta yeyote awe CCM au upinzania, inategemea yuko katika swala gani ambalo halielewi au kafanya maamuzi kizembe.
Pili nimekueleza hivi kuwa na katiba ambayo hiko loosely kisiwe kigezo cha Raisi kujiamulia bila kutumia busara zake kwa manufaa ya Taifa.
Na ndo maana tunaitaji President Mwenye Busara katika kuamua mambo yake katika nchi kama ya Tanzania ambayo Katiba iko loosely,
Hivyo Raisi lazima awe na maamuzi ya Busara kwa kuangalia manufaa ya nchi na sio kwa sababu tu yeye ni raisi tu basi, Hiyo sio Busara kwa Mh. President kufanya mambo tu, eti kwa sababu Katiba haisemi kitu fulani, hayo yatakuwa maajabu basi anatakiwa kuirekebisha hiyo katiba wakati huo huo akiamua mambo kwa kutumia busara na kwa Manufaa ya Watanzania
 
FMES,
Kwanza ni lazima ukumbuke kuwa;
  1. Mwalimu alikuwa anajibu mashambulizi baada ya nchi kuvamiwa. Kwa hiyo tayari hii ni tofauti na kujiingiza katika vita ya kujitakia sifa.
  2. Pili, mwalimu alifanya majadiliano makubwa na baraza lake la mawaziri na hata kufikia kutuma ujumbe OAU kuwa inabidi sasa aikomboe nchi yake, ingawa OAU walipinga kitendo cha vita.
  3. Tatu, enzi za mwalimu zilikuwa ni za udikiteta, hata yeye alijua hili pale aliposema kuwa raisi ana madaraka makubwa kiasi kuwa kama angeyatumia vibaya angekuwa dikiteta, bila ya kujua kuwa alishawahi kuwa ka-dikiteta ingawa ilikuwa sio type ya akina Amini na Bokasa.
  4. JK ni mzembe na atakuwa ni mjinga kama atafikiria kuwa utawala wake una mazingira sawa na ya JKN.



Huu ni uongo, hatuna mkataba wowote unaotulazimisha kwenda vitani, na ndio maana hatukwenda Iraq.



Nakushari ukasome upya katiba ya US, declaration of war ni kazi ya congress tu.



Hii ni sababu ya kitoto kama ndio unayotaka kutufanya tuwajibike na Komoro.

Kubwajinga,
JF ni darasa kama madarasa mengine, tunajifunza na kuelimika.

Je, unaweza kurudi nyuma katika posting yangu uisome na kunijibu umeelewa nini?

Pili, Je, unaweza kutuambia ni zipi kazi na wajibu wa Amiri Jeshi Mkuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama Tanzania?
 
Jamani Rais hawezi kufanya jambo ambalo hana nguvu ya kisheria kulifanya. Kuna baadhi ya watu wanaamini kwa vile Rais ni Rais basi anaweza kufanya lolote na kuamuru lolote. Si kweli. Rais anaweza kufanya kile tu ambacho Katiba imempa uwezo kufanya. Tatizo ambalo linatukabili mara nyingi ni watu kuamini kuwa Rais anaweza akaamka asubuhi na kuamuru kuvunja Bunge, kuamuru mtu akamatwe nk. Ni imani hii kimsingi ndiyo inayoupa nguvu Urais kuliko nguvu uliyonayo kisheria.

Hata hivyo, Rais anazo nguvu ambazo zimepewa kwake kisheria. Swali ni je Rais ana nguvu gani katika kutangaza vita na kuyaamuru majeshi ya ulinzi na Usalama? Hakuna haya ya kuangalia Marekani wanafanya nini kwani wao wanaoongozwa na Katiba yao. Badala ya kuandikia mate, angalieni kama wino upo?. Na wino hapa ni Katiba, angalieni Katiba inasema nini kuhusu uhusiano kati ya Rais na Majeshi ya Ulinzi.
 
Tatizo litaibuka ikiwa tu hao majeshi waliopelekwa watafyekwa wote hapo ndio patajulikana kusuka au kunyoa,nakumbuka kuna wakati baadhi ya Majeshi ya Comoro walijaribu kukivamia kisiwa hicho ,inasemekana hakurudi mtu,wasifikiri wanaenda kuivamia Pemba waue halafu wapeane vyeo,Anjuani wamejizatiti kwa miaka mingi na wameshazima mavamizi mengi tu na wana wataalam wa hali ya juu wenye uzoefu wa kivita,tuombe Mungu.
Kitu kimoja nawashauri wajeshi wetu wachukue ramani za huko isije ikawa kama vita vya Uganda waliingia Uganda bila ya ramani.
 
Its interesting jinsi hili suala linavyozungumzwa sasa. Na mbaya zaidi tunalizungia not from an informed point of view na hii inachangiwa na muundo wa KISIRI SIRI wa Serikali yetu na mbaya zaidi inachangiwa na kwa kiasi kikubwa na vyama vya upinzani ambavyo navyo inprinciple viko defunct

nilipokuwa nikilalamika kuhusu website za IKULU na FOREIGN mlifikiri mimi mwenda wazimu

kazi kwenu mie kwenye hili zilishasema sana lakini wapi...
 
Tunatakiwa kuwa na haki ya kuuliza jeshi letu linapelekwa wapi na kufanya nini na kwa maslahi ya nani. Who foots the bill. Kama tukiendeleza ujinga wa awamu zetu zilizopita za kuonesha upendo wa mshumaa, tunateketea kwa ajili ya wengine, wengine wanaendelea kuwa na maendeleo, sisi tunadumaa!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom