Majawabu ya Kigwangalla: Tunawezaje Kuleta Usawa Kwenye Ubora wa Elimu Yetu?

HKigwangalla

JF-Expert Member
Feb 6, 2008
717
971
HUU NI MMOJA WA MICHANGO YANGU KWENYE BAJETI YA ELIMU MWAKA JANA WAKATI BUNGE LIMEKAA KAMA KAMATI.




MWENYEKITI: Ahsante, Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla!


MHE. DKT. HAMISI A. KIGWANGALLA: Mheshimiwa Mwenyekiti,
ahsante kwa kunipa fursa hii.


Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mchango wangu wa maandishi niliongelea kwa kirefu
kuhusu jitihada za Serikali katika ku-foster equity kwenye utoaji wa elimu nchini ili kupunguza gap
kati ya walio nacho na wasio nacho, na pia ili kuondoa uwezekano wa kuunda matabaka ya watumwa
na watawala kwa kuruhusu uwepo wa kundi la watu wenye elimu bora na la wale wasio na elimu kabisa.
Hii inatokana na uwepo wa shule za sekondari za kata zenye ubora huu wa elimu tunaoufahamu, ambazo
wanasoma watoto wa pangu pakavu na uwepo wa private schools wanazosoma watoto wa wenyenacho. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nimependekeza na kutoa ushauri kwa Serikali ili kuweza kupunguza

tofauti iliyopo kati ya walio nacho na wasio nacho ni lazima walimu ambao wanafanya kazi katika mazingira
magumu wapewe motisha maalum ambazo zinaweza zikawa calculated kijiografia au kwa vigezo vingine ambavyo
vinatokana na tafiti mbalimbali. (Makofi)


Je, Serikali imejipanga vipi katika kutoa motisha kwa walimu wanaoishi katika
mazingira magumu ikiwa ni pamoja na nyumba, mikopo ya vyombo vya usafiri na posho
za hardship katika kazi zao. Ahsante.
 
HUU NI MMOJA WA MICHANGO YANGU KWENYE BAJETI YA ELIMU MWAKA JANA WAKATI BUNGE LIMEKAA KAMA KAMATI.




MWENYEKITI: Ahsante, Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla!


MHE. DKT. HAMISI A. KIGWANGALLA: Mheshimiwa Mwenyekiti,
ahsante kwa kunipa fursa hii.


Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mchango wangu wa maandishi niliongelea kwa kirefu
kuhusu jitihada za Serikali katika ku-foster equity kwenye utoaji wa elimu nchini ili kupunguza gap
kati ya walio nacho na wasio nacho, na pia ili kuondoa uwezekano wa kuunda matabaka ya watumwa
na watawala kwa kuruhusu uwepo wa kundi la watu wenye elimu bora na la wale wasio na elimu kabisa.
Hii inatokana na uwepo wa shule za sekondari za kata zenye ubora huu wa elimu tunaoufahamu, ambazo
wanasoma watoto wa pangu pakavu na uwepo wa private schools wanazosoma watoto wa wenyenacho. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nimependekeza na kutoa ushauri kwa Serikali ili kuweza kupunguza

tofauti iliyopo kati ya walio nacho na wasio nacho ni lazima walimu ambao wanafanya kazi katika mazingira
magumu wapewe motisha maalum ambazo zinaweza zikawa calculated kijiografia au kwa vigezo vingine ambavyo
vinatokana na tafiti mbalimbali. (Makofi)


Je, Serikali imejipanga vipi katika kutoa motisha kwa walimu wanaoishi katika
mazingira magumu ikiwa ni pamoja na nyumba, mikopo ya vyombo vya usafiri na posho
za hardship katika kazi zao. Ahsante.

Mawazo ya jinsi ya kuboresha elimu yetu pamoja na mfumo wetu wa elimu yamekuwa yakitolewa na wadau mbalimbali na kwa upana sana tena katika mitazamo mbalimbali, lakini binafsi sijawahi kushawishika kama serikali yetu iko tayari kutekeleza maboresho muhimu katika sekta ya elimu yatakayosaidia kuliinua kundi kubwa la masikini ambalo watoto wao wameendelea kupata elimu duni na hatimaye kuishia kufeli na kurudi vijiweni kuvuta bangi na kujiajiri kwa kutembeza soksi na chewing gums barabarani.

Na hii inafanyika makusudi na watawala kwakuwa wanataka watoto wao na wajukuu wao waendelee kuwaburuza watanzania masikini hawa miaka baada ya miaka. Lakini pamoja na hayo kitu ambacho watawala hawa wanatakiwa kufahamu ni kwamba siku hawa watanzania masikini wakichoka hawatokuwa na cha kupoteza kwahiyo wataamua liwalo na liwe, na siku hiyo ndipo kutakuwa na kilio na kusaga meno.
 
Hivi mheshimiwa kigwangalla ni wakati gani unakaa kwenye ofisi yako kuwasaidia na kukusanya kero za wapiga kura zako muda mrefu upo kwenye vyombo vya habari kama una hamu ya kusema sana nenda kwenye kampeni Arumeru useme mpaka mdomo ukauke
 
Ushauri umekuwa ukitolewa since alipokuwepo Mzee Ruksa mpaka leo hamna kitu.
 
Mkuu kama unataka kuleta usawa katika elimu ya Tanzania anzia hapa sio kumungunya maneno na kuzunguka

SALAMA KIKWETE PEDIATRICS DENTISTRY,UK

Source:
[url]http://www.moh.go.tz/POSTGRADUATE-TO-BE-SPONSORED.pdf[/URL]

Ndugu wana JF,
Ninajua kuna maswala mengi ambayo yako mbele yetu kwa ajili ya kuyajadili na kutafutia ufumbuzi. Lakini nimesikitishwa sana na list ambayo nimeona kwenye website ya wizara ya afya inayoonyoshe majina ya postgraduate students ambao watakuwa sponsored na wizara ya afya. List yenyewe ni hii hapa
http://www.moh.go.tz/POSTGRADUATE-TO-BE-SPONSORED.pdf. Kilichonifanya niweke thread hii hapa ni kuwa Wizara imeamua kusomesha mtoto mmoja wa mkubwa UK ambaye kwa jina anajulikana SALAMA KIKWETE. Cha kusikitisha zaidi ukiangalia hitimisho la list hii kuna usemi huu: THOSE CANDIDATES WHO APPLIED FOR SPONSORSHIP FROM THE MINISTRY OF HEALTH AND SOCIAL WELFARE AND DO NOT APPEAR IN THIS LIST SHOULD CONSIDER THEMSELVES UNSUCCESSFUL .
Je, ni wanafunzi wangapi zaidi wangesomeshwa hapa bongo kwa pesa hii itakayoyumika kusomesha huyu mtoto mmoja wa kigogo?
Je, ni wanafunzi wangapi walipewa opportunity ku-compete na huyu mtoto wa kigogo kwa hii nafasi ya kusoma UK?
Je, hatuna pediatric dentistry educators hapa bongo?

Kama uliapply for sponsorship ukakosa na upo humu jamvini ni vizuri ukatujulisha ili tupate a true picture ya madakitari ambao hawakuweza kujiunga postgraduate kwa kukosa sponsor.


 
Hivi mheshimiwa kigwangalla ni wakati gani unakaa kwenye ofisi yako kuwasaidia na kukusanya kero za wapiga kura zako muda mrefu upo kwenye vyombo vya habari kama una hamu ya kusema sana nenda kwenye kampeni Arumeru useme mpaka mdomo ukauke

hahahah aliyekuambiaukaa ofisini ndo utajua matatizo ya wananchi wako ni nani? magamba bwana, nakupongeza kingwangalla sisi ndo wapiga kura wako tujadili na kuelimishana jinsi ya kuiendesha nvhi hii achana na hawa magamba wenzio wenye upeo mdogo, tatizo la wafanyabiashara kwenye siasa ndo hiloo mkuu!
 
Kila mwajiriwa akiweka report ya vikao vya kazini na jinsi alivyochangia????!!!!!!!!!

1. Mkuu hii si routine work kwako na you got paid for the job????
2. Do you believe kuna watu wana attend na Kuchangia mikutano mingi sana kwa mwaka kuliko wewe???
3. Hawa wote pia watuwekee humu jinsi walivyo participate kwenye ujenzi wa taifa???

Kwa kiongozi kijana na msomi kama wewe kwa kweli vijana wenzako tunatarajia mengi makubwa kuliko feedback ya kikaoni.

Angalizo; Vijana wasomi ni wengi sana ambao hawako katika siasa lakini ni miongoni mwa nguvu kazi ya Taifa na yawezekana wana matumaini makubwa juu yenu viongozi vijana mlioelimika. Ni jukumu lenu kuonesha njia kwa vitendo; as you get served from silver plates(available opportunities) your health (productivity) should reflect this
 
Hivi mheshimiwa kigwangalla ni wakati gani unakaa kwenye ofisi yako kuwasaidia na kukusanya kero za wapiga kura zako muda mrefu upo kwenye vyombo vya habari kama una hamu ya kusema sana nenda kwenye kampeni Arumeru useme mpaka mdomo ukauke
Mbona kuna kero nyingi sana za wapiga kura ninazo na bado nahangaika kuzitatua hata sijafika nusu kuzimaliza, sasa unataka niendelee kukusanya tu kero zao kila siku? Halafu unadhani inachukua muda gani ku-copy hansard ya mchango wangu kama huu na kuanzisha mjadala? Hivi unadhani hii ninayofanya hapa siyo kazi yangu? Unaelewa maana ya uraghibishi?
 
hahahah aliyekuambiaukaa ofisini ndo utajua matatizo ya wananchi wako ni nani? magamba bwana, nakupongeza kingwangalla sisi ndo wapiga kura wako tujadili na kuelimishana jinsi ya kuiendesha nvhi hii achana na hawa magamba wenzio wenye upeo mdogo, tatizo la wafanyabiashara kwenye siasa ndo hiloo mkuu!
bora yako umemjibu wewe
 
Kila mwajiriwa akiweka report ya vikao vya kazini na jinsi alivyochangia????!!!!!!!!!

1. Mkuu hii si routine work kwako na you got paid for the job????
2. Do you believe kuna watu wana attend na Kuchangia mikutano mingi sana kwa mwaka kuliko wewe???
3. Hawa wote pia watuwekee humu jinsi walivyo participate kwenye ujenzi wa taifa???

Kwa kiongozi kijana na msomi kama wewe kwa kweli vijana wenzako tunatarajia mengi makubwa kuliko feedback ya kikaoni.

Angalizo; Vijana wasomi ni wengi sana ambao hawako katika siasa lakini ni miongoni mwa nguvu kazi ya Taifa na yawezekana wana matumaini makubwa juu yenu viongozi vijana mlioelimika. Ni jukumu lenu kuonesha njia kwa vitendo; as you get served from silver plates(available opportunities) your health (productivity) should reflect this
Saidimu, sitegemei kila mtu kuweka hapa michango yake yote na hata mimi sijaweka hapa michango yangu yote na tena kila siku. Huu ndiyo mchango wangu mmoja tu nimeuweka hapa leo. Na lengo langu ni kuanzisha mjadala unaohusu jitihada zetu za kuleta usawa kwenye elimu, na hapa sileti kama MB tu eti natoa feedback ya kazi zangu, la. Naleta kama mwanabodi mwingine tu hapa, sema nina kiti cha ubunge pia (utata). Kwa mimi kama MB kuleta mjadala unaohusiana na kazi zangu ni kuamsha mjadala unaopelekea kunipanua mawazo na kunipa fikra mpya kwenye mjadala husika pia kupata picha ya wanachokitaka watanzania wenzangu kama wewe. kwangu mimi hii ni fursa ya kujifunza zaidi na pia kukusanya maoni na kisha kuyafanyia kazi. Ninaamini hii ni njia effective sana ya kufanya uwakilishi unaotarajiwa. Na zaidi nikuambie tu kuwa thru mitandao jamii nimepata marafiki wengi waliojificha nyuma ya kompyuta zao na waliotaka tuonane na kujadili mustakabali wa Taifa letu kwenye mambo mbalimbali, na wengi wamekuwa wakinipa mawazo mazuri na ushauri. Pia mitandao hii wanasoma watu wengi, kuna wahusika watasoma michango yetu hapa na kuifanyia kazi, wewe kama unakuja hapa kucheza unapoteza muda wako na unatakiwa ujifikirie mara mbili, wenzako tuko serious na hii ni kama kazi zetu za kila siku. Na nadhani hii inatosha kukuelewesha kwa nini nachangia na kushiriki hapa effectively.
 
HUU NI MMOJA WA MICHANGO YANGU KWENYE BAJETI YA ELIMU MWAKA JANA WAKATI BUNGE LIMEKAA KAMA KAMATI.




MWENYEKITI: Ahsante, Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla!


MHE. DKT. HAMISI A. KIGWANGALLA: Mheshimiwa Mwenyekiti,
ahsante kwa kunipa fursa hii.


Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mchango wangu wa maandishi niliongelea kwa kirefu
kuhusu jitihada za Serikali katika ku-foster equity kwenye utoaji wa elimu nchini ili kupunguza gap
kati ya walio nacho na wasio nacho, na pia ili kuondoa uwezekano wa kuunda matabaka ya watumwa
na watawala kwa kuruhusu uwepo wa kundi la watu wenye elimu bora na la wale wasio na elimu kabisa.
Hii inatokana na uwepo wa shule za sekondari za kata zenye ubora huu wa elimu tunaoufahamu, ambazo
wanasoma watoto wa pangu pakavu na uwepo wa private schools wanazosoma watoto wa wenyenacho. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nimependekeza na kutoa ushauri kwa Serikali ili kuweza kupunguza

tofauti iliyopo kati ya walio nacho na wasio nacho ni lazima walimu ambao wanafanya kazi katika mazingira
magumu wapewe motisha maalum ambazo zinaweza zikawa calculated kijiografia au kwa vigezo vingine ambavyo
vinatokana na tafiti mbalimbali. (Makofi)


Je, Serikali imejipanga vipi katika kutoa motisha kwa walimu wanaoishi katika
mazingira magumu ikiwa ni pamoja na nyumba, mikopo ya vyombo vya usafiri na posho
za hardship katika kazi zao. Ahsante.

Umepost ili tukupongeze?
Gamba chovu wewe!
 
Naomba msome makala ya Jenerali wiki hii katika RAIA MWEMA la wiki hii....ameeleza vizuri sana
 
Dr. Hamisi nimeanza kukufuatilia muda mrefu naona unashika hichi unaacha unarukia kingine mpaka unakuwa hueleweki na pia humalizi hebu jaribu ku concentrate kwenye jambo moja liishe ndio uanze lingine unaviporo kibao
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Mbona kuna kero nyingi sana za wapiga kura ninazo na bado nahangaika kuzitatua hata sijafika nusu kuzimaliza, sasa unataka niendelee kukusanya tu kero zao kila siku? Halafu unadhani inachukua muda gani ku-copy hansard ya mchango wangu kama huu na kuanzisha mjadala? Hivi unadhani hii ninayofanya hapa siyo kazi yangu? Unaelewa maana ya uraghibishi?

Mh Mbunge, nilipoona hii title na kuwa imatumwa na wewe, niliacha shughuli zangu na kuifungua haraka sana. Sababu ni kwamba mimi nina shauku sana ya kupata jukwaa litakalojadili hili suala 'kisayansi'. Pamoja na nia yako nzuri ya kuuleta huu mjadala, lakini preamble uliyotoa hata haihamasishi. Can you please carry a litle research and come up with a touching data enriched introduction?
 
baada yakutoa mchango huo ulijibiwa nini?je,ulilizishwa na majibu uliyopata?wewe kama mwakilishi wawananchi ulichukua hatua gani au uliishia kuunga mkono hoja na kugonga meza kishabiki? kwayanayo endelea ndani ya nchi hii hakika mwisho wake unakalibia watanzania wasasa wameanza kujua haki zao hawatatishiwa na askali 250 kama walivyopelekwa ARUMERU? Mh kigwangalla unajisikiaje mwisho wa mwezi pale nzega unatoka bank kuangalia ballance unakuta mamilioni yako yameshaingizwa halafu mtaani WALIMU WAPYA wapo kwenye mgomo wakidai mshahara wa 200000?ukipata nafasi yakuzungumza na watawala waambie mtaani tumechoka kusubili MAISHA BORA kwakila mtanzania,tumechoka kuona madini yetu yakisafilishwa nje bila kutunufaisha,tumechoka kuona twiga wetu wakipanda ndege,tumechoka kufanya manunuzi halafu baadae tunaludishiwa chenchi kama ilivyotokea kwenye rada.....TANZANIA YENYE NEEMA NI YETU SOTE"
 
HUU NI MMOJA WA MICHANGO YANGU KWENYE BAJETI YA ELIMU MWAKA JANA WAKATI BUNGE LIMEKAA KAMA KAMATI.




MWENYEKITI: Ahsante, Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla!


MHE. DKT. HAMISI A. KIGWANGALLA: Mheshimiwa Mwenyekiti,
ahsante kwa kunipa fursa hii.


Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mchango wangu wa maandishi niliongelea kwa kirefu
kuhusu jitihada za Serikali katika ku-foster equity kwenye utoaji wa elimu nchini ili kupunguza gap
kati ya walio nacho na wasio nacho, na pia ili kuondoa uwezekano wa kuunda matabaka ya watumwa
na watawala kwa kuruhusu uwepo wa kundi la watu wenye elimu bora na la wale wasio na elimu kabisa.
Hii inatokana na uwepo wa shule za sekondari za kata zenye ubora huu wa elimu tunaoufahamu, ambazo
wanasoma watoto wa pangu pakavu na uwepo wa private schools wanazosoma watoto wa wenyenacho. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nimependekeza na kutoa ushauri kwa Serikali ili kuweza kupunguza

tofauti iliyopo kati ya walio nacho na wasio nacho ni lazima walimu ambao wanafanya kazi katika mazingira
magumu wapewe motisha maalum ambazo zinaweza zikawa calculated kijiografia au kwa vigezo vingine ambavyo
vinatokana na tafiti mbalimbali. (Makofi)


Je, Serikali imejipanga vipi katika kutoa motisha kwa walimu wanaoishi katika
mazingira magumu ikiwa ni pamoja na nyumba, mikopo ya vyombo vya usafiri na posho
za hardship katika kazi zao. Ahsante.

We jamaa mbunge…nimekusikia ukijishughulisha na maswala ya afya ya uzazi pia……hivi una taarifa gani kuhusu muswada mpya feki wa afya ya uzazi unaohalalisha utoaji mimba(abortion) na ambao unalazimishwa kuletwa TZ kwa shinikizo la international NGOs…..na mtaletewa soon bungeni muupitishe kama kawaida yenu ya wengi wape!!.......Pia unazungumziaje kwa undani muswada huu utakaohalalisha uuwaji wa viumbe(watoto)….uki consider kuwa wanaotaka muswada huu TZ wanasema utachangia kupunguza ongezeko la watu TZ(over population) na pia maternal mortality …wakati takwimu za kidunia zimethibitisha kuwa kwenye nchi zilizowahi kuhalalisha abortion zilijikuta zikiwa na vifo zaidi (maternal mortality) kuliko nchi zile zilizokuwa zimepiga marufuku abortion???.....nataka msimamo wako juu ya hili maana hata spika wako Makinda nimemsikia akiufagilia huu muswada wa kuletwa TZ na NGOs za nje….naona nchi hii sasa mnafanya kazi kwa manufaa ya wageni na si watanzania……..soma hii link kwa mchango wako zaidi……Radical pro-abort bill being pushed on Tanzania by international organizations | LifeSiteNews.com
 
Tatizo tulilonalo si tu tabaka za kielimu, kati ya walionacho na wasionacho. Bali pia ni aina ya elimu itolewayo na shule zetu. Elimu itolewayo si elimu ya kumkomboa mtanzania kutoka katika lindi la umasikini, bali ni elimu ya kumfungamanisha na umasikini na utumwa wa wakati. Wakati tunaongelea kujitegemea, elimu yetu inafundisha utegemezi. Ili tuendelee tunahitaji mapinduzi ya kilimo, viwanda, resources, madini, sekta za huduma n.k. Na ili tuendelee tunahitaji taifa la wabunifu katika sekta zote za uzalishaji mali. Lakini elimu yetu ya sasa inaendeleza utegemezi na ndio maana kumekuwa na wimbi kubwa la vijana kukosa ajira, kwa sababu maelfu ya vijana wa nchi yetu wamepata elimu ya kutegemea kuajiriwa na sekta rasmi (e.g Serikalini, Mabenki, makampuni n.k). Elimu inayofundisha, Geography, History, Kiswahili, English, Mathematics, Civics, Biology, Chemistry, Physics, Commerce and Book Keeping, kwa mtaala tulionao, vijana wetu walio wengi wanatoka patupu na hauwasaidii chochote, sana sana kuwasindikiza wenzao wachache, kisha kurudi vijiweni kucheza kamari. Kwa nchi yetu mfumo wa elimu utakaotukomboa ni ule utakaoibua vipaji na kuzalisha wabunifu katika nyanja mbalimbali, kwa mfano: -
1. Fani ya kilimo, tuwe na somo la kilimo na ufugaji (Commercial agriculture) kuanzia darasa la tatu na kuendelea mpaka form 4. Masuala ya agrochemistry, agro commerce, agro financing, crops what what, yoote yapatikane humu. Subject specialisation ianzie form three.
2. Fani ya biashara, masuala ya biashara na uchumi yaanzie ngazi ya msingi. Biashara ni sayansi ya jamii, na kila shughuli ya kiuchumi katika jamii ni biashara (Business). Watu wetu wanapaswa kuwa na ufahamu wa elimu ya biashara, walau basic knowledge.
3. Huduma - (Customer service), tunapaswa kufahamu kwamba kila mtu anayesababisha uwepo wa shughuli yako ni mteja wako. Mbunge, wateja wako ni wananchi unaowawakilisha, Polisi ni raia unaowalinda n.k. Ni vema kuwa na elimu ya huduma kwa wateja kwa kila mmoja wetu.
4. Uraia. Elimu ya kujua haki na wajibu wa kila raia (Suala la kodi, rushwa, usalama wa raia, usalama wa taifa, huduma ya kwanza, uzalendo), ni muhimu kwa kila raia kuanzia darasa la kwanza.
5. Somo la Sayansi na Ufundi. Lijumuishe aina zote za ufundi (Basics), Specialization ianzie darasa la nne.
6. Sanaa na Michezo, watoto wafundishwe michezo mbalimbali, wajengwe kimwili na kisaikolojia, specialization ianzie darasa la nne.
7. Masomo kama Hisabati, Lugha yawe ya lazima kwa kila fani.
8. Masomo kama Historia, Biolojia, Jiografia, Fizikia, Kemia yawe ni ya lazima kwa ngazi za awali kwa Shule za msingi na Sekondari, kisha yafundishwe kama masomo ya kuchagua.
Huu ni mtazamo wangu.
 
Hivi mheshimiwa kigwangalla ni wakati gani unakaa kwenye ofisi yako kuwasaidia na kukusanya kero za wapiga kura zako muda mrefu upo kwenye vyombo vya habari kama una hamu ya kusema sana nenda kwenye kampeni Arumeru useme mpaka mdomo ukauke
kwani kazi ya MB ni kukaa ofisini tu?
 
Back
Top Bottom