Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,949
- 22,116
Habari za asbh, leo hii nilipita pale Sinza ofisi za TRA saa kumi kamili baada ya dk 2 kulipita lile jengo nilisikia mirindimo ya RISASI polisi wakitunukiana na majambazi kama wengi wenu mngefanya nilikiingiza kistarlet changu katikati ya nyumba za watu kuokoa roho yangu na huku wengine wakipaki na kuacha magari pembeni ya barabara na kukimbia. Baada ya muda nikapita tena na kukuta jambazi moja limelala pale chini na askari wakilizunguka. Mwenye data zaidi tuhabarisheni..