Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,870
- 155,827
MZIMU wa ujambazi umeendelea kutesa jijini ambapo jana kundi la majambazi wamevamia tena Kimara Stop Over na kumuua kwa kumpiga risasi mgongoni Afisa Mauzo wa Kampuni ya Lubricant, Gosbert Kanyika (32).
Chanzo chetu cha habari kutoka eneo la tukio kimedai kuwa majambazi hayo yalivamia katika nyumba ya afisa huyo muda mfupi baada ya marehemu na familia yake kuingia ndani wakitoka hospitali kutibiwa.
Imedaiwa kuwa mara baada ya Gosbert na familia yake kutibiwa walikodi taksi na kurejea nyumbani na walipoingia ndipo majambazi hao waliokuwa na bunduki walipovamia na kuwalazimisha kutoa fedha.
Katika purukshani hizo majambazi hao walimvaa Gosbert na kumlazimisha awape fedha na ndipo walipoanza kumpiga sehemu mbalimbali za mwili wake kwa kutumia silaha zenye ncha kali walizokuwa nazo.
Wakati uhalifu huo ukiendelea, majambazi wengine walianza kupekua nyumba hiyo wakitafuta fedha na mali ambapo inadaiwa kuwa waliambulia sh 8,000.
Majambazi hao kuona hivyo walianza kumshambulia mke wa mwenye nyumba hiyo kwa kumpiga na silaha zenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake.
Kisha majambazi hao walimchukua Gosbert na kwenda naye nje kisha kumpiga risasi mgongoni na kufariki papo hapo na kisha majambazi hao kutoweka.
Majeruhi aliyefahamika kwa jina la Catherine, ambaye ni mke wa marehemu Gosbert, amelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili akiendelea kupata matibabu na maiti imehifadhiwa hospitalini hapo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema taarifa kamili zitatolewa baadaye leo.
SOUCE
MAJIRA
Chanzo chetu cha habari kutoka eneo la tukio kimedai kuwa majambazi hayo yalivamia katika nyumba ya afisa huyo muda mfupi baada ya marehemu na familia yake kuingia ndani wakitoka hospitali kutibiwa.
Imedaiwa kuwa mara baada ya Gosbert na familia yake kutibiwa walikodi taksi na kurejea nyumbani na walipoingia ndipo majambazi hao waliokuwa na bunduki walipovamia na kuwalazimisha kutoa fedha.
Katika purukshani hizo majambazi hao walimvaa Gosbert na kumlazimisha awape fedha na ndipo walipoanza kumpiga sehemu mbalimbali za mwili wake kwa kutumia silaha zenye ncha kali walizokuwa nazo.
Wakati uhalifu huo ukiendelea, majambazi wengine walianza kupekua nyumba hiyo wakitafuta fedha na mali ambapo inadaiwa kuwa waliambulia sh 8,000.
Majambazi hao kuona hivyo walianza kumshambulia mke wa mwenye nyumba hiyo kwa kumpiga na silaha zenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake.
Kisha majambazi hao walimchukua Gosbert na kwenda naye nje kisha kumpiga risasi mgongoni na kufariki papo hapo na kisha majambazi hao kutoweka.
Majeruhi aliyefahamika kwa jina la Catherine, ambaye ni mke wa marehemu Gosbert, amelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili akiendelea kupata matibabu na maiti imehifadhiwa hospitalini hapo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema taarifa kamili zitatolewa baadaye leo.
SOUCE
MAJIRA