Kalunguine
JF-Expert Member
- Jul 27, 2010
- 2,543
- 134
Waliamua kwa maslaihi ya waliowateua.So wamelinda maslahi yao na si ya Taifa.
kuuliza si ujinga hivi mgombea binafsi ataendesha vipi shughuli zake na kupitisha vipi sera zake katika bunge la muundo uliopo? maana at times nadhani kama vile tunalilia mvua wakati visima vya kuhifadhia maji atujajenga.Majaji hawa 7 wa Mahakama ya Rufaa wakiongozwa na aliyekuwa Jaji Mkuu Augustino Ramadhan,akisaidiwa na majaji wenzake 6 ambao ni Eusebio Munuo, Januari Msofe, Benard Luanda, Mbarouk Mbarouk, Nathalia Kimaro na Sauda Mjasiri;hapo Juni 16, 2011 walikataa TZ isiwe na mgombea binafsi tena wakitupilia mbali andiko ndani ya katiba linalosema kuwa"Kila mtz ana haki ya kupiga na kupigiwa kura";Kama kupiga kura hatuhitaji kuwa na udhamini wa chama cha siasa iweje kupigiwa kura lzm udhaminiwe na chama cha siasa?
Bado nitazidi kuwaheshimu hadi siku yangu ya kufa Majaji watatu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Amir Manento, Salum Massati na Thomas Mihayo kwa kuruhusu mgombea binafsi kabla ya majaji wengine 7 wa Mhakama ya Rufaa kuhujumu demokrasia yetu!
Tuseme ukweli na wala kutoa maoni yako huru kusichukuliwe kama ni kuingilia uhuru wa mhimili mwingine wa dola!Kama mgombea binafsi angeruhusiwa unahisi hii fukuza fukuza ya wabunge na madiwani tunayoishuhudia sasa hivi ingekuwepo?
hivi haiwezekani kufungua tena hii kesi ya kudai mgombea binafsi, au kuna hamakama ya kimataifa tunayoweza kwenda kufungua tena hili shauri wataalamu wa sheria tujuzeni. na ikiwa inawezekana je mnaonaje sasa tukajiunga kama watanzania tukawawezesha wanasheria makini kama mtikila wenye kuweza kufungua na kutete kesi tukapata ushidi na hatimae haki ikatenda?
Nchi hii imewahi kuwa na Jaji Mmoja tu nakumbuka alikuwa akiitwa Rugakingira!
kuuliza si ujinga hivi mgombea binafsi ataendesha vipi shughuli zake na kupitisha vipi sera zake katika bunge la muundo uliopo? maana at times nadhani kama vile tunalilia mvua wakati visima vya kuhifadhia maji atujajenga.
Majaji hawa 7 wa Mahakama ya Rufaa wakiongozwa na aliyekuwa Jaji Mkuu Augustino Ramadhan,akisaidiwa na majaji wenzake 6 ambao ni Eusebio Munuo, Januari Msofe, Benard Luanda, Mbarouk Mbarouk, Nathalia Kimaro na Sauda Mjasiri;hapo Juni 16, 2011 walikataa TZ isiwe na mgombea binafsi tena wakitupilia mbali andiko ndani ya katiba linalosema kuwa"Kila mtz ana haki ya kupiga na kupigiwa kura";Kama kupiga kura hatuhitaji kuwa na udhamini wa chama cha siasa iweje kupigiwa kura lzm udhaminiwe na chama cha siasa?
Bado nitazidi kuwaheshimu hadi siku yangu ya kufa Majaji watatu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Amir Manento, Salum Massati na Thomas Mihayo kwa kuruhusu mgombea binafsi kabla ya majaji wengine 7 wa Mhakama ya Rufaa kuhujumu demokrasia yetu!
Tuseme ukweli na wala kutoa maoni yako huru kusichukuliwe kama ni kuingilia uhuru wa mhimili mwingine wa dola!Kama mgombea binafsi angeruhusiwa unahisi hii fukuza fukuza ya wabunge na madiwani tunayoishuhudia sasa hivi ingekuwepo?
Jamaa ameweka wazi kuwa hawa ndiyo majaji walioruhusu mgombea binasfi ambao uamuzi wao ulibadilishwa na hao wa mahakama ya rufaa.
Hivi TZ hatuna constitutional court??
Mkuu mbona umemsahau Jaji James Mwalusanya!!!
Nchi hii imewahi kuwa na Jaji Mmoja tu nakumbuka alikuwa akiitwa Rugakingira!
yPamoja na judge MWALUSANYA.
Article 107A "Mahakama ndiyo chombo cha mwisho ktk utoaji haki" Majaji wakasema "...suala hili lipelekwe bungeni..." Kazi ipo!!!!!!!!!!!