zomba
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 17,240
- 3,910
Acha kujifanya huwajui viongozi wa Tanzania, unategemea, hata akipewa mwingine unategemea jaji mmoja kujaji Kesi ya jaji mwenzake kwa umakini na kwa maslahi ya Taifa?? kwa taifa lenye kwenda kwa kuangaliana kama letu??
Na nafasi ya Masha kama waziri katika hii kesi kama yeye ni mmoja wa wahusika wakuu??
Kweli kazi hipi
Viongozi, wawe wa nchi hii au nyingine, aidha nawajuwa au siwajui, hiyo si hoja. Hilo la pili naomba ujibu wewe mwenyewe.
Maslahi ya Taifa ni matokeo ya hao wenye Taifa lao, la ki-demokrasia, wamemchaguwa nani awe ndie mwenye uwezo wa kuwateuwa kina nani ambao yeye (alie chaguliwa na wananchi) anaona kuwa hawa ndio wennye uwezo wa kuliendesha taifa kwa nyanja zao.
Laiti ingelikuwa mteuaji wa hao walioteuliwa, amejitekea madaraka bila ya kuchaguliwa na kukubalika na wananchi, basi hapo tungelikuwa na shaka na hasima zote za kutokuwa na imani na uchaguzi wa huyo aliejipachika madaraka kwa mabavu.