Maisha yamenishinda!!

Kwa kipato cha shs 542,000 hutakiwi kulalamika. Kuna watanzania kama 85% ambao wanapata 1/4 ya unachopata (135,000) na wanaishi na familia zao watoto wa3 and above na bado utakuta ana kibanda chake Charambe, Kongowe, Kitunda au Kipate.

Wewe una mke na mtoto mmoja na unatumia daladala unalalamika nini. Nakushauri kuwa na vipaumbele, acha makundi ya starehe kama ulevi. uzinzi then hicho kipato kinaweza kukutoa. Hebu tufanye mchanganuo hapa chini.

Tshs 542,000/=

1. Kodi ya nyumba shs 100,000
2. Chakula nyumbani shs 150,000
3. Chakula kazini shs 60,000
4. Nauli ya dala dala 30,000
5. Mengineyo shs 100,000

Jumla ya matumizi ni shs 440,000 hivyo unabaki na akiba ya 102,000. Ukitunza hii akiba kwa miezi sita unaweza ukampatie mke wake mtaji wa shs 612,000 baada ya miezi sita na mkaanza mkakati wa kununu ka plot Gongolamboto.

Chukua huo ushauri na usirudi kijijini utajuta.

Asisubiri miezi 6 ya kujibana. Ana ajira na ni dhamana tosha. Akubali hiyo laki 1 iwe inakatwa kutokana na mikopo iliyoko benki na inapatikana within a week. Tazama hesabu hii, laki 1 kwa mwaka ni 1.2ml. Na kama utakopa kwa miaka mi4 ni 4.8ml. Utapewa karibu 4ml. Huo ni mtaji maridadi wa kabiashara kwa mjasiriamali. Mpe mkeo na fungua biashara makini ya bidhaa isiyochacha. Dar kuzuri utatoka broda!
 
Ndugu maisha ya kijijini ni magumu kuliko hata huko mjini gharama zimepanda balaa.Huku kwetu Gege (samaki mdogo -tilapia) anauzwa sh. 500 hebu niambie ili ule na familia ya watu saba unaitaji magege mangapi? Kusanga na kukoboa debe moja ni sh. 1400 unga enyewe haumalizi hata wiki. Angalau ninaowaona wana wafuu ya maisha ni wale wenye bouble life. Yaani wanafanya kazi za offisini lakini pia wana plot vijijini ambazo hizalisha chakula cha kwao na ziada huiuza ili kuongeza kipata. Mimi mwenyewe nimeanza na experiment ya heka moja ya mpunga. nikiona inalipa naongeza zingine. Ila kijijini siendi hata kwa dawa. tutabanana hapahapa. Mwanangu komaa hapahapa cha msingi panua wigo wa mapato. Mishahara yetu kwa sasa ni hand to mouth basi no maendeleo!
 
wewe una maisha mazuri sana mpendwa ila hujitambui na ndio maana huridhiki. nimeona mahali unasema matumizi nyumbani kwa siku 8,000/-! mbona hapo unaishi kifalme kabisa? uliza wenzio kwa siku wanatenga kiasi gani kuacha nyumbani? utashangaa kuwa karibu nusu ya watanzania wote huacha si zaidi ya 3,000/- ya matumizi kwa siku na hiy ni kwa ajili ya unga, mafuta ya taa, ya kula, maharage, na viungo vyake, na on top of that wana vibanda vyao.

kwenye ofisi ninayofanya mimi (ya serikali) madereva na wahudumu wote wanavibanda vyao na walishajikomboa na nyumba za kupanga na wote hawa ni wa kima cha chini achilia mbali nyongeza za mishahaa za kila mwaka (JK akipenda), yaani hata pendekezo la TUCTA la 350,000/ wanalimezea mate. but wana furaha na courage ya kusonga mbele! sasa wewe una 840,000/ nyumbani kwako kila mwezi kisha unataka kuutupa na kurudi kijijini?

hebu muogope Mungu ndugu yangu, usitamani magari ya watu au kitu chochote usicho na uwezo nacho. mshukuru Mungu kwa kila alichokupa hata kama ni kidogo na usaidie wasio na uwezo kwa kadiri ya uwezo wako, hapo ndipo utakapoona furaha ya maisha na baraka za Mungu zikiongezeka maishani mwako.

kwa kweli mi sioni sababu ya kukata tamaa na maisha kiasi ulichofikia

pia ni vizuri ukajiendeleza kielimu, elimu ni njia ya mkato ya mambo mengi. ukistruggle kuongeza kipato chako mara kumi unaweza kustruggle hadi mwisho wa maisha yako bila kufikia lengo hilo, ila ukiamua kusoma, ni kiasi cha miaka mitatu au minne tu utafikia lengo hilo. tena hata wpte na mkeo mnaweza kwenda shuleni mkaomba mkopo HESLB kulipia masomo yenu na baada ya miaka mitatu/minne hivi, wote mnaona maisha katika mwanga bora! hebu wekeni akili kichwani hapo.

mbarikiwe

Thanks, nimeona kuna baadhi ya vitu vya kufanyia kazi hapa. ushauri mzuri.
 
Wanaume tumeumbwa.. mateso.. mateso kuhangaikaa! (tafuta hii CD ya Idd Moshi - RIP).

Fuso acha kulalama jipange uzuri tu na si kweli kwamba wanaokwenda kijijini ni kwa vile maisha yamewashinda town.
Kama umeshindwa kupambana na changamoto za town haimanishi bush utakuwa na akili tofauti na sasa.

Unakipato kizuri sana wewe na wala huna haja ya kudunduliza mtaji wa laki sita (kutafuta mtaji wa 600,000 wakati unamake 542,000 ni utani.
Unadhani mtaji wa 600,000 utakupa faida gani??

Wewe ni kati ya watanzania wanaokopesheka: Chukua salary slip yako, Barua ya mwajiri kisha nenda benki yoyote yenye kutoa personal loans. Kwa mshahara wako una uhakika wa kupata up to millioni 5, ambao ni mkopo wa miezi 36 ukirejesha kitu kama 175,000 kwa mwezi.
Kwa hela hiyo waweza kununua:

Option 1. Bajaji yenye kuingiza karibu 500,000 kwa mwezi ukitoa marejesho ya mkopo utakuwa na ziada ya kama 300,000. Utahitaji another 10 months kuongeza bajaji ya pili.

Option 2: Nunua pikipiki ya muguu mitatu lakini ina tank la maji. Fanya biashara ya maji maeneo ya Makongo, Kimara, Goba n.k ambapo utakuwa unatengeneza faida ya zaidi ya 25,000 kwa siku. Sitoshangaa kama utatengeneza milioni moja kwa mwezi ambayo itakupa kipato sawa na mnachopata sasa.

Zingatia maoni ulopewa ya kuishi ndani ya kipato chako. Fanya manunuzi ya vyakula kwenye masoko yetu sio ukimbilie mlimani city. Maduka ya jumla wanauza nafaka na jamii ya kunde zote kwa pungufu ya mpaka 35%.

Usitishike na wenye magari, wengi ni mikopo ya mabenki bahati mbaya wananunua magari ya kutembelea (peer pressure).
Soma vitabu ili kuamsha hamasa ndani yako. Robert Kiyosaki (Rich Dad Poor Dad) ana-define Asset as Something that puts money in your pockets sasa kama hizo Rav4 haziwaingizii kitu jua ni liability tu na epuka kunasa kwenye mtego huu.
 
Wakuu Maisha ya Mjini yamenishinda, yaani nikiangalia kipato changu na majukumu niliyonayo naona siwezi kabisa.

Maisha kama haya naona afadhali yale maisha niliishi kwa wazazi wangu enzi za mwalimu pamoja na kuwa babangu alikuwa mkulima lakini tulienda shule na tuliishi maisha mazuri.

Mimi sijui wenzangu mnaishije? mnapata haya machungu nayoyaona mimi? nasimama asubuhi kituoni kwenda kazini naona magari yanapita tu huku mmefunga vioo hivi kweli mna matatizo kama yangu kweli? Hivi nyie pesa mnazipata wapi? mbona najiona mpweke katika nchi yangu hii?

Wakuu siyo siri natafakari kama mambo yakizidi kuwa magumu basi nitafute nauli nirudi kwetu angalau huko nitakuwa na uhakika wa kusogeza siku.

Kipato changu wakuu ni Tshs 542,000/- Nina Mke na mtoto mmoja (5), nimepanga nyumba viwili na sebure - Mambo yamegoma kabisa.

Nipeni ushauri nateketea mtanzania mwenzenu.
Wakati nasona hili bandiko lako, kichwani alinijia yule jasiri wa Tunisia-msomi aliyeamua kujitia kiberiti. Anaitwa Mohamed Bouazizi. Mcheki hapo chini

_50600918_010913837-1.jpg


Kwa kuwa watanzania wengi hali zao n kama hiyo yako, ukilianzisha wengi tutajumuika nawe na kwa mtaji huo tutakuwa tumepatia pa kuanza kuuondoa utawala huu madarakani. Unasemaje
 
Ha Tshs 542,000/- mbona nyingi sana mie napata 233,415/= na ninaishi dala dala kwa sana. Pole mwaya
 
Mkuu hii post imeniumiza sana kwani umeandika kwa hisia kali na hope ni ukweli. Kimsingi unapaswa kujitahidi kupunguza matumizi hasa ambayo ni WANTS na kubaki na only NEEDS na pili jitahidi mkeo umtafutie kazi ya kuwaingizia kupato (ikiwezekana mkeo asuggest mwenyewe). Jitahidi kupanga uzazi kwani ukiwa nao wengi (si mbaya ila) kwa muda mfupi itakuwia vigumu kuwatunza.

Mwisho jitahidi kuwa unaangaliaangalia kazi nyingine ambayo inaweza kukulipa zaidi na usiiache hiyo kazi yako hadi umepata uhakika wa asilimia mia kwa mia kuwa una nyingine ya maana zaidi!
 
Hapo kazini hakuna chance ya kuiba? :usa2:

kaka hii njia yako si nzuri kabisa ingawa nina full access ya store's hapa kazini, ila naapa siwezi itumia sababu haitanitatulia matatizo yangu kwa ujumla wake, nitadokoa leo na kupata chakula cha siku mbili tatu then narudi palepale kudokoa tena na tena mwishowe zinafika zile siku arobaini. Mkuu mimi naangalia future zaidi ya familia yangu hasa hasa huyu dogo wa miaka 5.
 
KAZINI KWAKO hakuna account ya madeni ya nje (EPA) ?

huna NDUGU ANAYEFAHAMIANA NA dOWANS au Kagoda?

Huna mtu anaweza kukupa connection na meremeta au richmond?

Pole sana, kama vipi wewe songa tu kijijini waache mafisadi watanue mjini au kama una hasira kama mimi tuungane tuwa - Misri na kuwa - Tunisia hao wezi wetu!
 
Mshahara wako mkubwa sana kwa walio wengi hapo Dar..Tembelea viwanda vya nguo kama URAFIKI..NIDA..KTM au viwanda vyote vya Wahindi na Wachina hapa Dsm ndo utajua wewe ni Managing Director katika viwanda hivyo.Kwa hiyo tafuta mradi mpe mama afanye hapo nyumbani au atafute vinguo na khanga Kariakoo akopeshe akina mama kwa mwezi baadae utoka tu..Mama asiwe na aibu alafu na wewe ondoa WIVUUUUUUUUUU....:hand:
 
kwa kipato cha shs 542,000 hutakiwi kulalamika. Kuna watanzania kama 85% ambao wanapata 1/4 ya unachopata (135,000) na wanaishi na familia zao watoto wa3 and above na bado utakuta ana kibanda chake charambe, kongowe, kitunda au kipate.

Wewe una mke na mtoto mmoja na unatumia daladala unalalamika nini. Nakushauri kuwa na vipaumbele, acha makundi ya starehe kama ulevi. Uzinzi then hicho kipato kinaweza kukutoa. Hebu tufanye mchanganuo hapa chini.

Tshs 542,000/=

1. Kodi ya nyumba shs 100,000
2. Chakula nyumbani shs 150,000
3. Chakula kazini shs 60,000
4. Nauli ya dala dala 30,000
5. Mengineyo shs 100,000

jumla ya matumizi ni shs 440,000 hivyo unabaki na akiba ya 102,000. Ukitunza hii akiba kwa miezi sita unaweza ukampatie mke wake mtaji wa shs 612,000 baada ya miezi sita na mkaanza mkakati wa kununu ka plot gongolamboto.

Chukua huo ushauri na usirudi kijijini utajuta.
nakauunga mkono mkuu, kwa mshahara wake anaonekana yuko juu kama ni take home basi huyu mshahara wake(nominal wage) ni kama 700,000. Akope hata mkopo benki ya posta anaweza kupata 6m na watamkata kama 180,000 kwa mwezi sii mbaya akanunue plot ya 1,500,000 zitakazobaki ajenge msingi utakamalika then kila mwezi atafute kama lakin na nusu anunue tofali na mchanga kidogo dogo apandishe vyumba wiwili taratibu.hakuna mtu anaeweza kuwa na cash ya kujengea labda awe fisadi.mambo ya harusi nk hakuna kuchangia,sasa ukilalamika ww na mwalimu au karani mdogo au mhudumu atasema nini? Pia kwani ofisi yako haina allowance ndogo ndogo labda vikao vya hapa na pale(real wage? Jitahidi ndugu kufanya hivo usilale.kama hapo mnapokaa kodi ni kubwa hamieni gongo la mboto huko huko nyumba ni cheap na utapata kiwanja au tafuta viwanja barabara ya bagamoyo ukishavuka tegeta kule vipo na ni rahisi zaidi. Sasa yawezekana unakaa sinza kila siku uko bar na kodi huko ni kubwa lazima maisha yawe magumu.


 
Ndugu yangu hayo ndo maisha ya serikali ya sisiem. Chama chetu kinachotuongoza watu waliahidiwa maisha bora nazani kwa miadi ya sisiem HAYO NDO MAISHA BORA.
 
Kwa mara ya kwanza leo nime appreciate kwamba JF ni shule, pili naunga ushauri wa realman, ukiufuata utakutoa maramoja.
Kipato cha laki nane kwa mwezi ni kikubwa sana. Lakini chek kosa lako, lunch ya buku tano na wife buku tano, bado home inaenda buku 8. Kwa mshahara wako una uwezo wa kukopa sh 6m. Ukizipata nunua boda boda 5. Tafuta watu 5, waambie kwa siku elfu 10, matengenezo juu yao, baada ya mwaka zinakua za kwao. Hapo lazima utapata pesa yako, na wao watazitunza wakijua zinakua za kwao soon. Haya tupige hesabu hapo. 300dys*10,000=3,000,000 mara piki pik 5=15m hapo tumeondoa 65dys*10,000=650,000 mara pikpik 5 sawa na 3.25m hizo tuziite unforeseen costs. Baada ya mwaka unawakabidhi za kwao unanunua zingine unalipa deni huku ukipanga mipango mingine.
 
kikubwa hapo mtafutie mkeo kabiashara kadogo kakumkeep bzy ili kuongeza kipato home , yaan i hate familiez ambazo mwanamke anakaa tuu km golikeeper home anasubiri kuletewa hasa ktk situation hii ambayo unalalamika maisha magumu wkt option ya mkeo kutafuta kipato ipo
 
Back
Top Bottom