Maisha ya usingle mother je, how do I cope?

Naandika post hii nikiwa sijui pa kuanza, il a kwa kifupi tu, nimeanza maisha mapya ya kuwa single mother.
mimi na baba mtoto havijawork out kwa kweli na imenibidi nifanye maamuzi magumu. ni mwanaume nimekuwa nae kwa muda wa miaka saba ila hatujaoana, tumefanya mambo mengi ya maendeleao pamoja,ila gafla tabia yake ikabadilika akawa ni mtu wa kunigombeza bila sababu, chochote nikifanyacho kwakwe ni kibaya,lugha anayotumia kwangu akiwa na hasira ni mbovu, ila at the same time anasema ananipenda,nimekuwa ni mtu wa kuumia moyo kwa muda wote huo,najiuliza ni kupenda gani kwa namna hiyo.

Hivi karibuni nimeamua isiwe tabu kila mtu aendelee na ustaarabu wake,yeye amekuwa akitumia mtoto kunisema nina roho mbaya, sina huruma na maneno kedekede,ila kusema ukweli nimevumilia vya kutosha na sasa nimeona basi inatosha, ninampenda ndio na ingetokea miujiza abadilike ningemrudia ila ndo hivyo.kwa hasira amegoma hata kumuhudumia mtoto anasema akifika miaka saba nimpe sasa hivi akimuona atasikia uchungu kisa mimi simtaki.

Kwa wenye uzoefu jamani naanzaje kuishi maisha ya usingle mother wakati kila siku lazima mtoto aulizie daddy au hata akilia atalia daddyyy dadyyy,nitakuja kumwambia nini akiwa mkubwa?na je nikija kuanza mahusiano mengine mtoto atanionaje?

Ili kudumu lazima uvumilie, kuachana si suluhu ya matatizo ni mwanzo wa kupata matatizo mengine. Lugha chafu za mumeo zinajadilika kwakuwa ktk miaka saba umekuwa nae unaweza kumbadilisha kwa kumpa upendo na kuonyesha wewe ni mama bora kuliko wanaompa kiburi na dharau huko nje.

Dhambi ya utengano ni mbaya itaendelea kukufuata popote uendapo hutoweza kutulia na mwingine kwa kuwa sababu za utengano haziishi.kuwa mvumilivu na simama imara usiyumbe.mshirikishe mungu nae atalinda usijiamini kupita kiasi tambua na mpe mungu akupe busara na hekima nawe utashinda.
 
Dear Noella, pole sana kwa yaliyokukuta.

Ninachoweza kusema ni kuwa mshukuru Mungu kwa hayo maisha unayoishi sasa, Mshukuru Mungu kwakuwa amekupa mtoto ambaye ni faraja tosha katika maisha yako.

Ungeweza kuwa kwenye hiyo ndoa/mahusiano na vipi kama ungekuwa huna amani?? Nina imani kuwa haikuwa mpango wa Mungu ndo maana mkatofautiana, kilichobaki ni wewe kujikbali.

Unahitaji ku accept hiyo hali ya u-single parent, na ujue siyo dhambi kuwa singo parent tho kuna watu wengine wanamtazamo tofauti sn.

Naomba kukuambiwa watu wengi wamelelewa na singo parents, wengi wanatumia hata majina ya mama zao kwakuwa baba zao hawakuwalea na wako mbali mno mno kimaisha ! Kikubwa ni wewe kumjengea mtoto wako msingi bora wa maisha kwa kumpa elimu bora.

Kama umeajiriwa, fanya kazi kwa bidii, kikubwa somesha mtoto wako, yaani ni heri ujinyime lakini mtoto wako apate elimu bora. Kwa Neema ya Mungu utapata mtu mwingine ambaye atakupenda na kuishi maisha ya furaha wewe na mtoto wako.

Pia Jiulize, je family yako imelipokeaje hilo? kama wamelipokea vizuri huna haja ya kupata wasiwasi maana hao ni watu muhimu pia , ingekuwa wao wanakuchukulia tofauti ingekuwa mbaya lakini kama wamekuelewa haina shida.

Maisha ni magumu ila ukisimama huku unamtegemea Mungu, hakika utasonga mbele bila matatizo. Kikubwa ni kutokumwonyesha mtoto kuwa nyinyi wazazi mna matatizo.
 
Ili kudumu lazima uvumilie, kuachana si suluhu ya matatizo ni mwanzo wa kupata matatizo mengine. Lugha chafu za mumeo zinajadilika kwakuwa ktk miaka saba umekuwa nae unaweza kumbadilisha kwa kumpa upendo na kuonyesha wewe ni mama bora kuliko wanaompa kiburi na dharau huko nje.

Dhambi ya utengano ni mbaya itaendelea kukufuata popote uendapo hutoweza kutulia na mwingine kwa kuwa sababu za utengano haziishi.kuwa mvumilivu na simama imara usiyumbe.mshirikishe mungu nae atalinda usijiamini kupita kiasi tambua na mpe mungu akupe busara na hekima nawe utashinda.

hamna shida ya kuishi sigle mother endapo una uwezo wa kutafuta. binafsi nina mabint wa2 fist yupo fm4 na last std3 wanaenjoy life kama kawaida na wanafanya vizuri shuleni. so nina uzoefu wa miaka 15 na life inasonga mbele. usiogope dunia ndivyo ilivyo take it easy
 
Kwanza napenda kukupa pole Noella.
Ninachokushauri do take care of our kid and whenever necessary tell the kid the truth that dad " dad left us when you was......... years old. he/ she'll understand. hakuna kitu kibaya kama moja kati ya wazazi kumsema mzazi mwenzie kwa mtoto. sijui mtoto wako ana miaka mingapi, lakini unapaswa kumwambia ukweli na kama unajiweza vizuri muhudimie mtoto wako vizuri ili asiathirike na kutengana kwenu.

Na huo mshenzi we achana nae siku mtoto akifikisha miaka saba hakuna kumpa!!!!!
 
Dada pole sana...
Situation kama hii iliwahi kumkuta mama nikiwa mdogo
na mama alichukua uamuzi kama wako na maisha yalisonga vizuri kabisa hata hata pale mama alipopata kuchumbiwa alinishirikisha na aliolewa na mtu mwingine na wanafurahia maisha
yao hadi leo na mimi namheshim
kabisa kama baba wa kunizaa
so usipoteze muda kabisa na huyo mshamba sababu he does nt respect your feelings.
Tulia then kuwa bussy na kutafuta
hela utapata anaekujali dada.
 
Asanteni wapendwa kwa ushauri wenu,napata faraja ninapowasoma.

Cha kushangaza sasa hivi when am fed up with his behaviour yeye ndo anasema ananipenda,eti alikuwa hajui maana ya kupenda mpaka alivyouliza kwa rafiki zake. Nashukuru sana Mungu nimeweza kutoka kwenye haya mahusiano maana nimeteseka mno.
 
Ndoa haivunjiki? hata itangazwe ndoa mwanamke kama huyu will end up in the same situation!!! ni design ya wale wanawake wa beijing ''tunaweza" "naweza type"

rate ya single mothers inakua kwa sababu wadada wamekuwa liberated wanasahau nini maana ya mwanaume

Hivi kwani maana ya mwanaume ni nini...?!!

Sent from my BlackBerry Smartphone
 
huyo mwanaume hajielewi, hebu songa mbele na maisha yako...... mwanaume unatesa mpenzi wako kwa maneno ya kijiweni? hawezi kujisimamia? ndo awe baba huyo na kichwa cha familia?

nyumba na fedha zinatafutwa, hebu tafuta utajenga tu...
kikubwa ni kumlea mwanao, sidhani kama ukiwa kwenye uhusiano wa kupigwa na kutukanwa kuna malezi bora utakayompa mtoto zaid ya kumfundisha matusi na kutokujiamini....





Wapendwa, asanteni kwa michango yenu.

Kusema ukweli mpaka nimefikia maamuzi haya nimevumilia sana.Ndani ya miaka hiyo saba kwa miaka mitatu mimi nimekuwa ni mwanamke wa kunung'unika tu mara nikutane na texts za ajabu akiandikiana na wanawake,pale napomuhitaji siku zote amechoka au amelewa,kugombezwa,kupigwa pasipo sababu za msingi halafu the next day ataomba msamaha eti alisikiliza maneno ya kijiweni kuwa mwanamke akipigwa ndo anakuwa na heshima.

Na pia katika muda wote huo hatujawahi kuishi pamoja,kila mtu anaishi kivyake ila tu numba tulisaidiana kujenga na anaishi yeye kwa sasa.najiona mwenye mkosi kwa maana haonyeshi mapenzi kwangu na amekuwa akisema kuwa yeye hapendi ila anatamani. kila akinipigia simu kw amfano sijaisikia akipiga tena ni ugomvi nilikuwa wapi na nani?najiuliza kwnaini aniwazie vibaya yawezekana ayawazayo niyo ayafanyayo. kwetu wanamjua na kwao wananijua,na kila siku akiulizwa maswala ya ndo anapeleka mbele akisema bado hajaaccomplish mambo mengi.

Kuna aliyesema kuwa mimi ni design ya wale wanawake wa 'beijing' la hasha, mimi ni mwanamke ninayependa nisipopendwa, kipindi cha nyuma tuliwahi kuachana kwa muda wa mwezi mmoja kwasababu ya maneno yake ya kejeli na kuniambia kuwa hakunipenda alikuja kwangu to prove a point to his friends but akajikuta yupo tuu..ila mimi kwa kumuwaza mtoto nikaona nimrudie,lakini naumia,sijui nielezeje mjue kuwa nina machungu kiasi gani yanayosababishwa na mapenzi haya. kila nikisema simtaki ananiambia wimbo wa taifa na sina ujanja wa kumuacha eti nisipompenda yeye nitampenda mwanaume gani. ni mambo mengi sana yanayonipelekea nifanye maamuzi haya,naandika post hii machozi yananitoka maana hata asubuhi hii binti yangu kataka kuongea na daddy kwenye simu.sijui ni jinsi gani nitacope na situation hii kwa kweli.
 
jamani pole sana! give yourself tym to heal, zoea hiyo hali, uambie moyo wako kuwa without him U CAN REALY SURVIVE, kip yourself busy kama huna kazi nenda hata shule, tafuta hausgal ili upate muda wa kukaa na rafiki zako and exchange ideas, PENDEZA SANA, hata ikitokea umekutana naye kwa bahati mbaya asipate sababu ya kuongea. jiendeleze kibiashara ili ajue u can stand with your own feet and WITHOUT HIM! SALI KWA BIDII NA UMUOMBE MUNGU AKUONGOZE! Believe me utamsahahu, tena utakuja kupata mtu ujione muda wote huo ulikuwa mjinga na umepoteza muda wako kwa mtu asiyedeserve! pole na yatapita! MBIA MOYO WAKO KWANZA KWAMBA HUMPENDI NA HUMTAKI TENA, NUIA KABISA!
 
NDIO MAANA Smile akisoma haya mambo, hatakagi kusikia habari za ndoa! lol, hebu tupa kuleeeeeeeee hakufai hata kukusindikiza toilet tu, achilia mbali kuwa naye!
 
Last edited by a moderator:

ni ngumu noella, ila piga moyo konde, utavuka tu hilo...





Asante BD,

Kuhusu kumuhudumia mtoto nitaweza bila kumpeleka ustawi wa jamii,ingawaje itabidi tu nimuhamishe shule mana aliyopo kwa sasa ni expensive kidogo sitoweza kuafford peke yangu. Nitajitahidi kumlea malezi yaliyo bora ila ninapata mawazo mengi sana baadae nitamjibu nini akiniuliza what happened between me and teh daddy, she is only 3 yrs now ila anampenda sana baba yake,tangu nifanye maamuzi haya sasa ni wiki mbili na nimekuwa nikimdanganyadanganya tu sitaki amchukie baba yake. na amekuwa akinitext kuwa ameanza relationship nyingine na blabla kibao mi sijamjibu.
Naomba Mungu anisaidie kwenye hili.Mapenzi yanauma jamani asikwambie mtu,mmh.
 
Last edited by a moderator:
Ndoa/mahusiano ni kitu kigumu sana especially kama ninavyosema kila siku wengi wa hawa wapendanao ambao mwisho wake unakuwa na misukosuko wanakuwa hawakupendana bali walitamaniana,inawezekana ni kwa uzuri,kwa pesa,kwa mali,kwa familia wanazotoka(wealth),kwa kuwa watu wanamsifia kuwa ni fundi wa sex,au maungo yake(ya ndani/ya nje),uongeaji wake nk,hivi vitu vinawa-cost sana jamani,ok kwa ushauri wangu kama umegundua kosa,make up your mind na anza kumtafuta yule ambaye mtakuwa mnapendana kwa dhati,ila ujue it's not that much easy inawezekana pia usimpate or else go back kwa yule yule for the sake of you child.ACHENI TABIA YA KUTAMANI BADALA YA KUPENDA,na usimpende mtu kwa kushauriwa it must be from your own heart.
 
Nyalotsi unaweza kutupa sababu ya wewe kutooa mwanamke alolelewa na single mother?

wengi wao wamezoea kusikia mama zao wakilalamika,aah,mwanaume kitu gani? Mbona mi nimewalea mwenyewe? Na maneno mengine ya aina hiyo ambayo yana negative atitudes towards wanaume. Hivyo akiingia kwenye taasisi ya ndoa ukimkosea kidogo tu, anajua, ohooo..ndo wale wale! Hata kwa kosa ambalo ni la kurekebishana. Wengi wao ukikaa karibu nao utasikia kauli zao za kuonesha dharau kwa wanaume wakirefer kwamba mbona mama zao waliwalea peke yao hivyo mwanaume siyo chochote. Kuna wadada kama wawili nimesoma nao ambao nilikuwa karibu nao sana nilikuja gundua baadaye kwamba mama zao waliachana na baba zao na kuwalea wao as a single parent. Wana dharau mpaka hata we unayeongea nao muda mwingine unawakwepa.
 
Pole sana noella na matatizo yaliyokukuta; kila la kheri katika kuweka sawa mambo yako. Kikubwa uwe mvumilivu na subira. time heals everything.
 
Nyalotsi unaweza kutupa sababu ya wewe kutooa mwanamke alolelewa na single mother?

aafu single mother aliyefiwa na mume ni tofauti na aliyeachana na mume. Mwenzako akiulizwa na mtoto wapi baba atamjibu alifariki, we utamjibu nini? Mnatufichaga watoto aafu baadaye tunaanza kuhangaika kuwatafuta. Mtu ambaye hajafa huwezi kumficha. Aafu unajua kumfanya mtu mwenye negative atitude kukipenda kitu ambacho amekua akisikia mabaya tu kuhusu kitu hicho ni tabu sana. Utatumia nguvu nyingu kumcontain mtu abadili mawazo yake badala ya kufanya maendeleo. Acha single parented people wawe single parents kama kina monalisa. Ni wachache wenye misimamo ya kuwa tofauti na mama zao kwa kuona wao ndo walikuwa na makosa. Nikimpenda msichana lazima nihakikishe nimejiridhisha na familia yao.
 
Ulichoongea kina ukweli mkubwa. Wamama wengi bila ya kujua wana train watoto wao kufuata maisha wanayoishi; kitu ambacho sio fair.

Nina rafiki yangu alizaliwa nje ya ndoa, na hakuwahi kaa na baba yake. Mama yake alikuwa anafukuza kiaina kila boyfriend aliyetaka kuwa serious na mwanaye. Mama anajua kubonda sijaona mfano. Alikuwa anamwimbia mwanae kila siku; wanaume hawana mpango wewe soma; elimu dio mume wako wa kwanza. Yule dada alishamshtukia mama yake kuwa ana mlostisha (mama mwenyewe anabadili tu waume za watu) lakini amini usiamini; wamama wana power ya ku controll watoto. Huyu dada sasa ana masters na kazi nzuri sana; na mama yake yuko very proud of her. Lakini hajaolewa na ana 37 year. Aliwahi pata ujauzito; sijuhi wa nani; bahati mbaya mtoto alikufa.

Cha muhimu single mothers wajifunze kutokupandikiza chuki kwa watoto wao; wawaache wa experience maisha wenyewe si kuwa tayari na negative attitude ya ndoa kwani maisha yanaweza kuwa jinsi unavyoyadefine. (predispositioning)


wengi wao wamezoea kusikia mama zao wakilalamika,aah,mwanaume kitu gani? Mbona mi nimewalea mwenyewe? Na maneno mengine ya aina hiyo ambayo yana negative atitudes towards wanaume. Hivyo akiingia kwenye taasisi ya ndoa ukimkosea kidogo tu, anajua, ohooo..ndo wale wale! Hata kwa kosa ambalo ni la kurekebishana. Wengi wao ukikaa karibu nao utasikia kauli zao za kuonesha dharau kwa wanaume wakirefer kwamba mbona mama zao waliwalea peke yao hivyo mwanaume siyo chochote. Kuna wadada kama wawili nimesoma nao ambao nilikuwa karibu nao sana nilikuja gundua baadaye kwamba mama zao waliachana na baba zao na kuwalea wao as a single parent. Wana dharau mpaka hata we unayeongea nao muda mwingine unawakwepa.
 
Naandika post hii nikiwa sijui pa kuanza, il a kwa kifupi tu, nimeanza maisha mapya ya kuwa single mother.
mimi na baba mtoto havijawork out kwa kweli na imenibidi nifanye maamuzi magumu. ni mwanaume nimekuwa nae kwa muda wa miaka saba ila hatujaoana, tumefanya mambo mengi ya maendeleao pamoja,ila gafla tabia yake ikabadilika akawa ni mtu wa kunigombeza bila sababu, chochote nikifanyacho kwakwe ni kibaya,lugha anayotumia kwangu akiwa na hasira ni mbovu, ila at the same time anasema ananipenda,nimekuwa ni mtu wa kuumia moyo kwa muda wote huo,najiuliza ni kupenda gani kwa namna hiyo.

Hivi karibuni nimeamua isiwe tabu kila mtu aendelee na ustaarabu wake,yeye amekuwa akitumia mtoto kunisema nina roho mbaya, sina huruma na maneno kedekede,ila kusema ukweli nimevumilia vya kutosha na sasa nimeona basi inatosha, ninampenda ndio na ingetokea miujiza abadilike ningemrudia ila ndo hivyo.kwa hasira amegoma hata kumuhudumia mtoto anasema akifika miaka saba nimpe sasa hivi akimuona atasikia uchungu kisa mimi simtaki.

Kwa wenye uzoefu jamani naanzaje kuishi maisha ya usingle mother wakati kila siku lazima mtoto aulizie daddy au hata akilia atalia daddyyy dadyyy,nitakuja kumwambia nini akiwa mkubwa?na je nikija kuanza mahusiano mengine mtoto atanionaje?

Mmmh nitasoma baadae comments zote nione watu walivyokushauri, ila binafsi sijafurahia uamuzi uliochukua unless umeficha ukweli halisi
 
noela pole sana ma dear. Nimesoma comments za waliochangia nimeona wamekushauri vizuri sana baadhi yao.

Naomba nikuongezee haya machache kama mwanamke mwenzio.

Uamuzi uliochukua siyo mbaya,hata kidogo. Haitakiwa hata siku moja uishi kwa kuwaza jambo moja tu tena lenye kusononesha miaka nenda miaka rudi. Hii kwangu mimi ni mwiko. Tatizo litokeapo tumia busara kulitatua kisha sahau piga hatua kwenda mbele ukiwaza mengine.

makosa uliyoyafanya nyuma hayana mantiki wala usijilaumu hata kidogo simple ni kwamba hukuwaza vizuri so there is no need of talking about it. Anachokifanya huyu mumeo ni tabia mbaya za kibaba ambazo baadhi ya wababa wasio na hekima huzitumia na kutufanya tuwone akina baba wote kama watu wabaya. usijali juu ya hili wewe siyo wa kwanza.

chakufanya sasa hivi:

mwanao wa miaka 3 muishishe maisha ya kawaida yasiyokuwa ya gharama sana hadi ushindwe kuyamudu baadae halafu aanze kulalamika kumtaka baba yake.

Kumbuka inquisitive mind ya mtoto inaanza kukua at thi age so its better to tell her the reality kama atauliza hii itamfanya apunguze maswali na pia haita muumiza kwakua hajui umuhimu wa kuwa na baba per-se ingawa huwa anapenda kucheza naye mara nyingi. so ukiweza kumfanyia haya hatakusumbua. kuna hatar ya kumficha nayo ni hii utakuja kumpa machungu kwa kitu ambacho kilisha pita zamani sana na atajenga hisia za kuongopewa mambo mengi na wewe mama yake kitu ambacho ni kibaya sana.

usimnyime baba yake kumuona mtoto kama atataka ila usimpe mtoto manake hataweza kumlea kwa stail ya huyu mwanaume. Tena usimjengee tabia ya kutoka sana na baba yake atakusumbua sana manake watoto ni rahisi kuwafeed information ambazo zinaweza kuwa destructive.

organize your self, tulia, lea mwanao kwa hekima sana ukijua kuwa unachangamoto ya kukosa a second hand but its not a big deal kama ukiamua. Jua kuwa huu siyo mwisho wa maisha yakwako au wa mwanao. wala kulelewa na mzazi mmoja hakumfanyi mtu kuwa nusu mtu au kutokulea mtoto ukiwa na baba yake hakukufanyi kuwa nusu mtu.maisha ya mwanao au ya kwako hayatakuwa na excuse ya kuwa mzazi mmoja au mtt anayelelewa na mama so kila kitu kiapatikana kwa binadamu wote na hapa ni juhudi binafsi tu zinazohitajika na nidhamu ya maisha. hivyo elewa kuwa unatakiwa umlee huyo mtoto ajue kuwa anatakiwa asome aje ajitegemee na maisha hayata mpa excuse ya kulelewa na mama tu.

wewe kwa upande wako futa hisia wala usiwaze kurudi nyuma once umeamua kuondoka just quit for good ever, jipange ma dia mengine nitakupm
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom