Maisha ya dada zetu wakiwa vyuoni

Dogo Tundu

JF-Expert Member
May 25, 2009
448
189
Mi mwenzenu nina tatizo moja na wanachuo.

Hivi kwanini, utakuta dogo kamaliza kidato cha sita akiwa na maadili mazuri tu kutoka kwa wazazi na walimu wake wa shule but akifika tu chuo within one to two month anakuwa kama si yule aliyekuwa akiambiwa mambo utamsikia akisema mambo kwa yesu?
hiyo ni moja, mbili kwanini wanapenda kuishi maisha ambayo siyo yao? Nina maana kuwa wanapenda maisha ya juu ambayo hata ukoo wake hawajawahi kuishi maisha hayo.

Wanakula chips kuku, mbuzi, kiti moto na mazagazaga kibao ya gharama tena maeneo ambayo ni expensive sana kila siku, pia wanataka kuvaa expensive kuwazidi hata mastaa wa amerika na ulaya lakini ukuwaona baada ya kumaliza masomo yao hupauka kama mhogo wa kiangazi majumbani mwao tena kuliko hata hawajaanza masomo ya chuo.

Nisaidieni wadau, hivi hii tabia ya wadada zetu kupenda maisha ya juu wakiwa vyuoni inatokana na nini? Na kwanini wanafanya hivyo hali wakijua wanatoka kwenye familia za namna gani?
 
Wewe kwani mademu huwajui au?

Kuna demu mmoja alikua class mate wetu pale mlimani, alikua ana jibaba lake flani hivi lilikua linakamua masters ya jioni, jamaa alikua na familia kabisa yaani mke na watoto, lakini mdada alihongwa ka-starlet.

Basi siku moja mama yake binti alifariki mazee, ile kwenda kwenye msiba huko Kigamboni mbona ilikua aibu, tena aibu ya mwaka, yule binti kwa jinsi alivyokua anajishebedua utadhani anaishi masaki kwao choka mbaya kinoma, bora hata angekua anasaidia kwao basi tungemuona wa maana.

Kingine maisha magumu sana mavyuoni huko, sasa wanafunzi wako tofauti kitabaka, wapo wale kwao mambo swafi, wapo wenzangu na mie wachovu.

Sasa unaweza kuta chumba kimoja wanaishi wasichana watokao familia tofauti, mmoja anaweza kuwa na jibaba huko mtaani mara limemnunulia TV, mara friji mara sijui nini, sasa wenzake watatamani, na wao watajitoa mhanga. Amini usiamini kuna madenti wa vyuo wanajiuza mitaani.

Siku moja enzi hizo niko na shemeji/wifi yenu alikua anasoma chuo kimoja kikubwa (jina kapuni) aliniambia nikamtembelee, ebwanaeeeeeeeee hiyo room huwezi kuamini kama ni ya wanafunzi!, iko full kila kitu, nikamuuliza hivi nyie mko kusoma kweli au? Akasema ni vya mwenzake, sasa ndo ujue hapo wadada vyuoni wanamambo.
 
Sasa unaweza kuta chumba kimoja wanaishi wasichana watokao familia tofauti, mmoja anaweza kuwa na jibaba huko mtaani mara limemnunulia TV, mara friji mara sijui nini, sasa wenzake watatamani, na wao watajitoa mhanga. amini usiamini kuna madenti wa vyuo wanajiuza mitaani.

Mkuu hiyo niliyo highlight siyo yakuhitaji ushahidi milioni ni hali halisia.Mi wakati nipo chuo chetu cha bongo nilikuwa nipo mabibo hostel kwa muda wangu wote wa chuo.sasa ulikuwa unakuta mashoga zangu tukishapiga buku muda kama wa saa sit hivi wanavaa nguo zao wanaanza kushuka kwenda town sasa nikawa najiuliza hiyo ndo starehe au.Ila kwa kuwa nilikuwa uswahili nikasema heli yangu mambo ya mjini siyajui.

Kwa hiyo ndo hali halisi. Mahitaji yetu ni mengi wazazi wetu hawawezi kutumia hizo extra expenditure inabidi tuwatafute kama akina Fid hivi au masanilo watufanyie mambo.
 
Malezi Ya Watoto Wa Kike na wakiume katika tanzania hii ni wachache sana hufundishwa kukabiliana mbadiliko wa maisha kutoka hatua moja kwenda hatua ingine...wazazi wanakaba sana watoto wao mpaka dakika ya mwisho.Mtoto hana uhuru wa kueleza lolote hata uhuru wa kutembelea hata marafiki zake..hii ni mifano midogo ambayo huanzia toka nyumbani uko tutokako.

Ambayo sasa inapelekea mtoto sasa akitoka mikononi kwa wazazi kwa mara ya kwanza...ndipo balaa la dunia linapo anza kumfundisha...uhuru wa ajabu aupatao..
Ndio inakuwa tatizo yaani anahisi uhuuru wa ajabu ndani ya maisha yake..akiangalia uku na uku haoni mtu wa kumwambia acha hilo..hana ndugu..hata dada hana kaka..hata anasahau kidogo nyumbani....anaweza kudanganya lolote home na akasikilizwa...kwani kwa familia zingine utakuta yeye ndio wa kwanza kwenda chuo au hakuna kabisa aliye hata fikisha form four yaani hali kama hizi zinapekea kuwa na maamuzi ambayo kwa sasa yanakuwa ni kuwa hivyo kabisa...angalia hata wanao pata kazi mwanzoni...ni guudi time kwanza..then baadae ndio kujipanga..

Kwa hiyo tatizo halianzii chuoni...linaanzia home kabisa...wazazi kuwaandaa watoto kwani mabadiliko makubwa ya uhuru...kuwaandaa watoto kuanza kujitegemea..kufanya maamuzi yao binafsi...wewe mpaka f6 mtu unanuliwa nguo ya ndani huna uchaguzi unakuta tu iko home.
 
wewe kwani mademu huwahui au?
kuna demu mmoja alikua class mate wetu pale mlimani, alikua ana jibaba lake flani hivi lilikua linakamua masters ya jioni, jamaa alikua na familia kabisa yaani mke na watoto, lakini mdada alihongwa kastarlet.
basi siku moja mama yake binti alifariki mazee, ile kwenda kwenye msiba huko kigamboni mbona ilikua aibu, tena aibu ya mwaka, yule binti kwa jinsi alivyokua anajishebedua utadhani anaishi masaki kwao choka mbaya kinoma, bora hata angekua anasaidia kwao basi tungemuona wa maana.

kingine maisha magumu sana mavyuoni huko, sasa wanafunzi wako tofauti kitabaka, wapo wale kwao mambo swafi, wapo wenzangu na mie wachovu.
sasa unaweza kuta chumba kimoja wanaishi wasichana watokao familia tofauti, mmoja anaweza kuwa na jibaba huko mtaani mara limemnunulia TV, mara friji mara sijui nini, sasa wenzake watatamani, na wao watajitoa mhanga. amini usiamini kuna madenti wa vyuo wanajiuza mitaani.

siku moja enzi hizo niko na shemeji/ wifi yenu alikua anasoma chuo kimoja kikubwa (jina kapuni)
aliniambia nikamtembelee, ebwanaeeeeeeeee hiyo room huwezi kuamini kama ni ya wanafunzi!, iko full kila kitu, nikamuuliza hivi nyie mko kusoma kweli au?, akasema ni vya mwenzake, sasa ndo ujue hapo wadada vyuoni wanamambo.

Kwanini hakukauza hata hako (highlight) akajenga house ya mgongo mmoja? Nway ndio bakora za chuo hizo
 
Mkuu hiyo niliyo highlight siyo yakuhitaji ushahidi milioni ni hali halisia.Mi wakati nipo chuo chetu cha bongo nilikuwa nipo mabibo hostel kwa muda wangu wote wa chuo.sasa ulikuwa unakuta mashoga zangu tukishapiga buku muda kama wa saa sit hivi wanavaa nguo zao wanaanza kushuka kwenda town sasa nikawa najiuliza hiyo ndo starehe au.Ila kwa kuwa nilikuwa uswahili nikasema heli yangu mambo ya mjini siyajui.

Kwa hiyo ndo hali halis.mahitaji yetu ni mengi wazazi wetu hawawezi kutumia hizo extra expenditure inabidi tuwatafute kama akina Fid hivi au masanilo watufanyie mambo.

Kwahiyo ndio sababu ya msingi ya kujiuza jamani??? let us change please
 
hizo extra expenditure inabidi tuwatafute kama akina Fid hivi au masanilo watufanyie mambo.

Hehehehe mimi iwa wananiita papaa duh yaani ulaini laini kama namsukuma mlevi vile nikienda mabibo pale napoint tu nasepa nakifaa cha ukweli na cha uhakika akikiona Yo Yo au Masanilo au NN lazima wanikabe koo.
Iwa tunaita niwezeshe nikuwezeshe maisha yanasonga.
 
kaka George huyo alikudanganya vingine vilikuwa vya kwake, sema aliogopa tu,

teh teh teh teh

Rom
 
Hehehehe mimi iwa wananiita papaa duh yaani ulaini laini kama namsukuma mlevi vile nikienda mabibo pale napoint tu nasepa nakifaa cha ukweli na cha uhakika akikiona Yo Yo au Masanilo au NN lazima wanikabe koo.
Iwa tunaita niwezeshe nikuwezeshe maisha yanasonga.

ee bwana ndio!
 
Kwa kweli inasikitisha sana jinsi wadogo zetu wanavyoishi maisha ya sasa. Bahati mbaya sana na UKIMWI huu. Enzi za wazee wetu pamoja na kwamba temtetions zilikuwa si za kiivyo ila zilikuwepo cha kuhofia ilikuwa na Mimba nje ya ndoa na/au gono lakini kwa sasa ni balaa.

Ila kusema ukweli mtoa mada amesema ilivyo sie tulio katika maeneo haya tunajionea viroja kama mchvu kama mimi hapa MwanajamiiOne unaweza usiwe unaingia kufundisha maana ukishuka theatre rooms kule unapishana na magari ya nguvu ya wanafunzi wako wakati we mwenyewe hata bajaj huna!
 
nikiwa mwaka wa pili chuo hapo,kuna siku niliona kioja cha mwaka!ilikuwa ijumaa moja hivi,tulikuwa tuna mafungo na kukesha tukisali,kuabudu ekaristia(wakatoliki wanaelewa)!

.baada ya rozali kwa muda mrefu sana ,mida ya kama saa tisa hivi nikatoka pale kanisani,natembea tembea naelekea Hall five walau usingizi utoke!dah!nilikuta madada wawili na men mmoja njemba hivi ''wanafanya ngono'' kwenye mtalo.kwakweli nilimuonea huruma sana wazazi wa wale ma-binti!

Maisha halisi ya wasichana vyuoni ni huzuni
 
Wanapractice mafiga ma3 ya kipwanipwani....mmoja wa kusoma naye asiliwe kichwa....mmoja atm(mara nyingi wana umri kama baba zao)....mmoja handsomeboy(presentable wa kutoka naye)
hizi siyo hadithi...ni real. nimeona kwa macho.....watu ambao mna wachumba vyuoni jitahidini kuwa nao karibu though siwafundishi kuwa na wivu kupindukia...
 
Wasichana wengi unakuta hawaja andaliwa kuishi maisha pekee yao. Wanaume unakuta tokea ni wadogo wanapewa uhuru kidogo lakini madada huchungwa zaidi. Sasa dada huyo atakapo onja uhuru kwa mara ya kwanza ata taka kulipizia au atakua tu hajui jinsi ya kujilinda.
 
Wasichana wengi unakuta hawaja andaliwa kuishi maisha pekee yao. Wanaume unakuta tokea ni wadogo wanapewa uhuru kidogo lakini madada huchungwa zaidi. Sasa dada huyo atakapo onja uhuru kwa mara ya kwanza ata taka kulipizia au atakua tu hajui jinsi ya kujilinda.
Hii nayo ni sababu kubwa sana. Na wengine ni ulimbukeni tu
 
Hii nayo ni sababu kubwa sana. Na wengine ni ulimbukeni tu
Wengine ni HULKA tu!wanasema alivyo ndivyo alivyo.Kuna wanawake wanaamini wanapotongozwa sana na ''kutoa huduma'' sana ndio wanakuwa wanawake kamili
 
Mada nzuri sana ingawa naona wachangiaji wanaelezea zaidi uzoefu wao bila kutueleza ni kwa nini hali inakuwa hivyo. Kwangu naona sababu hizi
1: Uhuru kamili kwa mara ya kwanza. Ukiwa chuo kikuu nani anakuuliza ulikuwa wapi, na nani, ukifanya nini, hakuna rollcall. ni full kujiachia
2: Wanaanza kukumata pesa za kwao kabisa (posho ya chakula haina cha asilimia wote ni 6500/- kwa siku).
3: Wahakuandaliwa kuukabili ukweli wa maisha
4: Ulimbukeni wa vijana wetu hasa wa kike wanaodhani wamechelewa mambo mengi sana hivyo wanajitahidi kufidia muda

Sijui kama nimejaribu kutoa sababu ingaa naamini animejaribu.
 
ni Ushamba tu kuona Ukifika Chuo ndio umeibuka kimaisha...!!!...

Uhuru nao unachangia kwa kiasi Kikubwa MNO...!!! Vijana wa Kiume waliokuwa Boys tupu wakifika Vyuo Moto chini....na Mabinti waliokuwa Girls nao usiseme....Watu wa Geti kali nao mmhhh....!!!

I still believe kuwa Asasi za KIDINI bado zinajukumu la kuwafundisha Vijana Roles zao wanapokuwa vyuoni...!!!
 
Back
Top Bottom