wanajamvi nisaidieni, je ni kupuuzwa kwa mawazo ya wataalam?, Kutothaminiwa kwa wataalam? Nchi kuongozwa na wanasiasa ambao ambao hawathamini taaluma? Tanzania tunatumia fedha nyingi kusomesha wataalamu wengi ndani na nje ya nchi lakini matunda hayaonekani kwenye nyanja za kiuchumi, kisiasa na kijamii. Tunachoshuhudia ni ufisadi na uwizi wa rasilimali zetu unaofanywa na hao tuliowasomesha kwa kodi zetu. Watanzania wangapi walisomea uhandisi na wengine uchumi lakini matunda yao yako wapi? Na kama hawana faida au hawathaminiwi kwani kuharibu fedha zetu? Nafuu waalimu na madaktari ambao kazi za zinaonekana. Kwanini kadri wanavyokuwa wengi hali inakuwa mbaya kuliko jana na juzi?