tindikalikali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 4,855
- 1,117
Habari zenu wana JF, naamini wote ni wazima.
Husika na kichwa cha habari hapo juu, Mimi ni kijana mwenye miaka takribani 26. Mwaka 2006 nikiwa masomoni katika mkoa mmojawapo hapa Tanzania, nilitokea kumpenda msichana ambaye alikuwa akisoma shule jirani na ile tuliyokuwa.
Nilifanya kila jitihada za kumzoea na kumwambia yale yaliyokuwa moyoni mwangu. Hapo ndipo safari yenye utata na machungu mengi ilioanzia, huyo binti hakutaka hata kunisikia. Nilikutana na kila aina ya dharau na ukatishaji tamaa. Ni wazi alionesha kutonipenda kwa namna yeyote lakini cha ajabu niliendelea kukomaa huku nikiamini kuna siku mambo yatakaa sawa.
Hali hiyo iliendelea mpaka nilipomaliza form 6, hapa nataka kusema niliondoka mkoa huo ambao mimi sikuwa mwenyeji pasipo kukubaliwa kwa lolote.
Niliendelea kuwasiliana naye, na alikuja kunikubalia miezi miezi mitatu mbele. Tuliendelea kuwasiliana kama wapenzi japo kwa mawasiliano ambayo yalikuwa yakinipa shaka.[ningefanyeje na nilishapenda?]
mwezi october wa 2008 nilifunga safari toka DSM ambako nilikuwa nimeshaanza masomo ya chuo kikuu, na kwenda kumtembelea huyo binti. Nilijiandaa kweli kweli huku nikijua kwamba naenda kulijenga penzi jipya. Niliyoyakuta sitaki hata kuyakumbuka mpaka leo, nilikanwa na yule binti na akadai alifanya makosa kunikubalia, na moyo wake huwa unamsuta akiniita mpenzi. Sikuwa na jinsi, niliondoka nikiwa na majonzi tele, kwa kifupi aliuvunjavuja moyo wangu, nilikaa kimya pasipo kuwasiliana naye hali iliyomfanya naye akae kimya.
Baada ya hapo mara nyingi amejaribu kurudi, ila kila nilipokuwa nikimuuliza msimamo wake kwangu alikuwa akiruka kimanga
Maisha hayakusimaa, nilipiga moyo konde na kuamua kusonga mbele.
TATIZO LINAPOANZIA...
Hivi karibuni [hata wiki mbili hazijapita], nimefanikiwa kuanzisha mahusiano mapya. Huyu binti niliyenaye kwa sasa bado sijamsoma kiundani, hasa ile nia ya dhati aliyonayo juu yake, bado simuelewi elewi ila sina shaka kwa kuwa nampenda, bado nampa muda.
TATIZO ZAIDI NI HILI HAPA...
Yule binti aliyenikana 2008 anarudi tena kwa speed kubwa, anadai anatamani kuishi na mimi katika maisha ya ndoa....hizi ni sms zake za jana na leo...
"mcmamo wako wa maisha ya upendo ulonao unanivuta kuja kuish nawe je umeplan lini uishi maisha ya ndoa"....sikujibu hii sms yake, na leo asubuhi katuma hii sms...
"Mapenzi ya kweli huchukua muda kujengeka, na yakijengeka ni vigumu kuisha.)kwel nw napata hamu ya kuishi na mwanaume nahc unanifaa ktk maisha yangu,labda kama nimechelewa kufunguka moyo plz dont tell me dat im late."....
NASHINDWA KUFANYA MAAMUZI...
Huyu wa zamani nampenda na yeye analijua hilo, ila hii gia aliyokuja nayo ya kutaka ndoa na kunipenda kwasababu tu nampenda vinanitisha kidogo. Na huyu mpya sina hakika kama kweli kanipenda, maana kwa mahusiano tuliyonayo yananiaminisha hivyo.
Husika na kichwa cha habari hapo juu, Mimi ni kijana mwenye miaka takribani 26. Mwaka 2006 nikiwa masomoni katika mkoa mmojawapo hapa Tanzania, nilitokea kumpenda msichana ambaye alikuwa akisoma shule jirani na ile tuliyokuwa.
Nilifanya kila jitihada za kumzoea na kumwambia yale yaliyokuwa moyoni mwangu. Hapo ndipo safari yenye utata na machungu mengi ilioanzia, huyo binti hakutaka hata kunisikia. Nilikutana na kila aina ya dharau na ukatishaji tamaa. Ni wazi alionesha kutonipenda kwa namna yeyote lakini cha ajabu niliendelea kukomaa huku nikiamini kuna siku mambo yatakaa sawa.
Hali hiyo iliendelea mpaka nilipomaliza form 6, hapa nataka kusema niliondoka mkoa huo ambao mimi sikuwa mwenyeji pasipo kukubaliwa kwa lolote.
Niliendelea kuwasiliana naye, na alikuja kunikubalia miezi miezi mitatu mbele. Tuliendelea kuwasiliana kama wapenzi japo kwa mawasiliano ambayo yalikuwa yakinipa shaka.[ningefanyeje na nilishapenda?]
mwezi october wa 2008 nilifunga safari toka DSM ambako nilikuwa nimeshaanza masomo ya chuo kikuu, na kwenda kumtembelea huyo binti. Nilijiandaa kweli kweli huku nikijua kwamba naenda kulijenga penzi jipya. Niliyoyakuta sitaki hata kuyakumbuka mpaka leo, nilikanwa na yule binti na akadai alifanya makosa kunikubalia, na moyo wake huwa unamsuta akiniita mpenzi. Sikuwa na jinsi, niliondoka nikiwa na majonzi tele, kwa kifupi aliuvunjavuja moyo wangu, nilikaa kimya pasipo kuwasiliana naye hali iliyomfanya naye akae kimya.
Baada ya hapo mara nyingi amejaribu kurudi, ila kila nilipokuwa nikimuuliza msimamo wake kwangu alikuwa akiruka kimanga
Maisha hayakusimaa, nilipiga moyo konde na kuamua kusonga mbele.
TATIZO LINAPOANZIA...
Hivi karibuni [hata wiki mbili hazijapita], nimefanikiwa kuanzisha mahusiano mapya. Huyu binti niliyenaye kwa sasa bado sijamsoma kiundani, hasa ile nia ya dhati aliyonayo juu yake, bado simuelewi elewi ila sina shaka kwa kuwa nampenda, bado nampa muda.
TATIZO ZAIDI NI HILI HAPA...
Yule binti aliyenikana 2008 anarudi tena kwa speed kubwa, anadai anatamani kuishi na mimi katika maisha ya ndoa....hizi ni sms zake za jana na leo...
"mcmamo wako wa maisha ya upendo ulonao unanivuta kuja kuish nawe je umeplan lini uishi maisha ya ndoa"....sikujibu hii sms yake, na leo asubuhi katuma hii sms...
"Mapenzi ya kweli huchukua muda kujengeka, na yakijengeka ni vigumu kuisha.)kwel nw napata hamu ya kuishi na mwanaume nahc unanifaa ktk maisha yangu,labda kama nimechelewa kufunguka moyo plz dont tell me dat im late."....
NASHINDWA KUFANYA MAAMUZI...
Huyu wa zamani nampenda na yeye analijua hilo, ila hii gia aliyokuja nayo ya kutaka ndoa na kunipenda kwasababu tu nampenda vinanitisha kidogo. Na huyu mpya sina hakika kama kweli kanipenda, maana kwa mahusiano tuliyonayo yananiaminisha hivyo.