Usidanganyike kumfuata, utaenda kufa bure! unacheza na wanawake wewe? Ilishatokea mabibo hostel mtu kapigiwa kelele za mwizi kisa kamfumania mchumba wake na mwanaume mwinginen chumbani. Huyu bwana alipofika chumbani alimkuta mdada yupo na mwanaume mwingine, yule dada kwa kuona aibu akajifanya hamfahamu yule mwanaume wa mtaani. Yule jamaa akajaribu kulazimisha na kwa kutaja jina la yule dada. Ili kuficha aibu ya kugonganisha magari yule dada akaamua kupiga kelele za mwizi dhidi ya yule mwanaume wa mtaani. Sina uhakika kama yule mwanaume alipona maana kipigo alichokula hakikuwa cha kawaida. Mwanamke roho ya ubinadamu huwa anaiazima tu, wenye nayo wakiichukua, anaweza kukukula nyama huku unaona.Mapenzi sinema, kama unaweza mfate ukajionee kwa macho!!
Kuna watu wengine wanapenda sana ku argue about the silliest of things whereas others argue about things that are important to them...Yani huyo jamaa anashangaza sana ameisha ambiwa na mchumba wake yuko kwenye mitihan...Amesahau kama mtu anapokuwa kwenye mtihani ana focus kwenye masomo tu.Si kasha kwambia yupo bize na maandalizi ya mitihani??
MWACHE MWENZIO ASOME
Siku hizi mapenzi yamekuwa maigizo ukijifanya unampenda demu atakuumiza tu sex ndio imepewa kipaumbele. Mabinti wa chuo sio kabisa wengi wao ni vicheche wanawezana wao kwa wao. Huyo raia achana nae atakupotezea time mzazi
Sinaham na vibinti dawa ni kuwa navyo vingi kisipo pokea sim kimoja unakipigia kingine,. Mi kunakimoja kishanitesa sana asante mungu nimekisahau,.. Hela yako ndo mapenzi yako
hooooooooo solembaHii kitu imenitokea live, demu wng anayesoma UDSM mwaka wa mwisho, na tukiwa tumepanga mikakati mingi ya maisha ghafla akawa hapokei simu. Mwanzo nilidhani simu yake kaiacha mbali hasa ukizingatia mazingira ya kupanga nje ya hostels za vyuo husika, nikahisi kuwa huenda kaiacha simu room. Hivyo nikasitisha kwanza zoezi la kupiga simu, kwa lengo la kumpigia usiku, nikiamini kuwa muda huo pilika pilika zitakuwa zimeisha. Na kama atakuwa aliitelekeza simu yake, muda huo lazima atakuwa nayo, pamoja na imani yangu kuwa kuziona tu missed calls angepiga tu. Ajabu ni kwamba hakupiga, na nilipompigia bado hakupokea. Nikamtumia ujumbe bado haukujibiwa. Siku ya tatu alinitumia meseji, baada ya mimi kupiga sana na kumtumia ujumbe kuwa 'yupo bize' na maandalizi ya mitihani! Toka hapo mawasiliano yamekatika, hakuna simu wala meseji. Hivi naona ni viroja. Hivi waungwana ninyi mmesoma vyuoni wengi wenu! Katika hali ya kawaida mchumba wako au mpenzi wako akikupigia simu unaweza kubehave namna hiyo hata kama upo bize? Je, ni komedy gani hiyo ninayochezewa wanajukwaa?