Mahusiano, mapenzi, urafiki

Masanilo

Platinum Member
Oct 2, 2007
22,286
4,493
Kwanza nianze kwa kuwatakia Mwaka mpya 2011 uwe wa fanaka na mafanikio. Kwangu Mwaka uliyopita ulikuwa na changamoto nyingi sana ila nashukuru Mungu kwa yote.

Leo nitapenda zungumzia silaha zitumikazo kwenye kuangamiza mahusiano katika ndoa. Urafiki wa kimapenzi hudumu zaidi na kuwa na faraja pale tendo zima takatifu la ndoa linapofanyika kwa maridhiano ya wote. Huleta matatizo iwapo mwanamke anatumia sex kama silaha, siku akichukia basi mnapeana migongo ama mzungu wa nne. Mara nyingi wadada wanaotumia njia hii husababisha wenzi wao kutafuta wagombea wenza. Tendo la ndoa ni muhimu katika kuboresha mahusiano tafiti nyingi zimeonyesha hilo, sitaki kurudia umuhimu wa sex kwenye maisha ya kila siku. Wanawake wanaotumia Ngono kama silaha mara nyingi hawadumu kwenye ndoa zao maana hujifananisha wao na kama chombo cha burudani ambayo anaweza mpatia mteja mwingine.

Ulevi kupindukia, pamoja na kuwa na madhara kiafya pombe husababisha kuyumba kwenye suala zima la ndoa. Wanaume walevi wengi wao wamekuwa hawana uwezo wa kukidhi haja za kingono kwa wenzi wao. Wanawake waliolewa na wanaume walevi wanaongoza kwenye suala zima la cheating, tafiti zinaonyesha hivyo.

Kudumisha ndoa cha muhimu ni kusikilizana na kupeana kile roho na matamanio ya mwili yanachohitaji. Sababu za kichwa kinauma, leo sijisikii ama baba anarudi amelewa kila siku na kuishia lala sebuleni ni hatari sana kwenye ndoa.

The Most Rev Masanilo ni mtafiti huru aliyebobea katika masuala ya Mahusiano, mapenzi na urafiki
 
Kwanza nianze kwa kuwatakia Mwaka mpya 2011 uwe wa fanaka na mafanikio. Kwangu Mwaka uliyopita ulikuwa na changamoto nyingi sana ila nashukuru Mungu kwa yote.

Leo nitapenda zungumzia silaha zitumikazo kwenye kuangamiza mahusiano katika ndoa. Urafiki wa kimapenzi hudumu zaidi na kuwa na faraja pale tendo zima takatifu la ndoa linapofanyika kwa maridhiano ya wote. Huleta matatizo iwapo mwanamke anatumia sex kama silaha, siku akichukia basi mnapeana migongo ama mzungu wa nne. Mara nyingi wadada wanaotumia njia hii husababisha wenzi wao kutafuta wagombea wenza. Tendo la ndoa ni muhimu katika kuboresha mahusiano tafiti nyingi zimeonyesha hilo, sitaki kurudia umuhimu wa sex kwenye maisha ya kila siku. Wanawake wanaotumia Ngono kama silaha mara nyingi hawadumu kwenye ndoa zao maana hujifananisha wao na kama chombo cha burudani ambayo anaweza mpatia mteja mwingine.

Ulevi kupindukia, pamoja na kuwa na madhara kiafya pombe husababisha kuyumba kwenye suala zima la ndoa. Wanaume walevi wengi wao wamekuwa hawana uwezo wa kukidhi haja za kingono kwa wenzi wao. Wanawake waliolewa na wanaume walevi wanaongoza kwenye suala zima la cheating, tafiti zinaonyesha hivyo.

Kudumisha ndoa cha muhimu ni kusikilizana na kupeana kile roho na matamanio ya mwili yanachohitaji. Sababu za kichwa kinauma, leo sijisikii ama baba anarudi amelewa kila siku na kuishia lala sebuleni ni hatari sana kwenye ndoa.

The Most Rev Masanilo ni mtafiti aliyebobea katika masuala ya Mahusiano, mapenzi na urafiki

Ahsante Baba Mchungaji.
Wanaume nao wanatumia pesa zao kama silaha kwenye mapenzi...kwa njia 1 au nyingne.
 
"Nina mwezi wa 3 sasa sijamruhusu kunigusa"...!
Ni jana tulikuwa na mkasa wa aina hii ukiwa umeletwa na mdada ambaye ni family friend wetu, kisa amepata habari kuwa bwanake ambaye anafanya kazi na kontrakta wa barabara ya Arusha-Namanga, ana mahusiano na mwanadada mwingine...

Kwa ufupi ni wazi silaha hiyo ya kunyimana tendo takatifu la ndoa ni ya hatari sana...maana party inayolalamika lazima itatafuta namna fulani ya kumkomoa mwenzie kwa kuwa na mahusiano ya tofauti nje ya ndoa, halafu meli yote inakuwa inazama taratibu...
Maongezi ni ufunguo...familia zipate wakati muafaka wa KUSEMEZANA...kwa mazuri na mabaya, hapo mndipo miarobaini ya shida zote itatolewa.
 
"....Nina mwezi wa 3 sasa sijamruhusu kunigusa"...!

Ni jana tulikuwa na mkasa wa aina hii ukiwa umeletwa na mdada ambaye ni family friend wetu, kisa amepata habari kuwa bwanake ambaye anafanya kazi na kontrakta wa barabara ya Arusha-Namanga, ana mahusiano na mwanadada mwingine...

Kwa ufupi ni wazi silaha hiyo ya kunyimana tendo takatifu la ndoa ni ya hatari sana...maana party inayolalamika lazima itatafuta namna fulani ya kumkomoa mwenzie kwa kuwa na mahusiano ya tofauti nje ya ndoa, halafu meli yote inakuwa inazama taratibu...
Maongezi ni ufunguo...familia zipate wakati muafaka wa KUSEMEZANA...kwa mazuri na mabaya, hapo mndipo miarobaini ya shida zote itatolewa.
 
"Nina mwezi wa 3 sasa sijamruhusu kunigusa"...!
Ni jana tulikuwa na mkasa wa aina hii ukiwa umeletwa na mdada ambaye ni family friend wetu, kisa amepata habari kuwa bwanake ambaye anafanya kazi na kontrakta wa barabara ya Arusha-Namanga, ana mahusiano na mwanadada mwingine...

Kwa ufupi ni wazi silaha hiyo ya kunyimana tendo takatifu la ndoa ni ya hatari sana...maana party inayolalamika lazima itatafuta namna fulani ya kumkomoa mwenzie kwa kuwa na mahusiano ya tofauti nje ya ndoa, halafu meli yote inakuwa inazama taratibu...
Maongezi ni ufunguo...familia zipate wakati muafaka wa KUSEMEZANA...kwa mazuri na mabaya, hapo mndipo miarobaini ya shida zote itatolewa.

Ni tatizo kubwa sana hili! Mwezi wa tatu hawajagusana unategemea kweli hao hakuna anayegusa nje? Kuna wadada mkikosana ama akisikia chochoko zozote mtaani basi anahama chumba, na kukwambia hali yangu kiafya si nzuri kabisa nina breed Mwezi mzima lol?
 
Swali, kama mwanaume ameoana na mwanamke Rasmi yaani kwa Ndoa au harusi. Kwa bahati wakazaa watoto angalau 2. je Wakija kuachana tatizo linakuwa ni kukosa uvumilivu, au shetani ameingilia ndoa.
 
Swali, kama mwanaume ameoana na mwanamke Rasmi yaani kwa Ndoa au harusi. Kwa bahati wakazaa watoto angalau 2. je Wakija kuachana tatizo linakuwa ni kukosa uvumilivu, au shetani ameingilia ndoa.

Mkuu inategemea na sababu! Kama ni uzinzi basi ndoa hiyo is beyond repairable hakuna kusingizia shetani
 
Ndoa nyingi huingia matatizoni kwa kunyimana Tunda!
Masanilo uliyoyasema ni ya kweli
Nakutakia Maisha mema kwa Mwaka 2011 uwe wenyewe utafiti wa hali ya Juu!
 
Mchungaji asante lakini mimi naona wadada ufanya hivyo kwasababu yawezekana umemkwaza hivyo sidhani kama ummkwaza bado utake show upewe utapewa mgongo tu!!sasa kama umemkosea bado ukanyimwa show ukaona suruhisho latatizo lenu nukwenda kumtafuta mgombea mwenza utakuwa umepotoka!! nimtizamo wangu.
 
Mkuu inategemea na sababu! Kama ni uzinzi basi ndoa hiyo is beyond repairable hakuna kusingizia shetani

Heri ya Mwaka mpya Rev Masa,

Hili suala ni gumu sana mkuu. Ingawa sex inatakiwa kuwa immotional deal, mara nyingi watu wamelifanya kuwa physical zaidi na kupoteza maana yake ya msingi.

Kuna dada mmoja nilisikia habari zake kuwa yeye anaamini sex ni sawa na kumgusa mtu mkono na alikuwa tayari kutoa kwa mtu yeyote... A very complex business ingawa hatuwezi kukwepa kununua shea katika hizo kampuni!
 
kutumia sex kama silaha ni makosa sana,,hata kama kuna makwazo ni muhimu kuongea na kutatua tatizo,,,lkn mchungaji kuna wanandoa wanatengana chumba kabisa kutokana na chronic cheating,,hii unaizungumziaje?
 
Heri ya Mwaka mpya Rev Masa,

Hili suala ni gumu sana mkuu. Ingawa sex inatakiwa kuwa immotional deal, mara nyingi watu wamelifanya kuwa physical zaidi na kupoteza maana yake ya msingi.

Kuna dada mmoja nilisikia habari zake kuwa yeye anaamini sex ni sawa na kumgusa mtu mkono na alikuwa tayari kutoa kwa mtu yeyote... A very complex business ingawa hatuwezi kukwepa kununua shea katika hizo kampuni!

Duuuh hii iko complicated sana! Sasa huyo dada akikutana na vijana wa sasa mikono si itaota sugu kwa kusalimiana mara kwa mara? Kazi kweli kweli
 
kutumia sex kama silaha ni makosa sana,,hata kama kuna makwazo ni muhimu kuongea na kutatua tatizo,,,lkn mchungaji kuna wanandoa wametengana chumba kabisa kutokana na chronic cheating,,hii unaizungumziaje?

Kutengana vyumba nadhani si suluhisho! Ningependa wakae chini wamalize tatizo. Kuna Dr mmoja mkoa wa Shinyanga alikufa akiwa chumbani kwake bila mkewe kujua kwa siku mbili, sababu za kutengana.
 
Duuuh hii iko complicated sana! Sasa huyo dada akikutana na vijana wa sasa mikono si itaota sugu kwa kusalimiana mara kwa mara? Kazi kweli kweli

Mbona bado anakata mitaa? Ukipenda naweza kukutumia contacts zake labda unaweza kumpatia ushauri nasaha!
 
"Ingawa sex inatakiwa kuwa immotional deal, mara nyingi watu wamelifanya kuwa physical zaidi na kupoteza maana yake ya msingi." upendo katika ndoa ni muhimu zaidi, mapenzi ni zaidi ya tendo la ndoa. mapenzi ni kauli nzuri, na maneno kama samahani, asante na mawasiliano. Mawasiliano ni kwa kumwambia mwenzio kile unachojisikia kama hupendi hiki, au unaudhika kwa jambo fulani au unapenda kitu fulani. Pia uvumilivu na kuacha anasa vinadumisha ndoa hasa akina dada zetu, msishindane kwa mavazi, hereni, au mapishi au kwenda out. ishi kulingana na kipato cha Mume wako. ukiepuka anasa, vishawishi utavipata wapi????
 
Mbona bado anakata mitaa? Ukipenda naweza kukutumia contacts zake labda unaweza kumpatia ushauri nasaha!

Hahahahah huyo hawezi nielewa labda nami nisalimiane naye kwa kugusana mikono! Hahahahahahahahhh
 
Kutengana vyumba nadhani si suluhisho! Ningependa wakae chini wamalize tatizo. Kuna Dr mmoja mkoa wa Shinyanga alikufa akiwa chumbani kwake bila mkewe kujua kwa siku mbili, sababu za kutengana.

Mkuu hii kitu ni biashara ya hovyo sana. Yaani mtu anaweza kuwekeza mtaji wake hata kama anajua fika toka rohoni kwamba kampuni yenyewe iko mahututi.

Tatizo langu ni watu kujidai kuwa wanaweza kuisha na matatizo ya kimahusiano bila kuchukua jitahada za kuyatatua kwa kudhani kuwa yatajimaliza yenyewe. Kwangu mimi natumia mtindo wa zege halilali. Kila kitu kinaisha siku hiyo ili panapowezekana siku mpya ianze na mambo mapya. But...ni kazi ngumu sana, tena kwetu sisi wanaume wa kibongo kwani wakati mwingine inatutaka kujishusha na kuwapigia wenzetu magoti! Na ukizingatia mila zetu zimetuaminisha kuwa wao ndio lazima wapige magoti na kulilia wanaume siku zote..

Afadhali safali yangu ilianza 1947, sijui hawa dot.com wanakwenda kwendaje!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom