Elli
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 55,499
- 86,035
Kisa kizima kinapatikana hapa 1 Wafalme 13:1-34
Kwa ufupi sana, Mfalme Yeroboamu alimtenda MUNGU dhambi, na dhambi hii ilipozidi kuwa kubwa MUNGU akamwinua Nabii MWINGINE ambaye alikwenda hadi kwa Yeroboamu na akatoa Unabii wake kama alivyotumwa, LAKINI aliamriwa kuwa asije akanywa wala kula kitu chochote katika nchi hii maana nchi ilikua najisi kwa kumtenda MUNGU dhambi. Baada ya kutoa unabii wake katika nchi ya Betheli akawa anaondoka kwenye nchi ile ili kuerejea kwake. Nabii mmoja Mzee wa Betheli aliposikia habari zile kwa watoto wake akamfuata hadi alipokutana naye njiani huko na kumsihi yule nabii arudi nyumbani kwake pamoja naye.
Manabii wote wawili walirejea nyumbani na kula chakula pamoja na mara baada ya kula chakula kile ndipo Roho wa Bwana alimpojia na kumkumbusha neno lile aliloambiwa, USILE wala KUNYWA. Adhabu yake kwa kutokutii neno hili ilikua ni kutokuzikwa kwa heshima yaani hatalazwa mahali walipolazwa ndugu zake, na unabii huu ulitimia kwani alishambuliwa na Simba na kuuwawa lakini Punda hakuguswa na Simba huyu.
Sasa, Mzee Siita alionekana kama Nabii, alietumwa akaiokoe Tanzania kwa kusaidia upatikanaji wa Katiba Mpya, katiba ambayo ingesaidia sana kuwatoa watanzania kwenye umaskini uliokithiri, kuonea na kuibiwa mali zao. Hakika Sitta alisimama kwenye nafasi yake LAKINI hakutakiwa kamwe kujiunga tena na kundi hili la Walafi, wenye kula na kuendekeza anasa huku mamia ya watanzania wakifa njaa na magonjwa.
Maskini, Mzee Sitta alianza vyema na kwamba MUNGU alilenga kumwinua zaidi na zaidi lakini amesahau sharti lile la kujipambanua na Walafi wale, wenye Njaa na damu za watu, akarudi, akarejea na amekaaa amekula nao tena chakula cha Unajisi, hivyo amelinajisi neno lile lililowekwa ndani yake, lile alilotumwa alihubiri limemshinda. MUNGU asema hivi, ile ndoto yake ya kuwa mgombea Urais haipo tena, imeondoshwa na kwamba Jamii yake iliyomtia unajisi huu itamtenga very soon. Atakuwa na mwisho mbaya kuliko mwanzo mwema.
Lakini, analo neno la mwisho lililobaki mkononi mwake, KUMBUKA NI WAPI ULIPOANGUKA UKATUBU, NA USIPOTUBU TAZAMA NAKUJA UPESI NAMI NITAPAONDOA MAHALI PAKO PASIWEPO KAMWE.
Kwa ufupi sana, Mfalme Yeroboamu alimtenda MUNGU dhambi, na dhambi hii ilipozidi kuwa kubwa MUNGU akamwinua Nabii MWINGINE ambaye alikwenda hadi kwa Yeroboamu na akatoa Unabii wake kama alivyotumwa, LAKINI aliamriwa kuwa asije akanywa wala kula kitu chochote katika nchi hii maana nchi ilikua najisi kwa kumtenda MUNGU dhambi. Baada ya kutoa unabii wake katika nchi ya Betheli akawa anaondoka kwenye nchi ile ili kuerejea kwake. Nabii mmoja Mzee wa Betheli aliposikia habari zile kwa watoto wake akamfuata hadi alipokutana naye njiani huko na kumsihi yule nabii arudi nyumbani kwake pamoja naye.
Manabii wote wawili walirejea nyumbani na kula chakula pamoja na mara baada ya kula chakula kile ndipo Roho wa Bwana alimpojia na kumkumbusha neno lile aliloambiwa, USILE wala KUNYWA. Adhabu yake kwa kutokutii neno hili ilikua ni kutokuzikwa kwa heshima yaani hatalazwa mahali walipolazwa ndugu zake, na unabii huu ulitimia kwani alishambuliwa na Simba na kuuwawa lakini Punda hakuguswa na Simba huyu.
Sasa, Mzee Siita alionekana kama Nabii, alietumwa akaiokoe Tanzania kwa kusaidia upatikanaji wa Katiba Mpya, katiba ambayo ingesaidia sana kuwatoa watanzania kwenye umaskini uliokithiri, kuonea na kuibiwa mali zao. Hakika Sitta alisimama kwenye nafasi yake LAKINI hakutakiwa kamwe kujiunga tena na kundi hili la Walafi, wenye kula na kuendekeza anasa huku mamia ya watanzania wakifa njaa na magonjwa.
Maskini, Mzee Sitta alianza vyema na kwamba MUNGU alilenga kumwinua zaidi na zaidi lakini amesahau sharti lile la kujipambanua na Walafi wale, wenye Njaa na damu za watu, akarudi, akarejea na amekaaa amekula nao tena chakula cha Unajisi, hivyo amelinajisi neno lile lililowekwa ndani yake, lile alilotumwa alihubiri limemshinda. MUNGU asema hivi, ile ndoto yake ya kuwa mgombea Urais haipo tena, imeondoshwa na kwamba Jamii yake iliyomtia unajisi huu itamtenga very soon. Atakuwa na mwisho mbaya kuliko mwanzo mwema.
Lakini, analo neno la mwisho lililobaki mkononi mwake, KUMBUKA NI WAPI ULIPOANGUKA UKATUBU, NA USIPOTUBU TAZAMA NAKUJA UPESI NAMI NITAPAONDOA MAHALI PAKO PASIWEPO KAMWE.