Usiku wa kuamkia leo - Jumatatu - (saa tatu na robo hivi) nilifungua Radio Station moja ya Kiislamu hapa Tanzania na kusikiliza mahubiri yaliyonisikitisha sana. Mhubiri/mwalimu (sheikh mmoja au mtaalamu wa dini ya Kiislamu) alikuwa akikosoa sana kongamano lliloandaliwa na Mwalimu Nyerere Foundation hivi karibuni. Aliwakosoa waliochangia mada katika conference hiyo.
Aliponda sana Serikali ya Awamu ya Kwanza, akasifia ya Awamu ya Pili na hii ya Awamu ya Nne. Ya Awamu ya Tatu sikusikia akiitaja. Nadhani aliiweka kwenye kundi sawa na ya Awamu ya Kwanza. Alidai katika Awamu ya Kwanza hali ya umaskini ilikuwa mbaya sana nchini na neema iliaanza kuja wakati wa Awamu ya Pili. Na hiyo, alisema ilitokana na uongozi mzuri wa Rais Mstaafu Ali Hassani Mwinyi.
Aliuliza, Mbona rushwa ilikuwepo sana enzi za Serikali ya Awamu ya Kwanza na hakuna aliyejitokeza waziwazi kuikosoa Serikali kama baadhi ya watu wanavyofanya leo hii? Hii inasababishwa na nini? Mimi sikuelewa kabisa mantiki yake. Yaani, kama kitu hakikukosolewa enzi za Mwalimu Nyerere basi kisikosolewe tena hadi mwisho wa dunia?
Mbona mazingira yamebadilika na watu pia wamebadilika? Ni kama kusema kwa vile hapakuwepo maendeleo fulani wakatu ule basi yasiwepo tena! Kwa vile barabara wakati ule zilikuwa chache basi ziendelee kuwa hizohizo! Mbona ni mawazo mgando sana kutoka kwenye kinywa cha kiongozi wa kiroho? Huyu kwa mtazamo wake finyu hawezi kuwakosesha watu anaowaongoza kama watafuata mawazo yake mgando hayo?
Kuhusu kongamano, alisema wote waliochangia ni wanafiki na wana underplay juhudi za Rais Jakaya Kikwete kwa vile ni Mwislamu. Mbona hawakufanya hivyo enzi za Mwalimu Julius Nyerere? alihoji.
Alinukuu mchango wa askofu mmoja wa KKKT aliyechangia: Shule za Kata zitaleta ukabila. Baada ya nukuu hii akasema, Kwa juu juu mtu anaweza kusema ni kweli alichosema askofu wa KKKT kwani wanafunzi wanasoma katika mazingira yaleyale kuanzia shule ya msingi hadi sekondari, hivyo hawataweza kuchanganyikana na wenzao wanaotoka kata/wilaya/mikoa mingine ya Tanzania. Lakini ukiangalia kwa makini sana, issue siyo ukabila bali ubaguzi wa kidini.
Hawa maaskofu wana akili sana. Wameona kuwa kukiwa na shule nyingi za kata, Waislamu wengi watapata elimu na ili kuwanyima hiyo fursa, wanakuja na mbinu mpya eti shule hizi zitaleta ukabila. Huu ni uongo wa kutunga unaoenezwa na viongozi wa Kikristo kwa nia ya kuwafanya Waislamu wakose nafasi ya kusoma, alisisitiza.
Halafu alihoji inakuwaje enrolment katika shule za msingi watoto wengi wanatoka familia za Kiislamu lakini wanaanza kuenguliwa wanapoingia elimu ya sekondari na chuo kikuu na badala yake wanachukuliwa Wakristo kwa zaidi ya 80%. Alisema kwa upande wa elimu ya sekondari ni 30% tu ya watoto kutoka familia za Kiislamu wanaochukuliwa kujiunga na elimu hiyo lakini kwa Wakristo ni 70%. Ndiyo maana hata kwenye ajira utakuta wengi wa walioajiriwa ni Wakristo, alisema na kuuliza: Hii inakuaje kama siyo mchezo mchafu unaochezwa?
Halafu kaja kwa askofu Methodius Kilaini. Akasema: Kilaini alisema hapa Tanzania tunatembea uchi na ni vizuri kuona watu wanaanza kuamka na kushughulikia maswala yanayohusu maisha yao. Endeleeni kupiga kelele, msichoke. Pambaneni na ufisadi
Akasema: Kama askofu Kilaini anasema watu wanatembea uchi basi vazi sahihi ni hijabu tu Yeye anajifanya kupinga ufisadi wakati wao wenyewe ndio mafisadi.
Nilisikitika sana kusikia kiongozi kama huyo anayesikilizwa na kuaminiwa na waumini wake na pengine na wasikizaji wengine wasio waumini wa dini ya Kiislamu anaweza kuongea pumba kama hizo.
Kwa upande wangu waliochangia kwenye kongamano walitoa maoni yao kwa kuangalia nchi inaelekea wapi na issues walizozizungumzia zinahusu maslahi ya Watanzania wote. Cha kushangaza ni kuona baadhi ya watu wanajaribu kupotosha kabisa lengo la kongamano lenyewe.
Hivi Watz tumebaki tu watu wa kusifia viongozi wetu hata kama tunaona udhaifu na kama wakitokea watu wa kukosoa kitu wanaonekana hawafai? Binafsi, hata Rais Kikwete mwenyewe anaona unafiki wa wale apologetics. In fact, watu wanapokosoa Serikali inawezekana hata Rais Kikwete mwenyewe anafurahi kuona mambo ambayo yangetakiwa kufanyika na hayafanyiki yakiibuliwa ili wahusika wawajibike.
Ila anajua fika wanaopinga mchango chanya ni wapiga debe (opportunists) tu, hawasemi kinachotoka moyoni mwao. Na mambo yatakapoharibika zaidi watu haohao watamgeuka. Kweli kwa kuona hali tuliyo nayo hapa nchini kwa kulinganisha na raslimali tulizonazo mtu anadiriki kukubali kabisa were on the right path na hakuna cha kurekebisha? Maana kukosoa kuna maana kwamba baadhi ya mambo yangeweza kufanywa vizuri zaidi kuliko ilivyo sasa hivi. Kwa nini tusitunie muda huo kujifunza kuboresha zaidi hayo yanayokosolewa?
Nakubaliana kabisa na wote wanaoikosoa Serikali na hii ni kwa sababu naipenda Serikali yetu kuliko Serikali yoyote duniani na ninataka iendelee kufanya vizuri na ili ifanye hivyo inabidi irekebishe baadhi ya mambo.
Hebu angalia adha ya usafiri msongamano wa abiria ndani ya gari moja (zero distance). Na tunafanya hivyo ili tuwahi kazini kwani hakuna atakayechelewa na kusema usafiri ulikuwa mgumu na boss wake kukubali hoja yake. Na mtu anaona kuchelewa kila siku kazi inaweza kumwiishia. Hivyo anaamua tu kuikubali hali yenyewe ili aendelee kuwa kibaruani.
Jioni baada ya kutoka kazini ni shida pia. Na unakuta akina mama wakichelewa waume zao hawatasema ni tatizo la usafiri. Baadhi yao tunasikia wanavyopigiwa simu na waume zao na wanavyojitetea, lakini aliye nyumbani anadhani ni fix tu na wakati mwingine kumwabia mkewe ikifika muda fulani hajafika asikanyage nyumbani kwake!
Hebu angali mgambo wanavyonyanyasa wamachinga lakini wameshindwa kuwadhibiti wapiga debe ambao sasa hivi ndio wanaopanga nauli za magari ya abiria. Nenda Kariakoo jioni kuanzia saa 12 au hata kabla. Ikifika saa moja hivi baadhi ya magari yanasitisha 'routes zao na kuanza kupakia abiria wa kwenda Mbagala kwa nauli inayotangazwa na wapiga debe kuanzia Sh500, Sh1,000 na wakati mwingine Sh1,500 badala ya Sh250. Kwa vile mtu amekaa kituoni muda mrefu akisubiri usafiri bila kupata, analazimika kulipa hicho kiasi, afanye nini?
Hebu angalia sekta binafsi: junior staff wanakaa miaka nenda rudi bila kupandishwa mshahara lakini vitu vinapanda karibu kila mwezi. Je, kweli hawa wataweza kuinuka kiuchumi? Lini wataweza kutunza hela ili waweze kujenga nyumba au hata kusomesha watoto kwenye shule nzuri? Wakinunua kiwanja kilichopimwa, kina time limit miaka mitatu. Kama hawatakuwa wamekiendeleza (na mara nyingi ni kwa sababu kipato chao ni kidogo, wananyanganywa) na kupewa wenye uwezo.
Hebu angalia maisha ya wananchi wa kawaida Kanda ya Ziwa Viktoria wala mapanki. Sehemu wanakoruhusiwa kuvua ni katikati ya ziwa. Wavuvi wadogowadogo wakienda huko wanapigwa na wakati mwingine kutumbukizwa majini kwa vile wavuvi wakubwa wanawachukulia wao kama wezi wa nyavu zao. Wavuvi wakubwa wana patrol boats na wengine wana silaha za moto.
Hawa wavuvi wadogo wakivua maeneo mengine, wanakuwa wavuvi haramu wanakamatwa, nyanganywa kila kitu (wenye uwezo wanaweza kuhonga na wasio na uwezo wanaishia jela) na kushtakiwa kwa kukutwa na zana haramu za uvuvi au kuvua maeneo yaliyokatazwa na Serikali. Wataishije?
Hebu angalia jinsi wananchi wanavyohamishwa kupisha mradi fulani au mwekezaji utadhani wanaosimamia zoezi hilo wameambiwa bila kutumia nguvu zote hizo mwekezaji huyo atakufa. Utaratibu wa kufidia wanaohamishwa mara zote siyo mzuri na unaacha malalamiko mengi kwa wananchi.
Hebu angalia madini tuliyo nayo na faida tunayopata kama taifa. Nchi nyingine madini haya ndiyo yanayochangia kuborsha huduma za jamii na kuongeza quality of life ya wananchi. Siyo hivyo hapa Tanzania.
Hebu angalia aina ya magari yanayonunuliwa na vigogo wa Serikali. Hata baadhi ya wafadhili wanatushangaa kuendelea kuomba misaada na wakati matumizi yetu ni ya anasa.
Hebu angalia customer care kwenye ofisi za Serikali. Watu wako pale utadhani wamelazimishwa kufanya kazi na wanaona udhia kumdhudumia mteja. Kwenye baadhi ya ofisi utakuta mtu anacheza game kwenye komputa au simu na anaona shida kukwambia mteja: Karibu, nikusaidie nini? Wengine unakuta wanapiga soga ofisini na hawana muda wa kumsikiliza mteja.
Angalia behaviour ya askari wetu hasa kama wanaendesha gari. Ni wao wa kwanza kutanua kwa vile gari lao lina namba zinazoanza na PT au JWTZ. Itokekee kwa bahati mbaya ugongane na askari wa JWTZ au ukwaruze gari lao utakiona cha moto makofi, push-up, viringika etc. Na hawa ndio walinzi wetu! Ila wao wakikwaruza gari lako, wanakuomba samahani na kwa vile huna nguvu yanaisha!
Yaani kuna mambo mengi sana ambayo yanaonekana hayako sawa na bila kurekebisha haya, maendeleo yatabaki kuwa ndoto Tanzania.
Ili tuweze kuondokana na ufisadi na wizi uliokithiri wa mali ya umma - mali ya Watanzania ambao wengi wao wanazidi kuwa maskini na matajiri wanazidi kuneemeka inabidi tubadilike.
Tuchague viongozi wenye sifa na waadilifu na wanovurunda tuwatoe. Lakini akitokea mtu, taasisi fulani kutoa changamoto tunamkemea au tunaikemea utadhani kuna kosa la uhaini. Hivi hapa Tanzania, nani atamkosoa mwingine? Akijitokeza mmoja tutamshambulia ili akae kimya!
Ni kweli nchi yetu inaharibika na tunaiharibu wenyewe. Na hasa viongozi kama huyu mhubiri au mwalimu wa dini ninayemzungumzia anawaingizia waumini wake mawazo mfu kama hayo, si na wao wanaamini kabisa kama alivyosema? Jamani tuwe na uchungu na nchi yetu na hali za Watanzania wenzetu!
Aliponda sana Serikali ya Awamu ya Kwanza, akasifia ya Awamu ya Pili na hii ya Awamu ya Nne. Ya Awamu ya Tatu sikusikia akiitaja. Nadhani aliiweka kwenye kundi sawa na ya Awamu ya Kwanza. Alidai katika Awamu ya Kwanza hali ya umaskini ilikuwa mbaya sana nchini na neema iliaanza kuja wakati wa Awamu ya Pili. Na hiyo, alisema ilitokana na uongozi mzuri wa Rais Mstaafu Ali Hassani Mwinyi.
Aliuliza, Mbona rushwa ilikuwepo sana enzi za Serikali ya Awamu ya Kwanza na hakuna aliyejitokeza waziwazi kuikosoa Serikali kama baadhi ya watu wanavyofanya leo hii? Hii inasababishwa na nini? Mimi sikuelewa kabisa mantiki yake. Yaani, kama kitu hakikukosolewa enzi za Mwalimu Nyerere basi kisikosolewe tena hadi mwisho wa dunia?
Mbona mazingira yamebadilika na watu pia wamebadilika? Ni kama kusema kwa vile hapakuwepo maendeleo fulani wakatu ule basi yasiwepo tena! Kwa vile barabara wakati ule zilikuwa chache basi ziendelee kuwa hizohizo! Mbona ni mawazo mgando sana kutoka kwenye kinywa cha kiongozi wa kiroho? Huyu kwa mtazamo wake finyu hawezi kuwakosesha watu anaowaongoza kama watafuata mawazo yake mgando hayo?
Kuhusu kongamano, alisema wote waliochangia ni wanafiki na wana underplay juhudi za Rais Jakaya Kikwete kwa vile ni Mwislamu. Mbona hawakufanya hivyo enzi za Mwalimu Julius Nyerere? alihoji.
Alinukuu mchango wa askofu mmoja wa KKKT aliyechangia: Shule za Kata zitaleta ukabila. Baada ya nukuu hii akasema, Kwa juu juu mtu anaweza kusema ni kweli alichosema askofu wa KKKT kwani wanafunzi wanasoma katika mazingira yaleyale kuanzia shule ya msingi hadi sekondari, hivyo hawataweza kuchanganyikana na wenzao wanaotoka kata/wilaya/mikoa mingine ya Tanzania. Lakini ukiangalia kwa makini sana, issue siyo ukabila bali ubaguzi wa kidini.
Hawa maaskofu wana akili sana. Wameona kuwa kukiwa na shule nyingi za kata, Waislamu wengi watapata elimu na ili kuwanyima hiyo fursa, wanakuja na mbinu mpya eti shule hizi zitaleta ukabila. Huu ni uongo wa kutunga unaoenezwa na viongozi wa Kikristo kwa nia ya kuwafanya Waislamu wakose nafasi ya kusoma, alisisitiza.
Halafu alihoji inakuwaje enrolment katika shule za msingi watoto wengi wanatoka familia za Kiislamu lakini wanaanza kuenguliwa wanapoingia elimu ya sekondari na chuo kikuu na badala yake wanachukuliwa Wakristo kwa zaidi ya 80%. Alisema kwa upande wa elimu ya sekondari ni 30% tu ya watoto kutoka familia za Kiislamu wanaochukuliwa kujiunga na elimu hiyo lakini kwa Wakristo ni 70%. Ndiyo maana hata kwenye ajira utakuta wengi wa walioajiriwa ni Wakristo, alisema na kuuliza: Hii inakuaje kama siyo mchezo mchafu unaochezwa?
Halafu kaja kwa askofu Methodius Kilaini. Akasema: Kilaini alisema hapa Tanzania tunatembea uchi na ni vizuri kuona watu wanaanza kuamka na kushughulikia maswala yanayohusu maisha yao. Endeleeni kupiga kelele, msichoke. Pambaneni na ufisadi
Akasema: Kama askofu Kilaini anasema watu wanatembea uchi basi vazi sahihi ni hijabu tu Yeye anajifanya kupinga ufisadi wakati wao wenyewe ndio mafisadi.
Nilisikitika sana kusikia kiongozi kama huyo anayesikilizwa na kuaminiwa na waumini wake na pengine na wasikizaji wengine wasio waumini wa dini ya Kiislamu anaweza kuongea pumba kama hizo.
Kwa upande wangu waliochangia kwenye kongamano walitoa maoni yao kwa kuangalia nchi inaelekea wapi na issues walizozizungumzia zinahusu maslahi ya Watanzania wote. Cha kushangaza ni kuona baadhi ya watu wanajaribu kupotosha kabisa lengo la kongamano lenyewe.
Hivi Watz tumebaki tu watu wa kusifia viongozi wetu hata kama tunaona udhaifu na kama wakitokea watu wa kukosoa kitu wanaonekana hawafai? Binafsi, hata Rais Kikwete mwenyewe anaona unafiki wa wale apologetics. In fact, watu wanapokosoa Serikali inawezekana hata Rais Kikwete mwenyewe anafurahi kuona mambo ambayo yangetakiwa kufanyika na hayafanyiki yakiibuliwa ili wahusika wawajibike.
Ila anajua fika wanaopinga mchango chanya ni wapiga debe (opportunists) tu, hawasemi kinachotoka moyoni mwao. Na mambo yatakapoharibika zaidi watu haohao watamgeuka. Kweli kwa kuona hali tuliyo nayo hapa nchini kwa kulinganisha na raslimali tulizonazo mtu anadiriki kukubali kabisa were on the right path na hakuna cha kurekebisha? Maana kukosoa kuna maana kwamba baadhi ya mambo yangeweza kufanywa vizuri zaidi kuliko ilivyo sasa hivi. Kwa nini tusitunie muda huo kujifunza kuboresha zaidi hayo yanayokosolewa?
Nakubaliana kabisa na wote wanaoikosoa Serikali na hii ni kwa sababu naipenda Serikali yetu kuliko Serikali yoyote duniani na ninataka iendelee kufanya vizuri na ili ifanye hivyo inabidi irekebishe baadhi ya mambo.
Hebu angalia adha ya usafiri msongamano wa abiria ndani ya gari moja (zero distance). Na tunafanya hivyo ili tuwahi kazini kwani hakuna atakayechelewa na kusema usafiri ulikuwa mgumu na boss wake kukubali hoja yake. Na mtu anaona kuchelewa kila siku kazi inaweza kumwiishia. Hivyo anaamua tu kuikubali hali yenyewe ili aendelee kuwa kibaruani.
Jioni baada ya kutoka kazini ni shida pia. Na unakuta akina mama wakichelewa waume zao hawatasema ni tatizo la usafiri. Baadhi yao tunasikia wanavyopigiwa simu na waume zao na wanavyojitetea, lakini aliye nyumbani anadhani ni fix tu na wakati mwingine kumwabia mkewe ikifika muda fulani hajafika asikanyage nyumbani kwake!
Hebu angali mgambo wanavyonyanyasa wamachinga lakini wameshindwa kuwadhibiti wapiga debe ambao sasa hivi ndio wanaopanga nauli za magari ya abiria. Nenda Kariakoo jioni kuanzia saa 12 au hata kabla. Ikifika saa moja hivi baadhi ya magari yanasitisha 'routes zao na kuanza kupakia abiria wa kwenda Mbagala kwa nauli inayotangazwa na wapiga debe kuanzia Sh500, Sh1,000 na wakati mwingine Sh1,500 badala ya Sh250. Kwa vile mtu amekaa kituoni muda mrefu akisubiri usafiri bila kupata, analazimika kulipa hicho kiasi, afanye nini?
Hebu angalia sekta binafsi: junior staff wanakaa miaka nenda rudi bila kupandishwa mshahara lakini vitu vinapanda karibu kila mwezi. Je, kweli hawa wataweza kuinuka kiuchumi? Lini wataweza kutunza hela ili waweze kujenga nyumba au hata kusomesha watoto kwenye shule nzuri? Wakinunua kiwanja kilichopimwa, kina time limit miaka mitatu. Kama hawatakuwa wamekiendeleza (na mara nyingi ni kwa sababu kipato chao ni kidogo, wananyanganywa) na kupewa wenye uwezo.
Hebu angalia maisha ya wananchi wa kawaida Kanda ya Ziwa Viktoria wala mapanki. Sehemu wanakoruhusiwa kuvua ni katikati ya ziwa. Wavuvi wadogowadogo wakienda huko wanapigwa na wakati mwingine kutumbukizwa majini kwa vile wavuvi wakubwa wanawachukulia wao kama wezi wa nyavu zao. Wavuvi wakubwa wana patrol boats na wengine wana silaha za moto.
Hawa wavuvi wadogo wakivua maeneo mengine, wanakuwa wavuvi haramu wanakamatwa, nyanganywa kila kitu (wenye uwezo wanaweza kuhonga na wasio na uwezo wanaishia jela) na kushtakiwa kwa kukutwa na zana haramu za uvuvi au kuvua maeneo yaliyokatazwa na Serikali. Wataishije?
Hebu angalia jinsi wananchi wanavyohamishwa kupisha mradi fulani au mwekezaji utadhani wanaosimamia zoezi hilo wameambiwa bila kutumia nguvu zote hizo mwekezaji huyo atakufa. Utaratibu wa kufidia wanaohamishwa mara zote siyo mzuri na unaacha malalamiko mengi kwa wananchi.
Hebu angalia madini tuliyo nayo na faida tunayopata kama taifa. Nchi nyingine madini haya ndiyo yanayochangia kuborsha huduma za jamii na kuongeza quality of life ya wananchi. Siyo hivyo hapa Tanzania.
Hebu angalia aina ya magari yanayonunuliwa na vigogo wa Serikali. Hata baadhi ya wafadhili wanatushangaa kuendelea kuomba misaada na wakati matumizi yetu ni ya anasa.
Hebu angalia customer care kwenye ofisi za Serikali. Watu wako pale utadhani wamelazimishwa kufanya kazi na wanaona udhia kumdhudumia mteja. Kwenye baadhi ya ofisi utakuta mtu anacheza game kwenye komputa au simu na anaona shida kukwambia mteja: Karibu, nikusaidie nini? Wengine unakuta wanapiga soga ofisini na hawana muda wa kumsikiliza mteja.
Angalia behaviour ya askari wetu hasa kama wanaendesha gari. Ni wao wa kwanza kutanua kwa vile gari lao lina namba zinazoanza na PT au JWTZ. Itokekee kwa bahati mbaya ugongane na askari wa JWTZ au ukwaruze gari lao utakiona cha moto makofi, push-up, viringika etc. Na hawa ndio walinzi wetu! Ila wao wakikwaruza gari lako, wanakuomba samahani na kwa vile huna nguvu yanaisha!
Yaani kuna mambo mengi sana ambayo yanaonekana hayako sawa na bila kurekebisha haya, maendeleo yatabaki kuwa ndoto Tanzania.
Ili tuweze kuondokana na ufisadi na wizi uliokithiri wa mali ya umma - mali ya Watanzania ambao wengi wao wanazidi kuwa maskini na matajiri wanazidi kuneemeka inabidi tubadilike.
Tuchague viongozi wenye sifa na waadilifu na wanovurunda tuwatoe. Lakini akitokea mtu, taasisi fulani kutoa changamoto tunamkemea au tunaikemea utadhani kuna kosa la uhaini. Hivi hapa Tanzania, nani atamkosoa mwingine? Akijitokeza mmoja tutamshambulia ili akae kimya!
Ni kweli nchi yetu inaharibika na tunaiharibu wenyewe. Na hasa viongozi kama huyu mhubiri au mwalimu wa dini ninayemzungumzia anawaingizia waumini wake mawazo mfu kama hayo, si na wao wanaamini kabisa kama alivyosema? Jamani tuwe na uchungu na nchi yetu na hali za Watanzania wenzetu!