Mahojiano ya polisi na Sheikh Ponda Issa Ponda

Mkuu wangu mimi na sheria mbalimbali! Huyo wakili aliyemuhoji ndiyo anajua sheria!Mimi ni mwanajamvi huru tu niliyeleta hii habari kwenu!Au nimekosea?
Samahani mkuu,mimi nilijua wewe ndiye wakili uliyeshughulikia suala la yule gaidi wa kimataifa!
 

Hizi lugha za kigaidi zinatafuta nini humu??

هذا الأخ هي لغة العربية جيد جدا أنا مسيحي، ولكن أود أن استخدامه
 
Etiiiii??? Huyo ni panya mdogo sana. Subiri tu utaskia mustakabali wake sasa hivi. Kwanini alikimbia basi alipogundua kashaingia kwenye mtego?
Huyu jamaa wakati wa utawala wa Mkapa alikimbia nchi,nakumbuka lile sekeseke la mwembe chai,akarudi baada ya mkapa kuondoka madarakani!
 
nakunya sasa...
Unakasirika uku unajua natania...
وقف النكات والمتدينين، وأنا هنا أنا أكتب ليس فقط الأكاديمية العربية
 
Asalaam Alaykum! Saa 4 asubuhi nilifika Central Police kusimamia mahojiano yake na Polisi kwa mujibu wa haki za mtuhumiwa nilionana na msaidizi wa ZCO baada ya utambulisho na kumfahamisha haki zake wakati wa mahojiano alihojiwa. Ukiacha namna alivyokamatwa mpaka naondoka polisi saa 10 kasoro alikuwa ktk hali nzuri na polisi akiwa kituoni hawakumfanyia lolote lililokinyume na haki za mtu aliyechini ya ulinzi.
Sheikh anatuhumiwa na mambo yafuatayo:-
1. Kuhamasisha maandamano kwenda Wizara ya Mambo ya Ndani. Wakati wa mahojiano walitaka kujua yafuatayo:-
i. kwanini waliandamana ii. nani aliandaa mabango
iii. kwanini walisema kuwa baada ya maandamano yale wataenda kumng'oa Mufti na Ndalichako
iv. nani aliandaa maandamano
Sheikh alikiri kuhamasisha maandamano na pia alikubali ujumbe uliuokuwa katika mabango ulikuwa umebeba hisia za waislamu. Isipokuwa yeye hajui nani aliyaandika hayo mabango. Kuhusu Mufti na Ndalichako alisema wanastahili kuondolewa kwasababu ya kuongoza kwa dhulma dhidi ya waislamu. Pia alisema maandamano yaliandaliwa na Taasisi na Jumuiya za Kiislamu na yeye ni katibu wake.
2. Kuvamia kiwanja cha chang'ombe
Hapa alijibu kuwa huo ni mgogoro wa ardhi na waislamu wapo pale kwasababu ni kiwanja cha waislamu. Na kama kuna mtu anadai amevamiwa eneo lake huo ni mgogoro wa ardhi aende kushitaki mahakama ya ardhi na waislamu wapo tayari kufika mahakamani kujibu. Pia alikiri kuwa amehusika ktk ujenzi wa msikiti unaojengwa ktk eneo hilo.
3. Kuhamasisha maandamano kidongo chekundu
4. Vurugu mbagala.
Haya mawili ya mwisho hakuhojiwa kwasababu mafaili yanayohusu malalamiko hayo yalikuwa hayajafika central lakini vilevile muda ulikuwa umeenda sana. Kwani mpaka tunamaliza mahojiano ilikuwa ni saa kumi kasoro hivi toka saa nne asubuhi.
DHAMANA.
Baada ya mahojiano niliomba apatiwe dhamana na kesho afike polisi kwa mahojiano zaidi. Polisi waliokuwa wanamhoji walikataa kwa hoja kuwa suala hilo liko kwa viongozi wakuu wa jeshi la polisi. Waliomba nikamwone ZCO Bw. Msangi, yeye alisema hawezi kulitolea maamuzi akanitaka nimwone Kamanda Kova. Nilienda kuonana na Kamanda Kova naye aliniambia kuwa hawawezi kutoa dhamana mpaka amalize mahojiano yaliyobaki. Na vile vile alisema wanasubiri wapate ushauri toka ofisi ya DPP. Lakini zaidi akasema kwa kuwa issue ya mbagala kuna watu wameshitakiwa kwa armed robbery kosa ambalo halina dhamana si vizuri kumpa dhamana sasa kwani huenda katika upelelezi wao wanaweza kumuunganisha na washitakiwa wa armed robbery mbagala. Kwa ufupi hiyo ndio hali iliyokuwepo. NAOMBA WAISLAMU WAAMBIWE WAWE NA SUBIRA WAKATI HUU WAIFANYE LOLOTE LITAKALOWAPA NAFASI MAADUI WA UISLAMU MANENO YA KUSEMA


umepata mgao wako kutoka alshabaab mheshimiwa wakili?

wewe ni mchochezi maana sioni haja ya wewe mtu ambaye nafikiri umeenda shule kuegemea upande wa gaidi ambaye anachafua waislamu na waislamu na kuleta kutokuelewana ndani ya jamii. Siamini kuwa kinachofanywa na Ponda ndiyo matakwa ya uislamu, mara kadhaa nimekuwa nashirikiana na waislamu na hata kuishi nao miaka nenda rudi sijaona uumini wa namna hii.

Nafikiri wewe ungefanya kazi yako ya uwakili, sisi hatuhitaji maelezo ya Ponda maana sisi sio mahakimu na hatutaki hata kusikia hilo jina maana ni pepo hillo.

hapa tunataka ishu za maana sio hadithi za wahalifu
 
وقف النكات والمتدينين، وأنا هنا أنا أكتب ليس فقط الأكاديمية العربية
TEh teh teh!Hii ni lugha ya kiarabu au kiislamu!!
 
Sisi waislam hata tukisoma hatuelewi kaka!

Hata mkifundishwa kwa lugha hii[وقف النكات والمتدينين، وأنا هنا أنا أكتب ليس فقط الأكاديمية العربية] bado hamuelewi?
 
Sisi waislam hata tukisoma hatuelewi kaka![/QUOTE

وقف النكات والمتدينين، وأنا هنا أنا أكتب ليس فقط الأكاديمية العربية
 
ha ha ha ha JF Rahaaaa!! nawaonea huruma sana wamwaminiao subuana

وقف النكات والمتدينين، وأنا هنا أنا أكتب ليس فقط الأكاديمية العربية
 
chonde chonde sana ndugu, nawaunga mkono muundelee kudai haki zenu kama zipo,lakini tunaomba mambo ya BOKOHARAMU yasijetokea hapa nchini kwetu. Moja ya jambo ambalo mimi nalikubali sana ni kwa upande weak always unadai haki kwa upande strong. Kwa mfano weusi Marekani tunadai haki kutoka kwa Wazungu. Weusi South Afrika tunadai haki kutoka kwa Boers. Wanawake wanadai haki kutoka wanaume.Wasudani kusini na Wadaful wanadai haki kutoka kwa North Sudan. Waislamu wa india wanadai haki kutoka kwa Wahindu.Wasuni wachache wa Iran wanadai haki kutoka kwa washia waliowengi wa Irani. Wakurdi wachache wa Iraki wanadai haki kutoka kwa washia na wasunni wa Iraki. Na waislamu wa Tanzania wanadai haki kutoka kwa Wakristo wa Tanzania. Wafanyakazi wanadai haki kutoka kwa Matajiri wao.Raia wanadai haki kutoka kwa Serikali. Watoto wanadai haki kutoka kwa Baba zao. Nchi za dunia ya tatu zinadai haki kutoka kwa nchi za dunia ya kwanza. Maskini wanadai haki kutoka kwa matajiri. Wasiojiweza na wazembe wanadai haki kwa wanajioweza na wenye bidii. Hii ndiyo dunia na hata yesu alisema wenye uwezo wawasaidie wasio na uwezo na maskini, na hakuangalia hata kama asiye na uwezo ni mzembe au la. Tutengeneze sera ya kuwasaidia wengine ili kupunguza migongano.Kila kundi hapo juu linalodai haki linapenda kuhalalisha kwamba upande strong ndio ulisababisha madhira ya upande wao Weak.Hawatajali wala kuangalia ulifanya nini kufikia hapo.
 
Kova naona anajikanyaga tu,mara armed robbery,mara kavamia kiwanja cha watu hata sijaelewa vizuri mie!

Wala huwezi kumwelewa maana WAISLAMU na SERIKALI lenu moja sema tu serikali imewageuka maana ninyi ni mtaji wa CCM bila ninyi kujua.hivyo sasa hivi mko CROSSROAD Mnacheza na MAGAMBA ninyi.
 
chonde chonde sana ndugu, nawaunga mkono muundelee kudai haki zenu kama zipo,lakini tunaomba mambo ya BOKOHARAMU yasijetokea hapa nchini kwetu. Moja ya jambo ambalo mimi nalikubali sana ni kwa upande weak always unadai haki kwa upande strong. Kwa mfano weusi Marekani tunadai haki kutoka kwa Wazungu. Weusi South Afrika tunadai haki kutoka kwa Boers. Wanawake wanadai haki kutoka wanaume.Wasudani kusini na Wadaful wanadai haki kutoka kwa North Sudan. Waislamu wa india wanadai haki kutoka kwa Wahindu.Wasuni wachache wa Iran wanadai haki kutoka kwa washia waliowengi wa Irani. Wakurdi wachache wa Iraki wanadai haki kutoka kwa washia na wasunni wa Iraki. Na waislamu wa Tanzania wanadai haki kutoka kwa Wakristo wa Tanzania. Wafanyakazi wanadai haki kutoka kwa Matajiri wao.Raia wanadai haki kutoka kwa Serikali. Watoto wanadai haki kutoka kwa Baba zao. Nchi za dunia ya tatu zinadai haki kutoka kwa nchi za dunia ya kwanza. Maskini wanadai haki kutoka kwa matajiri. Wasiojiweza na wazembe wanadai haki kwa wanajioweza na wenye bidii. Hii ndiyo dunia na hata yesu alisema wenye uwezo wawasaidie wasio na uwezo na maskini, na hakuangalia hata kama asiye na uwezo ni mzembe au la. Tutengeneze sera ya kuwasaidia wengine ili kupunguza migongano.Kila kundi hapo juu linalodai haki linapenda kuhalalisha kwamba upande strong ndio ulisababisha madhira ya upande wao Weak.Hawatajali wala kuangalia ulifanya nini kufikia hapo.

الثناء يسوع المسيح
 
Kesho si Ijumaa........!!
swala ifanyike pale Central police.....!!

Wachochezi utawajua tu kwa kauli zao. Tafadhali usiwachochee Waislamu kwenda Central wakapate madhara, na si ajabu wewe mwenyewe hutakuwepo. Epuka lugha za uchochezi tafadhali.
 
Back
Top Bottom