Mahita ajitosa ubunge Moro

Kukataa mtoto na ubunge ni vitu viwiwli visivyo na uhuhusiano kabisa.kama mtanzania na katiba inamruhusu atumie nafasi hiyo.
kweli wenye visa watu.

R U SURE MKUU?
Kwa uelewa wako unadhani kutafuta ubunge ni ile iweje? Ubunge ni uwakilishi wa watu wa jimbo lako - kwa maneno mengine mbunge ni mwakilishi na mtetezi wa watu kupata haki na stahili zao.Mahita alipokataa mtoto maana yake ni sawasawa na kushindwa kutekeleza kile anachotegemewa kukifanya kwa magnitude kubwa zaidi akiwa mbunge.Kama anashindwa kumtetea mtoto mmoja tena damu yake, ataweza wapi kuwatetea maelefu tena asiokuwa na nasaba nao?Labda utuambie kuwa unaamini ubunge ni kumpa mtu fursa kwenda kujitetea maslahi yake yeye binafsi.Kama ndivyo basi kagonga mwamba maana zama hizi watu wanajua haki zao.
Ushauri wa bure - kama ni ndugu yako basi mshauri aachane na hiki kipute ataaibishwa bure maana agenda yake ni irrelevant na point ya kummaliza ni ndogo sana.Na sasa ajue wanaharakati wa haki za binadamu wako macho - achilia mbali PCCB wanaoangalia rushwa kwenye uchaguzi.Kama ni vijisenti vinamsumbua basi amtunze mwanae aliyezaa namjakazi wake atapata sifa zaidi kuliko kujitosa kwenye kinayang'anyiro 2010.
 
Morogoro ni mojawapo ya majimbo ambayo hayana ubaguzi wa kikabila wala kidini. Toka mwaka 1959 wamekuwa na wabunge kutoka nje ya mkoa huo - Mbunge wa kwanza wa Morogoro alikuwa Julius Nyerere [TANU] mwaka 1959 na alimshinda Chief Patrick Kunambi [UTP]; aliyemfuata akaja Oscar Kambona [TANU] mpaka 1967 alipokosana na Julius Nyerere kwa sababu ya Azimio la Arusha.

Kambona alifuatiliwa na Amir Jamal [TANU/CCM] toka mwaka 1970 mpaka 1985 - ndipo hapo Morogoro ilipata viwanda vingi sana -kuanzia vya tumbaku, nguo; canvas; viatu; risasi/silaha; mafuta; pia mashirika kama Tumbaku; Pamba yalikuwa na makao makuu hapo Morogoro. Pia instutions nyingi za Serikali zilijengwa hapo e.g. SUA; IDM/Mzumbe University; Kigurunyembe TTC; Kilakala sec. School; TAFORI; MATI/LITI; Vikosi kadhaa vya jeshi etc. Vyote hivi vilisaidia ushindi wa Jamal kwa wakati huu. Kutoka hapo Amir Jamal akampa Shamim Khan [CCM] ambaye alibakia na ubunge mpaka 1995 wakati siasa ya vyama vingi ilipoanza.

Kwa hiyo sitashangaa Mahita akibwagwa chini licha ya yeye kuwa mzawa wa Morogoro/Kilosa! Wakina Professor Ishengoma wameshaota mizizi hapo Morogoro!
 
Wabongo bwana!!... Kila mkubwa akistaafu au akijua anakaribia kustaafu anakimbilia ubunge duh!!! Kali politics ni ishu!!!! Angalia mifano michache km Prof Msolla... alipojua umri umesogea akakimbilia kwenye ubunge, haya tena akina tibaigana/mahita wameshastaafu wanataka wagombee.. Prof Ishengoma muda umeshasogea nayeye anakimbilia hukohuko...duuuuuuuh kaaazi kweli kweli!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kila mwananchi ana haki ya kuomba uongozi ili mradi tu atimize masharti ya kisheria.

hakuna mwenye hati milki ya kuhodhi Ubunge.

Hongere sana Bi Amina said, Prof Ishengoma na Aziz Aboud na Mzee mahita kumchallenge Dr Mzeru.
 
Hakuna kitu humo ni Politics mzee wangu ndio maana Taifa limebaki vacuum bila ya watu wengi wanakwenda kwenye Politics za Kibongo
 
Wizi mtupu!!! Kwa level ya ujambazi aliopalilia akiwa IGP, hatakiwi kuwa hata kiongozi wa shina. Anatafuta mahali pa kufichia madhambi yake au kuiba kwa aina tofauti.
 
Kama kweli sasa siasa za Kibongo zimeingiliwa kuanzia kwa Tibaigana na Mahita wote wanatafuta nini
 
Kukataa mtoto na ubunge ni vitu viwiwli visivyo na uhuhusiano kabisa.kama mtanzania na katiba inamruhusu atumie nafasi hiyo.
kweli wenye visa watu.

Mkuu naona hapa hatuko pamoja
Kiongozi mwadilifu utamjua kwa matendo yake, historia yake huko nyuma inaelezwa na mambo ya kiuongo uongo na ubabe ata kwenye mambo yasiyoitaji ubabe na uongo uyu sie ndie alijiita "nguri", husitegemee mkimpa jukumu kubwa kama la ubunge atakuwa mkweli! Kitendo cha kumkataa mtoto wake mwenyewe kinaonesha alivyo mkaidi na mtu hasiyeweza kuaminiwa kupewa madaraka makubwa kama ubunge! Angekuwa muungwana tungemfahamu, lakini yote tisa, kumi nikwa wananchi wa jimbo la morogoro mjini wao ndo watakaomchagua, ila sie wanajamii hana sifa tena za kuwa kiongozi.
 
Huyu hakukataa mtoto tuu hata jeshi la polisi chini ya uongozi wake lilikuwa garbage tuu na Dar ujambazi uliongezeka na hakufanya lolote la maana,naamini watu wa Morogoro wana akili za kutosha kuzuia huyu fisadi kuwa mbunge wao
 
Back
Top Bottom