Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 77
JOTO la kuwania nafasi ya ubunge ndani la Jimbo la Morogoro Mjini limezidi kupanda, baada ya kuwapo habari za kuaminika kuwa zaidi ya watu wanne wamejitokeza kutaka kuchukua fomu katika uchaguzi mkuu ujao.
Walioamua kujitosa kwenye kinyang'anyiro hicho kukabiliana na Mbunge wa jimbo hilo, Omari Mzeru, ni pamoja na aliyewahi kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali mstaafu, Omari Mahita, Aziz Abood, Profesa Ishengoma na mwanahabari Amina Said, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuia ya Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Morogoro Mjini.
Kwa mujibu wa taarifa za ndani za kuaminika, kila mmoja anajigamba kupata nafasi hiyo ndani ya kura za maoni kupitia CCM, hali ambayo inaonyesha kuwapo upinzani mkubwa.
Kwa muda sasa, jimbo hilo limeonyesha kuwa na upinzani mkubwa wa vyama vya CCM na Chama cha Wananchi (CUF), ambapo kwa upande wa CUF, Mkurugenzi wa Siasa wa chama hicho, Mbalare Maharagande, ametangaza jana nia ya kugombea tena nafasi hiyo.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara jana wakati wa mwendelezo wa mikutano ya chama hicho iliyopewa jina la Operesheni Zinduka kwenye viwanja vya Soko la Mawenzi, alisema dalili za kujitokeza kwa wagombea zaidi ya wawili ndani ya CCM kunaonyesha wazi mbunge aliyeko madarakani ameshindwa kuwatumikia wananchi wake.
Alisema kuwa wananchi wamechoshwa na umaskini uliopo kwa sasa ingawa Morogoro ndicho kituo kikuu cha kati cha biashara, lakini hakuna hata mapato yanayoweza kusimamiwa na kuwafaidisha wananchi. Katika kadi zilizorudishwa, kulikuwa na wenyeviti wawili wa serikali za mitaa kutoka CCM, Kulwa Shaaban na Jamponi Gaston waliojiunga na CUF.
Walioamua kujitosa kwenye kinyang'anyiro hicho kukabiliana na Mbunge wa jimbo hilo, Omari Mzeru, ni pamoja na aliyewahi kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali mstaafu, Omari Mahita, Aziz Abood, Profesa Ishengoma na mwanahabari Amina Said, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuia ya Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Morogoro Mjini.
Kwa mujibu wa taarifa za ndani za kuaminika, kila mmoja anajigamba kupata nafasi hiyo ndani ya kura za maoni kupitia CCM, hali ambayo inaonyesha kuwapo upinzani mkubwa.
Kwa muda sasa, jimbo hilo limeonyesha kuwa na upinzani mkubwa wa vyama vya CCM na Chama cha Wananchi (CUF), ambapo kwa upande wa CUF, Mkurugenzi wa Siasa wa chama hicho, Mbalare Maharagande, ametangaza jana nia ya kugombea tena nafasi hiyo.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara jana wakati wa mwendelezo wa mikutano ya chama hicho iliyopewa jina la Operesheni Zinduka kwenye viwanja vya Soko la Mawenzi, alisema dalili za kujitokeza kwa wagombea zaidi ya wawili ndani ya CCM kunaonyesha wazi mbunge aliyeko madarakani ameshindwa kuwatumikia wananchi wake.
Alisema kuwa wananchi wamechoshwa na umaskini uliopo kwa sasa ingawa Morogoro ndicho kituo kikuu cha kati cha biashara, lakini hakuna hata mapato yanayoweza kusimamiwa na kuwafaidisha wananchi. Katika kadi zilizorudishwa, kulikuwa na wenyeviti wawili wa serikali za mitaa kutoka CCM, Kulwa Shaaban na Jamponi Gaston waliojiunga na CUF.