Wakuu,
Nimesikitishwa sana na kitendo cha serikali yetu kuisaidia CCM kuipa ushindi kwa kugawa mahindi ya chakula igunga kwa kisingizio eti inasadia watu, wote tunajua njaa ni adui wa haki na hata mimi ningekuwa igunga ningemuheshimu sana mtu anayenipa uhai - mtu anayenipa uhakika wa kuiona kesho.
Lakini cha kujiuliza je kwa nini mahindi yagawiwe igunga tu? tena wakati wa kampeni?. Mimi ni mwenyeji wa Tabora, ndugu zangu Tabora kuna njaa sana karibia wilaya zote je kwa nini igunga pekee ndiyo ipate chakula?
Hizi njama za wazi wazi za serikali kuisaidia CCM kwenye chaguzi na ninaungana na wananchi wenzangu kupinga hatua hii ambayo inadhoofisha demokrasia nchini.
Kutumia njaa kuwashawishi wapiga kura ni rushwa na dhambi kwa mwenyezi mungu, sikatai kugawa msosi lakini wakati wa kampeni? ndiyo maana tunasema hii Tume ya uchaguzi si tume ya taifa ila ni tume ya kuhakikisha CCM inashinda chaguzi.
Mpira gani usio na Refa? Mpira gani usio na sheria, taratibu na udhibiti? uonevu huu utaisha lini ndugu zangu? sisi sote ni watanzania tunahitaji haki, je utapataje haki kama vitui hivi vinaendelea nje nje tena bila kificho, woga wala aibu?
Nimesikitishwa sana na kitendo cha serikali yetu kuisaidia CCM kuipa ushindi kwa kugawa mahindi ya chakula igunga kwa kisingizio eti inasadia watu, wote tunajua njaa ni adui wa haki na hata mimi ningekuwa igunga ningemuheshimu sana mtu anayenipa uhai - mtu anayenipa uhakika wa kuiona kesho.
Lakini cha kujiuliza je kwa nini mahindi yagawiwe igunga tu? tena wakati wa kampeni?. Mimi ni mwenyeji wa Tabora, ndugu zangu Tabora kuna njaa sana karibia wilaya zote je kwa nini igunga pekee ndiyo ipate chakula?
Hizi njama za wazi wazi za serikali kuisaidia CCM kwenye chaguzi na ninaungana na wananchi wenzangu kupinga hatua hii ambayo inadhoofisha demokrasia nchini.
Kutumia njaa kuwashawishi wapiga kura ni rushwa na dhambi kwa mwenyezi mungu, sikatai kugawa msosi lakini wakati wa kampeni? ndiyo maana tunasema hii Tume ya uchaguzi si tume ya taifa ila ni tume ya kuhakikisha CCM inashinda chaguzi.
Mpira gani usio na Refa? Mpira gani usio na sheria, taratibu na udhibiti? uonevu huu utaisha lini ndugu zangu? sisi sote ni watanzania tunahitaji haki, je utapataje haki kama vitui hivi vinaendelea nje nje tena bila kificho, woga wala aibu?