Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,082
MAHARUSI WAPUUZA MBWEMBWE, WASAFIRI KWA BODABODA'
Maharusi hao wakiwa kwenye bodaboda baada ya kufunga ndoa.
KATIKA kile kilichoonekana kupuuza mbwembwe za harusi, maharusi wawili walioamua kufunga ndoa maeneo ya Uwanja wa Ndege katika Manispaa ya Morogoro hivi karibuni, waliamua kutumia usafiri wa pikipiki ambazo ni maarufu kama Bodaboda na kuyapa kisogo magari ya kifahari licha ya kuwa walikuwa na uwezo wa kuyatumia.
Maharusi hao ambao majina yao hayakupatikana, walifunga ndoa yao ya Kiislam na baadaye kuanza kuelekea nyumbani maeneo ya Mawezi ambapo walitumia usafiri huo wa pikipiki ambayo ilikuwa imepambwa maalum kwa ajili yao ambapo waliwaacha watu wengi waliohudhuria wakishangaa.
Pamoja na vimatatizo kadhaa vilivyoambatana na usafiri huo, bado shughuli yote ilifana na kuwaacha watu wengi wakipongeza hatua hiyo ya aina yake katika shughuli za kufunga ndoa.
ZIFUATAZO NI PICHA ZA TUKIO HILO:
PICHA NA DUNSTAN SHEKIDELE, /GPL, MOROGORO