Uncle Jei Jei
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 1,684
- 2,157
Zamani wakati wa harusi, bibi harusi alikuwa hawezi hata kumtizama padri au mchungaji anapofungisha ndoa! Mda mwingi alikuwa kainama kitu kilichotafsiriwa kuwa alikuwa na aibu aibu na heshima kwa mumewe! Siku hizi mambo tofauti kabisa,! Utakuta bibi harusi katoa macho, muda wote anacheka, achilia mbali wengine kuserebuka ukumbuni mpaka jasho kuwatoka! Kifupi, wengi wao wanakuwa hawana utulivu kama tuliozoe kuuona, kinyume chake mwanaume ndo huonyesha utulivu! Jamani, hii husababishwa na nini?? Wadada mnaotarajia kuolewa, jaribuni kutulia siku ya harusi, msituache na mishangao!