Mahari bei gani

Hakuna bei gani is right wal bei gani is wrong.(hata angetumia "kiasi gani kinafaa," dhana ni ile ile)

Mahari ni zawadi kimsingi kwa hiyo inaweza kuwa kumfundisha kusoma na kuandika, pete ya bati au shehena nzima abebeshwayo ngamia. Zawadi haiwezi kupangiwa kiasi

Mwanamme anampa zawadi mwanamke kwa kukubali kuwa wake wa milele, kumzalia watoto na hata kuchukua jina lake wakati mwingi mwengine

Hakuna suala la utumwa hapo, mbona mwanamke anabadili jina na kuwa la mwanamme na hawi mtumwa wake?

Kama zawadi basi angemwambia "nichagulie unayotaka".

Hili lishakuwa dili sasa.

Na kama zawadi mbona anapewa mwanamke tu?
 
Nimefurahi kukuona, tangu siku nikuwekee "chapati" ukapotea moja kwa moja, au ndo ulienda nawe kugombania? :lol:
Hahahahaha... Gaijin umeanza kunichokoza...chokochoko mchokoe pweza...nimekaa Zanzibar wiki mbili utanikoma na maneno yangu sasa hivi :lol::lol:
 
Last edited by a moderator:
Huyu mchumba alikuwa HG au? Maana mil 4 ni kidogo sana kuwa mahari kwa nyakati za sasa...!
 
Mahari ni ujinga kabisa,mie binti yangu siwezi kumuuza kabisa hakuna hela ambayo ina worth utu wake! Nampa Bure tu akajisosomole!!!
 
Kama zawadi basi angemwambia "nichagulie unayotaka".

Hili lishakuwa dili sasa.

Na kama zawadi mbona anapewa mwanamke tu?


Ndio hasa msingi uliopo kuwa "nichagulie unayotaka" na mwanamme kwa kujitutumua husema "nitakupa utakacho wewe" ndio akaambiwa bibie anachokitaka.

Kwa hiyo ni suala la kukubaliana baina ya hao wapeana zawadi, kisha kwa wazazi ni kwenda rasimisha na kuthibitishiana mapenzi mbele ya wazazi ......

..........Na mwanamme anapewa, sema kwa siri siri.......:lol:
 
Hahahahaha... Gaijin umeanza kunichokoza...chokochoko mchokoe pweza...nimekaa Zanzibar wiki mbili utanikoma na maneno yangu sasa hivi :lol::lol:

......binaadamu hutomuweza! Shushu hilo la nguvu :dance:

Naona kweli huko Zanzibar kumekufunda, umeanzia na gia ya reverse kabisa!
 
Ndio hasa msingi uliopo kuwa "nichagulie unayotaka" na mwanamme kwa kujitutumua husema "nitakupa utakacho wewe" ndio akaambiwa bibie anachokitaka.

Kwa hiyo ni suala la kukubaliana baina ya hao wapeana zawadi, kisha kwa wazazi ni kwenda rasimisha na kuthibitishiana mapenzi mbele ya wazazi ......

..........Na mwanamme anapewa, sema kwa siri siri.......:lol:

Hatutaki siri zama za ukweli na uwazi huu.

Ndio maana wengine kuoa tunakusikia kwenye bomba tu, mambo yenyewe biashara ya utumwa?
 
Hatutaki siri zama za ukweli na uwazi huu.

Ndio maana wengine kuoa tunakusikia kwenye bomba tu, mambo yenyewe biashara ya utumwa?

Kama wewe hutaki siri, utamwambia akitangaze hicho alichokupa ili wende sambamba na zama za uwazi na ukweli.

Mahari yakifutwa ili kuondoa dhana ya utumwa, na kubadilisha jina kuchukua la ukoo wa mume nako kufutwe ili utumwa umalizike kabisa

Vijana inabidi wapelekwe jando kufundishwa uanamume.

Kwa hiyo mwanamme mwenye uanaume hasa haulizi, akiambiwa milioni nne na yeye ana elfu 20 anafanya nini?
A%20S%20embarassed.gif
 
Kama wewe hutaki siri, utamwambia akitangaze hicho alichokupa ili wende sambamba na zama za uwazi na ukweli.

Mahari yakifutwa ili kuondoa dhana ya utumwa, na kubadilisha jina kuchukua la ukoo wa mume nako kufutwe ili utumwa umalizike kabisa



Kwa hiyo mwanamme mwenye uanaume hasa haulizi, akiambiwa milioni nne na yeye ana elfu 20 anafanya nini?
A%20S%20embarassed.gif

Tangia hapo mi sitaki kumpa jina langu mtu mwingine kama bwana wa mtumwa.

Mwanamme mwenye uanamme hasa atajua anasimama wapi.

Ama mambo ya upuuzi wa mahari hayataki na atachagua mwanamke wanayeendana naye asiyetaka kulipiwa mahari.

Ama kama anayataka atajua kwamba huyo mwanamke wake "chuna buzi" si mtu sahihi wa kumuuliza hilo.

Watoto hawa wanavamia mambo kwa pupa.Usikute hata neno "mshenga" halijui.

Mie abadan habari hizi.
 
Hapa nadhani suala ni unalipa kwa nani? Kama baba wa mtoto na mume mnabadilishana mtoto kwa mahari, inaweza kuwa na mantiki hiyo uliyotaja. Lakini ikiwa ni binti mwenyewe ndie anaepanga mahari, na ndie anaekabidhiwa hicho alichopewa kama tunzo au tunu kutoka kwa mume wake mtarajiwa, sioni ila hapo.

Nijuavyo mimi mahari hutolewa kwa familia ya binti na mara nyingi baba hupokea kwa sababu yeye ndiye huhesabika kama kiongozi wa familia.

Sijawahi sikia binti akipanga na kupokea mahari mwenyewe. Ni utaratibu wa wapi huo?

Tukumbuke kuwa mahari si lazima yawe mali.

Una mfano wa jamii ambazo kwao hawatoi mahari ambazo ni mali?
 
Well. . . .Mil 4!Nanunua gari?Mahari?Kwani kuna nini kwenye kuoa?
 
Mahari kimsingi inategemea watu na watu. Hata wasiokuwa yatima, wenye wazazi wote hai hadi babu na bibi, wapo wanaompa mahari yote anaeolewa.

Kimsingi kwao mahari ni ya anaeolewa (na yeye ndie husema iwe kiasi gani wakati mwengine) na akiamua kuwagaia wazazi wake ni kwa mapenzi yake tu.

Wewe usie jamaa bila ya shaka ni yako wewe na wewe ndie utakaepanga atoe ngapi.

Hivi anayeolewa zaidi ya mara moja naye anatakiwa kupokea mahari kwenye kila ndoa mpya?
 
Tangia hapo mi sitaki kumpa jina langu mtu mwingine kama bwana wa mtumwa.

Mwanamme mwenye uanamme hasa atajua anasimama wapi.

Ama mambo ya upuuzi wa mahari hayataki na atachagua mwanamke wanayeendana naye asiyetaka kulipiwa mahari.

Ama kama anayataka atajua kwamba huyo mwanamke wake "chuna buzi" si mtu sahihi wa kumuuliza hilo.

Watoto hawa wanavamia mambo kwa pupa.Usikute hata neno "mshenga" halijui.

Mie abadan habari hizi.

Hahaha kwa hiyo wadai mahari wote ni "chuna buzi"!!!

Nyinyi ndo mnaiharibu dhana nzima ya mahari, mie nataka kudai kutungiwa shairi, hapo chuna buzi imehusikaje?

Nasindikiza kwa muziki
"Si hasara asilani, nyuki kufa asalini
Tuchekeni, furahani haha haha haha haha
 
Nijuavyo mimi mahari hutolewa kwa familia ya binti na mara nyingi baba hupokea kwa sababu yeye ndiye huhesabika kama kiongozi wa familia.

Sijawahi sikia binti akipanga na kupokea mahari mwenyewe. Ni utaratibu wa wapi huo?

Una mfano wa jamii ambazo kwao hawatoi mahari ambazo ni mali?

Ujuavyo wewe si sahihi. Jamii za nchi za Asia kama Indonesia, Malaysia, Brunei na Kiarabu mahari anapanga binti na anakabidhiwa yeye akishayapokea.

Namjua dada mmoja Mu-Indonesia, alidai mahari mwanamme ajifundishe Quran yote kwa moyo kisha ndio ende akamuoe (hili halikuwa na faida kwa mwanamke moja kwa moja, alidhani akiweza hilo maisha yake yatakwenda kwa taratibu za dini anayoiamini tu)

Kwa hiyo wasiodai mali wapo tele duniani.
 
Back
Top Bottom