Lole Gwakisa
JF-Expert Member
- Nov 5, 2008
- 4,726
- 2,255
- Thread starter
- #61
Si afadhali hawa wanaojenga hapa kuliko hawa maharamia wa madini ambao watatuachia mashimo na sumu ardhini baada ya kuondoka na kila kitu,Gwasika pia nahisi una personal vendetta baada ya kukwaruzana na mmoja kwenye biashara this is beyond hate.
Mkuu uporoto1, nashindwa kundi la kukuweka, pamoja na facts zote zilizochangiwa hapa.
Sijui kama ni ugumu wa kuelewa au kutokuwa na uwezo wa kufikiri sijui.
Pengine tuweke kwa lugha rahisi ambayo unaweza kuielewa vizuri.
Unaambiwa kitandani kwako kuna nyoka mwenye sume-wee unajibu upuuzi huo nyoka ataingiaje katika nyumba nzuri hii na ina magrilli.
Unaambiwa , jirani yako ameumwa na nyoka jana tu-wee unasema aah bahati mbaya tu.
Na wewe huchukui tahadhari yoyote.
Sasa mkuu kama wewe uporoto1 kuumwa na nyoka ni stahili yako.
Uporoto1 kuniweka katika kundi la kuwa na bifu na hawajamaa (Wasomali) ni kujiaibisha kwa upande wako kwa vile swali langu la kwanza ni kutafuta ukweli, kitu ambacho kimedhihirika kutokana na michango tofauti.
Mkuu uporoto1, una matatizo ya kimsingi na hakuna uafadhali wa maharamia wala wale wanaoacha sumu ardhini katika migodi.
Na hapo ndo unaonekana huna dira ya kimaisha kama mtanzania.