Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,894
Waziri Mahanga akimbilia mahakamani kudai fidia ya Sh3bilioni
Na James Magai
10/26/2009
NAIBU waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Dk Makongoro Mahanga amemshtaki mkazi wa jijini, Kainerugaba Msemakweli pamoja na gazeti la Nipashe akidai fidia ya Sh3bilioni kwa madai ya kumkashifu.
Mbali na Msemakweli ambaye ni mdaiwa wa kwanza na Nipashe (mdaiwa wa tatu), wengine walioshtakiwa katika kesi hiyo ya madai namba 145 ya mwaka 2009 ni mwandishi wa habari wa gazeti hilo Muhibu Said, ambaye ni mdaiwa wa pili na Kampuni ya The Guardian Limited, ambayo ni mdaiwa wa nne.
Katika hati yake ya madai iliyowasilishwa na wakili wake Kenedy Fungamtama, Mahanga anadai kuwa alikashifiwa na washtakiwa hao kuwa ameghushi vyeti vya shahada ya uzamivu.
Kwa mujibu wa hati hiyo mdaiwa wa kwanza (Msemakweli) anadaiwa kuitisha mkutano wa waandishi wa habari Oktoba 18 mwaka huu na kutoa taarifa kwamba amefanya uchunguzi na kubaini kuwa Makongoro hajawahi kusoma shahada hiyo wakati wowote na mahali popote duniani.
Mdaiwa wa pili, wa tatu na wa nne wadaiwa kuandika, kuchapisha uongo na kwa nia mbaya taarifa hiyo iliyotolewa na mdaiwa wa kwanza katika ukurasa wa mbele wa gazeti la Nipashe, toleo la namba 05443 la Oktoba 19, ikiwa na kichwa cha habari "Vyeti vya Elimu: Mawaziri sita wanasa"
Habari hiyo iliambatana na vichwa vidogo vya habari kuwa vyeti vyao vya elimu vyadaiwa kuwa na mushikeli. Yumo mkuu wa mkoa na wabunge watatu; Orodha yawasilishwa kwa spika wa Bunge.
Mahanga anadai katika hati hiyo kuwa taarifa hizo zilishusha heshima ya mlalamikaji katika jamii na kwamba kutokana na nafasi yake kama naibu waziri na mbunge imemuathiri kisaikolojia. Mlalamikaji huyo anaiomba mahakama iwakemee wadaiwa kwa hatua hiyo na kuwaamuru wamlipe fidia ya Sh3 bilioni au kiasi ambacho mahakama itaridhika nacho, lakini kisichopungua Sh200,000, gharama zote za kesi, kuwaagiza kuomba radhi kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti hilo, kuzuia wadaiwa na wakala wao kurudia kuchapisha na kusambaza habari hiyo au habari yoyote kuhusiana na mlalamika huyo .
Na James Magai
10/26/2009
NAIBU waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Dk Makongoro Mahanga amemshtaki mkazi wa jijini, Kainerugaba Msemakweli pamoja na gazeti la Nipashe akidai fidia ya Sh3bilioni kwa madai ya kumkashifu.
Mbali na Msemakweli ambaye ni mdaiwa wa kwanza na Nipashe (mdaiwa wa tatu), wengine walioshtakiwa katika kesi hiyo ya madai namba 145 ya mwaka 2009 ni mwandishi wa habari wa gazeti hilo Muhibu Said, ambaye ni mdaiwa wa pili na Kampuni ya The Guardian Limited, ambayo ni mdaiwa wa nne.
Katika hati yake ya madai iliyowasilishwa na wakili wake Kenedy Fungamtama, Mahanga anadai kuwa alikashifiwa na washtakiwa hao kuwa ameghushi vyeti vya shahada ya uzamivu.
Kwa mujibu wa hati hiyo mdaiwa wa kwanza (Msemakweli) anadaiwa kuitisha mkutano wa waandishi wa habari Oktoba 18 mwaka huu na kutoa taarifa kwamba amefanya uchunguzi na kubaini kuwa Makongoro hajawahi kusoma shahada hiyo wakati wowote na mahali popote duniani.
Mdaiwa wa pili, wa tatu na wa nne wadaiwa kuandika, kuchapisha uongo na kwa nia mbaya taarifa hiyo iliyotolewa na mdaiwa wa kwanza katika ukurasa wa mbele wa gazeti la Nipashe, toleo la namba 05443 la Oktoba 19, ikiwa na kichwa cha habari "Vyeti vya Elimu: Mawaziri sita wanasa"
Habari hiyo iliambatana na vichwa vidogo vya habari kuwa vyeti vyao vya elimu vyadaiwa kuwa na mushikeli. Yumo mkuu wa mkoa na wabunge watatu; Orodha yawasilishwa kwa spika wa Bunge.
Mahanga anadai katika hati hiyo kuwa taarifa hizo zilishusha heshima ya mlalamikaji katika jamii na kwamba kutokana na nafasi yake kama naibu waziri na mbunge imemuathiri kisaikolojia. Mlalamikaji huyo anaiomba mahakama iwakemee wadaiwa kwa hatua hiyo na kuwaamuru wamlipe fidia ya Sh3 bilioni au kiasi ambacho mahakama itaridhika nacho, lakini kisichopungua Sh200,000, gharama zote za kesi, kuwaagiza kuomba radhi kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti hilo, kuzuia wadaiwa na wakala wao kurudia kuchapisha na kusambaza habari hiyo au habari yoyote kuhusiana na mlalamika huyo .