Mahakama Kuu ya Tanzania kuzuia malipo kwa DOWANS?

Hapo bado sijakuelewa. Mahakama Kuu itawezaje ku annul kitu ambacho yenyewe haikuwa privy? Ninachoweza kuelewa ni kama watakataa kuiandikisha na kuitarifu International Court of Arbitration kuhusu sababu zao, ambao kama watakubaliana nao, ndio watakaoweza ku-set aside award. Na mahakama yetu itatoaje uamuzi kuhusu kuweko kwa rushwa wakati haina mandate ya kuchunguza? Watasemaje kuwa pana rushwa hapa bila prosecutors kuwapelekea ushahidi wa kitendo hicho kuwepo? Hapa si Spain au Italy ambako Mahakama wana madate ya kuchunguza. Halafu hilo la public interest/policy litakuwa gumu mno kulitetea maana wengi wametumia kama fig leaf ya kuwadhulumu wengine.

Wanasheria wa Tanesco walikuwa na uwezo wa kukataa hiyo provision maana si lazima iwepo. Lakini ukweli ni kuwa hakuna mtu ambaye anaingia katika mkataba wa kimataifa atakayekubali kuwa dispute ziwe resolved kwa litigation au arbitration laws za upande mmoja. Tanesco wangekataa , wangeonyesha bad faith.

Mimi naamini gharama kubwa zaidi ya kutoheshimu uamuzi huu si kukamatwa kwa asset zetu bali ni kupoteza credibility duniani. Kwa kufanya hivyo, gharama za kufanya biashara na wenzetu zitapanda sana. Au mbaya zaidi, wafanyabiashara wwale wanaojiheshimu watatukwepa na kutubakiza na matapeli.

Tulipe na tujifunze kutokana na hili. Mikataba si lele mama.

Amandla......
Mimi nauelewa wangu mdogo wa sheria sijawahi ona na sitaraji kuona hukumu yoyote dunia ambayo haiwezi kupitiwa upya au kupitiwa upya, hata iran na sheria zao za kiislamu lakini bado tunaona kuna hukumu za kifo/ kupigwa mawe zinapitia na kutolewa uamuzi upya.
sasa tukija katika suala la dowans na icc, bado naamini kuna njia za kuweza kulirejea jambo hilo kwa mfano kama alivyo sema fareed kwamba ppa haikutumika ipasavyo, kulikuwa na issue of fraud or even rushwa katika kuingia kwa mkataba huo, sasa sema kwa kuwa gt ndio watoaji rushwa wenyewe hawawezi kutumia kifungu hiki kujishtaki.
na kuhusu mambo ya abitration ni njia mbadala ambayo inakuwa encourage kufwatwa katika commercial issues, lakini upande moja ukishindwa kuridhia then case inaweza kwenda kwenye full hearing iwe costa rica au tanzania.
sasa mtu unapo sema wanaweza kuattach mali yetu , watakuwa wametumia amri ya mahakama ipi? mahali ambapo mali ya tanzania inaweza kuattach labda amri itoke kwenye mahakama huko costa rica/tanzania ambapo hawa jamaa wakiweza kusajili huu uamuzi na mahakama hiyo itoe uamuzi huo ku-enforce icc ruling.
mahali ambapo mali ya tanzania iliwahi kushikwa ni pale mwl alipo taifisha mali ya muholanzi moja steyn aliyekuwa na mashamba huko arusha na kuchukuliwa na nafco, nakumbuka kwa mbali walizuia meli ya mafuta iliyo kuwa inakuja bongo.
kuhusu suala la reputation hatuta poteza reputation yoyote kwa kushindwa kutekeleza amri ya kuilipa kampuni ya kitapeli-costa rica? ingekuwa bae system , airbus, boeng, gm etc ningekuelewa lakini kampuni ya costa rica iliyo tumia rushwa au fraud kupata contract. basi mambo ya fair trade , or equal playing field lingekuwa halizungumziwi.
rejea weakleaks ya airbus vs boeing na rejea hukumu dhidi ya bae system usa na uk.
halafu pia rejea case kama ya micro soft walivyo pigwa faini kwenye mahakama za eu, halafu uende kwenye case ya toyota wanavyo nyanyaswa huko usa.
ni sisi kusi mama kama nchi na kunyongana na mtu kwa sheria zetu.
 
Pamoja na kwenda ICC, The Arbitration Act inasema kuwa Mahakama ya Tanzania ndiyo yenye uamuzi wa mwisho iwapo maamuzi ya ICC yatekelezwe au la. Hivyo mwenye final say kwenye hili jambo ni the High Court of Tanzania na si ICC kwani ruling ya ICC lazima iwe registered kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania na mahakama iseme kama malipo haya ni halali au siyo halali na kuyakataa. Kama ilivyokuwa quoted kwenye hii habari ya THISDAY, sheria ya Tanzania inasema:

"Where an arbitrator or umpire has misconducted himself or an arbitration or award has been improperly procured, the court may set aside the award."


Mahakama Kuu ikifanya kweli tutaona akina Werema, Pinda, Ngeleja watatokea mlango upi....lakini kwa nchi yetu ilivyokuwa ya kifisadi hao watakaohusika na uamuzi huu kule mahakama kuu watakuwa kwenye shinikizo la hali ya juu ili wafanye maamuzi ya kuukamilisha ufisadi wa Dowans.

 
Kitendo hiki cha ICC kuidharau sheria ya Tanzania kwenye hukumu yake kinaweza kabisa kutafsiriwa kuwa hukumu hii ya ICC in favour of Dowans has been "improperly procured" hence the High Court of Tanzania may set aside the award.

Are you talking about manifest disregard of the law? Here the AA would be clear. Kutofuata sheria sawasawa si sawa na kupata hukumu improperly. That is literal meaning rather than legal meaning. Hata hivyo improperly procured award yaweza kuwa si rushwa tu hata ubaguzi dhidi ya one of the parties na masuala mengine ya maadili kwa arbitrators. Asante kwa maelezo yako ya ufafanuzi yenye mantiki
 
Ahsante kwa mchango wako, lakini nadhani tafsiri ya "improperly procured" kwenye sheria haimaanishi kuwa lazima ICC award iwe imetokana na rushwa peke yake. The term "improperly procured" can be interpreted in many different ways, ndiyo maana imewekwa hivyo ili mahakama itumie busara kufanya interpretation yake. Ingekuwa maana ya hiyo phrase ni rushwa tu peke yake (exclusively referring to corruption) basi sheria ingesema hivo. Imeweka the term "improperly procured" kwa makusudi ili mahakama itumie busara yake kusema ni vitendo gani vinaendana na hiyo caveat.

Mimi si member of the Tanzanian judiciary, lakini kwa mtazamo wangu ICC has deliberately and unlawfully disregarded sheria halali ya Tanzania ya Public Procurement ya mwaka 2004 ambayo inasema wazi kuwa mkataba wa aina ya Richmond/Dowans na TANESCO is an illegal contract, hence TANESCO's decision to terminate the said contract.

Kitendo hiki cha ICC kuidharau sheria ya Tanzania kwenye hukumu yake kinaweza kabisa kutafsiriwa kuwa hukumu hii ya ICC in favour of Dowans has been "improperly procured" hence the High Court of Tanzania may set aside the award.

Soma article 6. 65.4 ya rule zao. Hata kama mkataba ni null and void lakini as long as kipengele hicho kilikuwepo hapo awali basi ICC bado wana jurisdiction. Haya maswala unayokazania hapa recourse yake ni litigation kwa kuishtaki Dowans kwa fraud., kitu ambacho ICC haihusiki. Nadhani wengi tuliingia mkenge tukidhani ICC walikuwa wanaangalia uhalali wa mkataba wakati wao walikuwa wanaangalia uhalali wa MADAI ya Dowans. Na ndicho hicho walichoamua. Service ilitolewa na Tanesco walistahili kumlipa Dowans, full stop. Au nimekosea?

Amandla....
 
Mimi nauelewa wangu mdogo wa sheria sijawahi ona na sitaraji kuona hukumu yoyote dunia ambayo haiwezi kupitiwa upya au kupitiwa upya, hata iran na sheria zao za kiislamu lakini bado tunaona kuna hukumu za kifo/ kupigwa mawe zinapitia na kutolewa uamuzi upya.
sasa tukija katika suala la dowans na icc, bado naamini kuna njia za kuweza kulirejea jambo hilo kwa mfano kama alivyo sema fareed kwamba ppa haikutumika ipasavyo, kulikuwa na issue of fraud or even rushwa katika kuingia kwa mkataba huo, sasa sema kwa kuwa gt ndio watoaji rushwa wenyewe hawawezi kutumia kifungu hiki kujishtaki.
na kuhusu mambo ya abitration ni njia mbadala ambayo inakuwa encourage kufwatwa katika commercial issues, lakini upande moja ukishindwa kuridhia then case inaweza kwenda kwenye full hearing iwe costa rica au tanzania.
sasa mtu unapo sema wanaweza kuattach mali yetu , watakuwa wametumia amri ya mahakama ipi? mahali ambapo mali ya tanzania inaweza kuattach labda amri itoke kwenye mahakama huko costa rica/tanzania ambapo hawa jamaa wakiweza kusajili huu uamuzi na mahakama hiyo itoe uamuzi huo ku-enforce icc ruling.
mahali ambapo mali ya tanzania iliwahi kushikwa ni pale mwl alipo taifisha mali ya muholanzi moja steyn aliyekuwa na mashamba huko arusha na kuchukuliwa na nafco, nakumbuka kwa mbali walizuia meli ya mafuta iliyo kuwa inakuja bongo.
kuhusu suala la reputation hatuta poteza reputation yoyote kwa kushindwa kutekeleza amri ya kuilipa kampuni ya kitapeli-costa rica? ingekuwa bae system , airbus, boeng, gm etc ningekuelewa lakini kampuni ya costa rica iliyo tumia rushwa au fraud kupata contract. basi mambo ya fair trade , or equal playing field lingekuwa halizungumziwi.
rejea weakleaks ya airbus vs boeing na rejea hukumu dhidi ya bae system usa na uk.
halafu pia rejea case kama ya micro soft walivyo pigwa faini kwenye mahakama za eu, halafu uende kwenye case ya toyota wanavyo nyanyaswa huko usa.
ni sisi kusi mama kama nchi na kunyongana na mtu kwa sheria zetu.

Ndio maana nilisema kuwa mambo hayayanahitaji tuwe sober sana na naona mjadala hapa unakuwa sober. Arbitration agreement ikisema haina appeal ndio hivyo haina appeal. Suala la kupitia hukumu ni suala la conventional system. Kama TANESCO wanahoja ya msingi wanapaswa kuanzisha proceedings za ku set aside, vacate au annul the award. Mahakama Kuu haina power zozote za kusema itapitia hukumu. Tusidanganyane. Rhetorics hazitatusaidia kitu maana zitaishia kuwa kelele tu.
 
So if what you are saying is true
Soma article 6. 65.4 ya rule zao. Hata kama mkataba ni null and void lakini as long as kipengele hicho kilikuwepo hapo awali basi ICC bado wana jurisdiction. Haya maswala unayokazania hapa recourse yake ni litigation kwa kuishtaki Dowans kwa fraud., kitu ambacho ICC haihusiki. Nadhani wengi tuliingia mkenge tukidhani ICC walikuwa wanaangalia uhalali wa mkataba wakati wao walikuwa wanaangalia uhalali wa MADAI ya Dowans. Na ndicho hicho walichoamua. Service ilitolewa na Tanesco walistahili kumlipa Dowans, full stop.

So whats the heck ..TOP LEGAL EXPERTS IN GOVERNMENT... mean???

According to top legal experts in government, the High Court is well-placed to reject the ICC ruling because of gross irregularities in the proceedings of the case and the illegallity of the actual ruling itself.

Section 15 of the Arbitration Act gives the High Court of Tanzania outright powers to dismiss the ICC ruling.

"Where an arbitrator or umpire has misconducted himself or an arbitration or award has been improperly procured, the court may set aside the award," says the legislation.

Dont these so called experts know what they are saying????
:angry: Am flipping tired of this Country.....
 
Soma article 6. 65.4 ya rule zao. Hata kama mkataba ni null and void lakini as long as kipengele hicho kilikuwepo hapo awali basi ICC bado wana jurisdiction. Haya maswala unayokazania hapa recourse yake ni litigation kwa kuishtaki Dowans kwa fraud., kitu ambacho ICC haihusiki. Nadhani wengi tuliingia mkenge tukidhani ICC walikuwa wanaangalia uhalali wa mkataba wakati wao walikuwa wanaangalia uhalali wa MADAI ya Dowans. Na ndicho hicho walichoamua. Service ilitolewa na Tanesco walistahili kumlipa Dowans, full stop. Au nimekosea?

Amandla....

Yote yaliangaliwa, hata uhalali wa mkataba maana hoja hii ya uhalali TANESCO waliitoa kama defence yake ya kuvunjwa kwa mkataba.

Suala la Rushwa, ni suala ambalo linaweza kusaidia kweli kukwepa kuwalipa dowans. Mahakama ikipewa uhakika wa kuwepo kwa rushwa itakuwa ni rahisi sana kuamua. Hebu tukumbushane, katika Richmond ni nani alitajwa kula au kutoa rushwa na kiwango gani? Zikipaikana affidavit za watu kuhusu kuwepo kwa rushwa inaweza kusaidia. Kwenye Radar kwa mfano tuliambiwa kiwango na hata nani walipata rushwa. Kwenye Richmond hili swala lipoje? Can somebody prove to the court beyond doubts kuwa rushwa ilitembea?
 
NY Convention inahusika hapa kwani one of the parties is foreign ie Dowans SA. DTL ni ya Tanzania kama subsidiary ya Dowans SA na katika kesi ni Dowans SA na Dowans T ltd v TANESCO. Arbitral situs, Dar na laws of Tanzania applicable. Kwa kusoma kwangu kidogo arbitration hii ni foreign award kwa maana ya kuwa mmoja wa washitaki ni foreign. Siioni hii kama domestic award ambapo NYC isinge apply. I stand to be corrected.

Nimeisoma arbitration provision. Hata hivyo kama TANESCO wana uhakika kulikuwa na bribery katika kufikia uamuzi au masuala ya maadili kwa arbitrators wanaweza kuanzisha mchakato wa ku set aside, vacate au annul the award. Ni jukumu la TANESCO kufanya hivi na sio mahakama kuamua baada ya Dowans kuanza mchakato wa ku confirm the award.

Nime refer kwenye dictionary sasa hivi, neno "improper" lina maana ifuatayo: "not conforming to legality, moral law, or social convention." Kwa hiyo hapa, the onus of proof is not on TANESCO to prove beyond reasonable doubt kuwa kulikuwa kuna bribery kwenye utoaji wa ruling ya ICC. Hata kama bribes exchanged hands huko ICC, it's impossible for anyone to prove this.

Mahakama has a legal and moral obligation kupitia ruling ya ICC kuona kama haki ilitendeka. Haiwezi tu kuikubali blindly, kwani inaweza kuwa inabariki kitu ambacho ni illegal.

Tukirejea tena The Arbitration Act of Tanzania:

"Where an arbitrator or umpire has misconducted himself or an arbitration or award has been improperly procured, the court may set aside the award."

Kitendo cha kuwa hukumu ya ICC imekiuka sheria ya Tanzania ya Public Procurement ya mwaka 2004 kina maana kuwa hukumu ya ICC ni "improper" because it does not conform to legality.

Suala la bribery au rushwa ni aspect moja tu ya "improperly procured," hatuna haja ya kwenda huko kwa kuwa ni vigumu kuwa na evidence ya corruption. Hoja nzito hapa ya kuweza kutumia kipengele hiki cha sheria ni kuwa ruling ya ICC does not conform to legality (Public Procurement Act of Tanzania, 2004), hence Mahakama Kuu inatupilia mbali hukumu wa ICC.
 
So if what you are saying is true


So whats the heck ..TOP LEGAL EXPERTS IN GOVERNMENT... mean???


Dont these so called experts know what they are saying????
:angry: Am flipping tired of this Country.....

kwa media zetu huyo top legal expert aweza kuwa wa kuchongwa maana hata namna habari yenyewe ilivyoandikwa imenitia mashaka sana na hata uelewa wa mwandishi mwenyewe kuhusu masuala ya arbitration. Top legal expert Serikalini ni AG au Mkurugenzi wa Sheria za Kimataifa........ i doubt hawa wamesema haya.
 
Naona kuna ugumu wa kukubali kilicho wazi tangu siku ya kwanza - kabla haya hawajaenda kwa ICC - nilisema Dowans watalipwa no matter what. Nilitoa hoja wakatu le tungeikamata mitambo na kulipa gharama ya kuichukua kwa nguvu. Lakini sasa hivi tunajaribu kutafuta kuridhishana tu uwekli nikuwa tuwalipe yaishe.

Na tukimaliza tujiandae kuwalipa wa Airbus na wale wengine kwani guess what vipengele vya aina hiyo hiyo vimo. Tuendelee kuwalipa hadi tutapoona kweli inatosha.
 
Nime refer kwenye dictionary sasa hivi, neno "improper" lina maana ifuatayo: "not conforming to legality, moral law, or social convention." Kwa hiyo hapa, the onus of proof is not on TANESCO to prove beyond reasonable doubt kuwa kulikuwa kuna bribery kwenye utoaji wa ruling ya ICC. Hata kama bribes exchanged hands huko ICC, it's impossible for anyone to prove this.

Mahakama has a legal and moral obligation kupitia ruling ya ICC kuona kama haki ilitendeka. Haiwezi tu kuikubali blindly, kwani inaweza kuwa inabariki kitu ambacho ni illegal.

Tukirejea tena The Arbitration Act of Tanzania:

"Where an arbitrator or umpire has misconducted himself or an arbitration or award has been improperly procured, the court may set aside the award."

Kitendo cha kuwa hukumu ya ICC imekiuka sheria ya Tanzania ya Public Procurement ya mwaka 2004 kina maana kuwa hukumu ya ICC ni "improper" because it does not conform to legality.

Suala la bribery au rushwa ni aspect moja tu ya "improperly procured," hatuna haja ya kwenda huko kwa kuwa ni vigumu kuwa na evidence ya corruption. Hoja nzito hapa ya kuweza kutumia kipengele hiki cha sheria ni kuwa ruling ya ICC does not conform to legality (Public Procurement Act of Tanzania, 2004), hence Mahakama Kuu inatupilia mbali hukumu wa ICC.

very good arguments. Sasa hii hukumu imekiuka vipi sheria ya manunuzi? Hukumu imeonyesha mapungufu ya sheria ya manunuzi. soma 510 ya hukumu. Labda sijaelewa unifafanulie zaidi. TANESCO walijenga hoja ya illegality ya mkataba kwa mujibu wa PPA of 2004 na Tribunal imejenga hoja zake kwa sheria hiyo hiyo. Nifafanulie kuhusu kudharau PPA by the Tribunal. Kwa mwono wangu hukumu imezigatia vifungu vya sheria ya manunuzi.
 
Naona kuna ugumu wa kukubali kilicho wazi tangu siku ya kwanza - kabla haya hawajaenda kwa ICC - nilisema Dowans watalipwa no matter what. Nilitoa hoja wakatu le tungeikamata mitambo na kulipa gharama ya kuichukua kwa nguvu. Lakini sasa hivi tunajaribu kutafuta kuridhishana tu uwekli nikuwa tuwalipe yaishe.

Na tukimaliza tujiandae kuwalipa wa Airbus na wale wengine kwani guess what vipengele vya aina hiyo hiyo vimo. Tuendelee kuwalipa hadi tutapoona kweli inatosha.

Tutakuwa tunatimiza utawala wa sheria kama tulivyokumbushwa na Pinda. Utawala wa sheria wa nchi yetu ni katika kulipa madeni tu lakini ikija katika kuwashughulikia mafisadi utawala huo wa sheria hutoweka.
 
Yote yaliangaliwa, hata uhalali wa mkataba maana hoja hii ya uhalali TANESCO waliitoa kama defence yake ya kuvunjwa kwa mkataba.

Suala la Rushwa, ni suala ambalo linaweza kusaidia kweli kukwepa kuwalipa dowans. Mahakama ikipewa uhakika wa kuwepo kwa rushwa itakuwa ni rahisi sana kuamua. Hebu tukumbushane, katika Richmond ni nani alitajwa kula au kutoa rushwa na kiwango gani? Zikipaikana affidavit za watu kuhusu kuwepo kwa rushwa inaweza kusaidia. Kwenye Radar kwa mfano tuliambiwa kiwango na hata nani walipata rushwa. Kwenye Richmond hili swala lipoje? Can somebody prove to the court beyond doubts kuwa rushwa ilitembea?

Tanesco walijipotezea wakati kwa kujaribu kutumia uhalali wa mkataba kama defence. Ni wazi kuwa ICC wasingekubali na ndio maana nampinga Fareed anayekazania kuwa bado ni defence. Wao walijitetea kama vile wako mahakamani wakati hawa ni arbitrators na si majaji ambao wanabanwa na sheria peke yake.

Vile vile hatuwezi kutumia kigezo kuwa kuna mtu wa Tanesco au serikali alihongwa na Dowans ku-set aside award hii. Utetezi pekee ni kama mmoja wa arbitrators alikuwa compromised na ushahidi wawe nao Tanesco. Kama tuna ushahidi kuwa mkataba ulipatikana kinyume na sheria basi recourse yetu ni moja na ni ku-washtaki wahusika. Tutalalamikaje ICC kuwa rushwa ilikuwepo wakati sisi wenyewe tunashindwa kuwashtaki katika mahakama zetu! ICC sio mahakama ya uingereza. Mbaya zaidi tukigeuka leo na kuwashtaki kwa rushwa itaonekana ni sour grapes tu kwa vile tumeshindwa. Hapa tumepatikana.

Amandla.....
 
walipeni yaishe jamani.. hatuwezi kukaa na Dowans mwaka wa tatu sasa! c'mmon now.. Sisi sote ni watu wazima; we all know what happened, and we also know why it happened. We are acting as if this is so extraordinary or unthinkable to have happened. We screwed up, its time to pay up!
 
very good arguments. Sasa hii hukumu imekiuka vipi sheria ya manunuzi? Hukumu imeonyesha mapungufu ya sheria ya manunuzi. soma 510 ya hukumu. Labda sijaelewa unifafanulie zaidi. TANESCO walijenga hoja ya illegality ya mkataba kwa mujibu wa PPA of 2004 na Tribunal imejenga hoja zake kwa sheria hiyo hiyo. Nifafanulie kuhusu kudharau PPA by the Tribunal. Kwa mwono wangu hukumu imezigatia vifungu vya sheria ya manunuzi.

Tatizo hukumu kamili ya ICC bado ni siri kwetu sisi wananchi wa kawaida. Ni watu fulani tu wachache wameiona, pengine usiri wenyewe ni kujaribu kuficha jina la ROSTAM AZIZ kuwa ndiye atakayepokea malipo ya Dowans. Labda hii ndiyo sababu kumekuwa na unexplained delays kuipeleka hukumu kamili ya ICC Mahakama Kuu ya Tanzania ikasajiliwe.
Nimefanikiwa kusoma vipande vipande tu vya hukumu yenyewe. Kutokana na hivyo vipande vya hukumu ya ICC nilivyoviona ni dhahiri kuwa hukumu hiyo inapingana na sheria ya PPA ya mwaka 2004.

This is the argument -- TANESCO ambayo ni legal entity ndani ya Tanzania iliitumia sheria ya PPA na kuamua kuwa mkataba wa Richmond/Dowans ni illegal na ikauvunja. ICC judges ambao ni foreigners walifanya tafsiri yao ya sheria hiyo ya Tanzania ya PPA na kudai kuwa mkataba ulikuwa legal.

Hapa kuna opportunity ya Mahakama Kuu ya Tanzania nayo kufanya tafsiri yake ya sheria ya PPA na kuamua kama mkataba wa Richmond/Dowans kweli ulikuwa illegal. The High Court of Tanzania ikiona kuwa the foreign judges at ICC erred in their interpretation of Tanzanian law, basi inaweza kuamua kisheria kabisa kutupilia mbali maamuzi ya ICC.

Hapa ni suala la sovereignty, inakuaje foreigners wa ICC waamue wao tafsiri yao ya sheria ya Tanzania ya PPA na kusema kuwa TANESCO ilikosea. Ndiyo maana tunahitaji sasa Mahakama Kuu ya Tanzania nayo itoe tafsiri yake ya sheria hii na iseme nani alikuwa sawa, TANESCO au the foreign judges at the ICC?
 
walipeni yaishe jamani.. hatuwezi kukaa na Dowans mwaka wa tatu sasa! c'mmon now.. Sisi sote ni watu wazima; we all know what happened, and we also know why it happened. We are acting as if this is so extraordinary or unthinkable to have happened. We screwed up, its time to pay up!

Who are you and what have you done to the real Mzee Mwanakijiji?
 
Tatizo hukumu kamili ya ICC bado ni siri kwetu sisi wananchi wa kawaida. Ni watu fulani tu wachache wameiona, pengine usiri wenyewe ni kujaribu kuficha jina la ROSTAM AZIZ kuwa ndiye atakayepokea malipo ya Dowans. Labda hii ndiyo sababu kumekuwa na unexplained delays kuipeleka hukumu kamili ya ICC Mahakama Kuu ya Tanzania ikasajiliwe.
Nimefanikiwa kusoma vipande vipande tu vya hukumu yenyewe. Kutokana na hivyo vipande vya hukumu ya ICC nilivyoviona ni dhahiri kuwa hukumu hiyo inapingana na sheria ya PPA ya mwaka 2004.

This is the argument -- TANESCO ambayo ni legal entity ndani ya Tanzania iliitumia sheria ya PPA na kuamua kuwa mkataba wa Richmond/Dowans ni illegal na ikauvunja. ICC judges ambao ni foreigners walifanya tafsiri yao ya sheria hiyo ya Tanzania ya PPA na kudai kuwa mkataba ulikuwa legal.

Hapa kuna opportunity ya Mahakama Kuu ya Tanzania nayo kufanya tafsiri yake ya sheria ya PPA na kuamua kama mkataba wa Richmond/Dowans kweli ulikuwa illegal. The High Court of Tanzania ikiona kuwa the foreign judges at ICC erred in their interpretation of Tanzanian law, basi inaweza kuamua kisheria kabisa kutupilia mbali maamuzi ya ICC.

Hapa ni suala la sovereignty, inakuaje foreigners wa ICC waamue wao tafsiri yao ya sheria ya Tanzania ya PPA na kusema kuwa TANESCO ilikosea. Ndiyo maana tunahitaji sasa Mahakama Kuu ya Tanzania nayo itoe tafsiri yake ya sheria hii na iseme nani alikuwa sawa, TANESCO au the foreign judges at the ICC?

Majina ya recommended arbitrators yanapelekwa kwa parties wote wa arbitration ili wayapitie na kukubaliana. Ni arbitrators wanaokubaliwa na pande zote mbili ndiyo wanasimamia ugomvi. Ili wakubalike na pande zote mbili ni muhimu wanapokuwa hawana uhusiano na hizo pande. Ndiyo maana hawatoki Tanzania.

Hii ni kama arrest warrant iliyotolewa na ICC kwa ajili ya Rais bashir wa Sudan. Mahakama Kuu nchini mwake wanaweza kusema hawaitambui, maswahiba wake katika AU wanaweza kumuunga mkono lakini anajua kuwa akikanyaga tu nchi nyingine anaweza kujikuta The Hague!

Uwezo wa kukataa kulipa tunao maana hela si zetu bana, na sisi si nchi huru . Lakini tujue kuwa tuli-sign hizo convention na kuna nchi ambazo zitakuwa tayari kuheshimu maamuzi ya ICC.

Amandla.....
 
Now action must be taken Kunyoa au Kusuka...... It comes a time when we need to cut losses. Lakini I would prefer culprits waliotufikisha hapa ndio wachangie mchango mkubwa kuwalipa hawa mabwana.... na sio our taxes
 
kwa media zetu huyo top legal expert aweza kuwa wa kuchongwa maana hata namna habari yenyewe ilivyoandikwa imenitia mashaka sana na hata uelewa wa mwandishi mwenyewe kuhusu masuala ya arbitration. Top legal expert Serikalini ni AG au Mkurugenzi wa Sheria za Kimataifa........ i doubt hawa wamesema haya.

Kwa kiingereza cha kawaida top legal experts in government ni watu waliobobea kwenye sheria walio serikalini.
Attorney General is the government's chief legal adviser -- he is not necessarily the top legal expert in government kwa ueledi wake binafsi.
Ni cheo tu kapewa, na tunajua kuwa vyeo kwenye serikali ya JK havitolewi kutokana na merit.
Kwanza waliosoma na AG Werema chuo wanasema alikuwa mwanafunzi zezeta. Mwalimu wao alikuwa ni Dk. Harison Mwakyembe. Werema wala hana uelewa mzuri wa sheria ingawa ana vyeti na aliwahi kuwa jaji. Kuna wataalamu wengi serikalini wamebobea kwenye sheria za kimataifa na kimikataba wanaoweza kustahili kuitwa top legal experts in government kutokana na utaalamu wao, si vyeo vyao.

Kwanza wewe Zitto kusema kwa uhakika kuwa unatilia mashaka iwapo AG au Mkurugenzi wa Sheria za Kimataifa wamesema maneno yaliyoandikwa na THISDAY ina maana you are in bed with senior government officials ama?
 
Back
Top Bottom