Mahakama kuu kanda ya dar es salaam kutoa maamuzi juu ya pingamizi la dowans.

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797

January 28 2012

Na Grace Ndossa

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imesema itatoa uamuzi wa pingamizi lililowasilishwa na Kampuni ya Dowans la kuitaka mahakama hiyo isiwape Tanesco kibali cha kukataa rufaa Febuari 16 mwaka huu .

Amri hiyo ilitolewa mahakamani hapo jana na Jaji Fauz Twalib ambapo alieleza kuwa hawawezi kusikiliza kesi hiyo leo kwani Wakili wa Kampuni ya Dowans Bw. Kennedy Fungamtama ameshawasilisha pingamizi.

Pingamizi hilo la Dowans l;inahusu kupinga Tanesco wasipewe kibali kwani hukumu iliyotolewa hawawezi kukata rufaa kutokana na makubaliano waliyokubaliana kwenye mkataba.

Jaji Twaib alidai kuwa hataweza kusikiliza kesi hiyo hadi hapo watakaposikiliza pingamizi lilowasilishwa na Kampuni Dowans.

Awali baada ya hukumu kutolewa na mahakam kuu Tanesco iliwasilisha maombi yao kuomba kibali cha kukata rufaa kupinga hukumu iliyotolewa na Jaji Mushi ya kuitaka tanesco kusajili tuzo ya fidia ya sh bilioni 94 ya kampuni ya Dowans mahakama hiyo kwa njia ya maandishi

Kesi hiyo ambayo ilifunguliwa na wakili wa Dowans,Bw. Kennedy Fungamtama kwa ajili ya kuiomba mahakama hiyo iiweze kuisajili tuzo waliyoipewa Novemba 15 mwaka juzi na Mahakama ya Kimataifa na Usuluhishi wa Migogoro ya Biashara(ICC)



 
Mahakama kuu inasubiri nini? ni miaka mingapi inasema itatoa maamuzi?

Our Court System is a Joke...
 
..Tanzania Nakupenda...... Haki yangu naililia.....

Hata Mimi nakupenda Tanzania; Siwapendi Viongozi woote wa Sasa Wanasafiri Wanatuliza Matumbo Yao na Watoto Wao

Kwanini Hawaijali Tanzania ninayokupenda kwa Moyo wangu Wote?
 
This appeal is unnecessary, costly and time consuming. The Court of Appeal will not reverse the ruling of the High Court because it does not lightly entertain appeals from arbitration awards. It is in the interests of international commerce that arbitration awards should be final, and it is to be hoped that the Court of Appeal will not only strongly support this policy but also ensure that Tanzania complies with the international agreements on the enforcement of arbitral awards to which it has ratified.
 
  • Thanks
Reactions: mka
Back
Top Bottom