Mahakama Kisutu yapiga stop mkutano wa Yanga wa Oktoba 23, 2016

Najiuliza hivi ni nani mwenye njaa kati ya wanaojikomba kwa Manji na wanaopinga utaratibu wa manji kuwekeza Yanga?
 
Naona uzi umeshambuliwa na mikia fc,mambo ya yanga hayajadiliwi kwenye vikao vya kahawa kila kitu ni kupitia mkutano na utafanyika tu.
 
aijengee Yanga uwanja ili iweje? umesikia wapi kuwa Barrick Gold / Acacia wanachimba dhahabu wanaiacha Tanzania? au gesi ya Mtwara inatolewa bure kuzalisha umeme wa Tanesco??
Ushawai ona timu inakodishwa duniani?
 
Subirini tu haya maandalizi watayalipa hao wanafiki wachache waliopeleka mahakamani.chaajabu kama kweli wanaipenda yanga kwanini waogope mkutano mkuu ?
Kule mkutanoni wapo watu wengi fuata upepo, ao m/kiti akisema hawaoji chochote wala kidadisi
 
Sina upande wowote ila mi hilo la kumilikiwa na mtu mmoja hiyo timu lilikuwa zuri ila tatizo ni staili anayotumia mkatakaba umejaa vipengele vya kuwakandamiza zaidi Yanga hata hiyo bodi ya wadhamini sijui hawakuliona hilo na hata ukisema eti mkaseme kwe mkutano pale utazomewa na watu walonunuliwa au kupewa posho ili wapitishe yaliyopangwa
Harafu hii kitu bana eti mkodishaji ndo huyohuyo mwenyekiti wa timu,sasa hapo watasaini vipi huo mkataba. Harafu mtu anataka kukodisha anaanza kukwambia nakudai sh bil.11 wakati huko mwanzo hakuwahi kusema kama kuna deni,kina Lloyd Chunga waliwahi ongoxa kwa shida bila hata hela hawakuacha hata nusu ya hilo deni wapo kina Madega wao walipoondoka waliacha bil.kadhaa kwe akaunti

Bado tuna safari ndefu sana na mpira wetu wa Tanzania....mi naona hakuna tofauti hata na miaka ya nyuma enzi za kina Sunday Kayun na kina Muhidin Ndolanga ni yale yale....nilipataga matumaini kweli mwaka 2004 wakati wanaenda kuibadili FAT kuwa TFF nikajua mambo mazuri yanakuja kumbe wapi
Timu inapima mafanikio kwa kuifunga Simba na Simba nayo inajipima mafanikio kwa kuifunga Yanga.....ujinga mtupu......ngoja nijandae nikaangalie EPL bora maana hapa hakuna tunachokitaka wala kukijua
 
Mkutano Mkuu wa Yanga uliokuwa umepangwa kufanyika kesho Jumapili, Oktoba 23, 2016 unadaiwa kuota mbawa baada ya Mahakama kuupiga ‘stop’ kufuatia kesi iliyofunguliwa na baadhi ya wanachama kupinga mkutano huo wa dharura unaodaiwa kukiuka taratibu na uhalali wa siku za uitishwaji wake.

Mmoja wa wanachama hao ni Frank Chacha ambaye amethibitisha kufungua kesi hiyo, akizungumza kupitia ktuo kimoja cha redio nchini, amesema mkutano wa kwanza ulikuwa una makosa na mkutano wa pili pia umeitishwa kwa makosa na huku mkataba ukiwa umeshasainiwa na wakati huu sio wa kwenda kuujadili.

“Ni Kweli mkutano ulikuwa umepangwa kufanyika tarehe Oktoba 23, 2016 ambapo agenda zaidi ya 13 zingepaswa kujadiliwa lakini tumeiomba mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutoa amri ya kuahirisha huo mkutano.

Ombi hili lilitolewa kupitia kesi namba 293 (2016) kesi ndogo namba 214 (2016) kati ya Frank Chacha muombaji wa kwanza na Magoma mwombaji wa pili huku walalamikiwa wakiwa ni Bodi ya Udhamini ya klabu ya Yanga na kampuni ya Yanga Yetu.”

“Katika maombi yetu ya dharura tuliomba mambo yafuatayo, Mkutano wa Oktoba 23, uzuiliwe kwasababu ni mkutano batili ambao haujafata taratibu za kisheria kwasababu notisi imekuja nje ya utaratibu pia makabrasha yalitakiwa yatolewe siku saba kabla ya mkutano kitu ambacho hakijafanyika,” ameongeza Chacha.

Ameongeza kuwa maombi mengine ni kusitishwa kwa utekelezaji wa mkataba kati ya Yanga Yetu na Bodi ya wadhamini uliosainiwa mnamo Oktoba 3, 2016.

Hatimaye Mahakama hiyo mbele ya Mheshimiwa Mwambapa, ikatoa amri ya kuzuia mara moja mkutano huo usifanyike na tayari tumeshaipa taarifa Bodi ya Wadhamini na Klabu ya Yanga kuwa mkutano huo usifanyike na mabango mengine kuhusiana na order hiyo tayari yameshabandikwa kwenye uwanja wa Kaunda.
View attachment 422314 View attachment 422315
Mbona hayo maombi hayana muhuri wa kupokelewa na mahakama
 
Subirini tu haya maandalizi watayalipa hao wanafiki wachache waliopeleka mahakamani.chaajabu kama kweli wanaipenda yanga kwanini waogope mkutano mkuu ?
Mmeshaongwa buku kumi na viroba ili wakija muwapige.Wao wameamua wawazuie kwa mbele.
 
Yanga hamtafika popote kwa kumtuka au kumkejeli mzee akilimali.Ninachoamini ni kua kuna wanayanga wengi sana walionyuma ya huyu mzee.Bila kukaa chini na kumaliza tofauti kwa amani na busara yanga yenye migogoro inanukia.
Akae chini na nani huyo msaliti
 
Kweli mkuu angejitoa basi u mwenyekiti halafu wengine ndio wafanye mchakato. sio kila kitu anasimamia yeye tena kwa mikutano ya dharura. mi ni Simba ila kwa hili unaona kabisa watani wanaamua kwa kukurupuka.
We ni simba ? Mkia upo wapi?
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom