Magufuli augua ghafla, alazwa

Status
Not open for further replies.

nyasaland

Member
Jul 3, 2009
46
16
Naomba mnijuze juu ya uvumi wa kuwa waziri wa miundombinu yupo dodoma anaumwa na kuna mdogo wangu kaniambia hilo

======
UPDATE:

WAZIRI wa Ujenzi, Dk John Magufuli jana (Aprili 18, 2012) aliugua ghafla akiwa kwenye Viwanja vya Bunge, Dodoma na kupelekwa katika Hospitali ya Mkoa ambako alilazwa.

Taarifa za Dk Magufuli kuugua ghafla mbali na kuthibitishwa na Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Dkt. Zainab Chaula pia zilitangazwa bungeni na Naibu Spika, Job Ndugai.

Akitoa maelezo hayo muda mfupi baada ya kuanza kwa Kikao cha Bunge, Ndugai alisema Waziri Magufuli akiwa katika maandalizi ya kwenda bungeni, alijisikia vibaya ghafla na alipokimbizwa hospitali ilibainika kuwa alikuwa akikabiliwa na tatizo la Shinikizo la Damu.

“Waheshimiwa wabunge, Mheshimiwa Magufuli aliugua ghafla leo (jana) asubuhi na kukimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma lakini, tunaelezwa kuwa presha (shinikizo la damu) iliyokuwa inamsumbua sasa imeshuka na kinachoendelea kumsumbua sasa ni vichomi ambavyo bado vimembana,’’ alisema Ndugai na kuongeza:

“Madaktari wanaendelea kushughulikia afya yake ili iweze kuimarika sawasawa kwa hiyo msiwe na shaka juu ya afya yake.’’

Wandishi wa habari na hata baadhi ya wabunge hakuruhusiwa kumwona Dk Magufuli hospitalini hapo na muuguzi wa zamu alisema: “Haiwezekani kumuona. Yupo katika eneo ambalo haturuhusu watu kufika na kumuona lakini anaendelea vizuri.’

Dkt. Chaula alisema Dkt. Magufuli amelazwa katika chumba maalumu ili kuwawezesha madaktari kuangalia afya yake kwa karibu… “Siyo kwamba yuko mahututi, bali tumemuweka huko kwa makusudi ya kuwa karibu naye zaidi na utulivu mzuri katika chumba hicho.”

Baadhi ya viongozi akiwamo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah walifika hospitalini hapo kwa nyakati tofauti kumjua hali Waziri huyo.

Wakati Naibu Spika Ndugai akiwa hakueleza Magufuli aliugua akiwa katika eneo lipi, taarifa kutoka kwa baadhi ya watumishi wa Bunge, zilieleza kuwa alipatwa na tatizo hilo asubuhi akiwa viwanja vya Bunge.

Hii ni mara ya pili wabunge kuugua ghafla katika Mkutano huo wa Saba wa Bunge baada ya Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Clara Mwatuka kuugua wiki iliyopita na kupelekwa kwenye hospitali hiyo ambako alilazwa kwa siku mbili.
 
Naomba mnijuze juu ya uvumi wa kuwa waziri wa miundombinu yupo dodoma anaumwa na kuna mdogo wangu kaniambia hilo

Mkùu ikiwa mdogo wako amekwambia nafikiri atakuwa kwenye position ya kutoa taarifa ya uhakika halafu kama anaumwa kila mtu huwa anauumwa au unamànisha amezidiwa?
 
Kuna taarifa nimezipata hivi punde kwamba waziri wa Ujenzi Jojn Magufuli ni mgonjwa na amelazwa ICU Dodoma kwa tatizo la heart attack.Naendelea kufuatilia kwa ukaribu zaidi.

Pole Dr magufuli kwa heart attack.
 
Kama ni kweli namuombea apone haraka.
.
"WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI".
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom