wewe ndiye usiyejua kabisa nini maana ya uwakilishi kama ni hivyo tusingekuwa na wabunge zaidi ya mmoja dsm, kama definition yako ya mbunge ndio hiyo. Wanapokuja kwenye kampeni zao hayo ndio mambo wanayoahidi, hivi unafikiri jimbo la ubungo litampima mh.mnyka kwa mafanikio ya kutetea watu wa kigamboni? Acha kukurupuka!!
Sasa wewe ndio umeanza kubaini matatizo ya Tanzania yapo wapi? Kwanza tambua katika kutatua mataizo ya Tanzania hayahusu ubunge wa Mnyika na jinsi atakavyopimwa. Nafikiri tunakubaliana kuwa mbinge ndio msimamzi mkuu wa Serikali katika utendaji wake iwe ni ukusanyaji wa mapato yaani kodi na mapato yatokanayo na raslimali zetu. Pia mbunge ana jukumu kubwa la kusimamia Serikali katika upangaji wa matumizi yake na mwisho katika matumiz ya fedha na raslimali k.m magari na mali zinginezo.
Utakabalina na mimi kuwa hili ni jukumu kubwa sana na linawalazimu wabunge wetu kufanya utafiti na kusoma sana taarifa mbali mbali, macapisho na ripoti, Hivyo muda wa kuleta maendelo jimboni hupo kabisa.
Matatizo na umaskini wa Tanzania chimbuko lake ni Serikali ya CCM kuwaaminish wananchi kuwa mbunge hupimwa kwa maendelo anayoleta jimboni badala ya jinsi anavyoisimamia Serikali, Katika mkakati huu Serikali ya CCM ikafanikiwa kujpunguzia au kujiondolea usimamizi wa bunge kwa kuwageuza wabunge kuwa matarishai wa maendelo ya jimbo badala ya wasimamizi wa Serikali.
Ili tutoke hapa ni lazima wapenda mabadiliko tuwe wa kwanza kusacrifice maendeleo ya majimbo yetu ili wabunge wetu wakafanya kazi za usimamzi wa Serikali na tuwaelimishe wananchi wenzetu.
Definition ya uwakilishi ni kuwa watu kadhaa wa jimbo fulani tunapatiwa nafasi moja ya kuismamia Serikali katika hayo niliyoyataja hapo juu na sio nafasi ya kupeleka tarishi wa kutubebea maendeleo toka Serikalini.
Hoja ya nini wanchosema wakati wa kampeni, hayo ni matokeo ya kuwa taifa la watu wasiokuwa na elimu ya uraia. Ni wazi kuwa wapinzani wamegundua udhaifu huo na kuutumia lakini kwa maoni yangu nafikiri haikuwa strategu nzuri sana kwani itawacost very soon.