Elections 2015 Magufuli anatukwepa - BBC Swahili

Kamanda Evelyne, Pengine Makufuli Aliogopa Swali Kwamba Lowasa Alisema Kipaumbele Cha Kwanza Mpaka Cha Tatu Elimu, Phd Yake Ya Ccm Ambayo Imeshindwa Kumtambua Raisi Wa Iraq! Anaitwa Nani!

Mara aseme kiwanda cha transfoma kitatengeneza bidhaa nzuri za ngozi teh huyu rais huyu duh aliepita ilisemekana alikua na nazi sio kichwa huyu sijui ye ana nini
 
Hapo sasa. Labda anaogopa kuulizwa kinachomshangaza wanafunzi kukaa chini au kwa nini maofisa wa serikali wanaishi hotelini wao, wake zao, wajukuu na mbwa zao kwa mwaka mzima huku wakilipiwa na Serikali

Hapo jibu lake litakua "matatizo ya Watanzania nayajua" mnipe kura sitawaangusha hapa kazi tu..... Kamaliza
 
Tatizo wengi wenu humu hamjui ufinyu wa muda ambao chama chetu kinakabiliana nao. Hizi kazi zetu ngumu sana.

Tuliwapa BBC njia mbadala ya kutumia skype katika hayo mahojiano ila halikuwezekana! Hivyo inakuwa ngumu kwetu kushiriki kutokana na sababu niliyoeleza hapo.
 
Leo kwenye taarifa ya habari ya BBC Swahili saa tatu usiku, imeripotiwa kuwa John Magufuli amekuwa akikwepa kila BBC wanapotaka kumfanyia mahojiano. Matumaini yao ilikuwa iwe jana, finally, cha ajabu, jamaa akasepa dakika za mwisho.

Kwa maswali yale aliyopigwa Lowassa, no wonder Magufuli anakimbia. Huu ni udhaifu pia.

Magufuli sio kwamba anawakimbikia BBC---BBC ndio wanamkimbia Magufuli kwasababu hawana cha kumuhoji. Unadhani BBC watamuhoji nini Magufuli ashindwe kujibu?
 
Ndio shida yenu, mnadhani kuonekana na Wazungu ni jambo la maana kuliko kujenga nchi yenu...

We wa wapi wewe?
BBC Swahili inarushwa na StarTv kila siku baada ya taarifa ya Habari ya saa 2 usiku Wazungu wamefika wapi tena.
 
Tatizo wengi wenu humu hamjui ufinyu wa muda ambao chama chetu kinakabiliana nao. Hizi kazi zetu ngumu sana.

Tuliwapa BBC njia mbadala ya kutumia skype katika hayo mahojiano ila halikuwezekana! Hivyo inakuwa ngumu kwetu kushiriki kutokana na sababu niliyoeleza hapo.
Muda haujawa excuse hata siku moja iwe shule au hata katika maisha, ukikuta mtu anasingizia muda huyo ni mzembe kama wazembe wengine hajui kupangilia muda wake (Time Management),

kwani vyama vingine vimetoa wapi muda wa kukutana na BBC.
 
Au aende na translator...!!! Huyu jamaa hafai jamani.... kazi kukariri tu...!! Akiwa jukwaani kakariri lugha zote hadi kihadzabe... sasa kuhojiwa anaogopa kama ukoma, maana akisikia BBC anajua ni Kiingereza tu... anaogopa kiingereza sanaaa... !!!

Hii ajabu kweli kweli...!!! Ana kariri vitu sana huyu jamaa...!!
 
Swali kwa nini Magufuli amewakimbia BBC linajibiwa vizuri na mwandishi Jenerali Ulimwengu katika makala yake kwenye gazeti la Raia Mwema la wiki hii. Jenerali anasema, "Kwa muda mrefu mno tumekuwa kama watu tuliokubaliana kwamba ili kupata watawala wa kuendesha mambo yetu ni lazima tupate wale wabovu kiasi kinachowezekana na tuepukane kabisa na watu wenye ujuzi, weledi na maono. Huu ndio utamaduni uliojengwa na CCM kwa muda mrefu. Kwa muda wa takriban miaka 25 sijawahi kuacha kulisema hili, na sikulisema hilo kwa sababu nilikuwa mtu wa upinzani".
 
hat lowasa alipokw anahojw nae alkw anajiknyaga tu na kulalmika kuw anaonelw hyo maguful yupo bze na kampn.

uko kidato cha ngapi? kwa huu uandishi wako ombea lowasa ashinde aanze kufanyia kazi kipaumbele chake. haujui hata matumizi ya sarufi!
 
Kuhutubia UN inaweza isiwe ishu. Si atakuwa anasoma tu kwenye karatasi. Halafu na alivyo hodari wa kukariri anaweza akaikariri hata robo tatu nzima ya hotuba.

Kasheshe akiwa sehemu kama Davos kwenye yale ma panel discussions ambapo mtu anakuwa hasomi hotuba.

Je, ataongea Kiswahili na kutumia mkalimani au ataongea Kiingereza?

Mimi natabari atachomoa kabisa kwenda huko Davos.

Naona El akiongea kuna mtu pembeni anabust ili asisahau alichoongea rais gani atakuwa
 
Muda haujawa excuse hata siku moja iwe shule au hata katika maisha, ukikuta mtu anasingizia muda huyo ni mzembe kama wazembe wengine hajui kupangilia muda wake (Time Management),

kwani vyama vingine vimetoa wapi muda wa kukutana na BBC.
Anataka kutuaminisha kuwa muda hana hivyo hata kulala halali na hata haja haendi. Hivi kwa nini asingelazimishwa tuu ili watu wamtambue pale anapoulizwa maswali na watu wasio na upande?
 
Magufuli ni mweupe sana kichwani yaani Kardashian.

Jana nilimsikia akitaja msururu wa mipango ya ujenzi wa barabara Dar nikashangaa tangu lini amekuwa afisa miradi wa Tanroads. Hiyo mipango itakuwepo tu bila kujali nani atakuwa rais. Hakika Magufuli hajui kazi na majukumu ya rais ni yapi.
 
Akwepe kwa lipi, swahili ndio lugha yake hata asipozungumza kingereza. Imeandikwa wapi lazima aongoze kwa sababu anajua kingereza. Mbona mataifa mengi kwa sasa viongozi wake wanatumia mitambo ya kutafsiriwa lugha watapokuwa wanaongea na viongozi wa mataifa na lugha nyingine. Lazima tuheshimu na kujivunia kiswahili chetu.
 
Back
Top Bottom