Magufuli alikoroga, Maandamano makubwa kumpinga leo

Dr Matola PhD

JF-Expert Member
Oct 18, 2010
55,784
90,545
Magufuli alikoroga

> Maandamano makubwa kumpinga leo

na Abdallah Khamis na Chalila Kibuda

WABUNGE wa mkoa wa Dar es Salaam, wameuomba uongozi wa juu wa nchi kumuonya na kumkemea Waziri wa Ujenzi Dk. John Pombe Magufuli kutokana na kauli yake na maamuzi mabaya ya kupandisha nauli ya kivuko cha Kigamboni ambayo itawaumiza wananchi.

Aidha wabunge hao wamemtaka waziri huyo kuwaomba radhi hadharani wakazi wa jijini la Dar es Salaam, hususan waishio Kigamboni kutokana na matamshi yake ambayo yamewachukiza wengi.

Akitoa taarifa ya kikao cha wabunge hao, Mwenyekiti wa Wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtenvu, alisema serikali imekuwa ya kwanza kuwakemea wamiliki wa vyombo binafsi vya usafirishaji wanapopandisha nauli kiholela, lakini imekaa kimya bila kumkemea waziri wake anayefanya maamuzi ya kuwaumiza wananchi.

Wabunge hao wa mkoa wa Dar es Salaam waliiomba pia serikali iwaachie muda wa wiki mbili wasimamie mapato katika kivuko hicho, ili kumthibitishia Magufuli kuwa kuna ufisadi wa kutisha na usimamizi mbaya unaofanywa na watendaji wake.

Walieleza kusononeshwa kwa kiwango kikubwa na lugha ya ubabe aliyoitoa Magufuli juzi alipozungumza na wakazi wa Kigamboni juu ya ongezeko la nauli ya kivuko.

Mtemvu alisema lugha ya waziri huyo aliyoitoa akiwataka wakazi wa Kigamboni wasiokubaliana na nauli mpya iliyotangazwa na serikali wazungukie Kongowe au wajifunze kupiga mbizi haikutakiwa kutolewa na kiongozi mwenye hadhi na heshima kama Magufuli.

"Mnajua ni wazi kabisa hata sisi wa mjini tuna maneno mengi na tunaweza kuongea lugha za kuudhi zaidi ya kauli za Magufuli isipokuwa tumefunzwa kuwa na adabu kwa kila mmoja," alisema Mtemvu ambaye ni Mbunge wa Temeke (CCM).

Mtemvu alisema maamuzi ya Dk. Magufuli katika sula la Kigamboni yamekuwa ya jazba na hakutaka kuwashirikisha wananchi kama serikali inavyojinadi siku zote.

"Dhamira ya serikali ya CCM ni kuona wananchi wanapata unafuu katika maisha, sasa hili la waziri kukurupuka na bila kutolea ufafanuzi na kujibu barua mbali mbali zilizofikishwa kwake, haileti sura nzuri kwa wananchi na mbaya zaidi anatumia lugha ya kuudhi kwa mbunge mwenzie," alisema mbunge mmoja akiungwa mkono na wenzake.

Dk. Faustine Ndugulile, Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, alisema Magufuli anawadanganya wananchi kwa kusema hajafikishiwa taarifa za maboresho ya kivuko, na kueleza namna alivyomuandikia barua ya kwanza Januari 19, 2011, juu ya changamoto mbalimbali za kufanyiwa kazi ili kuomgeza ubora wa huduma na mapato kwa serikali badala ya kuzidisha nauli.

Alizitaja changamoto hizo kuwa ni kuongeza kivuko kingine kwa ajili ya kukabiliana na wingi wa watu wanaotumia kivuko hicho, pamoja na kuongeza njia ya kutokea na kuingilia kwa ajili ya kurahisisha vivuko kufanya kazi kwa haraka.

Ushauri mwingine ni wa kuondoa kituo cha teksi na kudhibiti uuzwaji wa tiketi pamoja na kuondoa baadhi ya vibarua ambao hawana umuhimu katika kituo hicho.

Alisema licha ya kumuandikia barua hiyo ya Januari mwaka jana, alimwandikia nyingine mwezi Desemba mwaka huo huo, lakini Waziri Magufuli hakuonyesha kujali wala kutoa majibu ya mapendekezo hayo hadi walipoamua kupandisha nauli hizo.

John Mnyika Mbunge wa Ubungo na Katibu wa Wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, alisema kwa kuwa kazi ya Bunge kwa mujibu wa ibara ya 63 ni kuishauri, kuisimamia serikali pamoja na kutunga sheria, watamtaka Dk. Magufuli awaeleze alichukua hatua gani baada ya kushauriwa juu ya maboresho ya kivuko hicho kabla ya kupandisha nauli hiyo.

Alisema Magufuli ameyatumia kibabe mamlaka yake kwa kuamua jambo ambalo linapingana na sehemu nyingine ya sheria, kwa kuwa sheria mama ya nchi ambayo ni Katiba inatoa fursa ya watu kujadiliana katika mambo ya msingi.

"Tatizo la Waziri Magufuli ni kusoma sheria moja na kwa kuwa sheria zetu zingine ni mbovu yeye anatumia udhaifu huo kufanya maamuzi ya kibabe ikiwa ni pamoja na kutoa lugha ya kuudhi kwa wabunge na wananchi.

"Tunataka ajue hana tofauti na sisi kwa kuwa wote tumechaguliwa na yeye amepata dhamana ya kuwa waziri tu, pia ajue magari na ofisi anayotumia ni mali ya hao wananchi anaowataka wapige mbizi kwa ajili ya kuvuka," alisema Mnyika.

Mbunge wa Ilala Musa Azzan "Zungu" alisema lengo la serikali ni kusaidia wajasiriamali wadogo hivyo kuwapandishia gharama hizo kutaathiri mfumo mzima wa maisha yao kwa kile alichoeleza kila inapoongezeka gharama ya aina yoyote katika maisha ya kawaida anayeathiriwa ni mtumiaji wa mwisho ambaye ni mlalahoi.

Alisema katika mtazamo wa kawaida watu watafikiri kuwa kinachopingwa ni ongezeko la sh 200 toka 100, pasipo kuangalia athari la tukio zima kwa kuwa hata mwendesha guta itambidi aongeze nauli ya kusafirishia mizigo ya wafanyabiashara ambao nao wataongeza bei itakakayomgusa moja kwa moja mtumiaji wa bidhaa hizo.

Zarina Madabida Mbunge wa Viti Maalum, mkoa wa Dar es Salaam alisema si watu wote watakaokuwa na uwezo wa kulipa ongezeko hilo jipya na kubainisha watakaoathirika kwa kiasi kikubwa watakuwa wanawake kwa kile alichoeleza ndiyo wahangaikaji wa shughuli ndogo ndogo za biashara.

Anjela Kairuki anayewakilisha viti maalum mkoa wa Dar es Salaam, alisema Wizara ya Ujenzi inatengeneza hali ya ubaguzi kwa kukiuka Katiba ya Tanzania inayomtambua mtoto mdogo kuwa ni yule aliye chini ya miaka 18.

"Tangazo lao linasema watoto chini ya miaka 14 watavuka bure na wale wenye sare za shule watalipa sh 50 kwani wakiwa katika nguo za nyumbani ndiyo utoto unawatoka," alihoji Kairuki.

Mbunge wa Viti Maalum Temeke Mariam Kisangi, alisema katika suala hilo la kivuko Magufuli anajitengenezea chuki kwa wananchi wa kawaida na kujiongezea marafiki kwa upande wa mafisadi walio katika wizara yake wanaosimamia biashara ya Kivuko.

Maandamano ya kumpinga leo
Wakati hayo yakijiri, taarifa zimebainisha kuwa maandamano makubwa ya kumpinga Waziri Magufuli yatafanyika leo na kuwashirikisha wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu kikiwemo Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.

Habari za kuaminika kutoka ndani ya chuo hicho zimesema kuwa tayari jeshi la polisi limearifiwa juu ya kuwepo kwa maandamano hayo na tayari wanafunzi wa vyuo, sekondari na wale wa shule za msingi ambao bado wako majumbani, wamekwishatangaziwa kushiriki maandamano hayo.

Hata hivyo, juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, kuthibitisha kama wameruhusu maandamano hayo, hazikufanikiwa baada ya simu yake ya kiganjani kuita muda mrefu bila kupokelewa.
 
Mnang'ang'ania nini uko kigamboni? kwanza kumeshauzwa na mnatakiwa kuhama, akufukuzae hakwambii toka kaka, chura upenda maji lakini c ya moto! jifunzeni kuogelea, mia mbili mnaandamana? hacheni upuuzi, mbona watu toka mbezi ya kimara mpaka town wanalipa nauli ya 1000 na watu wamekaa kimya? kivuko cha misungwi watu wanalipa nauli ya 300, kamanga sh 800 mpaka 1000, kupandishiwa mia tu mnapiga makeleleeee! kama vp amieni masaki au upanga. mkiandamana tu virungu na mtakomaje!
 
mimi hapo naona waheshimiwa wabunge wetu wa dar wanatafuta pa kutokea au cheap popularity,naomba ni wachallenge je kwanini wasitoe pendekezo la kutoa sehemu ya posho zao za ubunge kama ruzuku ya kufidia ongezeko hilo la nauli ya kivuko kama kweli wana huruma na wanachi wa dar es salaam lengo likiwa ni kuwapunguzia mzigo wananchi at the same time kuchangia gharama za uendeshaji wa kivuko?

hebu just imagine nauli ya sh.100 pale kivukoni imedumu kwa miaka mingapi bila kupanda huku serikali ikijifunga mkanda kuboresha huduma pale ikiwamo kununua kivuko kipya kile kikubwa,leo kuomba wananchi wachangie sh 200 wala sio 500 wabunge wanakuja juu wakati wao wanapokea mamilioni ya posho!!!! magufuli ningekua mimi ningekomaa tu acha waandamane na hao wabunge wenye matumbo makubwa mpaka yanataka kupasuka na hawaridhiki kutwaa kudai posho wanazitumia wapi?
 
mimi hapo naona waheshimiwa wabunge wetu wa dar wanatafuta pa kutokea au cheap popularity,naomba ni wachallenge je kwanini wasitoe pendekezo la kutoa sehemu ya posho zao za ubunge kama ruzuku ya kufidia ongezeko hilo la nauli ya kivuko kama kweli wana huruma na wanachi wa dar es salaam lengo likiwa ni kuwapunguzia mzigo wananchi at the same time kuchangia gharama za uendeshaji wa kivuko?

hebu just imagine nauli ya sh.100 pale kivukoni imedumu kwa miaka mingapi bila kupanda huku serikali ikijifunga mkanda kuboresha huduma pale ikiwamo kununua kivuko kipya kile kikubwa,leo kuomba wananchi wachangie sh 200 wala sio 500 wabunge wanakuja juu wakati wao wanapokea mamilioni ya posho!!!! magufuli ningekua mimi ningekomaa tu acha waandamane na hao wabunge wenye matumbo makubwa mpaka yanataka kupasuka na hawaridhiki kutwaa kudai posho wanazitumia wapi?

Mkuu
Serekali nzima imekosa mikaati na Ubunifu wa kuendesha mambo mengi, nina hakika upo uwezekano wa hicho kivuko kutoa huduma bure. Kuna sekta nyingi zinazopoteza Pesa wachilia mbali zinazoibiwa katika Wimbi la Ufisadi na Rushwa. Serekali ya Jiji itakuwa na vitega uchumi chungu tele na vitakuwa havina uongozi na usimamizi mzuri hivyo Pesa nyingi Hupotea ambazo zingeweza kuendesha huduma hiyo muhimu bila kuwalipisha Wananchi ambao tayari wanakabiliwa na Malipo kila Kona.
Kinachoudhi zaidi ni Viongozi Kukosa Lugha ya kistaarabu kwa Waajiri wao (Wananchi) Na hii hutokea hasa kiongozi akishapewa sifa mbili tatu basi Anapanda kichwa na kusahau alikwenda mikono nyuma akitoa Shkamoo mpaka kwa walio wadogo kwake wakati akiomba kura.
Magufuli anaingia katika kundi hilo, wapo wengi, Jihadarini tutawaumbua Uchaguzi unapiga hodi....................!
 
Magufuli anatakiwa tu kuomba msamaha lakini nauli ya Tsh 200 lazima itumike maana tumeingia mfumo wa Kibepari Tsh 200 kwa kivuko hicho ni kiwango cha chini sana kulingana na gharama za uendeshaji. Tatizo kubwa ni kwamba maskini wamezidi kuwa maskini na matajiri wamekuwa matajiri zaidi, wananchi kushindwa kulipa Tsh 200 (about 13 cents of a Dollar) ni ushahidi tosha wa kushindwa kwa serikali yetu kiuchumi..
 
mimi hapo naona waheshimiwa wabunge wetu wa dar wanatafuta pa kutokea au cheap popularity,naomba ni wachallenge je kwanini wasitoe pendekezo la kutoa sehemu ya posho zao za ubunge kama ruzuku ya kufidia ongezeko hilo la nauli ya kivuko kama kweli wana huruma na wanachi wa dar es salaam lengo likiwa ni kuwapunguzia mzigo wananchi at the same time kuchangia gharama za uendeshaji wa kivuko?

hebu just imagine nauli ya sh.100 pale kivukoni imedumu kwa miaka mingapi bila kupanda huku serikali ikijifunga mkanda kuboresha huduma pale ikiwamo kununua kivuko kipya kile kikubwa,leo kuomba wananchi wachangie sh 200 wala sio 500 wabunge wanakuja juu wakati wao wanapokea mamilioni ya posho!!!! magufuli ningekua mimi ningekomaa tu acha waandamane na hao wabunge wenye matumbo makubwa mpaka yanataka kupasuka na hawaridhiki kutwaa kudai posho wanazitumia wapi?

THE ROMANTIC Umenena mkuu, Magufuli akomae ili mjitu ya Dar es Salaam iamke tikiyaaambia ccm inayakamua bira huruma hayatuelewi! Sasa kwa kauli ya Magufuli yawe tayari kukamuliwa la sivyo yajifunze kupiga mbizi ndipo yatakapoa jifunza kuwa kuipenda ccm ni mzigo na ghalama kubwa.
 
Mkuu
Serekali nzima imekosa mikaati na Ubunifu wa kuendesha mambo mengi, nina hakika upo uwezekano wa hicho kivuko kutoa huduma bure. Kuna sekta nyingi zinazopoteza Pesa wachilia mbali zinazoibiwa katika Wimbi la Ufisadi na Rushwa. Serekali ya Jiji itakuwa na vitega uchumi chungu tele na vitakuwa havina uongozi na usimamizi mzuri hivyo Pesa nyingi Hupotea ambazo zingeweza kuendesha huduma hiyo muhimu bila kuwalipisha Wananchi ambao tayari wanakabiliwa na Malipo kila Kona.
Kinachoudhi zaidi ni Viongozi Kukosa Lugha ya kistaarabu kwa Waajiri wao (Wananchi) Na hii hutokea hasa kiongozi akishapewa sifa mbili tatu basi Anapanda kichwa na kusahau alikwenda mikono nyuma akitoa Shkamoo mpaka kwa walio wadogo kwake wakati akiomba kura.
Magufuli anaingia katika kundi hilo, wapo wengi, Jihadarini tutawaumbua Uchaguzi unapiga hodi....................!

umeandika vizuri,maneno yako yanavutia kuyasoma lakini hujatuambia unadhani nini kifanyike kama mbadala wa kupandisha nauli kufidia gharama za uendeshaji wa kivuko chenyewe na shughuli zinazoendelea pale kivukoni kila siku..
 
THE ROMANTIC Umenena mkuu, Magufuli akomae ili mjitu ya Dar es Salaam iamke tikiyaaambia ccm inayakamua bira huruma hayatuelewi! Sasa kwa kauli ya Magufuli yawe tayari kukamuliwa la sivyo yajifunze kupiga mbizi ndipo yatakapoa jifunza kuwa kuipenda ccm ni mzigo na ghalama kubwa.

wafanye yote uliyoyaelekeza lakini kulipa bills ni lazima popote duniani!hakuna atakae kulipia bills zako,u have to pay on your self,hata wakitawala TPP MAENDELEO!
 
Wabunge D'salaam Wamvaa Magufuli

Monday, 02 January 2012

WAMTAKA AOMBE RADHI KWA KUTOA LUGHA CHAFU

Keneth Goliama na Zaina Malongo
Mwananchi

KAULI ya Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli kwamba watakaoshindwa kulipa nauli mpya ya Sh200 kuvuka Kigamboni ni vyema wakapiga mbizi kuvuka bahari, imewakera wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam ambao sasa wanamtaka aombe radhi.

Juzi, Dk Magufuli akiwa katika ziara eneo la Kivukoni alijaribu kuzungumza na wananchi wa Kigamboni kuhusu ongezeko hilo la nauli lakini badala ya wananchi hao kumsikiliza, walizomea ndipo alipowaambia kuwa watakaoshindwa ni vyema wakapiga mbizi baharini, kuzunguka Kongowe kuingia katikati ya jiji au warudi kijijini wakalime.jana, wabunge hao licha ya kumtaka Dk Magufuli aombe radhi, wameitaka Serikali kusitisha mara moja amri ya ongezeko hilo la nauli katika kivuko hicho kutokana na uamuzi huo kufikiwa bila ya kuwashirikisha wananchi.

Akitoa tamko kwa niaba ya wenzake, Mwenyekiti wa Wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu alisema tatizo lililopo katika kivuko hicho ni ubadhirifu mkubwa ambao umekuwa ukijitokeza na si nauli ndogo.Alisema ubadhirifu huo umesababisha makusanyo ya ushuru kuwa Sh9 milioni badala ya Sh18 milioni kwa mwezi na kuhoji fedha nyingine zinakokwenda.
Alisema kitendo kilichofanywa na Waziri Magufuli ni cha kuidhalilisha Serikali kutokana na kutokuwa na ushirikiano na viongozi wengine na kufanya kazi kwa hasira.Kwa hakika, Magufuli ametutukana kutokana na tabia yake ya kufanya kazi kwa hasira.

Tunamtahadharisha sisi ni wazaliwa wa Dar es salaam na ndiyo tunaujua huu mji. Hatutaki kuongea tu kama yeye, kinachotakiwa ni kusitisha ubabe wake maana hapa siyo Chato (Jimbo ambalo Dk Magufuli ni mbunge wake), alisema Mtevu.Mtevu alisema lazima Magufuli ajue nauli hizo hazikufuata sheria ya upandishaji kwa maana hata Sumatra (Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nchi Kavu na Majini), haijui kinachoendelea huku akisema kauli yake kwamba kupandisha nauli kunatokana na vituo vingine kupandisha ni ya kukurupuka inayotaka kuichonganisha Serikali na wananchi.

Alisema jiji la Dar es Salaam linachukua watu wengi kutoka Kigamboni hivyo, kupandisha nauli ni kuwaonea wananchi wanaoishi huko na ikifanya hivyo, Serikali itakuwa haijadhamiria kuwasaidia wananchi, bali kuwakomoa.Mtevu alisema kinachofanywa na Waziri Magufuli ni hasira na si uongozi bora akidai kwamba kila kitu anachoibua kinaleta mgongano katika Serikali huku akimsihi kuacha kukurupuka katika kutekeleza Ilani ya CCM.Kitendo cha kuongeza nauli ni kuwaongezea neema watu wachache. Zoezi hilo lisitishwe mara moja na kuleta amani.

Alisema kama Serikali imeshindwa kusimamia mapato ya vivuko viwili vya Mv Kigamboni na Mv Alina, vikabidhiwe kwa wabunge kwa wiki mbili ili kukusanya mapato.
Alisema Serikali inapaswa kujua kwamba, CCM ndicho kilichopandisha nauli kutokana na jimbo hilo kusimamiwa na chama hicho na kuongeza kwamba hatua hiyo itawaathiri zaidi ya watu milioni 2.5.

Baadhi ya wabunge waliohudhuria mkutano huo mbali na Mtemvu ni pamoja na John Mnyika (Ubungo), Mussa Azzan Zungu (Ilala), Dk Faustine Ndugulile (Kigamboni, Zarina Madabida, Angela Kairuki na Philipa Mtulano (Viti Maalumu).

Akizungumzia madai ya wabunge hao, Msemaji Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Martin Ntemo alisema msimamo wa Serikali kuhusu suala hilo ni ule uliotolewa na Serikali kupitia kwa Dk Magufuli wa kupandisha nauli tofauti na madai kwamba Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliwahi kutoa agizo la kusitishwa kwa ongezeko hilo... Hadi sasa kauli inayosimama ni ya Waziri (Magufuli).

Kilio cha Dk NdugulileDk Ndugulile alisema hali ya hewa imechafuka katika jimbo lake kutokana na kuwatangazia wananchi kuwa Waziri Mkuu amesitisha ongezeko hilo baada ya kupigiwa simu na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadik.Hata hivyo, Sadik alikaririwa na vyombo vya habari jana akikanusha kupokea maagizo hayo na kwamba alichoagiza ni kumtaka katibu mkuu katika ofisi yake kuwasiliana na mwenzake wa Ujenzi juu ya suala hilo kwa manufaa ya wananchi wa Kigamboni.

Dk Ndungulile alisema ongezeko hilo linagusa watu wanyonge kwa zaidi ya asilimia 800 akiwataja kuwa ni waendesha baiskeli za miguu mitatu (Maguta), baiskeli za kawaida, pikipiki na Bajaji wakati wenye magari ya kifahari hawajapandishiwa kiasi kikubwa cha nauli.Alisema haiingii akilini kuona guta likipaswa kulipiwa Sh1,800 kutoka Sh200 wakati gari dogo litalipa Sh1,300 kutoka Sh800... Bei hizo ni za kumkomoa nani?
Alisema tangu achaguliwe kuwa ubunge, amekuwa akimwandikia barua Waziri wa Ujenzi kuhusu kero mbalimbali za kivuko hicho lakini hakuna alichojibu zaidi ya kujitokeza jana (juzi) na kutangaza nauli mpya.Wakati naingia katika nafasi ya uongozi wa ubunge Jimbo la Kigamboni nilitaka kupata taarifa ya mapato ya uendeshaji wa kivuko ambapo nilipata taarifa ya makusanyo ya Sh8 milioni hadi 13milioni.

Baada ya kupokea taarifa hizo nilifanya uchunguzi wangu ambao baadaye nilibaini kuwa Serikali inapata kiasi cha Sh5 milioni kama mapato ya kivuko hicho huku kiasi cha Sh3 milioni kikiwa hakijulikani kinakwenda wapi, alisema. Dk Ndugulile alisema kama Serikali ingeweza kudhibiti hali hiyo, leo hii kusingekuwa na ongezeko hilo la nauli kutoka Sh100 hadi 200 kwa waenda kwa miguu huku magari yenye ujazo tofauti wakitakiwa kulipa kiasi cha Sh1,300 hadi 1,500.
Zungu:
Kilio cha wajasiriamali
Kwa upande wake, Zungu alisema gharama hizo zimewaathiri kwa kiasi kikubwa wajasiriamali kuliko wenye fedha. Alisema nauli zilizowekwa hazikufuata sheria kutokana na kutoshirikisha wananchi wala kiongozi yoyote na kuhoji ulizi gani shirikishi unaohubiriwa.Naomba tujiulize kikao cha kuongeza nauli kilifanyika wapi, maana huu ni mzigo ambao wananchi hawatakiwi kubebeshwa, alisema.

Madabida kwa upande wake alisema ongezeko hilo litawaathiri zaidi kina mama wanaofanya biashara ndogondogo kwa kutumia kivuko hicho.Alisema Magufuli anataka kuwachonganisha wananchi na wabunge kutokana kauli zake
 
Hawana lolote hao waheshimiwa wanatafuta cheap popularity tu kama wana uchungu kweli wananchi kwa nini wasitoe sehemu ya mamilioni yao ya posho kufidia ongezeko hilo?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom