Magufuli akiteua wakuu wa wilaya 171, sitoelewa azma yake ya kubana matumizi

mpk

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
3,115
3,862
Rafiki yangu ambaye ni mkuu wa wilaya aliwahi kuniambia wakuu wa wilaya wanapositaafu au kutoteuliwa tena au wakiambiwa msemo maarufu wa mzee watapangiwa kazi nyingine hulipwa kiinua mgongo cha Tsh milioni 80. Hii hajalishi unapandishwa kuwa mkuu wa mkoa au unahamishiwa wilaya nyingine. Ili mradi miaka mitano imeisha inahesabika umesitaafu.

Leo nchi yetu ina wilaya 171, kwa utaratibu huo wakuu wa wilaya 171 wanatakiwa kulipwa au wameshalipwa kiinua mgongo cha mil 80 kila mmoja! Hapo hujaesabu magari ya kifahari 171 ambayo hakuna linalopungua sh mil 300! na mshahara wa mil 3.8 kwa kila mkuu wa wilaya. Huu ni ubadhilifu!

Ningemuelewa rais wetu kama angewaacha hawa waliopo waendelee wakati anatafakari kukubaliana na rasmu ya Warioba ya kuundoa mfumo huu. Ikiwa rais atafanya uteuzi wa wakuu wa wilaya kitu ambacho najua atafanya, basi aache kutwambia ana adhima ya kubana matumizi.
 
Watu wengine bhana. Mtoa mada anajaribu kuangalia namna ya kupunguza ufujaji wa pesa yetu ili tufanye mambo ya kimaendeleo wengine mnamshambulia.
Kuna haja gani mtu kulipwa kiinua kifua mil.80 halafu baada ya miaka 5 hata kama ataendelea au atateuliwa kuwa mkuu wa mkoa?
Tusijipofushe ufahamu wetu. Magu lazima aendelee kuonyesha tofauti na aliyemtangulia hata ktk hili.
Angekuwa alishafanya angesifiwa sana tu lkn kwa sababu anakumbushwa, mkumbushaji anashambuliwa.
Poor Tanzania.
 
~~~>Watanzania zaidi ya 45M tukimuelewa Magufuli hata wewe usipomuelewa kuna tatizo gani????
 
Watu wengine bhana. Mtoa mada anajaribu kuangalia namna ya kupunguza ufujaji wa pesa yetu ili tufanye mambo ya kimaendeleo wengine mnamshambulia.
Kuna haja gani mtu kulipwa kiinua kifua mil.80 halafu baada ya miaka 5 hata kama ataendelea au atateuliwa kuwa mkuu wa mkoa?
Tusijipofushe ufahamu wetu. Magu lazima aendelee kuonyesha tofauti na aliyemtangulia hata ktk hili.
Angekuwa alishafanya angesifiwa sana tu lkn kwa sababu anakumbushwa, mkumbushaji anashambuliwa.
Poor Tanzania.




~~>Tuletee Uthibitisho wa Hayo Malipo ya 80M.....


~~>Ikiwa hayo malipo yapo Kisheria nani wa kuyabadilisha¿¿¿
 
Wakuu wa wilaya Na mikoa kulipwa milioni 80 Kwa miaka 5 in ufujaji Mkubwa wa fedha za walipa kodi
 
Watu wengine bhana. Mtoa mada anajaribu kuangalia namna ya kupunguza ufujaji wa pesa yetu ili tufanye mambo ya kimaendeleo wengine mnamshambulia.
Kuna haja gani mtu kulipwa kiinua kifua mil.80 halafu baada ya miaka 5 hata kama ataendelea au atateuliwa kuwa mkuu wa mkoa?
Tusijipofushe ufahamu wetu. Magu lazima aendelee kuonyesha tofauti na aliyemtangulia hata ktk hili.
Angekuwa alishafanya angesifiwa sana tu lkn kwa sababu anakumbushwa, mkumbushaji anashambuliwa.
Poor Tanzania.
Waache ukitaka kujua ni wanafiki ni pale ikitokea rais akisema hateui wakuu wa wilaya watakuwa wa kwanza kutumwagia povu humu eti wanapongeza uamzi wa kubana matumizi!
 
Acheni kumshambulia mleta mada anayo pointi kwenye hoja yake. Kama kweli kuna gharama kubwa namna hiyo sioni mantiki yoyote ya kuwa na hawa watu. Kama kweli kuna kubana matumizi hiv vyeo vya ajabu ajabu viondolewe abakizwe mkurugenzi anatosha kabisa kusimamia wilaya.

Hv kuna sababu ipi ya msingi kuwa na wateule wawili wa Rais katika wilaya?

Mkurugenzi na wawakilishi wa wananchi waliopo kwenye wilaya wanatosha kabisa.

Sielewi nini kilichowafanya CCM kukataa rasmu ya Warioba. Sielewi kama CCM kama kweli wana nia ya dhati kufanya Taifa hili kusonga mbele.

Mbona haya ni mambo yaliyo wazi tu hata kama mtu hana uwezo wa kupambanua jambo hili atakuwa na uwezo wa kuona hivi vyeo havina maana yoyote?

Tunamwamini Magufuli tusubiri. Tuna imani atatekeleza mapendekezo ya wananchi.. tuna imani hatatuangusha Watanzania. Tuna imani ataacha legacy ambayo wengine walishindwa. Tuna imani katika hili atakuwa mtu wa kukumbukwa katika uongozi. Tuna imani anawaangalia Watanzania na siyo waliotegesha meno kumaliza nchi hii. Tuna imani na wewe Magu hutatuangusha. We pray for you.
 
Wakuu wa Wilaya ni sahihi ila kuwepo kwa mkuu wa mkoa huu ni mlolongo isio na tija.

Wakurugenzi wangekuwa wangekuwa wanaripoti mmoja serikali kuu au wizarani.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom