Huyo dogo hapo mbele anayecheka mwenye t shirt ya blue anafanana na Nchemba Mwigulu.
Hamna..anafanana na mtoto wa slaa alizaliwa hivi majuzi na "mkewe" huyu wa sasa
Mkuu, huo unaofanya kama siyo upuuzi basi ni ujinga. Huyo mtoto mdogo ambaye hajaanza hata kuongea unamwingiza kwenye mambo yasiyomhusu ili iweje? Huo ni unyanyasaji wa watoto.
Huyo Mwigulu aliyesemwa hapo juu ni mtu mzima, na ni member hapa anaweza kuja kujitetea mwenyewe, lakini huyo mtoto unayemsema wewe siyo member na wala hawezi kujitetea mwenyewe. Haiingii akilini kwa mtu mzima kuanza kumkandia 'innocent child' kwa mambo ambayo hana hata uwezo wa kuyaelewa. Ni afdhali ungewasema wazazi wake maana ni watu wazima na ni member hapa wanaweza kujisemea wenyewe, lakini mtoto mchanga ni kumwonea.
Nakilaani hicho kitendo ulichofanya kwa nguvu zote. Mungu ambaye ni mtetezi wa wanyonge, na amlinde huyo mtoto dhidi ya kitendo chako ambacho ni cha uonevu usiokuwa na kiasi. Na Bwana mwenyewe akulipe kulingana na uovu wako.