Watanzania baada ya miaka 50 wamechoka na kasi ndogo ya maendeleo ya taifa lao. Ukiachilia mbali matatizo sugu ya afya na elimu, miundo mbinu isiyokidhi haja, kuzidi kuongezeka kwa tofauti ya kipato, kukithiri kwa rushwa na ukosefu wa ajira, utendaji wa serikali na sarakasi za kisiasa zisizo na tija vimeongeza zaidi hamu ya mageuzi ya kisiasa nchini.
Tukiwa na msukumo mkubwa wa mageuzi ya kisiasa inabidi tujiulize na tufikiri kama haya mageuzi yatatatua matatizo yetu ya kimaendeleo na kiuchumi kwa ujumla. Kwani sisi kama binadamu na jamii tunahitaji kuishi kwa matarajio yaliyo na uhalisi vinginevyo tutapoteza hata nguvu ya kutumaini na kutarajia chochote.
Sasa mageuzi ya kisiasa hayakwepeki, lakini je ni mageuzi gani ya kiuchumi na kimaendeleo tutachuma/tutavuna kutokana na haya ya kisiasa?
Serikali ya kimageuzi ikiingia madarakani itarithi mikataba mibovu ya kinyonyaji inayolindwa na sheria za kimataifa ambayo tanzania ni mshiriki, kuna swala la madeni ya nje ya kitaifa, kuna suala la maamuzi ya taasisi za kimataifa za kifedha za nje.
Kupingana na yote haya ni sawa na kujipiga risasi kwenye mguu. ili kuongeza kipato serikali inahitaji ufanisi wa hali ya juu sekta ya kilimo, sekta ya madini, utalii, na viwanda na biashara (sekta ya mabenki na soko la fedha na bidhaa).
Kipato cha serikali ni kidogo kuweza kuwekeza kwenye sekta ya kilimo sawa sawa na hivyo kuinua sekta hii iliyo kubwa nchini, hapo hapo tunatakiwa kulipa madeni ili tupate misaada ya hapa na pale ambayo ni sehemu kubwa ya bajeti yetu, tukijinga na soko la dunia ili viwanda vyetu vikue ili tuweze kukusanya kodi na kuongeza kipato na ajira nchini tunapewa adhabu na hawa WB na IMF. Sekta ya biashara (mabenki na soko la bidhaa) haiwezi kukua bila kuongezeka kwa kipato cha taifa yaani cha serikali na wananchi kwa ujumla na kipato cha taifa kinaletwa na uzalishaji kwenye sekta nilizozitaja ambazo zinahitaji mkono mkubwa wa serikali (ambayo itakua imefungwa na mikataba, mahusiano ya kimataifa nk).
Serikali ya kimageuzi itapata shida hapa na pato la taifa halitaongezeka vile wengi tunavyotarajia. wanamageuzi wataongeza ufanisi wa serikali, watapunguza ufisadi kwa kiwango kikubwa, watapunguza ukubwa na hivyo gharama za serikali, lakini hayo yote yatakua na athari za kawaida sana kwenye ujumla wa pato la taifa na hivyo kero zetu za elimu duni, afya duni, ajira, nk hazitapungua kama tunavyotarajia wengi wetu.
wanamageuzi angalau wataleta hari mpya, nguvu mpya na hamasa ya kujivunia tanzania yetu tena.
Tukiwa na msukumo mkubwa wa mageuzi ya kisiasa inabidi tujiulize na tufikiri kama haya mageuzi yatatatua matatizo yetu ya kimaendeleo na kiuchumi kwa ujumla. Kwani sisi kama binadamu na jamii tunahitaji kuishi kwa matarajio yaliyo na uhalisi vinginevyo tutapoteza hata nguvu ya kutumaini na kutarajia chochote.
Sasa mageuzi ya kisiasa hayakwepeki, lakini je ni mageuzi gani ya kiuchumi na kimaendeleo tutachuma/tutavuna kutokana na haya ya kisiasa?
Serikali ya kimageuzi ikiingia madarakani itarithi mikataba mibovu ya kinyonyaji inayolindwa na sheria za kimataifa ambayo tanzania ni mshiriki, kuna swala la madeni ya nje ya kitaifa, kuna suala la maamuzi ya taasisi za kimataifa za kifedha za nje.
Kupingana na yote haya ni sawa na kujipiga risasi kwenye mguu. ili kuongeza kipato serikali inahitaji ufanisi wa hali ya juu sekta ya kilimo, sekta ya madini, utalii, na viwanda na biashara (sekta ya mabenki na soko la fedha na bidhaa).
Kipato cha serikali ni kidogo kuweza kuwekeza kwenye sekta ya kilimo sawa sawa na hivyo kuinua sekta hii iliyo kubwa nchini, hapo hapo tunatakiwa kulipa madeni ili tupate misaada ya hapa na pale ambayo ni sehemu kubwa ya bajeti yetu, tukijinga na soko la dunia ili viwanda vyetu vikue ili tuweze kukusanya kodi na kuongeza kipato na ajira nchini tunapewa adhabu na hawa WB na IMF. Sekta ya biashara (mabenki na soko la bidhaa) haiwezi kukua bila kuongezeka kwa kipato cha taifa yaani cha serikali na wananchi kwa ujumla na kipato cha taifa kinaletwa na uzalishaji kwenye sekta nilizozitaja ambazo zinahitaji mkono mkubwa wa serikali (ambayo itakua imefungwa na mikataba, mahusiano ya kimataifa nk).
Serikali ya kimageuzi itapata shida hapa na pato la taifa halitaongezeka vile wengi tunavyotarajia. wanamageuzi wataongeza ufanisi wa serikali, watapunguza ufisadi kwa kiwango kikubwa, watapunguza ukubwa na hivyo gharama za serikali, lakini hayo yote yatakua na athari za kawaida sana kwenye ujumla wa pato la taifa na hivyo kero zetu za elimu duni, afya duni, ajira, nk hazitapungua kama tunavyotarajia wengi wetu.
wanamageuzi angalau wataleta hari mpya, nguvu mpya na hamasa ya kujivunia tanzania yetu tena.