Elections 2010 Mageuzi ya kisiasa 2010 vijana mpo

houseboy

Member
Jul 22, 2007
39
3
Jamani naomba tuanze kampeni rasmi kwa ajiri ya uchaguzi ujao nchini Tanzania bila ya kujali chama.kuna mwamko mkubwa sana duniani kwa kufanya vijana wawe viongozi wa leo.kwa kuanzia ni lazima kuanza kuweka viongozi wapa kabisa kwani viongozi walewale wameshidwa kufanya kazi.Tanzania inakaribia kufikisha miaka 50 tangu tupate uhuru,zaidi ya mashirika na tasisi 500 za taifa zimeuzwa kwa bei ya ubwete kabisa na baada ya kuuza kila kitu hakuna dili tena kwani zamani walikuwa wanapata pesa kutoka kwenye mashirika ya umma na sasa wengi wa viongozi hao baada ya kuuza kila kitu wanafanya ufisadi wa kwa njia ya TENDA,MIKATABA YA ULAGHAI na mambo mengine ya kiufisadi,fisadi.
Uchaguzi unaokuja ni kuwaondoa viongozi wote tukianzia na wabunge waliokaa madalakani muda zaidi ya miaka 10 kwani wabunge ndio wanakua mawaziri baada ya uchaguzi,tuchague vujana bila ya kujali chama,na slogan yetu iwe VIJANA TAIFA LA LEO NA SI KESHO.Ananteni naomba mniunge mkono kuanzisha rasmi kampeni kabambe ya kuondoa VIGOGO WOTE
 
Kwanza, Tanganyika na Zanzibar ndiyo zilizo pata uhuru. Labda kama unaongelea muungano.
Pili, weka wazi nini haswa unataka kifanyika na huo mpango utatekelezwaje? Maana sielewi hizo kampeni unazo ongelea bila kuangalia chama ni zipi maana kila mgombea anatoka chama fulani na kufuata itikadi za chama fulani. Tueleze vizuri.
 
Naanza
Zito kabwe(Kigoma kaskazini) Nape Nauye(kinondoni),Said Kubenea (mafia),Husein Bashe (Nzega) ,Jerry Slaa (UKONGA) ,Amos Makala (Mvomero) ,John Nchimbi (Kigamboni) Sango Kasera (Rorya) ,Dr Emanuel Nchimbi (Songea mjini), Martin Shigela (Kishapu) Denis Msacky (VUNJO), Alima Mdee(kawe) ,John Mnyika (ubungo),Tom Mwangonda(MBEYA mJINI
Greece Zinazohitajika
Phielemon Ndesamburo,Dr Mwakyembe ,Ole Sendeka ,Dr SLAA.Samwel SITA ,mama Kilango,
NB,tunakaribisha majina mengine
 
Naanza
Zito kabwe(Kigoma kaskazini) Nape Nauye(kinondoni),Said Kubenea (mafia),Husein Bashe (Nzega) ,Jerry Slaa (UKONGA) ,Amos Makala (Mvomero) ,John Nchimbi (Kigamboni) Sango Kasera (Rorya) ,Dr Emanuel Nchimbi (Songea mjini), Martin Shigela (Kishapu) Denis Msacky (VUNJO), Alima Mdee(kawe) ,John Mnyika (ubungo),Tom Mwangonda(MBEYA mJINI
Greece Zinazohitajika
Phielemon Ndesamburo,Dr Mwakyembe ,Ole Sendeka ,Dr SLAA.Samwel SITA ,mama Kilango,
NB,tunakaribisha majina mengine

Hii imekaa vizuri sana ila sasa vyama wanavyotoka wengine ndio taabu sasa ndio maana tunatofautiana hapa
 
Jamani naomba tuanze kampeni rasmi kwa ajiri ya uchaguzi ujao nchini Tanzania bila ya kujali chama.kuna mwamko mkubwa sana duniani kwa kufanya vijana wawe viongozi wa leo.kwa kuanzia ni lazima kuanza kuweka viongozi wapa kabisa kwani viongozi walewale wameshidwa kufanya kazi.Tanzania inakaribia kufikisha miaka 50 tangu tupate uhuru,zaidi ya mashirika na tasisi 500 za taifa zimeuzwa kwa bei ya ubwete kabisa na baada ya kuuza kila kitu hakuna dili tena kwani zamani walikuwa wanapata pesa kutoka kwenye mashirika ya umma na sasa wengi wa viongozi hao baada ya kuuza kila kitu wanafanya ufisadi wa kwa njia ya TENDA,MIKATABA YA ULAGHAI na mambo mengine ya kiufisadi,fisadi.
Uchaguzi unaokuja ni kuwaondoa viongozi wote tukianzia na wabunge waliokaa madalakani muda zaidi ya miaka 10 kwani wabunge ndio wanakua mawaziri baada ya uchaguzi,tuchague vujana bila ya kujali chama,na slogan yetu iwe VIJANA TAIFA LA LEO NA SI KESHO.Ananteni naomba mniunge mkono kuanzisha rasmi kampeni kabambe ya kuondoa VIGOGO WOTE

Houseboy, kwa uzoefu wangu Vijana ndio wapenda 'dili' wakubwa. Sidhani kwamba ujana ndio kigezo sahihi cha uadilifu. Utatuhakikishaje kwamba vijana wakiingia madarakani hawatachonga 'dili' mpya?

Maelezo yako ni ya jumla jumla mno. Viongozi unaowazungumzia wa Mashirika ya Umma enzi hizo ni wachache sana ambao wako kwenye uongozi hivi sasa. Kama bado wako hai basi watakuwa na umri wa miaka 70 kwenda juu na wamechoka mbaya maana hata pensheni hawana! "Vigogo" waliopo madarakani wengi ni wapya hata hao Wazee waliouza mashirika ya Umma ukiwauliza watakwambia hawawajui na hawajui viongozi wa sasa wametokea wapi maana hata ndani ya Chama cha CCM hawakuwa na nafasi yoyote ukiacha 'makada' wachache kama Rais Kikwete, Waziri Chiligati na watu kama Mkuchika.

Kama una nia ya kweli ya kutaka kuigeuza nchi iwe ya neema inayostahili, kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla, anza kampeni ya kufufua 'uadilifu' ndani ya vijana kabla hujawahamasisha kuwapindua 'vigogo' waliopo madarakani.
 
Back
Top Bottom