Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Magazeti yatia aibu kupotosha hukumu dhidi Mwanahalisi
Kuna habari kwamba baadhi ya wahahariri wa vyombo huru vya habari wameomba Jukwaa la Wahariri litoe tamko kuhusu upotoshwaji wa kimakusudi wa vichwa vya habari katika baadhi ya magazeti ya leo kuhusu Order iliyotolewa na Mahakama Kuu chini ya Jaji Robert Makaramba tarehe 30 April kuhusu kesi ya madai aliyoifungua Rostam Aziz dhidi ya gazeti la Mwanahalisi.
Habari ambazo nimezipata kutoka baadhi ya wahariri wa magazeti zinasema kuwa magazeti yanayomilikiwa na Rostam (Mtanzania na The African) pamoja lile linalomikiwa na serikali (Habari Leo) yamepotosha aliyoagiza jaji Makaramba kwa kusema kwamba mahakama imemsafisha Rostam kitu ambacho si kweli Mahakama haikusema hivyo.
Wahariri wanadai kwamba alichofanya Jaji Makaramba ni ni kutoa amri tu ya kuridhia madai ya Rostam katika shauri alililipeleka bila kusikiliza upande wa Mwanahalisi kwa sababu ya mawakili wa Mwanahalisi hawakuwapo Mahakamani. Kwa maana nyingine shauri halikusikilizwa kabisa, hivyo si kweli Rostam kasafishwa kuhusu madai ya umiliki wa kampuni ya Richmond.
Wahariri wanadai kuwa uandishi wa habari wa magazeti hayo yanakwenda kinyume cha maadili ya uandishi na yametia aibu medani nzima ya taaluma hiyo muhimu kwa umma.
Wahariri pia wamemuomba Jaji Makaramba kuyakemea magazeti hayo kwa kuandika kile ambacho hakukisema katika Order yake.