Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,570
- 19,442
Daktari wa MJ atiwa hatiani Send to a friend
Tuesday, 08 November 2011 21:44
0digg
LOS ANGELES, Marekani
DAKTARI wa Michael Jackson, Conrad Murray amehukumiwa kwenda jela baada ya kukiri mashtaka yake kusababisha kifo cha Mfalme wa Pop, Michael Jackson. Murray, 58, aliyekuwa mbele ya jopo la majaji saba wakiwemo wanawake watano, walimtia hatiani daktari huyo kwa kosa la kuua.
Hiyo nimeitoa kwenye website ya Mwananchi.
Ukweli ni kuwa
(1) Conrad Murray hajahukumiwa kwenda jela ingawa ameonekana na hatia ya kusabaisha kifo cha Michael na hivyo kupelekwa rumande hadi hukumu yake itakapotolewa.
(2) Conrad Murray hakukiri mashataka dhid yake: aliyakana yote
(3) Kesi ya Murray haikusikilzwa mbele ya jopo la majaji saba, bali ilisikilizwa na jaji mmoja Michael Pastor akisaidiwa na baraza la wazee (jurors) lenye watu 12: wanaume saba na wanawake watano.