Magazeti ya Kenya na dhihaka kwa Rais wetu

Asante kwa ujumbe wako ila nadhani wakenya wamezungumza ukweli kuhusu Rais wetu na kupenda kwake safari za nje na kuwa soft kwenye suala la rushwa. Hayo ni malalamiko ya watanzania wengi na Rais hataki kuyasikiliza kwa sababu anazojua mwenyewe. Najua wakenya wamepata mambo hayo kutoka kwa watanzania wasioridhika jinsi nchi inavyoendeshwa na jinsi JK anavyopenda safari za nje (yaweza kuwa kwa manufaa binafsi akiogopa kupokea rushwa waziwazi ila ajilipe kutoka kwenye posho za safari).

Mtazamo huo umekuwa ukizungumzwa na watanzania na wakenya wamecopy toka kwa watanzania kama mimi wasioridhishwa na mwenendo wa mkuu wetu wa kaya. Sioni tatizo la kutuchonganisha na wakenya hapa!

Kama unasema unaridhika na hali ilivyo tutakushangaa mwenzetu.
 
Jinsi alivyowaona GADO kwenye uhuru wa SS
attachment.php

cart-1807.jpg
 
Namtuma mtu sasa hivi akaniletee hilo gazeti, Ila unapoona hata jirani anaandika udhaifu ujue naye anakerwa kwa vile ukanda huu unaoitwa Afrika Mashariki naye unamhusu. Hakuna anayependa kuitwa raia wa nchi yenye ombwe la uongozi.
 
Wenye akili fupi wanaotawaliwa na fikra na itikadi zisizo huru watashangilia kitendo hiki na hawa ni wale wenye fikra fupi wasiotaka kuona mbali, wenye uwezo wa kuona mbali wataishia kusikitika hata kama anayosemwa nayo kikwete ni ya kweli ila je yanasemwa kwa lengo gani?

Baba yako hata kama kakunyima hela ya mtaji wa biashara haimvui thamani ya kuwa baba na hata kama ikitokea anasemwa kwa mabaya hata kama ni kweli inapaswa uzalendo ukuguse, na haya ndo mapenzi ya kweli kwa taifa lako. Kijana mwema ni yule ambaye hujenga nyumba kwa mikono na aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

A presidency institution can not be compared to a marriage institution and any attempt to do that will amount to insurbodination and be littling the presidency institution. A president goes beyond his country boundries, he is an international leader and he will always be judged using international lenses and by multi national standards. We should not forget that we have on several occasion judged other countries' presidents. The president of one country can be of a help to other people outside his own country. A president of one country will always pass the litmas test of other people outside his own country. We should learn to love our critics instead of hating them because they see our falt and they tell as to fix it. If we are used to accepting praise why this time can't we accept the opposite remarks.
 
Wenye akili fupi wanaotawaliwa na fikra na itikadi zisizo huru watashangilia kitendo hiki na hawa ni wale wenye fikra fupi wasiotaka kuona mbali, wenye uwezo wa kuona mbali wataishia kusikitika hata kama anayosemwa nayo kikwete ni ya kweli ila je yanasemwa kwa lengo gani?

Baba yako hata kama kakunyima hela ya mtaji wa biashara haimvui thamani ya kuwa baba na hata kama ikitokea anasemwa kwa mabaya hata kama ni kweli inapaswa uzalendo ukuguse, na haya ndo mapenzi ya kweli kwa taifa lako. Kijana mwema ni yule ambaye hujenga nyumba kwa mikono na aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
Mimi nafikiri wewe ndiye mwenye akili fupi zaidi unataka mwandishi adanganye, mwandishi kaandika sahihi kabisa kwani ni uongo kuwa Kikwete amezidi kusafiri nje na leo sijui kama yuko nchini, kwani ni uongo kwamba chama cha mapinduzi kinayumba ni uongo kwamba Rais ni soft on corruption. Nyie mliozoea kudanganya zamani mlidhani mna akili sana ndio maana mnapoona watu wanasema ukweli mnaona kama mnadhalilishwa.
 
hawa jamaa wako sahh kabisa.hiv janga kama hili la umeme ambapo mafanikio na solution yake sasa iko mikonon mwa rais cha kushangaza jamaa kakaa kimya kabisa eti anawaachia wasaidiz..cjui nani aje ampe semina elekezi..jaman hi sio normal
 
Hata mimi haya maneno yamenikera, ni sawa na kumsikia jirani anajadili mapungufu ya ndoa yako wakati hata ya kwake inaning'inia

Kama mtakuwa mnapigana huko ndani mke anapiga kelele mpaka watoto wakakimbilia kwa majirani mnawataka wajadili nini kuhusu ndoa yenu ebu jamani tuwe objective na tuache unafiki.
 
Mimi nafikiri wewe ndiye mwenye akili fupi zaidi unataka mwandishi adanganye, mwandishi kaandika sahihi kabisa kwani ni uongo kuwa Kikwete amezidi kusafiri nje na leo sijui kama yuko nchini, kwani ni uongo kwamba chama cha mapinduzi kinayumba ni uongo kwamba Rais ni soft on corruption. Nyie mliozoea kudanganya zamani mlidhani mna akili sana ndio maana mnapoona watu wanasema ukweli mnaona kama mnadhalilishwa.

Yuko South Africa bana na sijui kama amerudi; Mi nakuunga mkono hebu achana na wanaopinga yaliyoandikwa kwenye gazeti mbona tulishamwonya humu nchini akatuona mavuvuzela acha wa nje waanze sasa. Itafika mahali watamwambia " Thank you Mr. JK for showing interest in visiting our country but we are very sorry; we would like so see different faces. siku si nyingi Zuma atampa JK maneno kama haya kwani ameizoea nchi yake utafikiri msalani
 
huyu mtalii wacha aandikwe tu ni mzigo kwa taifa letu! yaani kila wakikata umeme namkumbuka mtalii namuomba mungu aitulize hasira yangu. hilo gazeti lipo sawia kabisaaa
 
Mkuu unataka kuleta mtindo wa kutete mwanao hata kama ni kibaka, wewe tetea tu! Kabla hujafikia kusema hayo maneno ni dhihaka ulipaswa kuyachambuwa na kusema lipi ni la uongo; kwa asillimia kubwa hilo gazeti limetoa hayo maneno ndani ya magazeti yetu ya ndani na vinywani mwa Watanzania.

Kama kinachokuhudhi si hayo maneno bali ni aliyeyasema, kuwa ulitaka yaongelewe na watanzania tu! basi unakosea, unakosea kwasababu ujue kuwa hilo gazeti ni la East Africa na ninadhani hata wewe unalisoma ukiwa Dar siyo Nairobi! basi linapaswa kuwa na taarifa za East Africa.

Ushahidi tosha wa hayo maneno ni pale ambapo katika serikali hii wakenya leo wanatuuzia hadi magazeti na wana-Benki imara ndani ya nchni yetu wakati hao viongozi wako wamesinzia hawana lolote wala mpango wowote juu ya soko la EAC wapo kama hawapo. Nadhani kama ni uzembe ni wazembe kuliko hata hao walivyosema.
 
mkiambiwa ukweli mnakasirika na kusema mnaonewa?

jk ndivyo alivyo yaani mimi nampa big up sana maana
 
Eti hujapenda yaliyosemwa am happy sababu hii inatia aibu na ni vizuri waongelee kumbuka ni EAU kwa hiyo good for him na bado wamchambue hadi akome

Kama sie tunaogopa tunabebwa kama wajinga acha wakenya waseme ila jua kuna watz wanaandika pia kwenye hilo gazeti.
 
You can cover the truth with cement nor can you cover the a lie with a piece of cake.people observes,people sees,people analyse,peopple sorts stuff, ok that is peoples power for judgement if its true let him speak out.for im sure it is a frank note
 
Tuachane na lilikosajiliwa pamoja na wamiliki mkuu maana itabidi tufunge pia safari hadi brella nk...... turudi kwenye hoja yako ya msingi. Kosa la gazeti hatulioni Afande!

Hoja ni kwamba sikupendezwa na habari hizo. Hayo ni mawazo yangu kama hukubaliani nayo sawa.
 
Bwana Yesu alisema " Toeni boriti machoni mwenu kabla ya kutoa vibanzi machoni kwa wenzenu". Mbona Rais wao Kibaki anamuacha mkewe anawapiga waandishi wa habari Kenya na hakuna wakusema chochote!!
 
Kwa kweli mimi binafsi nimefurahishwa na uhuru wa mwandishi husika wa gazeti ilo kwa kuchambua ukweli wa prezoo wetu pasipo kutafuna maneno.
Nitashangaa sana yeyote atakayekasirishwa na ukweli huu ulioainishwa na mwandishi wa gazeti husika.
Tofauti na hapo kama kuna atakaye lalama eti ohh mheshimiwa kadhihakiwa nitaidhinisha kwa kusema THE TRUTH IS AN OFFENCE.
 
Hakuna walichodhihaki hapo. Tena wamefanya uungwana kwa kuacha kuanika uozo mwingi tu.
 
waandishi wa habari wanasena huja balance story, kwanini haujapaste walivyozungumzia pia marais wengine? maanayake wachangiaji wengi wanalaumu gazeti hili kama vile limezungumzia rais wa TZ pekee. walichoandika ndicho kinachoongelewa hapa Tanzania mi sioni baya wameandika ambacho wewe na mimi tunakisikia kila siku
 
Mkuu, Nation Media inamilikiwa na Aga Khan lakini Wakikuyu wana stake kubwa sana katika hiyo Media House; in fact, hawa ndio wanaloliendesha, na mara zote wameitumia kuyumbisha siasa za Kenya.
Inaelekea hamuifahamu Kenya vizuri, fuatilia hata Wakenya wanaofanyia Mwananchi hapa kwetu au hata Daily Monitor kule UG, utakuta ni Wakikuyu na mara zote wana agenda zao wanazosimia.

Mkuu Wakikuyu ni hatari sana hawa. Nimewahi kufanya nao kazi nawajua vizuri sana. Huwa wanaitwa Wachagga wa Kenya!! Sijui kama kuna ukweli ndani yake.
 
sasa dhihaka iko wapi? leo hii hatuna umeme hatuna chakula cha kutosha wewe unalalamika wakenya wanamdhihaki rais wetu......acha mambo ya kis..ge

Mkuu mbona unatukana tena matusi ya nguoni? Huu ni mtandao wa jamii inaweza ikawa baba yako ndio ameandika hii post sasa unavyotukana hivyo ukikuta ndiye yeye utafanyaje? Najua unakubaliana na mwandishi kwamba ameandika ukweli ni sawa ingetosha tu kuandika hivyo hoja yako lakini kutukana wenzio si jambo la kiungwana. Kuwa muungwana basi ili ujitenge na watwana!
 
Back
Top Bottom