Magari yenye ZNZ Dar es salaam

..ZNZ ni nchi siyo wilaya au mkoa wa Tanzania Bara. Kwa msingi huo basi ni makosa kuendesha gari lenye number plate ya ZNZ ukiwa Tanzania Bara.

..wa-Zenj wanadai kwa ZNZ ni nchi, lakini wakifanya makosa yanayolingana na uhaini na wakashtakiwa wanageuka na kudai Zenj siyo dola/nchi.

..You can not eat your cake and have. Kama Wa-Zenj wanataka kufaidi matunda ya huku Tanzania Bara basi ni vizuri wakakubali ku-surrender utaifa wao.

..Muungano imekuwa kama kuchezeana akili tuu. we need some serious discussions on how we move forward.
 

Mimi nimeingia Zanziba mara nyingi tu kwa kutummia pasipoti. Mbona sikuwasikia hao ndugu zangu wakilalamika kuwa huu ni upumbavu katika nchi inayojiita imeungana? Badala yake nikajifunza neno 'chogo' lililokuwa likitumiwa kutusimanga sisi tunaotoka bara.

Fundi Mchundo,

Sii kweli- ni lini ulienda Visiwani ukapaswa kuwa na PassPort? Hii haipo we nenda tu hata leo huhitaji passport! Tena Visiwani kwa usalama wanazidi bara mara nyingi tu-- vibaka wapo wachache sana!

Wazenj ni watu wakarimu tu na wavumilivu, sema siasa chafu zinawarudisha nyuma!

Zenj could be a free port to serve hinterland ya Bara, E and C Afrika!

Halafu- kule kuna mabinti wazuri wenye heshima...Fundi kama hujaoa nenda Visiwani, au pia kama utataka bi mdogo ni poa tu!

Mie hata Pemba (Chanjaani, Utaani) pia nimefika na nimekupenda tu sana!
 
MzalendoHalisi,

..mbona hili suala la free-port naona kama Zenj hamna advantage. What if Tanzania Bara inaamua Mtwara au Tanga iwe free-port? Salmini si alishatangaza kwamba Zenj ni free-port?

..Zenj mngejitahidi kuanzisha viwanda na kukuza utalii. Hiyo itaondoa tatizo la ajira linaloanza kuwa sugu. Matatizo ya madawa ya kulevya yanasababishwa na frustrations za vijana kukosa kazi.
 
Watanzania tuna vichwa vigumu. Pesa haina mipaka ya nchi na serikali yetu inatakiwa kuelewa hivyo.

Suala ni kuwa Tanzania inalipisha kodi kubwa sana kuliko nchi zingine. Na wafanyabiashara siku zote wanatafuta upenyo wa kukwepa kulipa kodi zisizo na maana. Na hili sio suala la muungano ni upungufu wa akili.

Kwanini mwenye magari ya mizigo kutoka Tanzania watumie bandari ya Mombassa na sio DSM? Kuna watu wanapitishwa vitu Kenya, Burundi, Uganda na Rwanda kukwepa kulipa kodi. Na hao wanaofanya hivyo ni watanzania.

Sababu ya kulipa kodi kubwa ni kuwa ni asilimia ndogo ya watanzania wanaliolipa kodi. Na sehemu kubwa ya mapato inatokana na kodi ya ushuru wa kuingiza bidhaa. Na hiki kitu imefanya Tanzania ijitoe COMMESA.

Kodi kubwa haisaidi maendeleo ya nchi hata siku moja. Imefika wakati tuwe na flat rate kwa nchi zote za afrika mashariki.
 
Uzoefu unaonyesha kuwa TRA ilianza kutoza ushuru kwa namba za ZNZ, baada ya wingi wa magari hayo huko bara, na kuwepo na malalamiko ya mawakala wa uuzaji magari huko Bara. Katika awamu ya tano ya SMZ kulikuwa na viwango tofauti ya ushuru bandarini na SMT, kwani SMZ ilikuwa na idara yake ya forodha.

Awamu hii ndio iliyoshuhudia wingi wa wafanyabiashara ndogo ndogo toka kona zote za afika mashariki wakiingia Zanzibar kwa kutafuta bidhaa mbalimbali kama vile; TV, video, nguo, vitambaa, kanga, viatu n.k.

Kushamiri kwa biashara hizo kulifanya matajili wakubwa wa Zanzibar na Dar kuanza kutumia bandari ya zanzibar kwa manufaa yao binafsi zaidi. Hapa ina maana kuwa kutumia bandari hiyo kupitisha mizigo yao tu na kuipeleka Tz bara. Katika hali hii ndio ukawa mwanzo wa magari yanayonunuliwa Uarabuni na Japan kupitishwa na kusajiliwa Zanzibar kabla ya kupelekwa Dar na katika mikoa mingine. Wengi wanaweza kukumbuka wingi wa daladala za Dar zilizokuwa na namba za ZNZ.

Kilichofuata hapo kitu gani kifanyike ili kuondoa uingizaji wa magari hayo bara. Kwa maneno mengine SMT inanufaika vipi na biashara ya magari toka Zanzibar? Serikali ya muungano ikaamua kuibana SMZ na kufanikiwa kuanzishwa kwa TRA Zanzibar. Licha ya hatua hii kupingwa sana na SMZ, ilifanikiwa. Huu ndio ukawa mwanzo wa kuondoka kwa namba za ZNZ huko Bara. Kwa upande wa SMZ ukawa ndio mwanzo wa kuangalia sehemu nyingine ya kupata mapato yake zaidi ya biashara na karufuu.

This is the Answer, Thank you Kibunango.
 
..ZNZ ni nchi siyo wilaya au mkoa wa Tanzania Bara. Kwa msingi huo basi ni makosa kuendesha gari lenye number plate ya ZNZ ukiwa Tanzania Bara.

..wa-Zenj wanadai kwa ZNZ ni nchi, lakini wakifanya makosa yanayolingana na uhaini na wakashtakiwa wanageuka na kudai Zenj siyo dola/nchi.

..You can not eat your cake and have. Kama Wa-Zenj wanataka kufaidi matunda ya huku Tanzania Bara basi ni vizuri wakakubali ku-surrender utaifa wao.

..Muungano imekuwa kama kuchezeana akili tuu. we need some serious discussions on how we move forward.

...."Muungano umekuwa kama kuchezeana akili tuu. we need some serious discussion on how we move forward."

And I believe we're heading that way...to a serious discussion, sooner than later. Fortysome years tumekuwa na muungano ulioanzishwa na viongozi tu, lakini wananchi hatujapewa nafasi ya kuuzungumzia kiuwazi, why?
 
Bado sijaridhika na majibu yenu

sijapata jibu la kitaalam pamoja na kusifiwa kwa JF kuwa ina wataalam kede kede

Hiii tunaweza tukaifanya iwe hoja nzito ambayo ZITTO na wenzie wanaweza kuiwasilisha BUNGENI (kwa sababu hakuna mbunge wa VUF ambaye anaona umuhimu wa kuinteract na si humu)

JE WATU KUTOZWA KODI MARA MBILI KWENYE NCHI MOJA NI HALALI?

JE TRA ZANZIBAR NI OFAUTI NA TRA BARA?

KAMA HAKUNA TOFAUTI KWA NINI KUWE NA KODI TOFAUTI WAKATI SISI WAMOJA?

KWA NINI TULIPIE MAGARI PESA ZINGINE TUKISHALETA BARA?


KAMA ISSUE NI WIZI KAMA ALIVYOSEMA KIBUNAGO HIYO SI KAZI YA TRA KUWAAMBIA WANANCHI WAASUZE MAGARI YAO KWANI WASHALIPIA KODI ZOTE SASA YA NINI KUWAAMBIA WATU WASIFANYE WATAKAVYO NA MALI ZAO?


JAMANI NAOMBA MNIPE MAJIBU YA MASWALI HAYA

TUJENGE HOJA KISHA TUIWASILISHE KWA WAHUSIKA NA IKIWEZEKANA TUFANYE ONLINE PETITION

Brazamen: Haya ni maswali critical sana; ngoja niwa-forwad-ie wabunge wetu labda watauliza huko bungeni.
 
...."Muungano umekuwa kama kuchezeana akili tuu. we need some serious discussion on how we move forward."

And I believe we're heading that way...to a serious discussion, sooner than later. Fortysome years tumekuwa na muungano ulioanzishwa na viongozi tu, lakini wananchi hatujapewa nafasi ya kuuzungumzia kiuwazi, why?

Hapa cha kulaumu ni huo mfumo wa muungano.
kabla hujaanza kuhoji kwanini unatozwa ushuru mara mbili ktk nchi moja mie naona ungeanza kuhoji hivi?
kwanini ktk nchi moja kuna marais wawili,serikali mbili,mabaraza ya mawaziri mawili??
Mbona wabunge wa zanz wanaingia ktk bunge la tz na wabunge kutoka tz bara hawaingii huko zaz??

Mdau mmoja hapo pia kachangia kuhusu ushuru nami namuunga mkono ushuru mkubwa hauisadii nchi bali unabomoa.
 
Fundi Mchundo,

Sii kweli- ni lini ulienda Visiwani ukapaswa kuwa na PassPort? Hii haipo we nenda tu hata leo huhitaji passport! Tena Visiwani kwa usalama wanazidi bara mara nyingi tu-- vibaka wapo wachache sana!

Wazenj ni watu wakarimu tu na wavumilivu, sema siasa chafu zinawarudisha nyuma!

Zenj could be a free port to serve hinterland ya Bara, E and C Afrika!

Halafu- kule kuna mabinti wazuri wenye heshima...Fundi kama hujaoa nenda Visiwani, au pia kama utataka bi mdogo ni poa tu!

Mie hata Pemba (Chanjaani, Utaani) pia nimefika na nimekupenda tu sana!

Ni kweli. Kwa muda mrefu nimetumia sana pasi mpaka hapo haja hiyo ilipoondolewa. Nazungumzia wakati ule na sio sasa hivi.

Wazenj wakarimu sana unapokutana nao. Wasi wasi wangu ni pale ninapokuwa sipo. Au pale ambapo hawaonekani kama hapa mtandaoni.

Potential Zanzibar ipo lakini tatizo ni hii kubaki kulaumu badala ya kujenga kwenye hizo. Uwezekano wa kuwa Freeport upo lakini angalia hali ya port za huko! Si za bahari wala si za anga. Wanazuiwa na nani kuwekeza? Serikali ya Muungano?

Hata mie pemba nimefika. Ni kuzuri lakini si sehemu (pamoja na unguja) ambayo ningependa kuishi. Hao mabinti siwawezi. Masharti magumu maana mimi misheni. Hao nawaachia wenzangu.
 
Brazamen: Haya ni maswali critical sana; ngoja niwa-forwad-ie wabunge wetu labda watauliza huko bungeni.

Mkuu KItila hakuna Crutical yeyote katika maswali hayo. Kibunango kajibu vizuri saana tatizo huyo bwana anataka majibu yanayokidhi matakwa yake.

Unapozungumzia uhuru wa Zanzibar na sheria zake kama nchi lazima tuelewe pia na zinamipaka yake.Huwezi kuwa na sheria kama nchi huru basi ukataka sheria zako zitumike kwenye nchi nyingine.
Hiyo taarifu iliwekwa baada ya Zanzibar kuja juu na kusema wao wanakuwa na Taarifu zao wakakataa za Muungano. Sasa hapa lazima tuelewe kuwa kodi hizo nikwa matumizi ya within Zanzibar tu. Ukitaka kujitanua zaidi ya Zanzibar then lazima utanue na mfuko. Utakapotaka kuingia kwenye uwanja wa Muungano then lazima ufuate sheria na kodi za Muungano. Ndo maana wanakudai ile tofauti ili iendane na kodi ya Muungano inavyodai.
Lipia kodi ya Zanzibar na mali zako zikabaki Zanzibar,hakuna atakaye kusumbua.Ukilipia Kodi ya Muungano utazunguka na mali zako katika Muungano hakuna atakaye kusumbua.Bottom line kodi ya Zanziba ni kwa ajili ya matumizi ya Zanzibar tu
 
Hapa cha kulaumu ni huo mfumo wa muungano.
kabla hujaanza kuhoji kwanini unatozwa ushuru mara mbili ktk nchi moja mie naona ungeanza kuhoji hivi?
kwanini ktk nchi moja kuna marais wawili,serikali mbili,mabaraza ya mawaziri mawili??
Mbona wabunge wa zanz wanaingia ktk bunge la tz na wabunge kutoka tz bara hawaingii huko zaz??

Mdau mmoja hapo pia kachangia kuhusu ushuru nami namuunga mkono ushuru mkubwa hauisadii nchi bali unabomoa.

Now, these are the serious questions we should discuss "freely" as citizens of this United Republic!
 
Watanzania tuna vichwa vigumu. Pesa haina mipaka ya nchi na serikali yetu inatakiwa kuelewa hivyo.

Suala ni kuwa Tanzania inalipisha kodi kubwa sana kuliko nchi zingine. Na wafanyabiashara siku zote wanatafuta upenyo wa kukwepa kulipa kodi zisizo na maana. Na hili sio suala la muungano ni upungufu wa akili.

Kwanini mwenye magari ya mizigo kutoka Tanzania watumie bandari ya Mombassa na sio DSM? Kuna watu wanapitishwa vitu Kenya, Burundi, Uganda na Rwanda kukwepa kulipa kodi. Na hao wanaofanya hivyo ni watanzania.

Sababu ya kulipa kodi kubwa ni kuwa ni asilimia ndogo ya watanzania wanaliolipa kodi. Na sehemu kubwa ya mapato inatokana na kodi ya ushuru wa kuingiza bidhaa. Na hiki kitu imefanya Tanzania ijitoe COMMESA.

Kodi kubwa haisaidi maendeleo ya nchi hata siku moja. Imefika wakati tuwe na flat rate kwa nchi zote za afrika mashariki.

Mkuu, ishu ni jinsi unavyoitumia kodi hiyo. Nchi za Nordic zina kodi kubwa na ndizo zinazoongoza katika maendeleo ya binadamu. kodi inatumika kuinua hali ya maisha ya wananchi wote kiasi kwamba haukuti umasikini kama ulivyo katika nchi nyingi za kibepari.

Watu wanapitisha bidhaa zao Mombasa badala ya Tanga au Dar es Salaam si kwa sababu ya kodi tu. Ni ukiritimba uliojaa katika bandari zetu ambazo zinaongeza gharama ya kupitisha mzigo. Kwani hizo transit goods zinatozwa ushuru?

Zanziba kutoza kodi ndogo ya ushuru ili watu waweze kupenyeza mali zao kuingia bara ni kuwa myopic. Hakuna value inayoongozeka katika bidhaa hiyo isipokuwa hayo maduka ya darajani. Wajanja wakaacha hata kuingiza bidhaa zao darajani, wao ni mbele kwa mbele hadi bagamoyo. Biashara kichaa gani hiyo.
 
JE TRA ZANZIBAR NI TOFAUTI NA TRA BARA?


Nimepitai hii thread mwanzo mpaka hapa ilipofika sijapata jibu la swali hilo hapo juu...
 
JE TRA ZANZIBAR NI TOFAUTI NA TRA BARA?


Nimepitai hii thread mwanzo mpaka hapa ilipofika sijapata jibu la swali hilo hapo juu...

Hakuna tofauti katika utendaji wao, kwani maafisa waandamizi wote hutoka makao makuu ya TRA. Tatizo ambalo wengi hatujaligusa hapa ni katika usajili wa magari. Zanzibar wana shirika lao la usajili (Shirika la Magari) ambalo ndio hutoa namba za ZNZ, hali kadhalika bara kutakuwa na chombo husika katika hilo. Tofauti za viwango vya kodi ilikwisha mara baada ya kuanzishwa kwa TRA Zanzibar,

Hata hivyo bado kuna misamaha fulani fulani ya kodi katika TRA zanzibar, ambayo imeshindwa kueleweka kwa baadhi ya wajumbe wa bodi hii.

Tukirudi nyuma mara baada ya TRA zanzibar kuwashikia mabango wafanyabiashara wapitishao mizigo katika bandari hiyo, Bandari ya Tanga ilikuja kupata umaarufu wa ghafla sana,wafanyabiashara wengi wakubwa wa Zenj na Dar waliamua kupitisha mizigo yao katika bandari hiyo, kiasi kwamba SMZ ikaona kama inaonewa na SMT kwa kushusha viwango vya kodi katika bandari ya Tanga. Baadae ilikuja kufahamika kuwa TRA walikuwa bado kujipanga vizuri katika ukusanyaji wa kodi zao, na waliwekeza nguvu nyingi katika bandari mbili kwanza. Dar na Zenj.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom