Jatropha
JF-Expert Member
- Apr 9, 2009
- 1,151
- 199
- Thread starter
- #81
umesoma sheria niliyoambatanisha au unakurupuka tu kutoa jibu? Kama alivyofanya katika mabangi kuisima mia tanaroad akidai kuwa mabangi ni chanzo cha ajali, vivyo hivyo awsimamie kushughulika na chanzo halisi cha ajali.mkuu una mabango yako mahara nini ndo maana umemvaa mr pombe?
Waziri kuja kuvuta gari iliyo na breakdown khaaaaaaa naona kuna haja ya polisi kukaa chonjo kama ndo ivyo.
Alafu kumbuka mabango mengine ni nussance kwa watumiaji wa barabara alafu yako kwa reserve ya tanroad alafu wanaokusanya hayo mapato ni halmashauri wakati ni road reserve yaani ni sawa na kukusanya kodi ktk nyumba ambayo si yako.
Waziri mkuu alipotaka shule zijengwe kila kata, aliwaita dodoma mameya na wakurugenzi wa halamashauri na kuwapa agizo na kuwataka kutekeleza. Ndio maana wakabuni vyanzo kama hivyo, sasa watoto wapo tayari shuleni unaua mapato wakati ni serikali na chama kimoja. Kwani hapakuwa na njia zingine za busara za kuzungumza? Ndio maana tunaonyesha kuwa hayuko perfect kama anavyodai kuwa chanzo halisi kinachoua watu barabarani sio mabango ni magarai yaliyotelekezwa barabarani na sheria zake zinataka wayaondoe, au sheria wanazojua ni kubomoa bomoa tu?.
Kumbuka katika hiyo bomoa bomoa ameshalitia hasara mara kibao k.m petrolo station mwazan aliyodai ipo kwenye road reserve serikali iliamuriwa kulipa bilioni 2. Nataka atumie busra zaidi.