Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,422
- 911,172
'Mafundi Tanesco fanyeni kazi saa 24'
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 7th December 2010 @ 06:26
WAKATI makali ya mgawo wa umeme yakiendelea kuwaumiza wananchi , Serikali imewaagiza mafundi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kufanya kazi kwa saa 24 ili kuharakisha ufungaji wa transfoma ya megawati 36 iliyopo katika Kituo Kidogo cha Kipawa Dar es Salaam ili kupunguza makali ya mgawo huo.
Aidha, wenyewe wamesema wakifanya kazi kwa saa 24 kwa kupeana zamu, watamaliza kwa siku nane.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo alitoa maagizo hayo jana Dar es Salaam wakati alipofanya ziara katika kituo hicho.
Natoa wito kwenu muongeze kasi ili kupunguza makali ya mgawo wa umeme mgawo huu unaathiri uchumi wetu kwa kiasi kikubwa, alisema Jairo.
Kituo hicho cha Kipawa kina uwezo wa kuzalisha megawati 72, kikihudumia wilaya za Ilala na Temeke na mara nyingine kwa Wilaya ya Kinondoni pale panapotokea dharura; hivyo kuharibika kwa transfoma moja yenye uwezo wa megawati 36 iliyoharibika wiki moja iliyopita, ilisababisha kuongeza makali zaidi ya mgawo.
Katika hali hiyo, Jairo aliwaagiza mafundi hao kuongeza kasi ya kuweka mitambo hiyo ili kupunguza hasara zitokanazo na mgawo wa umeme katika uchumi ambapo Kampuni ya National Contracting Company Limited ya Saudi Arabia ndiyo iliyopewa kandarasi ya kusimika mtambo huo, lakini kutokana na kasi yao kutoridhisha, ndipo mafundi wa Tanesco walipolazimika kuingia kazini ili kuokoa jahazi.
Mapema katika maelezo yake kwa Katibu Mkuu, Meneja wa Mifumo na Usambazaji wa Tanesco, Abdullah Fereshi alisema, kuweka mitambo hiyo kutachukua takribani siku 12 kwani mafundi hao wa Tanesco watakua wakifanya kazi kwa saa 18.
Katika hatua hii, Jairo alihoji iwapo itawezekana kupunguza muda huo ikizingatiwa athari zinazoikumba nchi kutokana na mgawo. Kama tukifanya kazi kwa saa 24 kwa kupeana zamu tutaweza kumaliza kazi ndani ya siku nane, alisema Fereshi.
Kuharibika kwa transfoma hiyo kumeongeza makali ya mgawo wa umeme Dar es Salaam, kwani licha ya uharibifu huo, mikoa mingine imekumbwa na mgawo kutokana na uhaba wa maji katika mabwawa ya kuzalisha umeme huku mitambo miwili ya kuzalisha umeme katika kituo cha gesi cha Songas cha Ubungo pia ikiharibika.
Umeme unaozalishwa kutokana na maji ni takribani asilimia 51 ilihali umeme unaozalishwa kutokana na vyanzo vingine kama gesi asilia na mafuta ni asilimia 49.
Wakati makali ya mgawo huo yakiendelea, Jairo alisema serikali inachukua hatua kadhaa kushughulikia tatizo hilo, akisema tumeshatoa pesa kwa IPTL kununua mafuta na mpaka sasa wamezalisha megawati 70 lengo letu ni kuzalisha megawati 100.
Alitoa changamoto kwa Tanesco kujijengea uwezo kwa kununua vifaa na kuacha kutegemea makandarasi.
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 7th December 2010 @ 06:26
WAKATI makali ya mgawo wa umeme yakiendelea kuwaumiza wananchi , Serikali imewaagiza mafundi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kufanya kazi kwa saa 24 ili kuharakisha ufungaji wa transfoma ya megawati 36 iliyopo katika Kituo Kidogo cha Kipawa Dar es Salaam ili kupunguza makali ya mgawo huo.
Aidha, wenyewe wamesema wakifanya kazi kwa saa 24 kwa kupeana zamu, watamaliza kwa siku nane.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo alitoa maagizo hayo jana Dar es Salaam wakati alipofanya ziara katika kituo hicho.
Natoa wito kwenu muongeze kasi ili kupunguza makali ya mgawo wa umeme mgawo huu unaathiri uchumi wetu kwa kiasi kikubwa, alisema Jairo.
Kituo hicho cha Kipawa kina uwezo wa kuzalisha megawati 72, kikihudumia wilaya za Ilala na Temeke na mara nyingine kwa Wilaya ya Kinondoni pale panapotokea dharura; hivyo kuharibika kwa transfoma moja yenye uwezo wa megawati 36 iliyoharibika wiki moja iliyopita, ilisababisha kuongeza makali zaidi ya mgawo.
Katika hali hiyo, Jairo aliwaagiza mafundi hao kuongeza kasi ya kuweka mitambo hiyo ili kupunguza hasara zitokanazo na mgawo wa umeme katika uchumi ambapo Kampuni ya National Contracting Company Limited ya Saudi Arabia ndiyo iliyopewa kandarasi ya kusimika mtambo huo, lakini kutokana na kasi yao kutoridhisha, ndipo mafundi wa Tanesco walipolazimika kuingia kazini ili kuokoa jahazi.
Mapema katika maelezo yake kwa Katibu Mkuu, Meneja wa Mifumo na Usambazaji wa Tanesco, Abdullah Fereshi alisema, kuweka mitambo hiyo kutachukua takribani siku 12 kwani mafundi hao wa Tanesco watakua wakifanya kazi kwa saa 18.
Katika hatua hii, Jairo alihoji iwapo itawezekana kupunguza muda huo ikizingatiwa athari zinazoikumba nchi kutokana na mgawo. Kama tukifanya kazi kwa saa 24 kwa kupeana zamu tutaweza kumaliza kazi ndani ya siku nane, alisema Fereshi.
Kuharibika kwa transfoma hiyo kumeongeza makali ya mgawo wa umeme Dar es Salaam, kwani licha ya uharibifu huo, mikoa mingine imekumbwa na mgawo kutokana na uhaba wa maji katika mabwawa ya kuzalisha umeme huku mitambo miwili ya kuzalisha umeme katika kituo cha gesi cha Songas cha Ubungo pia ikiharibika.
Umeme unaozalishwa kutokana na maji ni takribani asilimia 51 ilihali umeme unaozalishwa kutokana na vyanzo vingine kama gesi asilia na mafuta ni asilimia 49.
Wakati makali ya mgawo huo yakiendelea, Jairo alisema serikali inachukua hatua kadhaa kushughulikia tatizo hilo, akisema tumeshatoa pesa kwa IPTL kununua mafuta na mpaka sasa wamezalisha megawati 70 lengo letu ni kuzalisha megawati 100.
Alitoa changamoto kwa Tanesco kujijengea uwezo kwa kununua vifaa na kuacha kutegemea makandarasi.