Zitto
Former MP Kigoma Urban
- Mar 2, 2007
- 1,562
- 10,880
TAIFA LA MAFUKARA MILIONI 30 NA MABILIONEA 30
Zitto Kabwe
Zitto Kabwe
MweziJuni, 2012 niliandika andiko katika lugha ya Kiingereza (The Bottom 30M, www.zittokabwe.com) kujibu swali la kwa nini Watanzania ni masikini licha ya utajiri mkubwa ulioponchini. Katika makala hiyo ‘Mafukara 30M' nilihitimisha kwamba Watanzania ni masikini kwa sababu watawala wetu wameamua hivyo kwa kutunga na kutekeleza sera na mikakati ambayo inanufaisha watu wachache katika tabaka la juu la maisha ambao wengi wanaishi mijini na kuacha watu wengi wanaoishi vijijini wakiwa masikini zaidi. Katika tafakuri ya leo nafafanua zaidi huu mtazamo. Watawala wetu ninaamini wakiulizwa tena na wanahabari kwanini Tanzania ni masikini hawatajibu hawajui (Rais Kikwete na Waziri Mkuu Pinda wamenukuliwa zaidi ya mara moja wakisema hawajui kwa nini nchi wanayoongoza ni masikini). Nimesema na kuandika mara kadhaa sababu za umasikini kuongezeka nchini licha ya kwambauchumi unaonekana kukua kwa kasi.
Waziriwa Fedha ndugu William Mgimwa wiki iliyopita amerudia tunayoyasema kila sikukwamba Ukuaji wa Uchumi Tanzania haujapunguza umasikini. Tumekuwa tukisema kwamba mikakati ya kiuchumi tunayotekeleza haimsaidii Mtanzania wa kawaida maana hatuoni tofauti ya maisha yake. Serikali ikaendelea na inaendelea kutekeleza mikakati ile ile ikitegemea kupata matokeo tofauti.
NduguMgimwa, Waziri wa Fedha, anasema, "Takwimu zinaonyesha kuwa katika kipindi chamiaka 10 iliyopita uchumi umekua kwa wastani wa asilimia saba lakini umasikiniumepungua kwa asilimia 2.1 tu ambayo ni ndogo ikilinganishwa na asilimia yaukuaji wa uchumi". Akanukuliwa "Umasikini umepungua kwa asilimia 2.1 kutokaasilimia 35.6 mwaka 2001 hadi kufikia asilimia 33.4 mwishoni mwa mwaka janakatika kundi la masikini,". Hakuna kauli mpya hata moja. Kinachosikitisha ni kwamba Serikali imeendelea kuona MKUKUTA ndio mkakati pekee wa kuondoa umasikini nchini. Sera na mikakati ya Serikali ya kuondoa Umasikini imeshindwa. Taarifa ya Shirika la SID ya mwaka 2012 imeonyesha kuwa kati ya mwaka 2001 na2011 watanzania takribani milioni 5 zaidi wameingia katika dimbwi la umasikini.Kwa nini Uchumi unakua kwa kasi kubwa lakini ukuaji huu haupunguzi umasikini, unazalisha masikini zaidi?
Taarifa za Serikali pia zinaonyesha kuwa ukuaji wauchumi hautengenezi ajira kwa watu. Kwa nini hali hii? Kama kawaida hatukosi majibu ya maswali haya. Tunayarudia majibu haya kila wakati tunapopata nafasi ya kueleza. Kwamba Sekta za Uchumi zinazokua hazina mahusiano yenye nguvu na wananchi wa kawaida – Madini, Utalii na Mawasiliano. Sekta yenye mahusiano makubwa na wananchi – sekta ya Kilimo - haikui kwa kiwango kinachoweza kupunguza umasikini. Ili kupunguzaumasikini Tanzania kwa kiwango kikubwa, sekta ya Kilimo inapaswa kukua kwaasilimia zaidi ya nane (8%) angalau kwa miaka mitatu mfululizo na kuendeleakukua kwa wastani wa asilimia sita (6%) kwa miaka kumi.
Jibulipo na limeshasemwa sana lakini jawabu halisemwi. Labda tuulize tena. Kwaninisasa sekta ya Kilimo haikui kwa kiwango kinachotakiwa ili kuondoa umasikini Tanzania? Jawabu langu ni kwamba Watawala hawataki. Watawala wetu wamechagua Watanzania wengi wabakie mafukara.
Umasikini wa Watanzania ni chaguo mahususila watawala kwa kuamua kutekeleza sera ambazo zinakuza kipato cha mwenye nachona kufukarisha wananchi wengi wa vijijini. Vile vile uamuzi wa watawala kushindwa kupambana na ufisadi na ubadhirifu wa rasilimali za umma ni ufukarishwaji wa mwananchi wa vijijini ambaye anakoseshwa huduma za jamii na miundombinu ya kumpa fursa ya kufaidika na shughuli zake za kiuchumi. Ufukara wa mamilioni ya Watanzania ni matokeo ya chaguo la watawala kisera, kimkakatina kimatendo.
Ufukarani tofauti na Umasikini ingawa tunatumia maneno haya tukiamini kuwa yana maana inayofanana. Wakati Umasikini (poverty) ni hali ya kukosa huduma za msingi kama Elimu, Afya, Chakula na Maji safi na salama kunakotokana na kukosa kipato au kuwa na kipato kidogo, Ufukara (impoverishment) ni hali ya kukoseshwa huduma za msingi za kibinaadamu hata kama kuna juhudi za dhati za kufanya kazi kwa bidii ili kupata uwezo wa kufikiahuduma hizo. Umasikini unaweza kusababishwa na masuala mbalimbali ikiwemo haliya kuwa masikini tu (‘we are poor because we are poor') au jiografia nk. Ufukara unatokana na kufukarishwa. Unatokana na maamuzi ya kisera ya Taifa husika (au mataifa ya nje) ambayo yananyonya juhudi za watu kupata maisha yenye kuwapa huduma zote za msingi kama Elimu, Afya Maji na muhimu zaidi chakula chauhakika. Mafukara wote ni masikini, ila Masikini wote sio mafukara. Nitafafanua.
Mwaka1991 Watanzania masikini wanaoishi Dar es Salaam walikuwa ni takribani asilimia28.1 ya wakazi wote wa Jiji. Miaka 16 baadaye, asilimia 16 ya wakazi wa Jiji laDar es Salaam walikuwa wanaishi kwenye umasikini. Kwa upande wa Watanzania wanaoishi Vijijini, mwaka 1991 kulikuwa na masikini asilimia 40 ya wakazi wote wa Tanzania vijijini. Mwaka 2007, miaka 16 baadaye, asilimia 37 ya Watanzaniawa vijijini walikuwa wanaishi kwenye dimbwi la umasikini. Takwimu hizi unazipata kutoka Ofisi ya Takwimu na Shirika la Twaweza limerahisisha taarifa hizi kupitia chapisho lao ‘Growth in Tanzania: Is it reducing poverty?'
Masikini wanaoishi Dar es Salaam na miji mingine nchini wanaweza kujikwamua kutoka umasikini kutokana na fursa zinazojitokeza mijini. Miundombinu ya usafiri nausafirishaji, viwanda vipya na fursa za ajira zinajengwa zaidi mijini kuliko vijijini. Huduma za Elimu na Afya zinaboreka zaidi mijini na hata Walimu naManesi wanakimbilia kufanya kazi mijini ambako wamerundikana kuliko vijijiniambapo kuna ukosefu wa kutisha wa wafanyakazi wa sekta hizo. Masikini wa mijinisio mafukara.
Masikiniwanaoishi vijijini licha ya kufanya kazi kwa bidii na hasa kazi za Kilimo hawana fursa za kuondokana na umasikini. Mfumo wa Uchumi wa nchi umejengwa kwamisingi kwamba watu wa vijijini hupokea Bei za kuuza mazao yao kutoka mijini na vilevile hupokea bei za kununua bidhaa zinazotengenezwa mijini kutoka hukohuko. Barabara za vijijini zina hali mbaya au hazipo kabisa. Huduma za jamiikama Elimu, Maji na Afya ni mbaya. Huduma za nishati ya Umeme hazipo kabisa katika vijiji 96 kati ya vijiji 100 nchini. Masikini wa vijijini ni Mafukara.Wamefukarishwa kutokana na sera zinazonyonya jasho la kazi yao kwa upande mmojana sera zinazowanyima maendeleo ya miundombinu kwa upande mwingine. Asilimia 75ya Watanzania wanaishi vijijini hivi sasa na kwenye ufukara mkubwa sana. Kwamakadirio ya idadi ya watu Tanzania, Watanzania milioni thelathini waishiovijijini ni mafukara.
Kufunguliwakwa miundombinu ya Vijijini kama Barabara, Maji na Nishati ya Umeme kunawezakuwaondoa watu wa Vijijini kwenye minyororo ya ufukara kwenda kwenye umasikini na hatimaye kutokomeza kabisa umasikini. Lakini Watawala wanaogawa rasilimaliya nchi hawataki. Wanasema hakuna rasilimali fedha za kutosha kusambaza umeme vijijini ili kukuza viwanda vidogo vidogo na kuongeza thamani ya mazao ya kilimo, kusambaza maji safi na salama ili kuboresha afya na kumpunguzia mwanamke wakijijini muda wa kutafuta maji na kujenga barabara za vijijini ili wakulimawafikishe mazao yao sokoni. Ikifika kujenga shule na zahanati na vituo vya afyawananchi wa vijijini wanaambiwa wajenge wenyewe, wajitolee. Ni kweli hakunafedha za kuwekeza vijijini?
Ufisadi unatengeneza Mabilionea
Itakumbukwa kwamba mwaka 2007 Bunge la Tisa liliibua kashfa mbalimbali zinazoonyesha namna ambavyo fedha za nchi zinavyoibwa na wenzetu wachache. Haina maana kwamba Mabunge ya nyuma hayakuwa na Wabunge wenye uwezo au ujasiri wa kuibua masualaya msingi kuhusu fedha za nchi, lakini nadhani wakati au mazingira hayakuwa yanaruhusu. Tulishuhudia Ufisadi uliofanywa Benki Kuu ya Tanzania kwa kuibwa kwa zaidi ya shilingi bilioni 133 za malipo ya Nje (EPA), Utoroshaji mkubwa wafedha zilizofikia dola za kimarekani milioni 136 kupitia mradi wa Meremeta uliokuwa chini ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (TPDF), Uingiaji wa Mkataba waMadini ya Dhahabu wa Buzwagi uliokuwa na thamani ya dola za Kimarekani milioni400 bila kuzingatia uhitaji wa kuboresha mazingira ya nchi kufaidika na utajiriwa Madini na Wizi mkubwa wa Fedha za msaada wa kuagiza bidhaa kutoka Serikaliya Japani (Commodity Import Support) ambapo zaidi za shilingi bilioni 40ziligawiwa kwa viongozi kadhaa wa Serikali na wafanyabiashara.
Kashfachache zilijadiliwa sana ikiwemo ile ya Mkataba wa kununua Umeme wa Richmond ambao sasa unelekea kuliingiza hasara Taifa ya zaidi ya shilingi bilioni 90kutokana na hukumu ya Kampuni iliyorithi mkataba wa Richmond dhidi ya Shirikala Umeme TANESCO, ile ya Buzwagi ambayo ilipelekea kuundwa kwa Kamati ya Bomani iliyopelekea kuandikwa kwa Sera mpya ya Madini ya mwaka 2009 na Sheria mpya ya Madini ya mwaka 2010 na ile ya EPA iliyopelekea baadhi ya watuhumiwa kufikishwamahakamani lakini kuacha kitendawili kikubwa kuhusu Kampuni ya KAGODA ambayoilikwapua zaidi ya shilingi bilioni 40 katika shilingi bilioni 133 zilizoibwa. Masuala ya MEREMETA na Import Support yamezimika na mshawasha wa wafuatiliaji wa mambo kufuatilia masuala haya umepungua sana.
Masuala hayo machache yaliyoibuliwa katika Bunge la Tisa yanaonyesha kwamba kunarasilimali fedha nyingi katika Taifa ambayo ingeweza kutumika kuwekeza kwenye maendeleo ya watu wa vijijini. Hata hivyo rasilimali fedha hii inatumika kufanya Watanzania wachache kuwa mabilionea kwa njia haramu za kifisadi. Bungela Kumi, ninaamini, litaibua masuala mengine zaidi yanayoonyesha namna ambavyo tumeamua kuwafukarisha Watanzania wengi na kuwabilionesha wachache.
Matrilioni ya shilingi yatoroshwa kila mwaka
Katika Kitabu cha 'Africa's Odious debts: Howforeign loans and capital flight bled a continent' waandishi Leonce Ndikumana na James Boyce wameonyesha kwamba katika kipindi cha miaka 40 jumlacya dola za kimarekani 11.4 bilioni zimetoroshwa kutoka Tanzania kwa njia mbalimbali. Hizi ni sawa na wastani wa dola za kimarekani 285 milioni kutoroshwa kila mwaka kuanzia mwaka 1970 mpaka 2010. Sehemu kubwa ya fedha hizizinatoroshwa na Makampuni makubwa ya Kigeni yanayofanya biashara na kuwekeza hapa nchini (utoroshaji mkubwa umefanyika mara baada ya Tanzania kuanza kuzalisha dhahabu kwa wingi na makampuni makubwa ya nje kuanza kutafuta mafuta na gesi asilia kwenye bahari ya Tanzania) na sehemu nyingine ni bakshishi wanayopewa maafisa wa Serikali wanaofanikisha utoroshaji huu. Watanzania hawa (Wanasiasa, Watendaji, Maafisa wa Jeshi na Usalama wa Taifa na Wafanyabiashara) huficha fedha hizi chafu kwenye Mabenki ughaibuni na hasa Uswisi, Dubai, Mauritius, Afrika ya Kusini na maeneo mengine (Tax Havens/Offshore/TreasureIslands). Wengine wamewekeza kwenye mali zisizoondosheka kama majumba na zinazoondosheka kama hisa kwenye makampuni mbalimbali duniani.
Taarifa rasmi ya Benki ya Taifa ya Uswisi inaonyesha kuwa Watanzania wameficha hukozaidi ya dola za Kimarekani 196 milioni. Uchunguzi unaoendelea unaonyesha kuwa takribani Watanzania 30 wameficha Fedha zao katika Mabenki ya Uswisi. Hii nibila kuhusisha wale ambao wameficha fedha zao kupitia majumba na hisa kwenye makampuni mbalimbali duniani na hasa katika nchi za Mauritius, Afrika Kusini naDubai. Uchunguzi pia unaonyesha kuwa Mtanzania mmoja ambaye hana rekodi yeyoteya Biashara zaidi ya utumishi wa Umma ameficha takribani dola milioni 56 katikaBenki mojawapo nchini Uswisi. Serikali ya Tanzania mpaka sasa imekataa kuchukuahatua za kuwajua Watanzania hawa na kuhakikisha kuwa mabilioni hayayanarejeshwa nchini na kuelekezwa kwenye miradi ya maendeleo vijijini. Serikaliya Senegal hivi karibuni imetuma maombi rasmi kwa Benki ya Dunia kuisaidiakufanya uchunguzi na kurejesha nchini mwao mabalioni ya fedha yaliyofichwakwenye mabenki ya nchi za Ulaya na hasa Uswisi.
Ufisadi unafukarisha
Tanzaniaina mtandao wa barabara wa zaidi ya kilometa 85,000 zikiwemo za vijijini nawilaya (zinazosimamiwa na Halmashauri za Wilaya) na za Mikoa na Barabara Kuu (zinazosimamiwa na TANROADS). Fedha zinazotoroshwa kila mwaka ni sawa sawa nakutorosha takribani kilometa 800 za babara za lami kila mwaka kwa kutumia gharama za sasa za ujenzi wa barabara. Fedha hizi pia zinaweza kuunganisha umeme kwenye vijiji 1300 (asilimia 10 ya vijiji vyote nchini) kila mwaka kwa gharama za sasa za kuunganisha umeme tena kwenye mikoa ambayo haipo kwenyegridi ya Taifa (REA wanatumia takribani shilingi bilioni saba kusambaza umemekatika vijiji 16 vya Jimbo la Kigoma Kaskazini). Fedha hizi pia zingeweza kuajiri walimu wengi zaidi wa vijijini na kwa kuwa miundombinu ya umeme, barabara na maji ingekuwa imeboreshwa walimu hawa wangekaa vijijini nakufundisha watoto wetu. Ufisadi kama huu umekosesha nchi rasilimali zakuendeleza watu wake.
Rushwana Ufisadi inatengeneza Watanzania wachache kuwa mabilionea. Mabilionea hawaambao wana ushawishi mkubwa katika kuunda sera za nchi na utekelezaji wake wanapelekea kuundwa kwa sera na sharia zinazolinda utajiri wa walionacho na kuendelea kuhakikisha masikini wanaendelea kuwa mafukara. Rasilimali za nchizinaboresha maeneo ambayo mabilionea na wasaidizi wao wanaishi na kusahau kabisa kwamba Watanzania wengi wanaishi vijijini na huko ndipo kuna umasikini mkubwa. Umasikini wa vijijini kwa kiasi kikubwa unatokana na sera na matendo yanayofukarisha wananchi wengi.
Ukuajiwa uchumi unaoambatana na ufisadi wa kiwango kinachotokea Tanzania unawafanya wenye nacho kupata zaidi na masikini kuwa mafukara zaidi. Tofauti ya kipato katika jamii imezidi kuongezeka na inaweza kuleta machafuko katika nchi. Takwimu za Pato la Taifa, kwa mujibu wa Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa 2011, zinaonyesha kwamba asilimia 30 ya Watanzania (the richest 30%) wanamilikiasilimia 75 ya Pato la Taifa.
Tumeonakwamba Watanzania mafukara wanaishi vijijini, asilimia 75 ya Watanzania, na hivyo takribani Watanzania milionithelathini wanaoishi vijijini wanaishi katika dimbwi la umasikini. Vile viletumeona kwamba asilimia 30 ya watanzania wanamiliki asilimia 75 ya Pato lote laTaifa. Pato la Taifa mwaka 2011 lilikuwa shilingi 40 trilioni na hivyo asilimia 30 ya Watanzania wanamiliki shilingi 30 trilioni katika jumla ya shilinig 40trilioni. Kutokana na muundo wa uchumi wetu ambapo sekta ya Huduma (Service sector) na ile ya Viwanda (Industrial sector) zinachangia zaidi ya asilimia 70ya Pato la Taifa na ukweli kwamba sekta zinazokua kwa kasi ni pamoja naMawasiliano, Madini, Ujenzi na Utalii, ni dhahiri Watanzania na Kampuni za Kitanzania zinamiliki zaidi ya shilingi trilioni moja hawazidi thelathini nakuna watu wanaweza kuwataja mmoja mmoja kwa majina yao au majina ya Kampunizao.
Kwahiyo Watanzania milioni thelathini wamefukarishwa kwa kunyimwa fursa zakiuchumi na hivyo kumiliki sehemu ndogo sana ya Pato la Taifa. Wanafanya kazikwa bidii lakini mfumo wa kinyonyaji unawaweka katika umasikini daima dumu. Tumeona kuwa uchumi wa nchi unazalisha kundi dogo la watu wenye utajiri mkubwa ambao sehemu kubwa umepatikana kwa njia haramu. Watu hawa pia wanamiliki sekta zauchumi zinazokua kwa kasi na hivyo utajiri wao unazidi kuongezeka. Hawa wanashirikiana na Watanzania walio katikati (walalaheri) kuhakikisha wanaendelea kumiliki uchumi wa nchi. Hawa watu wa kati ndio wanasiasa, warasimu serikalini, wafanyakazi wa kada ya kati ya makampuni ya matajiri hawa au yanayofanya biashara na matajiri hawa. Badala ya watu wa kati kuweka sera madhubuti za kumkomboa Mtanzania wa chini aondokane na ufukara, wanaweka mazingira mazurikwa matajiri kutajirika zaidi.
Hatimaye tunajenga Taifa la Watanzania Mafukara milioni Thelathini na Mabilionea Thelathini.
Tukatae. Tunawezakujenga Taifa la watu wenye fursa sawa kwa kufanya maamuzi ya kubomoa mfumo wa kiuchumi wa kinyonyaji tunaoujenga tangu kupata uhuru kwa kuacha kubomoa mfumowa uchumi wa kikoloni licha ya Azimio la Arusha. Juhudi za kujenga Taifa lenye watu sawa ziliyeyuka mara baada ya kuamua kufuata sera za ubinafsishaji ambapo zilitafsiriwa kwa kukabidhi mali za Taifa kwa kundi dogo la watu na hivyo kutengeneza mfumo wa kifisadi ambao sasa umeota mizizi. Kazi iliyofanywa kwamiaka ishirini ya kujenga uchumi wa viwanda ziliyeyushwa katika kipindi chamiaka mitano tu ambapo viwanda vyote viligawanywa kwa watu binafsi na vingi leoni maghala tu ya kuhifadhia bidhaa nyingine.
Ufisadi mkubwa ulishamiri kupitia sera ya ubinafsishaji ambapo watawala waliokuzwa kwa ‘kanuni' ya ‘kutosheka' walijawa na tamaa kubwa na uroho wa mali na kuanzakukusanya chochote kilichokuwa mbele yao. Hivi sasa nafasi yeyote ya uongoziimekuwa ni nafasi ya ulaji na sehemu kubwa ya tabaka la watawala kuanzia kwawenyeviti wa vijijiji, madiwani, Wabunge, Mawaziri na hata Marais wamekuwa ‘rent seekers' yaani watu ambao ni lazima kulimbikiza mali kutokana na nafasi za utawala walizo nazo. Mfano wa Wabunge kulilia nyongeza ya posho za kukaa kitako wakati walimu na madaktari wanaishi katika mazingira magumu ya kazi nimoja ya tabia za kutotosheka na tamaa zinazopamba viongozi wa kisiasa wa zamahizi.
Kutochukuamaamuzi madhubuti ya kutokomeza ufisadi na mfumo wake ni kufukarisha Watanzania kwa sababu rasilimali ambayo inapotea kupitia vitendo vya kifisadi ingeweza kuwekezwa katika maendeleo ya watu wa vijijini, kwa kukuza shughuli za kiuchumi na kupanua mapato ya wananchi. Hivi sasa vita dhidi ya ufisadi imekuwa niturufu ya kisiasa tu na sio mchakato maalumu wa kuondoa kabisa mfumo wakifisadi. Ni lazima kuondoka kwenye hali ya kwamba wa ushujaa ni kutaja tu Fulani na Fulani ni fisadi, hali ambayo imefikia hata watu wasio na chembe yauadilifu kuchafua wengine, na kwenda mbele zaidi kwenye hatua za kubomoa mfumowa kifisadi.
Hata uchumi ukue kwa kasi ya namna gani iwapo ukuaji huo unanufaisha kikundi kidogocha watu hauna maana na ni hatari kwa uwepo wa Taifa lenyewe. Ni lazima kuchukua maamuzi ya kujenga taasisi zenye nguvu ambazo zitaondoa hali hii yauchumi kutajirisha wachache na kufukarisha wengi. Taasisi na mfumo utakaohakikisha kuwa watawala wanawajibika kwa umma kwa wanayoyatenda na wasiyoyatenda. Mfumo utakaohakikisha kuwa rasilimali za nchi zinarudi kwa wananchi ili kujenga miundombinu vijijini ya barabara, maji, nishati ya umeme na huduma za kijamii hasa elimu na afya. Vinginevyo tutaendelea kuwa Taifa vipande vipande kutokana na tofauti kubwa ya kipato na fursa ndani ya jamii.
Tanzania yenye Mafukara milioni Thelathini na Mabilionea Thelathini haikubaliki!