Mafanikio ya miaka 50 ya uhuru ni kizungumkuti

tumpale

JF-Expert Member
Nov 20, 2010
200
35
Nikirejea kipindi cha keki ya taifa kilichorushwa na mlimani tv na redio, mada ikiwa ni mafanikio tuliyopata katika kipindi cha miaka hamsini ya uhuru, mmoja wa washiriki bwana Risasi Mwaulanga wa amani forum anaonekana mtalii na si mtanzania, lakini kama angekuwa mtanzania na anaishi tanzania asingethubutu kuelezea mambo ambayo hayapo kwani hata kwenye vitabu vya hadithi mafanikio ayaelezayo hayapo. sijui kama foleni, ajali za meli, mgawo wa umeme, ukosefu wa maji, ukosefu wa madawati, ukosefu wa madawa, uhaba wa walimu na nyumba za walimu, kutokuwa na ndege hata moja, mikataba ya madini iliyofeki na mengine mengi yanayotia kichefuchefu ni mafanikio, alienda mbali zaidi kwa kumsifia jk, anavyoonekana ni kijana ambaye anaweza kupata muda wa kusoma na kuuliza kwa weledi na wanaoyajua mambo. Mwisho wa unafiki ni fedheha, avoid kusema ndiyo kumbe ni hapana ili tu upate mlo wako. vijana tusijidharaurishe.
 
Back
Top Bottom