Maendeleo hayaletwi na vyama vya siasa

Mkuu: Ni kweli kuwa siasa ni moja ya nyanja kuu za maisha, pamoja na tamaduni(kwangu kama msingi mkuu), na uchumi. Vitu hivi havitengani kamwe! Kila mtu ni mwanasiasa, mwanauchumi, na mwanatamaduni katika taifa lake...yaani hizo ni sifa kuu zinazo m-shape binadamu! Tujiulize hapa, ni nani haishi siasa, tamaduni, ama uchumi? Mambo hayo yote hupaswa kusimikiwa mifumo ya kuyaendesha kufikia maendeleo ya watu. Mifumo hiyo ni lazima isadifu (a) MAZINGIRA yaani sura ya nchi na watu wake (b) NYAKATI, yaani mahusiano yaliyopo katika mazingira, yaani baina ya watu na watu, na watu na sura yao ya nchi. ,, Hapo ndipo tunapohoji ufanisi na uzito wa mifumo iliyopo katika kuendesha nyanja hizi za maisha kuleta maendeleo. Je, mifumo hiyo inakidhi haja?
Kisiasa tupo chini ya "demokrasia", kiuchumi tupo chini ya "uchumi huria-free economy" Kitamaduni nako tunasema "uhuru-freedom". Yote hayo yapo chini ya katiba inayoitwa "HAKI ZA BINADAMU-HUMAN RIGHTS"
Tukiruhusu fikra zetu, kufanya upembuzi yakinifu juu ya mifumo iliyopo "HUWEZI KUKATAA KWAMBA, KUAMINI MAENDELEO YATALETWA NA SIASA ILIYOPO NI KUJIDANGANYA"
Ubunifu haujawai kufika mwisho. Tunayo nafasi ya kuutumia!
Mungu wetu anaita!
Hapana mkuu wangu hapana na wale watoe wanaotaka kuaminisha watu wengine kwamba CCM sio sababu ya Umaskini wetu bali uzembe wa wananchi wenyewe ndio wale wasiokuwa na haya hata kukubali kwamba umaskini wetu unatokjana na SIASA MBAYA na UONGOZI MBOVU.

SIASA ni ramani blueprint ya ujenzi wa kile ulokusudia hata iwe nyumba huwezi jenga tu ukitumia nguvu au kila mjenzi afikirie yeye ataweza vipi kuweka tofali na kipimo cha mafanikio kiwe nguvu zake. Hakuna kitu maendeleo ati ni ya kila mtu kwa nguvu na juhudi zake ati kwa sababu kuna DEMOKRASIA maana Demokrasia ni kipimo tu cha wazo lipi linakubaliwa kama vile unavyochagua ramani ipi ya nyumba itakufaa, lakini hutaki kuamini kwamba kuna umuhimu wa kuwepo ramani ya nyumba ktk makadirio ya fedha, vifaa na matumizi mengine.

Hakuna mtu anayejenga nyumba bila kuelewa ana kiasi gani mfukoni, nyumba hiyo ni kwa ajili gani na malengo haya ndio pale siasa zinapoingia kwa maana kwamba wewe unaamini njia ipi ni bora zaidi ya wazo la mtu mwingine. Na hata sisi binafsi ktk bongo zetu hukabiriwa na mtihani wa kifira ktk kuchagua njia bora ya kukabiriana na matatizo hivyo sio nguvu ama uwezo wa mtu bali siasa ni maamuzi yanayokubalika kufuatwa na wengi.

Free economy ni jina tu ambalo linatupa fursa watu kumiliki biashara badala ya serikali lakini pia serikali inalazimika kuhakikisha fursa hizo zinapatikana sii kwa njia haramu na pia kuhakikisha kila pato linalipiwa kodi na kwa kiasi gani. Bila siasa ni sawa na kusema kodi za wananchi hazijengi nchi, sasa sijui hizo barabara, maji, umeme na kadhalika vitajengwa vipi?. Siasa ni tofauti za kimawazo ktk Vipaumbele ktk maendeleo ya nchi na umuhimu wake utabakia pale pale..

HAKI za BINADAMU ama human Rights hazina uzito wowote isipokuwa makubaliano ya kimataifa ktk UTU wetu lakini Haifungwi na mkataba ambao unaweza piga marufuku tamaduni ambazo sii za kijamii iliyopo. Kwa mfano ndo ya wake zaidi ya mmoja haikubaliwi Marekani wakati Tanzania inakubalika. Ushoga unapigwa vita wakati nchi nyingine unakubalika hivyo hata hiyo haki za binadamu inatambua haki ya pande zote mbili husika na sio matakwa ya mtu mmoja mmoja.
 
Umasikini wa Mtanzania(Afrika) ni wa kihistoria wala si CCM ndio iliyo sababisha sisi tukawa masikini na wenye fikra duni.

Kumbuka nchi zetu za kiafrika zilipo tawaliwa na wakoloni, hawakutawala tu maeneo bali pia walitawala fikra zetu na kutufanya sisi kuwa hatuwezi, kila tunachokifanya ni cha kishenzi. Hapo sasa wakatuweka sisi tuwe tegemezi kwao.
Wakatuwekea kwenye akili zetu kuwa kila kitu wanachokifanya wao wako sahihi. Wakatugawa na kutupandikizia chuki kati ya mtu na mtu ili wahakikishe kuwa hatuwezi kujikwamua kwa jambo lolote.

Wakatukandamiza kifikra na kuwa tegemezi ili kwamba kila tufanyalo tunaonekana kama vile tunaigiza wenyewe tayari wameshalifanya siku nyingi. Wakatukandamiza ili tusiwe wabunifu.


Wametupa uhuru ambo ni wabendera wakageuza mfumo wa kututawala wakaingia na mfumo wa Ukoloni mambo leo, ambao ndio unazila nchi nyingi za kiafrika. Akiamua sisi kwa sisi tupigane wanatuchochea na tunapigana.

Hakuna mtu yeyote atakaye kuja kutoka nje bali ni sisi tu kuamua tufanye nini.
Huu utofauti wa kisiasa ni njia nyingine tena inayotugawa ili tusiwe na nguvu.

Ni kufikiri kwa kina na kuamua kujenga nchi kwa pamoja si kwa kujisifu kuwa wewe umefanya nini.
 
Maendeleo yanaletwa na siasa ktk nchi yeyote duniani ndiyo maana wenzetu wanabadili chama cha siasa kutokana na swra zake na wanaangalia na uwezo wa mgombea kuliko tz tuache siasa za kukomoana na kuchagua viongozi wabadhilifu wasio na uchungu na taifa hili.

Una mawazo mazuri sana na kama watu wote wangekuwa na uelewa wako kwenye mambo ya siasa nchi hii tusingekuwa maskini kamwe.
 
Poa bwana kwa kunitukana. Mimi sitaki matusi.
Lakini pointi yangu ni hii. Sisi vijana tunashabikia sasa wanasiasa na kuacha mambo ya maendeleo na tukiamini kuwa wanasiasa ndio watatuletea maendeleo

Hii ndio pointi yangu.


watu wanakutukana, kwasababu hoja yako haina mashiko ya kisiasa kana kwamba hujui kujenga hoja za kisiasa kiasi hicho;hata namna ya kuhamasisha vijana unaowalenga itakuwa vigumu ,sababu ushawishi wa kujenga hoja hauna.tanzania ya leo ni watu waelewa, hata kama kuna ghiriba namna gani(kama operation jaza uwanja chadema square) wanajua;hasa hili kundi la vijana ,ni waelewa mno na wanajua kuchambua hoja ,sababu wengi wao ni wasomi vichwa bado vibichi kutambua hilo.Kwahiyo ,iwapo watakuwepo wanasiasa uchwara wasiokuwa na dira , mwelekeo, mikakati, sera, na mbinu za kuleta maendeleo, watawabeza .Hivyo huna haja kuja na thread ya kishamba isiyokuwa na mashiko hapa.jifunze kutoka wa members wengine nmana ya kuwasilisha hoja.
 
Mkandara mkuu:
Labda sijakuelewa, lakini nina hakika kuwa hujanielewa.
1. Hakuna sehemu niliyokataa uwepo wa siasa. Ila nimetaka katika hili tutenganishe kwanza siasa kama nyanja ya maisha, dhidi mifumo yake mbalimbali. Mfano, monopartism, multipartism, hierachy, dictatorship, na mingineyo iliyopo na isiyozaliwa bado ambayo naamini ipo na ni bora kuliko iliyopo. UBUNIFU HAUJAWAI KUFIKA MWISHO. Mfumo mbovu wa siasa, ni zao madudu yote katika taifa. Mfumo mzuri wa siasa ni ule unaosadifu au kuzingatia MAZINGIRA na NYAKATI za eneo husika. Ukiruhusu fikra zako kuichunguza demokrasia, utagundua kuwa haina inachosadifu katika mazingira yetu wala nyakati zetu. Hivi ni asilimia ngapi ya watu wenye elimu ya demokrasia tz? Nina hakika haizidi 20% (kwa tafiti yangu binafsi). Zaid ya 80% ya watz hawaelewi chochote zaidi ya USHABIKI na HISIA. Je, sio hao wapitishao viongozi kwa hongo ya kanga na kofia? Wangapi tunawaona wakiomba kumpigia kura Nyerere 2010, tunafanya assumptions ni ccm, sio upuuzi huo? Nani alaumiwe kama siye akumbatiae mfumo huo? Zao lolote la mfumo mbovu, ni uozo tu. Ccm, cuf, Chadma, nk.ni zao la mfumo huu mbovu wa demokrasia.
2. Hakuna nilikosema umasikini wetu hakusabishwa na serikali madarakani. Ccm inatakiwa itoke madarakani, lakini pia c Chadma, TLP, nccr wala Cuf ifaayo kuingia madarakani. Ni sisi wenyewe wananchi, baada ya kuumiza vichwa kupita kiasi. UBUNIFU HAUJAWAI KUFIKA MWISHO.
3. Siasa ni blueprint-ramani ya kile tutakacho kujenga. Yaweza kuwa sahihi. Tujiulize, ramani tu inatosha? Vipi kuhusu kuchunguza eneo utakalo kujenga? Majirani zako, sheria zao mila na desturi zao, hali ya hewa yake, asili ya aridhi ya eneo, na mengineyo, ni muhimu kuzingatiwa kabla hujaanza kujenga, usipozingatia hayo utajikuta katika migogoro mikubwa katika eneo, mwisho utasitisha ujenzi na kung'oa kabisa hata msingi. Ndicho kinachotushinda kuishi demokrasia, hatuendani nayo. Na ilipandikizwa kwetu makusudi kwa maslahi ya adui zetu. Mbona tunafundishana madarasani jinsi gani ukoloni mamboleo ulivyo, halafu bado tunapalilia uozo.
4. Lengo la Haki za Binadamu ni kulinda UTU. Ipi ni tafsiri ya UTU kwako? Je, ni hii ya kuegesha magari 10 uwani hali jirani yako na familia yake wanalala chini ya maboksi, juu ya mkeka mlo mmoja, shuka ngumi. Wewe unakula na kusaza, bajeti ya chakula cha mbwa wako tu ya siku moja, ni sawa na bajeti ya chakula cha jirani yako ya wiki nzima. Ndio UTU huo? Lakini ni haki kwako, si mzungu amekuambia haki. UBUNIFU HAUJAWAI KUFIKIA MWISHO.
5. Free Economy: Wewe ni mtu mzima above 40, mimi ni mtoto below 15. Inaingiaje akilini kubebeshwa mimi na wewe tubebeshwe mizigo sawa alafu tushindanishwe mbio? Tuna mtaji na teknolojia gani ya kuweza kushindana na mzungu katika uwekezaji? Ndoto gani tunazoota mchana huu?
Wasomi wetu wamelishwa unga wa ndele, kwao nyeusi ni nyeupe na nyeupe ni nyeusi. Mental Slavery.
Mungu wetu anaita!
 
Jambo la muhimu tunalopaswa kutambua ni kwamba, kila binadamu anafanya makosa lakini hatupaswi kujiridhisha na makosa yetu bila kutumia fikra zetu kutafuta ufumbuzi mkubwa kusahihisha makosa yetu. Ukweli hautaki kupuuzwa hivyo tusijidanganye wenyewe na kujiridhisha kana kwamba matatizo na shida zetu hazihitaji fikra za juu zilizojaa hekima, ubunifu, uadilifu na busara na njia rahisi ni kutenganisha maendeleo, siasa na vyama vya siasa. Kama suala ni MFUMO tutafakari na tudai mabadiliko na mabadiliko haya hayawezi kuja kwa kung'ang'ania mfumo ambao tunahisi unafanya kile unachokiita SIASA iliyopo chini ya DEMOKRASIA.


Nimependa uelewa wako mkuu, pamoja sana!
Ni kweli kabisa, ukweli ukipingana nao utaja lia mwenyewe, kwani ukweli ni MANTIKI, haiwezi kubadilika hata siku moja! Ndio maana INAUMA sana kuona watu wenye nafasi kubwa kabisa wakiendelea kuukwepa ukweli, hali kwa nafasi zao wangeweza kuuanika hadharani kwa kila mtu kuuona na kujifunza. Wameng'ang'ania kupigania wasifu za watu, kupakana matope, taifa linadidimia! Sauti yangu na yako ni ndogo sana kusikika kulinganisha na ya Kikwete ama Dr. Slaa, lakini mahubiri yao ni utumwa. Basi nasi wenye sauti ndogo, tusiache kuutoa ukweli huu hata kwa mtu mmoja mmoja, pia tupiganie kupata sauti sasa.
Mungu wetu anaita!
 
Niwakati muafaka kwa watanzania wenzangu kukubali mabadiliko kwani ni dhairi kwamba hakuna chama chenye kuleta uhuru na maendele,hii nitafiti iliyo fanywa ulimwenguni kote na wasomi mbalimbali,kama unabisha i need evidence from you.
 
Ndugu wananchi maendeleo hayaletwi na vyama vya siasa, maendeleo yanaletwa na watu walioamua kuendelea.
Nchi ikiwa na wananchi walioamua kuendelea itaendelea tu.

Vijana changamkeni tumieni nguvu zenu. Nchi yetu ipo wanasiasa hawataweza hata siku moja kutuletea maendeleo.
i

unashindwa kujua vizuri ya kuwa hawa viongozi ndio wanaojadili mustakabali wa nchi hii,wamfanya maauzi ya mikataba ya nchi hii leo unasema hayawezi kuletwa na chama cha siasa. UTAKUWA SAHIHI KAMA UKISEMA MAENDELEO YA NCHI HII HAYATALETWA NA CCM kwa vile kimeshashindwa
 
Niwakati muafaka kwa watanzania wenzangu kukubali mabadiliko kwani ni dhairi kwamba hakuna chama chenye kuleta uhuru na maendele,hii nitafiti iliyo fanywa ulimwenguni kote na wasomi mbalimbali,kama unabisha i need evidence from you.

Profesa, kuna kauli ya msomi anaitwa Dr. Bana alisema "...hakuna alternative ya CCM", Kwa watu makini wataielewa vyema hii kauli.
Vyama vya upinzani vilivyopo nchini havina sera zenye kutekelezeka, vingi ni vyama-NGO, Maamuzi ni ya watu wachache na ndio wamiliki. nakuhakikishia siku kikipatikana chama makini, au vilivyopo vikibabadilika CCM itakuwa historia kama KANU.
 
Huu ni mwanzo wa mwisho wa CCM, poleni sana watani, ushauri wangu ni kuwa kuleni kadri mnavyoweza (msivimbiwe) mmebakiwa na miaka miwili na nusu. Uzuri wenyewe ni kwamba nchi hii imejaliwa neema nyingi na kamwe hamtaweza kuzimaliza hata mkijilimbikizia vipi.

Kumbukeni hata bado hatuaanza ku-scratch the surface ya maliasili tulizonazo Tanganyika ambazo kila siku zinazidi kuvumbuliwa kwa kasi, na zote hizo zitakuwa chini ya CDM mda si mrefu.....Ndani ya miaka mitano tu ya mwanzo (2015-2020) tutazigeuza zile ahadi 150 za baba Ritz kuwe za kweli...:yo:
 
Niwakati muafaka kwa watanzania wenzangu kukubali mabadiliko kwani ni dhairi kwamba hakuna chama chenye kuleta uhuru na maendele,hii nitafiti iliyo fanywa ulimwenguni kote na wasomi mbalimbali,kama unabisha i need evidence from you.

Ngoja niperuzi kabla ya kunanihii.
 
ni kweli unalolisema kwani vyama vyoote vya ukombozi pindi waasisi wanapoondoka au in the long run huwa havina manufaa sana katika kuleta ukombozi wa kiuchumi hili linatokana hasa na wale walioshika madaraka kuona UHURU ni wao kwa hiyo wana haki ya kuendelea ku itafuna nchi
 
Kauli yako sina hakika kama ino ukweli wowote coz maendeleo ni neno lenye maana pana sana na sina hakika kama unavijua vyama vyote vilivoleta uhuru duniani but kwa upande fulani inatutia nguvu tunaoichukia ccm
 
Back
Top Bottom