Prodigal Son
JF-Expert Member
- Dec 9, 2009
- 1,067
- 696
Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, amesema mpango wa wizara kutoa ripoti ya uchunguzi wa uamuzi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kutumia zaidi ya Sh. bilioni 2.5 kujenga nyumba mbili za vigogo wake, hauna tija tena kwa vile wasiwasi uliojitokeza kuhusu suala hilo, umefafanuliwa vema na Gavana wa BoT, Profesa Beno Ndulu.
Mkulo alisema hayo alipotakiwa na Nipashe kueleza lini serikali itatoa ripoti ya uchunguzi wa suala hilo.
"Tulimwambia (Gavana) atoe ufafanuzi. Baada ya kutoa ufafanuzi vizuri, tumeona hakuna tija tena kutoa hiyo ripoti. nadhani alieleza vizuri tu, unaweza kupata hiyo ripoti kwa Gavana," alisema Waziri Mkulo.
Awali, Waziri Mkulo alieleza kushtushwa na taarifa za BoT kutumia zaidi ya Sh bilioni moja kujenga upya nyumba ya Ndulu na kuahidi kuwa wizara yake ingefanya uchunguzi kuona uhalali wa matumizi hayo na kuweka mambo hadharani.
Waziri Mkulo alipata kukaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa pamoja na kushtushwa na taarifa hizo, jambo hilo ni kubwa na linahitaji umuhimu wa kipekee kuchunguzwa ili walipakodi wajue ukweli wa matumizi ya fedha wanazoilipa serikali.
Akitoa ufafanuzi huo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), Profesa Ndulu alikanusha kukarabatiwa na
ilimwagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kuteua mthamini huru ambaye atachunguza na kupitia taratibu na hesabu zilizotumika katika ujenzi wa nyumba hizo.
CHANZO: NIPASHE
Mkulo alisema hayo alipotakiwa na Nipashe kueleza lini serikali itatoa ripoti ya uchunguzi wa suala hilo.
"Tulimwambia (Gavana) atoe ufafanuzi. Baada ya kutoa ufafanuzi vizuri, tumeona hakuna tija tena kutoa hiyo ripoti. nadhani alieleza vizuri tu, unaweza kupata hiyo ripoti kwa Gavana," alisema Waziri Mkulo.
Awali, Waziri Mkulo alieleza kushtushwa na taarifa za BoT kutumia zaidi ya Sh bilioni moja kujenga upya nyumba ya Ndulu na kuahidi kuwa wizara yake ingefanya uchunguzi kuona uhalali wa matumizi hayo na kuweka mambo hadharani.
Waziri Mkulo alipata kukaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa pamoja na kushtushwa na taarifa hizo, jambo hilo ni kubwa na linahitaji umuhimu wa kipekee kuchunguzwa ili walipakodi wajue ukweli wa matumizi ya fedha wanazoilipa serikali.
Akitoa ufafanuzi huo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), Profesa Ndulu alikanusha kukarabatiwa na
ilimwagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kuteua mthamini huru ambaye atachunguza na kupitia taratibu na hesabu zilizotumika katika ujenzi wa nyumba hizo.
CHANZO: NIPASHE