Maelezo ya Brig. Gen. Al-Adawi kuhusu Dowans Feb 20/02/2011

Hii sasa ni dharau iliyopita kiasi. Kuna haja ya wananchi kuonyesha nguvu zao dhidi ya upumbavu huu wa Dowans. Hivi akina RA wanaitakia mema nchi hii?
 
Kuna kitu hakiniingii akilini hata kidogo. Hivi karibuni watanzania tuliambiwa kupitia vyombo vya habari vilivyofanya mahojiano na Rostam Aziz kuwa mmiliki wa Dowans ametoa Power of Attorney kwa Rostam Aziz kufanya mambo yote yanahusu kampuni. RA ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama chake ambacho Mwenyekiti wake hivi karibuni ametamka hadharani kuwa WANATAFUTA NJIA YA KISHERIA KUTOILIPA Dowans. Hivi ni kweli wameshindwa kumbana mwizi huyu na genge lake kupitia vikao vya Chama? Kwanini wanazunguka sana? Mimi nilidhani kuwa CCM ingemuita Rostam na kumwambia kuwa aachane na dhuruma hii kwa wananchi kwani kwa kufanya hivyo anakiangamiza Chama chake. Lakini swali langu jingine ni kuwa, sote tunaelewa kwa kupitia Kamati ya Dr. Mwakyembe kuwa Richmond ni kampuni ya ubabaishaji. Matokeo ya uchunguzi ule ndio yaliyomfukuza mshirika mkubwa wa RA ktk nafasi ya Uwaziri Mkuu, na mawaziri wengine wawili kulazimishwa kujiuzuru. Hivi ni kwanini tunaendekeza ujinga huu wa kukaa na kuongea na the so called Dowans???? CCM inatakiwa kuwaambia wananchi kama Serikali yake italipa Dowans au haitalipa, pia watuambie pesa watakazolipa watazitoa wapi? Na kama pesa hizo zipo, je wameona malipo ya Dowans ni muhimi saana kuliko vifo vya masikini wanaokufa kwa kukosa huduma bora ya matibabu mahospitalini , elimu duni kwa kukosa vitendea kazi mashuleni, na umasikini uliokithiri kwa wananchi wake? Nadhani umefika wakati sasa wa nguvu za Umma kutumika kudai haki zao kama Serikali ya CCM imeshindwa na badala yake imeamua kushirikiana na wezi ambao ni wajumbe wa CC na NEC.
 
Hivi RA na genge lake la wezi hawasikii kilio hiki cha watanzania? au kwa sababu wanajua likitokea la kutokea wao watatambaa na kutuacha tukimalizana kama majirani zetu? Je, watanzania wapo tayari kuchukua njia hiyo? Wameshirikishwaje ktk maamuzi ya kwenda njia hiyo? Nina wasi wasi hasira za wananchi zitahamia kwa wezi hao binafsi kwani Chama chao na Serikali yao vimeshindwa kuwatetea. Tanzania ni nchi yangu, naipenda sana kwani hakuna Tanzania mbili ktk Dunia hii, lakini kwa mwendo huu, huko tunakokwenda sidhani kama kutakuwa na amani ya kutosha kama tuliyonayo hivi sasa, na anayetupeleka huko ni CCM ya leo iliyoruhusu mafisadi wapenye na kupewa uongozi ndani ya chama kilichokuwa na imani kubwa sana kwa watanzania.
 
Mtu yeyote akitaja neno Dowans basi waliopo karibu watakunja nyuso zao na kusema kila aina ya ubaya kwa kampuni ya dowans. Nafahamu kuwa mchakato wake haukuwa wa wazi lakini swali je hayo makampuni mengine ya kufua umeme kama IPTL, SONGAS na mengineyo yalifuata taratibu zote za kisheria bila kuhusisha ruswa kwenye mikataba yao na Tanesco? Ikiwa hivyo basi tuna haki ya kuisakama Dowans na wale wote wanaohusika kwa namna moja au nyingine na Dowans. Lakini ikiwa makampuni mengine yaliyosalia ukiitowa Dowans pia na yenyewe yamejaa usanii na mikataba yake haikuwa na tija na iliingiwa kwa hila basi sisi "Watanzania" ni wanafiki! Wanafiki na tuna sababu za nyuma ya pazia kuisakama Dowans!

Kuna habari nimepata kuzisikia kuwa Dowans ndio kampuni pekee inayochaji "capacity charges" kuliko makampuni mengine Dowans wanalipwa 152 mil per day, Songas over 250 mil per day na IPTL kwenye 300 mil per day.

Nadhani imefika wakati tujaribu kutafuta ukweli na kuyachambua makampuni yote yanayofua umeme tusiwe waitikia kiitikio "kolasi" na pili tuache unafiki kama kuna makampuni zaidi ya moja yanayohusika na hila basi yakemewe yote kwa nguvu zote yasishambuliwe makampuni baadhi kwa sababu ya hila na chuki binafsi huku mengine yakiendelea kutunyonya.


Kabla ya kuwakilisha na kukaribisha hoja napenda kukoselewa na kuelimishwa hayo ni maoni yangu binafsi na figures nilizotoa ni just round figures sina source ikiwa kuna mtu ana source itakuwa kafanya jambo la maana akituletea source ya charges zinazolipwa na Tanesco kwa makampuni husika.

Nawakilisha.....
 
Taarifa nilizozipata hivi punde zinadai kuwa "mwizi huyu" aliyeingia leo toka Oman ni mzaliwa wa Zanzibar aliyenusurika ktk mapinduzi ya Zanzibar na kukimbilia Oman. Ujio wa leo na kuongea na waandishi wa habari umekuwa ni wakushitukiza sana. Bado tuna muda wa kutosha kumuuliza maswali yanayotukera, na akileta ujinga, nguvu ya Umma itabidi imeshukie, kama vyombo husika vitasita kufanya hivyo, ama kwa kumuogopa au kwa kutojua vifanye nini. Uwezo wa nguvu ya Umma tunao, Sababu tunazo, na nia ya kumwadabisha "dhurumati" huyu tunayo. Tunataka dunia ielewe kuwa Tanzania ya jana sio ya leo ktk mambo ya mzaha kama huu.
 
Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi amewasili jijini Dar akijitambulisha kuwa ni mmiliki wa DOWANS. KWakuwa DOWANS ni mrithi wa shirika batili la RISCHMOND na kwakuwa DOWANS wanataka kuhukumu uchumi, nashauri serikali imuweke ndani huyu mwarabu koko. Naamini akiwa ndani atataja wamiliki halisi ambao naamini wapo TAnzania. Na pia akipewa apokezi mazuri hasa pale Oysterbay polisi, atataja hata wahusika kamili kuanzia ikulu mpaka kwenye serikali ya kijiji. Kamwe haiwezekani mtu toka Oman ambaye hajawahi kufika Tanzania aweze ku-pull deal kubwa kama la DOWANS bila kuungwa mkono. Kikwete mwisho wako wa ufisadi na marafiki zako akina Lowassa na Rostam umekaribia.
 
Taarifa nilizozipata hivi punde zinadai kuwa "mwizi huyu" aliyeingia leo toka Oman ni mzaliwa wa Zanzibar aliyenusurika ktk mapinduzi ya Zanzibar na kukimbilia Oman. Ujio wa leo na kuongea na waandishi wa habari umekuwa ni wakushitukiza sana. Bado tuna muda wa kutosha kumuuliza maswali yanayotukera, na akileta ujinga, nguvu ya Umma itabidi imeshukie, kama vyombo husika vitasita kufanya hivyo, ama kwa kumuogopa au kwa kutojua vifanye nini. Uwezo wa nguvu ya Umma tunao, Sababu tunazo, na nia ya kumwadabisha "dhurumati" huyu tunayo. Tunataka dunia ielewe kuwa Tanzania ya jana sio ya leo ktk mambo ya mzaha kama huu.
wanataka kurudi nini?
 
Brigedia Jenerali (mstaafu) Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi wa Oman anatakiwa atuambie watanzania ni kwanini alitoa "very strong power of attorney" Rostam Aziz? Je, Power of Attorney hiyo haijafanya kazoo mpaka ameamua kuja mwenyewe? ni lini amemnyang'anya power of attorney Rostam Aziz? Kwanini amefanya hivyo? Taarifa zinaonyesha kuwa Dowans ya Costa Rica haipo. Mwanasheria anayedaiwa kumiliki Dowans wa Costa Rica alikana kuhusika na kampuni hiyo. Wakati hukumu (ya kijinga) inatolewa na Mahakama ya ICC, ilionesha kutoitambua Dowans Tanzania, je yeye anakuja kuongea na Serikali kwa kupitia kampuni gani? Hapa wasitake kutufanya sie ni "mafara" saaaana wa kutokujua hata haki zetu.Bgd. Gen (Rtd) Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi wa Oman, hapa umekuja kushindana na nguvu ya Umma, itakudhalilisha kuliko unavyofikiria.
 
Natoa hima kwa watanzania wote kuwa tusikubali kwa namna yeyote kuchezewa na "wezi" hawa waliovaa joho la CCM. Tuwaonyeshe kuwa "YES WE CAN, IF WE WANT".
 
Why are we dialog with criminals anyway. Kinachoonekana hapa wazi ni wizi mkubwa wa kitaifa. Taifa la Tanzania lina wananchi sio watu wachache waamue vitu vya kitaifa na kudai wao ndio wanatuwakilisha. Umeme wa Dowans ni "Sawa na Utumwa" Hii Process inayotumiaka kurudisha Dowans Tanzania wakati hii kampuni iliingia Tanzania kwa nia ya "Kutuibia" is Really Dis respective to Tanzanians. Tunajua nani anapush hii kitu na January we already know you tactics of becoming reach quick.

Why Are Rushing and Not Looking For Alternatives Beside Dowans?
 
Thubutu! :A S 13: Serikali ipi hiyo? Hii ya JK iliyowekwa mfukoni mwa mafisadi! Hao watampa ulinzi na kisha kumkaribisha kwa cocktails! CCM na serikali yake wapo tayari kutowalipa wazee wa EA mafao yao lakini huyo hata tukila majani watamlipa!
 
Nijuavyo huyu alishawahi kuikana iweje leo awe mmiliki.

Nijuavyo mie huyu bwana kawekeza kwenye kiwanda cha kuchambua pamba lakini kikitumika pia ku-finance mambo ya dini fulani.

Hili kanyaboya coz mmiliki wa Dowans twamjua ni RA. Je, wamemwuliza ilikuwaje wakatoa PoA yenye mamlaka kubwa kiasi hicho kwa RA wakati si mwanahisa wala mkurugenzi wa Dowans.

Tatizo waandishi wetu wengi wanaenda kwenye press conference pasi maandalizi

Nilishangaa waandishi wa habari walishindwa kumuuliza Brigedia Majuzi kama wanaweza kuvumia kama Jeshi la Egypt nilikasirika sana kuona hakuna aliyekuwa na hilo swali.
 
Hivi mtu akikuibia halafu anakuja na kusema mjadiliane akurudishie pesa kiasi flani utamfanya nini?
 
Mtu yeyote akitaja neno Dowans basi waliopo karibu watakunja nyuso zao na kusema kila aina ya ubaya kwa kampuni ya dowans. Nafahamu kuwa mchakato wake haukuwa wa wazi lakini swali je hayo makampuni mengine ya kufua umeme kama IPTL, SONGAS na mengineyo yalifuata taratibu zote za kisheria bila kuhusisha ruswa kwenye mikataba yao na Tanesco? Ikiwa hivyo basi tuna haki ya kuisakama Dowans na wale wote wanaohusika kwa namna moja au nyingine na Dowans. Lakini ikiwa makampuni mengine yaliyosalia ukiitowa Dowans pia na yenyewe yamejaa usanii na mikataba yake haikuwa na tija na iliingiwa kwa hila basi sisi "Watanzania" ni wanafiki! Wanafiki na tuna sababu za nyuma ya pazia kuisakama Dowans!

Kuna habari nimepata kuzisikia kuwa Dowans ndio kampuni pekee inayochaji "capacity charges" kuliko makampuni mengine Dowans wanalipwa 152 mil per day, Songas over 250 mil per day na IPTL kwenye 300 mil per day.

Nadhani imefika wakati tujaribu kutafuta ukweli na kuyachambua makampuni yote yanayofua umeme tusiwe waitikia kiitikio "kolasi" na pili tuache unafiki kama kuna makampuni zaidi ya moja yanayohusika na hila basi yakemewe yote kwa nguvu zote yasishambuliwe makampuni baadhi kwa sababu ya hila na chuki binafsi huku mengine yakiendelea kutunyonya.


Kabla ya kuwakilisha na kukaribisha hoja napenda kukoselewa na kuelimishwa hayo ni maoni yangu binafsi na figures nilizotoa ni just round figures sina source ikiwa kuna mtu ana source itakuwa kafanya jambo la maana akituletea source ya charges zinazolipwa na Tanesco kwa makampuni husika.

Nawakilisha.....

Nadhani wewe endeleza nguvu ya kukemea hayo mengine pia, siyo ukataze watu kukemea Dowans! Kosa + Kosa siyo sahihi; kukemea Dowans ni sahihi kabisa kama unataka kuunganisha na hayo mengine karibu sana lakini husije na hoja ya kosa + kosa = sahihi; huwezi kupoze muda wako kutetea Dowans eti kwa kuwa kuna makampuni yenye makosa kama yake hayajachukuliwa hatua na wananchni, utakuwa umetumwa, endeleza ukurasa wa kudai haki juu ya hayo makampuni siyo ufunge ukurasa wa Dowans ilikufungua ukurasa wa hayo mauzo mengine, nadhani hujaelewa dhana ya Watanzania hata kidogo! Watanzania hawaitaki Serikali ya Kikwete Kwasababu walimuamini year 2005 na kumpa kura nyingi sana wakitegemea kuwa atakuwa Mzalendo na kupambana na Wizi na Ufisadi kwanguvu zake zote, lakini yeye ndio ametokea kuwa Fisadi Na.01; kwa hiyo ni lazima ujue Dowans ndio lakini yote yanapingwa yamekuwa yakiongelewa siku zote ndio maana wakaongeza na Katiba kama sehemu ya mjadala mpana wa kudai uhuru na haki zaidi.

Fumbua macho yako utaona
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom