Madiwani Arusha Jino kwa Jino na Dr. Slaa

FIDIVIN

Senior Member
Aug 4, 2010
187
41
MADIWANI wa Chadema katika Manispaa ya Arusha, wamesema chama hicho ‘hakina ubavu’ wa kuwafukuza kwa kuwa kufanya hivyo, kitakuwa kinacheza mchezo wa pata potea.

Wakizungumza na gazeti hili kwa masharti ya kutotajwa majina gazetini baada ya kuonywa kutozungumzia mgogoro wao na uongozi wa chama hicho Taifa, madiwani hao walisema wanaamini Kamati Kuu ya chama hicho haiwezi kufanya kosa hilo.

‘’Hili suala linapaswa kuamuliwa kwa hekima na busara, kunifukuza mimi ama madiwani wote hapa kuna mambo mawili; moja Chadema kupoteza viti vyote ama kupata na hiyo ni bahati nasibu na sidhani kama Kamati Kuu italikubali hilo,’’ alisema mmoja wa madiwani hao.

Juni 29 Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, alikaririwa akisema chama hicho kiko tayari kuwatimua madiwani wake wote wa Arusha kwa madai kuwa wamekisaliti chama baada ya kufikia muafaka wa Arusha kwa maslahi ya mkoa huo.

Dk. Slaa alikaririwa, akisema uamuzi wa madiwani huo, kumpata meya na naibu wake Arusha ambao ulipongezwa na Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), hawautambui kwa madai una upungufu ukiwamo wa kukosa barua ya Chadema ya kukubali maridhiano.

Baada ya kauli hiyo ya Dk. Slaa, iliyotolewa baada ya kauli nyingine ya Mbunge wa Arusha, Godbless Lema, kwamba hatambui maridhiano hayo ya amani na yenye lengo la kuharakisha maendeleo ya Arusha, madiwani hao Juni 30 waliweka kikao katika hoteli moja
kubwa mjini hapa kujadili kauli hizo.

Baada ya kikao hicho, diwani mwingine alisema Dk. Slaa amewatumia ujumbe kwa njia ya mtandao wa intaneti na kuwaamuru waache kuzungumzia suala hilo katika vyombo vya habari.

Alisema hata hivyo, kikao chao kimesisitiza kuwa muafaka waliofikia na madiwani wenzao wa CCM, ni sahihi uliofuata taratibu zote kwa maslahi ya chama na si uamuzi wa mtu binafsi wenye uroho wa madaraka na kamwe hawakukurupuka.

‘’Tumefikia muafaka kwa maslahi ya Chadema pia, hatukufanya hivyo kwa uroho wa kutaka vyeo katika kamati ndani ya Halmashauri.

Kauli kwamba tuliamua kwa uroho wa madaraka ni kutaka kuupotosha umma na kauli hizo hazifai kutamkwa na kiongozi kama Lema,’’ alisema diwani huyo.

Alisema wanawaheshimu sana viongozi wao wa juu, lakini na wao ni viongozi waliochaguliwa na wananchi kama Lema na uamuzi waliochukua Lema anaujua, lakini inasikitisha kuona madiwani wakiamua ni kosa, wakati ni kwa maslahi ya wakazi wa Arusha.

Diwani huyo alidai Lema anajua kila kitu, kwa kuwa katika mchakato wa awali, alishirikishwa na kuambiwa kila kitu kinachoendelea, lakini hakutoa uamuzi ila kinachoonekana ni ubinafsi wake na huo ndio unaosumbua ndani ya Chadema.

‘’Hapa suala ni kutoa uamuzi kwa maslahi ya chama na si mtu binafsi; hilo halitawezekana, kwani kila mmoja anapaswa kuheshimiwa na kusikilizwa katika kutoa uamuzi na wasitokee baadhi ya watu ndani ya chama kuonekana miungu watu,’’ alisema.

Mbali na Dk. Slaa na Lema, pia Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alinukuliwa kwa nyakati tofauti akipinga muafaka huo.
Habari Leo
 
let the circus begin......... shida ya kufanya kazi kwa kutumia vyombo vya habari
 
  • Thanks
Reactions: LAT
kwanini madiwani wa chadema arusha wasipewe nafasi wakatumikia wananchi kwa jinsi wanavyoona? mgawo wa madaraka umekaa vizuri sana na haujaonesha kupendelewa kwa cdm au ccm.
wekeni siasa pembeni mchape kazi kwani ikifika 2015 madiwani watakabwa kwenye kata zao ni sio slaa au lema.
 
MADIWANI wa Chadema katika Manispaa ya Arusha, wamesema chama hicho ‘hakina ubavu' wa kuwafukuza kwa kuwa kufanya hivyo, kitakuwa kinacheza mchezo wa pata potea.

Wakizungumza na gazeti hili kwa masharti ya kutotajwa majina gazetini baada ya kuonywa kutozungumzia mgogoro wao na uongozi wa chama hicho Taifa, madiwani hao walisema wanaamini Kamati Kuu ya chama hicho haiwezi kufanya kosa hilo.

''Hili suala linapaswa kuamuliwa kwa hekima na busara, kunifukuza mimi ama madiwani wote hapa kuna mambo mawili; moja Chadema kupoteza viti vyote ama kupata na hiyo ni bahati nasibu na sidhani kama Kamati Kuu italikubali hilo,'' alisema mmoja wa madiwani hao.

Juni 29 Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, alikaririwa akisema chama hicho kiko tayari kuwatimua madiwani wake wote wa Arusha kwa madai kuwa wamekisaliti chama baada ya kufikia muafaka wa Arusha kwa maslahi ya mkoa huo.

Dk. Slaa alikaririwa, akisema uamuzi wa madiwani huo, kumpata meya na naibu wake Arusha ambao ulipongezwa na Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), hawautambui kwa madai una upungufu ukiwamo wa kukosa barua ya Chadema ya kukubali maridhiano.

Baada ya kauli hiyo ya Dk. Slaa, iliyotolewa baada ya kauli nyingine ya Mbunge wa Arusha, Godbless Lema, kwamba hatambui maridhiano hayo ya amani na yenye lengo la kuharakisha maendeleo ya Arusha, madiwani hao Juni 30 waliweka kikao katika hoteli moja
kubwa mjini hapa kujadili kauli hizo.

Baada ya kikao hicho, diwani mwingine alisema Dk. Slaa amewatumia ujumbe kwa njia ya mtandao wa intaneti na kuwaamuru waache kuzungumzia suala hilo katika vyombo vya habari.

Alisema hata hivyo, kikao chao kimesisitiza kuwa muafaka waliofikia na madiwani wenzao wa CCM, ni sahihi uliofuata taratibu zote kwa maslahi ya chama na si uamuzi wa mtu binafsi wenye uroho wa madaraka na kamwe hawakukurupuka.

''Tumefikia muafaka kwa maslahi ya Chadema pia, hatukufanya hivyo kwa uroho wa kutaka vyeo katika kamati ndani ya Halmashauri.

Kauli kwamba tuliamua kwa uroho wa madaraka ni kutaka kuupotosha umma na kauli hizo hazifai kutamkwa na kiongozi kama Lema,'' alisema diwani huyo.

Alisema wanawaheshimu sana viongozi wao wa juu, lakini na wao ni viongozi waliochaguliwa na wananchi kama Lema na uamuzi waliochukua Lema anaujua, lakini inasikitisha kuona madiwani wakiamua ni kosa, wakati ni kwa maslahi ya wakazi wa Arusha.

Diwani huyo alidai Lema anajua kila kitu, kwa kuwa katika mchakato wa awali, alishirikishwa na kuambiwa kila kitu kinachoendelea, lakini hakutoa uamuzi ila kinachoonekana ni ubinafsi wake na huo ndio unaosumbua ndani ya Chadema.

''Hapa suala ni kutoa uamuzi kwa maslahi ya chama na si mtu binafsi; hilo halitawezekana, kwani kila mmoja anapaswa kuheshimiwa na kusikilizwa katika kutoa uamuzi na wasitokee baadhi ya watu ndani ya chama kuonekana miungu watu,'' alisema.

Mbali na Dk. Slaa na Lema, pia Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alinukuliwa kwa nyakati tofauti akipinga muafaka huo.
Habari Leo

Slaa safari hii ameingia choo cha kike atawajua sasa madiwani wake wa Arusha wakoje, watamsulubu vibaya !
 
Source: Habari Leo!,........ ni kichaa pekee anaeweza kuliamini gazeti hilo, ninachojuwa mimi hilo gazeti ni propaganda mashine ya chama cha magamba.
 
Dr Slaa anahofu kivuli chake mwenyewe.

Asipokuwa makini hapo ndio patakapo mshushia hishma yake kwani anaonekana ni mshari sana asiyetaka amani hata kidogo kwenye mji wa Arusha na wakazi wa Arusha.

Au anataka kitu kidogo?
 
Msaliti lazima aadhibiwe hawa Madiwani Watapigwa chini na bado Cdm itaibuka kidedea.
 
Slaa safari hii ameingia choo cha kike atawajua sasa madiwani wake wa Arusha wakoje, watamsulubu vibaya !

Maoni kama haya yanayotolewa na Pro CCM ndio yule engineer Bukuku anayapenda kwa vile yametolewa na wanaCCM wenzake.Hakika nyani haoni kundule...
 
MADIWANI wa Chadema katika Manispaa ya Arusha, wamesema chama hicho ‘hakina ubavu' wa kuwafukuza kwa kuwa kufanya hivyo, kitakuwa kinacheza mchezo wa pata potea.

Wakizungumza na gazeti hili kwa masharti ya kutotajwa majina gazetini baada ya kuonywa kutozungumzia mgogoro wao na uongozi wa chama hicho Taifa, madiwani hao walisema wanaamini Kamati Kuu ya chama hicho haiwezi kufanya kosa hilo.

''Hili suala linapaswa kuamuliwa kwa hekima na busara, kunifukuza mimi ama madiwani wote hapa kuna mambo mawili; moja Chadema kupoteza viti vyote ama kupata na hiyo ni bahati nasibu na sidhani kama Kamati Kuu italikubali hilo,'' alisema mmoja wa madiwani hao.

Juni 29 Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, alikaririwa akisema chama hicho kiko tayari kuwatimua madiwani wake wote wa Arusha kwa madai kuwa wamekisaliti chama baada ya kufikia muafaka wa Arusha kwa maslahi ya mkoa huo.

Dk. Slaa alikaririwa, akisema uamuzi wa madiwani huo, kumpata meya na naibu wake Arusha ambao ulipongezwa na Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), hawautambui kwa madai una upungufu ukiwamo wa kukosa barua ya Chadema ya kukubali maridhiano.

Baada ya kauli hiyo ya Dk. Slaa, iliyotolewa baada ya kauli nyingine ya Mbunge wa Arusha, Godbless Lema, kwamba hatambui maridhiano hayo ya amani na yenye lengo la kuharakisha maendeleo ya Arusha, madiwani hao Juni 30 waliweka kikao katika hoteli moja
kubwa mjini hapa kujadili kauli hizo.

Baada ya kikao hicho, diwani mwingine alisema Dk. Slaa amewatumia ujumbe kwa njia ya mtandao wa intaneti na kuwaamuru waache kuzungumzia suala hilo katika vyombo vya habari.

Alisema hata hivyo, kikao chao kimesisitiza kuwa muafaka waliofikia na madiwani wenzao wa CCM, ni sahihi uliofuata taratibu zote kwa maslahi ya chama na si uamuzi wa mtu binafsi wenye uroho wa madaraka na kamwe hawakukurupuka.

''Tumefikia muafaka kwa maslahi ya Chadema pia, hatukufanya hivyo kwa uroho wa kutaka vyeo katika kamati ndani ya Halmashauri.

Kauli kwamba tuliamua kwa uroho wa madaraka ni kutaka kuupotosha umma na kauli hizo hazifai kutamkwa na kiongozi kama Lema,'' alisema diwani huyo.

Alisema wanawaheshimu sana viongozi wao wa juu, lakini na wao ni viongozi waliochaguliwa na wananchi kama Lema na uamuzi waliochukua Lema anaujua, lakini inasikitisha kuona madiwani wakiamua ni kosa, wakati ni kwa maslahi ya wakazi wa Arusha.

Diwani huyo alidai Lema anajua kila kitu, kwa kuwa katika mchakato wa awali, alishirikishwa na kuambiwa kila kitu kinachoendelea, lakini hakutoa uamuzi ila kinachoonekana ni ubinafsi wake na huo ndio unaosumbua ndani ya Chadema.

''Hapa suala ni kutoa uamuzi kwa maslahi ya chama na si mtu binafsi; hilo halitawezekana, kwani kila mmoja anapaswa kuheshimiwa na kusikilizwa katika kutoa uamuzi na wasitokee baadhi ya watu ndani ya chama kuonekana miungu watu,'' alisema.

Mbali na Dk. Slaa na Lema, pia Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alinukuliwa kwa nyakati tofauti akipinga muafaka huo.
Habari Leo

Yaleyale ya Udaku niliyosema yanaandikwa na gazeti la serikali.HABARI LEO.Eti hao madiwani wameomba majina yao yahifadhiwe.Ina maana hao madiwani wasione gazeti lingine la kupeleka hiyo habari zaidi ya HABARI leo? Shame.Niliandika thread hapa kuhusu hilo gazeti la serikali kugeuka kuwa adui mkubwa wa kusambaza uongo kwa chadema.Thread yangu ilichangiwa na watu wengi sana nashangaa Mod ameiondoa ghafla.Nalalamika Mod please tenda haki rudisha thread yangu hapa jamvini...
 
Dr Slaa anahofu kivuli chake mwenyewe.

Asipokuwa makini hapo ndio patakapo mshushia hishma yake kwani anaonekana ni mshari sana asiyetaka amani hata kidogo kwenye mji wa Arusha na wakazi wa Arusha.

Au anataka kitu kidogo?

Hizi ni ndoto za mchana ambazo mmekuwa mkiziota wanamagamba kila siku lakini Slaa anazidi kujijenga na kujiongezea umaarufu.

Asiyetaka amani ndani ya jiji la Arusha anajulikana kwamba ni ccm sasa slaa anatokea wapi tena??

Slaa hanunuliki kwa kitu kidogo ama kikubwa, ndio maana chenkapa alijaribu kumpa nafasi ya ubalozi ili atoke chadema lakini akashindwa.

Kitu kidogo wapeni hao hao madiwani wa arusha na kwa bahati mbaya kwenu wanamagamba, kitu kidogo mmeliwa na muafaka feki hautambuliki.
 
Mimi nangoja kuona CDM ikifanya maamuzi magumu. Siamini kuwa ni sahihi kuogopa hata ikibidi kuwatimua hao madiwani. Tusiwe kama wana magamba, tufanye maamuzi magumu, kama hawatakuwa radhi kuufutilia mbali huo muafaka na kuomba radhi watimuliwe. Huu ndio utakuwa msingi mzuri wa chama. Haiwezekani suala lililochukua hisia za watanzania mamilioni, na kupoteza uhai wa wapendwa wetu likaishia kienyeji namna hiyo. Hilo halikuwa suala la madiwani, lilikuwa ni suala la Chama ngazi ya Taifa. La ajabu ni kuwa hata mwenyekiti wa CDM mkoa hakuhusishwa. No way. CDM ijipambanue.
 
Dr Slaa anahofu kivuli chake mwenyewe.

Asipokuwa makini hapo ndio patakapo mshushia hishma yake kwani anaonekana ni mshari sana asiyetaka amani hata kidogo kwenye mji wa Arusha na wakazi wa Arusha.

Au anataka kitu kidogo?
Lugha za madrasa uzilete hapa JF,.......
 
Lugha za madrasa uzilete hapa JF,.......
We pimbi unajua kama lugha ya madrasa haikwepeki mpka sun day schools wanaitumia

Swahili is a language that fuses African Bantu with Arabic. Arab sailors and traders have established links and ties with East Africa for centuries, their language strongly merged with the local language to produce a creole derivative. The word Swahili itself is derived from Arabic Sawahili سواحلي which is plural for ساحل meaning [Language] of the Coast.
This article gives some examples of Arabic words still in today's Swahili.
Here are some words.
hatari خطر Danger. Also the title of a 1962 movie starring John Wayne, set in Africa.
Safari سفر Travel. Also: trip
mahaliمحل Place
vitabuكتاب Book
msumariمسمار Nail
kataقطع Cut, chop
habari خبر news
huruحر free
dhamiriضمير conscience
kamusiقاموس dictionary
baridiبارد cold
samahaniسامحني forgive me, excuse me
rafikiرفيق companion, friend
tafadhali تفضل please
furahi فرح happy

[h=2]Time[/h] The terms for time are strongly influenced by Arabic. Many of it taken by the prayer times of Islam.
asubuhiصبح morning
dakikaدقيقة minute
saaساعة hour
wakatiوقت time
alasriالعصر late afternoon
magharibiالمغرب sunset
alfajiriالفجر dawn
karneقرن century

The Swahili names for the first five days of the week all start with Juma, then the order of the day of the week, Saturday being the first day of the week. Jumaa is derived from the Arabic word جمعة which means Friday, as well as "week. Only two days of the week got the Arabic names:
alkhamisi الخميسThursday
ijumaaالجمعة Friday

[h=2]Animal Names[/h] Animal names are all native African Bantu (e.g. simba lion). However, there are a few exceptions.
Tausi طاوس Peacock, being non-native to Africa, it took the Arabic name, which in turn took it from Persian.



[h=2]Numbers[/h] The number system is also heavily Arabic, although not exclusively so.
nusuنص Half. The proper classical Arabic word is نصف nisf. In many present day dialects it is "nus", like in Swahili.
roboربع Quarter
sitaستة 6
sabaسبعة 7
tisaتسعة9
ishriniعشرين20
thalathiniثلاثين30
arubainiأربعين40
hamsiniخمسين50
sitiniستين 60
sabiniسبعين 70
thamaniniثمانين 80
tisiniتسعين 90
miaمئة 100. The middle letter in classical Arabic is Hamza, however, in present day dialects, like Swahili, it is a Y sound.
elfuألف 1000

[h=2]Resources[/h] Here are some useful links on Swahili.

 
We pimbi unajua kama 75% ya lugha unayoiongea wewe (kiswahili) ni ya Madrasa na sio ya sunduy school?
Pimbi yupo pale Lumumba anaewalipa nyoko kama nyinyi kuja kuvuruga mijadala hapa JF, mimi lugha nimejifunza school na college, na sio madrasa.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom